Morogoro ni Mkoa mzuri namba Moja wa kuishi Tanzania

Morogoro ni Mkoa mzuri namba Moja wa kuishi Tanzania

Masaa matatu ukiwa mjini na viunga vyake ambapo ni 15% ya mkoa wa morogoro
65% Ya morogoro inakuchukua masaa 10 hadi 16 hivi kufika Dar (zaidi ya Arusha to Dar). Ni vizuri tukasema ukweli na sio hadithi za kufurahisha watu
Halafu Morogoro mjini ni ndogo sana unaweza ukazunguka kwa dkt chache ukaimaliza yote
 
Yawezekana Moro bado huijui vizuri Mzumbe ipo pembezoni kabisa Wilaya ya Mvomero , ina impact ndogo Sana kwa Moro town . Hebu taja mkoa wako hapa nisijekuwa nabishana na mlughalugha wa huko sitimbi

Wafanyakazi wa mzumbe wanaishi morogoro mjini
 
umenena
Kwema Wakuu!

Licha ya Tanzania kuwa na Mikoa mingi lakini Mkoa WA Morogoro ndio Mkoa namba moja Kwa uzuri Kwa kuishi. Nitaeleza sababu Kama ifuatavyo;

1. Tabia ya nchi na Hali ya Hewa.
Mkoa wa Morogoro tabia yake ya nchi na Hali ya hewa ni nzuri. Hakuna joto Sana wala hakuna baridi Sana.
Jua lake ni lakawaida ingawaje nyakati za kiangazi huongezeka kuwa Kali lakini ni afadhali zaidi kuliko jua la mikoa mingine.

Kuna msimu miwili ya Mvua, masika na kiangazi ambapo hutoa fursa Kwa kilimo kuvuna mara mbili Kwa Mwaka.
Tofauti na baadhi ya mikoa ambayo wanavuna mara moja kutokana na Baridi Kali au Ukame(joto Kali).

Vumbi lake sio Kali ukilinganisha na baadhi ya mikoa mingine Kama Dodoma, Singida, Mbeya, Iringa kipindi cha kipupwe hasa Maeneo ya Mufindi.

Maeneo yenye baridi ni milimani huko Mgeta matombo, Kibati kwenye kilele cha mlima Muscat huko Turiani,

Tabia ya nchi na Hali ya hewa inaufanya Mkoa huu kuwa moja ya mikoa tegemezi Kwa uzalishaji WA chakula hasa Maeneo ya Ifakara, kilosa, Mvomero, Na bonde la Mlali.

2. USO wa nchi(landscape) na Ardhi yenye Rutuba.
Morogoro ni moja Kati ya Mkoa wenye uzuri wa tambarare nzuri na Safu ya milima Uluguru.
Tambarare yenye udongo mzuri wenye rutuba ambao unasaidia zaidi kwenye kilimo.
Morogoro hakuna tatizo la chakula na ndio Mkoa unaolisha Mikoa inayoizunguka ikiwemo Dodoma, na Dar es salaam.

3. Connectivity (miundombinu ya barabara)
Morogoro ndio Mkoa pekee ambao Magari yote yanayoenda nchi za nje yanapitia hapo, yakitokea DAR es salaam kwenda Zambia, Malawi, South Afrika, Congo, Rwanda, Burundi, Uganda na wakati mwingine Kenya.

Ndio Mkoa pekee ambao ukitoka Mkoani huwezi kulala njiani, iwe unatoka Bukoba, Musoma, Mtwara, Songea, Rukwa au Kigoma. Ukienda Morogoro lazima ufike siku hiyohiyo,

Hii ni fursa ya kibiashara iwe Kwa usafirishaji wa mizigo inayoingia au kutoka.

Morogoro ndio Mkoa pekee ambao huwezi kukosa Usafiri muda wowote kwenda Dar es salaam, kwani usiku kuna Mabasi yatokayo mikoa ya mbali ambayo hufika usiku wa saa tano mpaka saa Saba.
Pia kuna IT na malori.

Reli ya Tazara, reli ya Kati, na sasa SGR zote zimepita hapo Morogoro.

Pia Morogoro ndio Mkoa pekee uliokatikati ya Majiji mawili makubwa ambayo ni Dar es salaam na Dodoma. Hii Kwa watu wenye akili za mbele wanaweza jua fursa hasa Kwa nyakati zijazo.

Morogoro ni Mkoa WA pili baada ya Dar ambao hakuna Basi kutoka Mkoa wowote lisiloenda Morogoro au kupita huko.

Hii ni tofauti na mikoa mingine Mfano, Hakuna Gari kutoka Mtwara to Mwanza,
Sumbawanga to Mwanza,
Hii ni tofauti na mikoa mingi.

4. Unafuu wa Maisha.
Morogoro ni moja ya Mkoa wenye unafuu mkubwa wa maisha kutokana na kuwa na chakula cha kutosha, matunda ya Aina yote.
Vyumba na nyumba za kupanga Morogoro ni nafuu na ni nzuri.
Vipo vyumba kuanzia Tsh 25 vyenye umeme na nyumba za laki na hamsini,

Usafiri wa kwenda mjini sio shida na nafuu.
Viwanja na ujenzi wa nyumba ni gharama nafuu.

5. Huduma za kijamii.
Mkoa WA Morogoro unajitahidi Kwa Huduma za kijamii Kama Hospitali, shule, Huduma za kibenki, vyuo vikuu, veta na vyuo vya Kati, Makanisa na Misikiti ya kuabudia ipo.
Huduma ya maji ipo ingawaje Maeneo ya Kihonda na Mkundi bado kuna uhaba kutokana na miundombinu ya maji.

Vituo vya Mafuta ya magari,
Viwanda ambavyo Vijana wengi wamepatiwa Ajira,
Vituo vya kisasa vya Ma Mabasi na abiria, Msamvu Bus Terminal ni moja Kati ya vituo vya mabasi vikubwa Kwa hapa Tanzania baada ya kile cha Magufuli Bus terminal cha Dar es salaam.

Viwanja vya mpira, Kama ulikuwa hujui Kwa Tanzania Morogoro ndio Mkoa namba moja Kwa kutoa wachezaji wengi WA mpira wenye kipaji na wanaocheza katika timu kubwa hapa nchini.

Masoko ya nguo na vyakula Morogoro sio tatizo.

Vituo vya redio na televisheni sio ajabu ndio Mkoa unaoshika nafasi ya pili baada ya Dar es salaam.

6. Vivutio
Morogoro ni Mkoa namba mbili Kwa vivutio vya mbuga na hifadhi baada ya Mkoa wa Arusha, Mbuga ya Mikumi na Hifadhi kubwa zaidi Duniani ya Selous inapatikana Morogoro.
Hui ni tofauti na mikoa mingi ambayo haikubahatika kuwa hata na mbuga au hifadhi ya wanyama hata moja, achilia mbali kuwa kubwa.

7. Uwepo wa mito Mingi.
Morogoro ndio Mkoa namba moja Kwa kuwa na vyanzo vingi vya maji hasa Mito. Hii ni tofauti na mikoa mingi Tanzania.

8. Ukarimu.
Mkoa WA Morogoro unawatu wenye ukarimu na ndio maana unaweza kumiliki Ardhi Kwa kiwango chochote unachotaka tofauti na baadhi ya mikoa mingi hapa nchi.
Sio ajabu Mkoa wa Morogoro ukakutaba na makabila karibu yote, hasa Waha, Wasukuma, Wachaga, Wapare, Wangoni, wamasai, Wahehe wabena na wakinga, Wanyakyusa, Wanyamwezi, Wabaya na makabila mengine mengi.

Mkoa WA Morogoro ndio Mkoa namba mbili Kwa kuwa na wageni wengi WA makabila mengine baada ya Mkoa WA DAR.

Hii ni tofauti na mikoa mingi hapa nchini ambayo mchanganyiko na makabila mengine utakuta ni mdogo.

Kwa kijana anayetaka kuanza maisha na hajui ni Mkoa gani akaanzie basi Morogoro ni moja ya mikoa ambayo unaweza ukaiweka kwenye Akili yako.

Karibuni MOROGORO.
kweli mkuu umenipa nguvu nina kiwanja changu kihonda kwa chambo nijiwekee hata kakibanda kakupangisha
 
Vyuo vya maana hapo ni viwili tu, SUA na Mzumbe, hivyo vingine ni zaidi ya vyuo vya Kata wanachuo wanachapwa bakora
Ukiachana na Dar kuna mkoa gani mwingine hapa Tz una vyuo vya maana hata viwili tu!?
 
Sasa tukikuita haraka dar, kuna party utawai kweli kuja?. Tunataka eneo tamu la karibu na dar au dom, na ndilo Moro.
Utakua una utoto au ujinga,kweni wewe tukikuita Mwanza kuna party,msiba au ndunguyo kapata shida hapa mjini utachelewa?ukichelewa ni umasikini wako,ila mimi ntakuja Dar chap na kurudi chap
 
Morogoro tatizo la maji sio la mitaa flani ni tatizo la mji mzima

Dar kuna mitaa ina shida ya maji Ila Morogoro labda uvune maji ya mvua Ila kama unategemea maji ya hilo bwawa sahau.

Nilishuhudia maji machafu yanatoka bombani nikapanyooshea mikono
Tatizo la maji Morogoro ni la mitaa utabisha hili labda kama ulienda mara moja tu na kurudi lakini sisi tulioishi kwa muda mrefu pale tunakuthibitishia tatizo la maji Morogoro ni la mitaa tu..Uzuri zaidi mimi kwa muda wote wa maisha yangu nimeishi hii mikoa miwili ya Dar na Morogoro,usichokijua chanzo cha maji Morogoro sio bwawa la mindu tu bwawa la Mindu linahudumia tu baadhi ya maeneo kwa mfano mimi niliishi Sabasaba tulihudumiwa na bwawa la Mindu na hatukuwahi kuona shida ya maji kwani maji ya bomba ilikuwa kila siku yanatoka halafu kuna wale ambao wanahudumiwa na maji kutoka mto Ruvu unaohudumia Dar pia kwa mfano maeneo kama bigwa,Kigurunyembe,na Kilakala wanahudumiwa na mto Ruvu hawa ndio kidogo wanaexperience shida ya maji kutokana na mto ruvu sometimes kupungua kina kumbuka unahudumia Dar,na maeneo ya pwani pia..Halafu kuna wale ambao wanaoishi sehemu za makao mapya kama Mkundi,Lukobe na Makunganya hawa nakiri wazi kwamba wanaexperience shida ya maji kama ilivyokuwa kwa maeneo mapya ya jiji la Dar ambao nao pia maji ya bomba wanayasikia kwenye redio
 
Naamini kibiashara ukitaka utoboe haraka

kama una mtaji wa kuanzia 20M kafungue duka la madawa ya mimea na mifugo Moro.

Ila u base hasa kwenye madawa ya mimea una weza piga sana pesa Moro.

Wana lima sana, ardhi na tabia ya nchi morogoro ina waruhusu kulima watakavyo.

kwahiyo wewe muuza madawa ya mime una weza kuwa tajiri mkubwa kwa kuwauzia madawa.


Hili wazo lina weza kumfaa mtu yeyote mwenye mtaji mzuri, hasa wa staafu, Pia hata kijana mungu aki bless ukawa na mtaji una weza lifanyia kazi hili wazo.
 
Elimu yangu nimeipatia morogoro na nikifikisha miaka 60 ntarudi kuishi morogoro na kufia ktk ardhi hio nnayo ipenda sana.
 
ila namba 7 sidhani kama ni sahihi, huu mkoa maji yake hata sio ya kuringia na maji ya mito hayatumiki kwa huduma za kawaida kama kunywa na kuoga yako full typod. ukisema mkoa wentr mito nadhani ni kagera na moshi huko hawana shida wale ya maji kwa moro hapa hapana hapana nakataa.mengine yote uliyoelezea uko sawa mia mia ni mkoa mzuri sana na sasa majengo makubwa marrfu yanaanza kujengwa soon linakuwa jiji.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nafikiri una matatizo kidogo kufikiri, Mkoa wenye milima Mingi Tanzania ni Morogoro (Uluguru, Nguru, Udzungwa, Rubeho, Nyanda za Mahenge, n.k). Mkoa wenye mito yenye maji mengi na mirefu Tanzania ni Morogoro, Mto Kilombero unaanzia Mlimba hadi Kisaki ambapo unabadiri Jina na Kuitwa Rufiji huko pwani, Pia Mto Ruaha unaingia Kilombero uku Morogoro. Mto Ruvu Unaanzia Uluguru hadi Bagamoyo, Mto Wami Unaanzia Kilosa hadi Bagamoyo. Tanzania ina Mito 5 maarufu na 4, ipo Moro, achana na vimto vya uko kama pangani na kagera ambavyo havina impact kwa nchi. 1. Kilombero (Moro). 2. Ruvu (Moro), 3. Wami (moro), 4. Ruvuma(Mtwara/Ruvuma), 5. Rufiji (Morogoro/Pwani). 6. Ruaha (Morogoro/Iringa). Usilinganishe Morogoro na Uchwara wowote kimazingira, ingawa yote ni mikoa na ina uzuri wake.
 
Tatizo la maji Morogoro ni la mitaa utabisha hili labda kama ulienda mara moja tu na kurudi lakini sisi tulioishi kwa muda mrefu pale tunakuthibitishia tatizo la maji Morogoro ni la mitaa tu..Uzuri zaidi mimi kwa muda wote wa maisha yangu nimeishi hii mikoa miwili ya Dar na Morogoro,usichokijua chanzo cha maji Morogoro sio bwawa la mindu tu bwawa la Mindu linahudumia tu baadhi ya maeneo kwa mfano mimi niliishi Sabasaba tulihudumiwa na bwawa la Mindu na hatukuwahi kuona shida ya maji kwani maji ya bomba ilikuwa kila siku yanatoka halafu kuna wale ambao wanahudumiwa na maji kutoka mto Ruvu unaohudumia Dar pia kwa mfano maeneo kama bigwa,Kigurunyembe,na Kilakala wanahudumiwa na mto Ruvu hawa ndio kidogo wanaexperience shida ya maji kutokana na mto ruvu sometimes kupungua kina kumbuka unahudumia Dar,na maeneo ya pwani pia..Halafu kuna wale ambao wanaoishi sehemu za makao mapya kama Mkundi,Lukobe na Makunganya hawa nakiri wazi kwamba wanaexperience shida ya maji kama ilivyokuwa kwa maeneo mapya ya jiji la Dar ambao nao pia maji ya bomba wanayasikia kwenye redio

Siwezi kubisha mkuu maana ni kweli huwa napita sana lakini nishaishi hapo zaidi ya mwaka na shida ya maji ilikuwa kubwa kiasi cha kutoa maji machafu hadi nikayasusia kuyatumia (around msamvu shule)

Na bado kwenye university year kuna marafiki zangu kibao walikuwa wanasoma SUA main & mazimbu campus, MUM, Jordan na wamepanga street lakini shida ilikuwa moja MAJI


Uzi mzima watu wanalalamikia maji kuwa tatizo ina maana wote hatuijui Morogoro isipokuwa wewe Tu mkuu
 
Sidhani. Tusubirie wataje Nauli ya SGR laah sivo Watumishi wa Umma hawatathubutu kujaribu, watabaki wafanya Biashara
Kama una biashara zako, unaingia ofisini mara mbili kwa wiki, unaachana na vurugu za Dar.
 
Comments za humu ni za watu wa Dar. Tuliosomea Moro tunajua shida za Maji na typhoid. Ukihamisha SUA na MZUMBE ujue umeiua Morogoro.
Kama watu wanatumia maji ya kutoka mindu basi kupata typhoid ni kawaida
Kuna makaz mengine wao wanatumia maji kutoka milimani hapo kdg nafuu

Ova
 
Back
Top Bottom