Mradi wa bandari ya Bagamoyo urejeshwe haraka sana

Mradi wa bandari ya Bagamoyo urejeshwe haraka sana

Sema tu mkuu kama uliahidiwa Ka pasent Fulani

Huo mradi ni watu wasiojua umhimu wa nchi Yao na athari zake
Kwani tatizo liko wapi kaeni na pori lenu la Mbegani mfugie swala na chatu kama mnadhani maendeleo ya kutuletea viwanda na Bandari ya kisasa havina maana.

J.K ni binadamu ambaye ni bingwa kwenye masuala ya diplomasia na ana heshimika sana Duniani, sasa kawaleteeni mradi mkubwa wa uwekezaji katika ujenzi na uendeshaji wa Bandari kubwa in eastern and southern Africa - nyie mlimpiga vita kwa kuwasingizia Wachina kwamba lengo lao ni kutuibia - zikapigwa propaganda lukuki kupitia vyombo vya habari nchini hasa TV na magazeti jinsi wachina walivyo kuwa wamepania kupiga mnada Taifa letu kupitia ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo! Propaganda hizo zilifanikiwa sana mpaka baadhi ya wananchi wakaingia laina na kuanza kuwasema sema wachina kwamba ni wezi, hawafai, kumbe ni ulaghai mtupu.

Propaganda hizo zenye walakini mkubwa Taifa letu likajikuta linapoteza mradi/investment ya maana kutokana na propaganda za kupikwa tu - mladi initiator ni Mh. Jakaya Kikwete basi watu wenye nia ovu wakapania kuupiga chini na kutunga adithi za kufikirika tu kuwazuga Watanzania ili wawasingizie Wachina kwamba ni wezi na walaghai, tunayasema hayo wakati mwaka jana nilimuona na kumsikia JPM akimuomba/sihi waziri mkuu wa China aliye tembelea Tanzania kwamba Serikali ya China isamehe Deni la ujenzi wa TAZARA, reli iliyo jengwa zaidi ya miaka hamsini iliyo pita kwa gharama ya matrillion ya TShillings , mpaka leo hatujawahi kuwalipa Wachina hata senti tano ya mkopo wao, vivyo hivyo mkopo wa ujenzi wa kiwanda cha nguo cha Urafiki - sasa kati ya yetu na Wachina walaghai ni akina nani?

Tumekalia mantra ya kuwasema vibaya Wachina kwamba ni wezi,wezi.

Ni suala la muda tu tutajikuta tunarudi kule kule kwa Wachina kuwabembeleza waje kutukamilishia ujenzi wa reli katika sections zilizo baki za SGR tena kwa mkopo wa riba nafuu yanarudi yale yale ya ushauri/maoni ya Mh. Jakaya Kikwete.
 
Mkuu, hapa hatufanyi hisani ya wao eti tumekaa na lupia zao miaka Mingi, hapa ni uhalisia Tu!! Mengine hayo hatutaki
 
Nani kakwambia ni Bandari isiyo na faida??? Kwa Unajua mradi wa Bandari ya Bagamoyo ulikuwa unahusisha mambo gani??? Au ndo tapeli wenu magufuli aliwalisha matango pori???
Kwa nini wewe unayejua usituwekee hapa hayo unayoyajua nasi tuyachambue?
 
Ww akili huna..!! Mjinga ww, kama hujui vitu vema acha ku post ujinga. Huu mradi ni wizi na wa kufilisi nchi yetu. Hell No
 
Sio 99.
Ni 50.mazungumzo yapo.
Mungu tusaidie! Mafisadi yanainuka kwa nguvu zote bila hata aibu! Hivi kweli biashara iendelee kwa miaka 50, bila kodi! Pia kwa sharti LA kutokuendeleza bandari zingine! Ni shetani tu anayeweza kuona upuuzi huo kuwa ni sawa!
 
Nani kakwambia ni Bandari isiyo na faida??? Kwa Unajua mradi wa Bandari ya Bagamoyo ulikuwa unahusisha mambo gani??? Au ndo tapeli wenu magufuli aliwalisha matango pori???
Kama una faida unadhani angeusitisha ili afaidike na nini?
 
Mungu tusaidie! Mafisadi yanainuka kwa nguvu zote bila hata aibu! Hivi kweli biashara iendelee kwa miaka 50, bila kodi! Pia kwa sharti LA kutokuendeleza bandari zingine! Ni shetani tu anayeweza kuona upuuzi huo kuwa ni sawa!
Natamani kusema sasa ni muda sahihi kwa Jeshi kuchukua nchi hii. Ni bora mara mia kuliko haya mafisadi yanayotaka kutumaliza kwa kuwa baba kalala.
 
Hivi mlimwamini Magu kuhusu masharti ya huu mradi? Kumbe kuna watu walikuwa wanamwamini kiasi hiki?

Ukweli ni kwamba Magu ali exaggerate masharti terms za huu mradi. Tafuteni ukweli mtajua
Hayo ndiyo masharti!! Kuna MTU alitaka kuuza nchi lakini ukimtazama usoni ni fundi wa kutabasamu!
 
Yaani miaka 50 nchi haichukui Kodi, haiendelezi bandari nyingine, haina mamlaka ya kuhoji na kukagua vitabu vya mapato na matumizi vya mchina.
BIG NOOOOO
Sasa hivi hiyo kodi ya bandari ya bagamoyo inakusanywa?

Kama jibu ni hakuna kodi inayokusanywa kwa sababu hiyo bandari haipo kwann ni tatizo kodi isipokuwepo kwa miaka kadhaa bandari ikiwepo?

Tukitumia pesa zetu za ndani tutajenga kwa muda gani na zitarudi baada ya miaka mingapi? Itakuwa ni miaka michache kuliko wakijenga wachina na pesa zao?

Hakuna aina nyingine za kodi na mapato yasiyo ya moja kwa moja yatakayotokana na bandari kama ajira(PAYE), indirect tax? Witholding tax etc?

Ikitokea Kenya wakachukua huo mradi bandari ya dar itakuwa salama?
 
Back
Top Bottom