Mpaka sasa unamshukuru Mungu kwa jambo gani kuu alilokutendea maishani mwako?

Mpaka sasa unamshukuru Mungu kwa jambo gani kuu alilokutendea maishani mwako?

Uliyeandika uzi huu ukiuliza hili swali; uko hai?
kwa Neema na Baraka za Mungu nafurahia uzima wa afya ya mwili na roho kwa uhakika na bila tashwishwi yoyote ya wasio muamini Mungu alie hai :pulpTRAVOLTA:
 
Mabaya, maovu na mateso ni matokeo ya dhambi, na kwa kuwa tunaishi katika Ulimwengu wa dhambi nina kila sababu ya kumshukuru Mungu kwa zawadi ya uhai, neema na rehema zake kwani hata nyakati za magumu bado alinipa amani ya moyo na ujasiri wa kushinda.

Hivyo ntamshukuru daima kwa kila kitu. Thank you Jesus🙏🏿
Uwepo wa ulimwengu wenye dhambi ni uthibitisho tosha kwamba kazi ya uumbaji ya huyo mungu haikuwa kamilifu na ina dosari na kasoro.

Mungu huyo alishindwa kuumba ulimwengu usiyo na dhambi na badala yake ameruhusu uwepo wa ulimwengu wenye dhambi uwepo.
 
Uwepo wa ulimwengu wenye dhambi ni uthibitisho tosha kwamba kazi ya uumbaji ya huyo mungu haikuwa kamilifu na ina dosari na kasoro.

Mungu huyo alishindwa kuumba ulimwengu usiyo na dhambi na badala yake ameruhusu uwepo wa ulimwengu wenye dhambi uwepo.
Mkuu,
Una comment hapa ukiwa mmeshiba na una kipato chako Cha kila mwezi
Tanzania hapa amani Ni bwerere Usha jiuliza kwanini HAUKUZALIWA UKANDA WA GAZA AU HUKO MASHARIKI YA MBALI ""FAR EAST""

Mwenyezi MUNGU akiamua unakua yeyote muda wowote..

Tumsifu yesu Kristi.
 
Achilia mbali zawadi ya uhai, afya na maisha aliyokujalia na bado anakukirimia wewe na mimi bure bila malipo wala gharama yoyote....

Nafahamu, Mungu amekutendea mambo mengi mno maishani mwako, na huenda ukiulizwa kuyasema, kwasababu ya muda na ufinyu wa platforms, usimalize kuyaorodhesha yote...

Hebu mbele ya hadhara hii ya familia ya wanaJF,
Shuhudia matendo mema na makuu ya Mungu kwa uchache, alioyokutendea maishani mwako, ili kwa pamoja kama watoto wa Mungu, tushuhudie sifa na utukufu wake kwa watoto wake katika ulimwengu huu....

Neema na Baraka za Mungu, ziandamane na kuambatana nawe daima, katika familia yako, kazi na majukumu yako ya kila siku daima na milele....

Amen..
Sijui nianzie wapi.
 
Hilo nalo bado halijathibitisha Mungu yupo.

Kunitizama mimi nikiwa Marekani kutoka mbali hata kwenye Whatsapp unaweza.

Thibitisha Mungu yupo.
Kuna Mambo ambayo akili zetu za udadisi na za kibinadamu zinafikia ukomo unakubaliana na HILI..
 
Kuna Mambo ambayo akili zetu za udadisi na za kibinadamu zinafikia ukomo unakubaliana na HILI..
Hilo nalo si uthibitisho kwamba Mungu yupo.

Nakubali akili zetu zina ukomo.

Lakini akili zetu kuwa na ukomo si uthibitisho kwamba Mungu yupo.

In fact, akili zetu kuwa na ukomo ni uthibitisho kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Umeelewa hapo?
 
Duh hv ukiwa umezoea kuishi na mwenzako miaka mingi hi

Duh hv ukiwa umezoea kuishi na mwenzako miaka mingi hivyo utakuja weza ishi peke yako mkuu,?
Ni kazi mno. Inahitaji msaada mkuu wa Mungu Baba. Mkubwa sana..... Ila lazima aidha utaishia kuchepuka mno au utafuta nyumba ya pili haraka.
Mimi nilichoose alcohol maana SI mara ya kwanza anaenda kwao na nilijua HARUDI TENA ABADANI.... SO YES, I NEARLY DRANK TO DEATH BUT NOW AM SOMEHOW GOOD....
 
Mkuu,
Una comment hapa ukiwa mmeshiba na una kipato chako Cha kila mwezi
Tanzania hapa amani Ni bwerere Usha jiuliza kwanini HAUKUZALIWA UKANDA WA GAZA AU HUKO MASHARIKI YA MBALI ""FAR EAST"".
Kwani hao waliozaliwa huko ukanda wa Gaza na Far East, Hawakupaswa kuwa na amani?

Au huyo Mungu ndio alifanya hizo nchi ziwe na vita na machafuko ili mtu yeyote akizaliwa nje ya hizo nchi ashukuru kwa kutozaliwa kwenye hizo nchi zenye vita?
Mwenyezi MUNGU akiamua unakua yeyote muda wowote..

Tumsifu yesu Kristi.
Kuzaliwa Tanzania, Kenya, Rwanda, Ukanda wa Gaza, Afghanistan, Iraq, Congo, Ulaya au Amerika Hakuna uhusiano wowote ule wa uwepo wa huyo Mungu.
 
Kwa hiyo wote waliotendewa mema ni sababu ya Mungu?? Je walio pata ajali,vilema,wagonjwa,waliochinjwa,walioliwa na wanyama-Mungu alikuwa wapi?
Hili swali wataliruka kama vipofu vile.

Wote hawa wanao comment mara ohh! Namshukuru Mungu kwa uhai, uzima, pumzi sijui afya n.k

Wanadhani kwamba kushukuru kwao hivyo, kutawaepusha na kifo, ajali, au kuumwa.

Kumbe ni uongo mtupu, muda wowote watakufa, wanaweza kuumwa au kupata ajali.

Lakini kwa vile watu hawa wamesha pumbazwa na dini zao wana comment urojo hapa mara uhai, uzima, pumzi n.k wala hawafikirii sawa sawa.
 
Japo sio kwa 100% ila kumponya mzee wangu, ashukuriwe sana kiukweli. Pili mpaka hapa nilipo ni mapenzi na baraka zake, nitalisifu jina lake milele na milele
 
Japo huwa naomba msamaha kila siku kwa MUNGU wa mbinguni lakini najikuta natenda dhambi tena na MUNGU ni mwema hanitupi mwanae sina mtu wa kunisaidia kama wenzangu lakini napata msaada kutoka kwa MUNGU sina cha kusema itoshe kumshukuru lakini nasema MUNGU ALIYENIUMBA NI MWEMA KWANGU.
 
Kwani hao waliozaliwa huko ukanda wa Gaza na Far East, Hawakupaswa kuwa na amani?

Au huyo Mungu ndio alifanya hizo nchi ziwe na vita na machafuko ili mtu yeyote akizaliwa nje ya hizo nchi ashukuru kwa kutozaliwa kwenye hizo nchi zenye vita?

Kuzaliwa Tanzania, Kenya, Rwanda, Ukanda wa Gaza, Afghanistan, Iraq, Congo, Ulaya au Amerika Hakuna uhusiano wowote ule wa uwepo wa huyo Mungu.
Sawa mkuu Ila Mungu yupo
 
Back
Top Bottom