Mnaomshauri Rais juu ya Ikulu mpya Chamwino muogopeni Mungu

Mnaomshauri Rais juu ya Ikulu mpya Chamwino muogopeni Mungu

Kuhusu wasomi wetu kwakweli hapo ni zaidi ya amajnga, nilikuwa kwenye project moja ya serekali sisi tulipewa tenda ya kusafirisha vifaa vya huo mradi sasa wakaja Ma Engineer wa Serekali kukaguwa vifaa cha ajabu wao wanatuuliza sisi hiki kinaitwaje? mburaaaa [emoji1787] [emoji1787] [emoji2369]
Kwa ujumla ndani ya Serikali, taasisi za Serikali, mashirika ya umma, hakuna utaalam kabisa. Unaweza kusikia mtu anaitwa doctor, lakini uwezo wake ni aheri mwenye certificate kwenye private sector.

Nenda huko TANESCO, utasikia tu huyu na yule ni engineer, lakini hawana uwezo wa kujenga njia kuu ya umeme hata ya urefu wa 10km, au kutengeneza bwawa la kuzalisha umeme wa kutosheleza kijiji kimoja. Wanazekea ofisini kwenye makaratasi lakini hawana uwezo wa kufanya kitu cha kuonekana.
 
Walienda kuchukua ramani ulaya huko sijui nchi gani, na kwa wabongo walivyo wakafikia hotelini wakala bata wakapewa ramani feki, sawa na yule aliyepewa maboksi ya dawa ya korona feki.

Hawa wasomi wetu walishindwa nini kuchora mchoro wa ikulu ?

Ulisikia wapi ikulu ndani mna soko?
Makubwaa
 
ndiyo sababu hata kupangilia miji hatujui. mpaka tukibananisha makazi ndiyo tunafurahi. Kumbi za mikutano Ikulu...za nini? Hata walivyorundika wizara zote pale mtumba ni poor planning, hata wageni wa serikali kutoka nje watakuwa wanashangaa. Wizara zinapaswa kutawanywa kuepusha msongamano na ikitokea tafrani, kwa mpangilio ule ni rahisi sana serikali kuminywa - wangekwenda hata Kinshasa wakaona namna ambavyo majengo ya serikali yametawanywa.

Hebu check hata bunge lilipo....ni aibu tupu, unawekaje bunge gereji jirani na stand ya mabasi; kisha unahamisha stand unaipeleka nje ya mji mahali pazuri penye hadhi nzuri panapostahili kujenga ofisi za bunge?

Ni aibu sana nchi hii makazi na hata majengo ya serikali yanavyobananishwa kama vile Tanzania ni nchi isyo na ardhi ya kutosha, ingekuwa ndogo kama rwanda sijui ingekuwaje!
Hii nchi ni aheri hata tungewachukua wakulima vijijini wahitimu wa darasa la saba wenye akili nzuri watupangie miji kuliko hao wapuuzi wanaojiita wataalam wa mipango miji.

Hawa nawaita wapuuzi kwa sababu wanakula pesa yetu, hakuna cha maana hata kimoja wanachokifanya. Hakuna hata mji mmoja ambao hawa wapuuzi wamefanikiwa kuupanga vizuri. Miji yote, maeneo yaliyokaa vizuri ni yale taliyopangwa na wakoloni, lakini siyo hawa wapuuzi.

Angalia Dodoma ambako mpaka kulianxishwa mamlaka maalum, CDA, ya upangaji mji. Tazama upuuzi waliotoka nao. Itazame Dodoma, kuna mpangilio gani hapo, hata barabara kuu zimekaa kama uchochoro.
 
Kuhusu wasomi wetu kwakweli hapo ni zaidi ya amajnga, nilikuwa kwenye project moja ya serekali sisi tulipewa tenda ya kusafirisha vifaa vya huo mradi sasa wakaja Ma Engineer wa Serekali kukaguwa vifaa cha ajabu wao wanatuuliza sisi hiki kinaitwaje? mburaaaa 🤣 🤣 🤷‍♂️
Wakiambiwa ukweli wanakua wakali
 
Labda nimeelewa vibaya kuwa eneo la Ikulu ni kubwa mno
Sidhani huo ukumbi utakuwa karibu na Ikulu

Kwanza mjue eneo la Ikulu ni ukubwa gani ndio muanzie hapo
Nasubiri wa karibu hapo
Eneo ni kubwa sana, hiyo Chamwino ipo takribani 40km toka mjini Dodoma. Yaani watu wakae Dodoma, wasafiri kilometer 40 kuufuta ukumbi? Ni fikra duni sana.
 
Tatizo si eneo.
Hebu linganisha na mfano huu.
Ikulu ni mahali nyeti kuliko kambi yoyote ya Jeshi.
Sasa pale Lugalo wewe kaweke ukumbi wa mikutano kwa watu 3000.
Mtu atakuona mwehu!
we hakuna unalojua mshamba tu wa kisukuma, nenda kaelimishe wale washamba wenzako waache kunya vichakani. Watu mnaokunya vichakani bado mtashauri nini. Kinachowauma ni rais kuwa Samia, yule shetani wenu ameshatwaliwa hakuna jinsi tena.
 
Kwanza naunga mkono yote uliyosema hapa, naomba nami kupitia hapa niongeze machache kuhusu mapungufu ya tukio la uzinduzi wa ikulu ya chamwino...
Moja, Hivi ni kwa nini hakukuwepo watoto wetu yaani wanafunzi wa shule na vyuo, tena pengine ilitakiwa wawepo kuanzia wale pre nursery..kwa sabab ikulu ni urithi wao na si wa hao walioalikana, tunashindwa kuonyesha thamani ya uwepo wa watoto wa Taifa hili kwa nini lakini..kuna faida gani kumualika Mpoto na Bella ili hali kila leo tunawaona na wanayosema wala si mageni masikioni mwetu, wangealikwa wanafunzi shule hata 3 tu wakaimba nyimbo nzuri kwa niaba ya wenzao ingeleta furaha, baraka na faraja, watoto mahali popote wana nafasi ya pekee, hata penye mifarakano watoto huleta mapatano..kama tunawatoa watoto kwenye matukio muhimu kama la jana, hivi ni wapi tena tunaweza kuwafundisha kupenda taifa lao, kujitegemea, utii, kupenda vitu vya kwetu nk, wapi??
Tatizo kubwa la wasaidizi wa viongozi kwanza ni mentality ya anasa, pili uchovu wa akili na ulevi wa kuaminiwa! Mambo mengi sana wanatukosea tena mara kwa mara..hivi kuna mzazi huwa anahangaika wakati wa sherehe za kiimani kuandaa mavazi, chakula, mapambo kwa ajili ya wageni halafu watoto wako wachafu, hawajaandaliwa kushiriki pasaka au idd, ndio hivyo kweli? wageni wanaojitambua wakikuta hali ya namna hiyo watatoa udhuru wa kuondoka mapema wakuachie hayo yote uliyoandaa utumie peke yako! Sababu utakuwa umekosea pakubwa mno! Watoto wanapaswa kuwa waalikwa namba moja!
Kuonyesha uungwana waandaji mtutake radhi tafadhali, sisi hatutoi kodi yetu zitumike kufadhili anasa za watu wazima kama sisi!
Jambo la pili, Mh. Rais alisema itajengwa complex ikulu hadi viwanja vya gofu, hivi jamani kwa nini tuna fikiria sana burudani kuliko kazi? Ikulu ni sehem ya kazi, hayo mengine yote ya nini? Tuna uhakika gani baada ya miaka 40 ijayo watakaokuwepo watatumia? Haina haja kabisa, hivyo ilivyo inatosha, madam nafasi ipo ya kutosha, huko mbele kama wataona hayo ni ya maana wataweka wao, hata mzazi anapojenga nyumba huweka vile vitu vya msingi tu, siku hayupo yule atakayerithi akiona anayotaka yeye yanakosekana ataweka yeye ili pia awe na uchungu wa kutunza, ukiweka kila kitu unaweza jikuta unapoteza nguvu, muda na rasilimali bure sabab siku haupo hakuna atayetumia tena, sasa si bora nguvu ulizotumia ungetoa sadaka zisaidie wahitaji..tusiweke mbele sana mtazamo wa kuonyesha ufahari hata kama haihitajiki..TUJIREKEBISHE!
 
Q
Mizania ya maamuzi ofisi ya Rais kwa masuala kama haya yananipa matatizo kuyawaza kama yamepitia critical thinking.
Mambo kama haya ndiyo yanasababisha wasomi wetu wazarauliwe
Tatizo la serikali ya CCM inaajiri chawa na watu wa kuisifu
Lakini watu wenye akili kubwa kama profesa Asad serikali haiwataki
Na ni vigumu kuondoa ujinga maradhi na umaskini kabila ya kuiondoa CCM.
 
Eneo ni kubwa sana, hiyo Chamwino ipo takribani 40km toka mjini Dodoma. Yaani watu wakae Dodoma, wasafiri kilometer 40 kuufuta ukumbi? Ni fikra duni sana.
Kwa hiyo ukumbi utakuwa mbali sana na Ikulu?
Hilo ndio swali la muhimu
Wanachezea hela tu ili kujaza data kwenye vitabu vya CAG
 
Walienda kuchukua ramani ulaya huko sijui nchi gani, na kwa wabongo walivyo wakafikia hotelini wakala bata wakapewa ramani feki, sawa na yule aliyepewa maboksi ya dawa ya korona feki.

Hawa wasomi wetu walishindwa nini kuchora mchoro wa ikulu ?

Ulisikia wapi ikulu ndani mna soko?
Au labda mama hana mpango wa kukaa hapo,ikulu kweli iwe na muingiliano na jamii?
 
Hii nchi ni aheri hata tungewachukua wakulima vijijini wahitimu wa darasa la saba wenye akili nzuri watupangie miji kuliko hao wapuuzi wanaojiita wataalam wa mipango miji.

Hawa nawaita wapuuzi kwa sababu wanakula pesa yetu, hakuna cha maana hata kimoja wanachokifanya. Hakuna hata mji mmoja ambao hawa wapuuzi wamefanikiwa kuupanga vizuri. Miji yote, maeneo yaliyokaa vizuri ni yale taliyopangwa na wakoloni, lakini siyo hawa wapuuzi.

Angalia Dodoma ambako mpaka kulianxishwa mamlaka maalum, CDA, ya upangaji mji. Tazama upuuzi waliotoka nao. Itazame Dodoma, kuna mpangilio gani hapo, hata barabara kuu zimekaa kama uchochoro.
Yaani dodoma imeharibiwa vibaya. unashangaa maeneno kama kisasa kuna viwanja vya mita 15x20 yaani dodoma imekuwa skwata. nilitegemea dodoma itapangika kuwa na viwanja na bustani za wazi, mji utajengwa kwa kutanuliwa, eneo la kuzika etc.

Yaani planners wetu hupanga mji hata hewa inakosekana. Kila kipande cha ardhi lazima kijengwe. Matokeo yake miji yetu inazeeka haraka mno - bar kila mahali, maduka, magenge na masoko kila mahali kelel ndiyo usiseme.
 
Walienda kuchukua ramani ulaya huko sijui nchi gani, na kwa wabongo walivyo wakafikia hotelini wakala bata wakapewa ramani feki, sawa na yule aliyepewa maboksi ya dawa ya korona feki.

Hawa wasomi wetu walishindwa nini kuchora mchoro wa ikulu ?

Ulisikia wapi ikulu ndani mna soko?
Kuna soko Ikulu?

Amandla...
 
Back
Top Bottom