Msigwa: Rais Samia hakukodi ndege ya Emirates wakati wa safari yake ya kwenda na kurudi Ufaransa na Ubelgiji

Kwanini akipanda ndege huwa hakuna ulinzi wa msafara wake kama ilivyo barabarani au angani hakuna maadui adui zake ni sisi walalahoi ambao hatuwezi kupanda ndege?
Acha kulalamika,kila kitu unalalamika,unajipa presha na maradhi bure,kuwa na furaha na kutabasam ni dawa pia.
 
Acha kulalamika kila kitu,kuwa na furaha,utajitia presha na maradhi bure.Kuwa na furaha na kutabasamu ni kinga na tiba ya maradhi.
 
Mambo mengine ni kutaka kuibua hisia za chokochoko

Msigwa alikuwa na sababu gani ya kuliongelea kama sio tu kuchomekea Kuwa watu Hojini hili?
 
Urais unae utamu au nasema uongo ndugu zangu?

Na mimi naomba Eeeh Mungu nisaidie niwe rais

Mbona ni raha jamani

Day first nimetoboa mawingu angani kwenye Airbus 380 Etihad 14 hours mawinguni business class nilimuelewa sana enzi hizo JK aka Vasco Dagama kwanini alikua anapenda kupumulia mawinguni full time
 
Ni vigumu kuwa na jibu moja kwani inategemea sana kama alisafiri peke yake akiwa abiria wa kawaida wa business class au aliongozana na entrouge kubwa ya wasaidizi ambayo yote ililipiwa business class. Kama alikuwa na watu kumi tu huko business class ambao walipangiwa kutokuwa na delay yoyote kwenye connection flights, tayari ni nafuu kwenda na gulfstream ambayo Kikwete alikuwa akisepa nayo kila kona ya dunia kuliko kutumia commercial airlines.

hakuna sababu ya kulinganisha na ATCL wakati kuna ndege ya rais ya masafa marefu kuliko hizo za ATCL. Ile Gulfstream ya rais inaweza kupiga non-stop kutoka Dar hadi uwanja wowote wa kimataifa duniani.
 

Jet Gulf Stream 50 Ipo Inazurura Tu Dar Es Salaam ~Dodoma

Sijui Kwanini Haitumiki Kwa Safari Maalum Za Kiongozi

 
Kuwajibu washinikizaji na vichaa ni kupoteza muda wako. Tunalalamika ATC pamoja na kujaza abiria kwenda ughaibuni bado linaendeshwa kwa hasara. Leo kuna vichaa wanata Rais atume dege hilo hilo kusafiri na watu 50 kwenda Ufaransa na Ubelgiji!! Utadhani wakiwa huko wangekuwa wanalala na kula ndani ya hilo dege😂😂
 
Reactions: Tui
Jamani Kuna Mdude huko Chadema amekuwa kinyonga. ati sasa anadai hata kama hajakosi Rais angetumia ndege ya Rais au Business Class ya ATCL badala ya Emirate. Wenzangu mumewahi kusikia ATCL ina route za Ulaya? Mbali na gharama za huduma na nishati kwa ndege ya Rais sijui accomodation ingalikuwa humohumo kwenye ndege ya Rais? Hii Mingwee wanayokula inawaletea shida.
 
Kwa hiyo safari ya rais Samia imetumia gharama kiasi gani kusafiri na ndege ya abiria na kuokoa kiasi gani?

Msigwa acha blah blah, njoo na facts&figures.
 
Tunakopa fedha nyingi sana lakini matumizi yake hayatutoi kwenye lindi la umaskini.

Na ndio wazungu wanavyotaka tufanye.
 
Tunakopa fedha nyingi sana lakini matumizi yake hayatutoi kwenye lindi la umaskini.

Na ndio wazungu wanavyotaka tufanye.
Wa kukutoa kwenye lindi la umaskini ni ubunifu wetu wenyewe, na kujituma. Msaada au mikopo ni nyongeza tu ya kujaribu kutukwamua tulipokwama.

Ni sawa na gari lililokwama kwenye matope linavyosaidiwa na jingine. Likishatoka jukumu la kufika liendako ni la mwenye gari mwenyewe.
 
Kumbe issue ni budget na siyo matumizi na kubana ajili ya wananchi? shame on you
Hivi kweli unaelewa haya mambo au basi muhimu unapinga tu? Pesa inabanwa wakati unapanga budget huko bungeni wanaweza kukataa sio unaomba Mia unapewa halafu mwisho wa mwaka umetumia 20 kawaida hupewi tena 100 ukiomba na pesa usipotumia kwa ilichopanga haina maana inapekwa kufanya matumizi mingine nje ya budget. Budget ya maendeleo inapangwa msiwe basi kila kitu kupinga tu.
 
Kwa hiyo kwenye bajeti ukiweka na hela za kupiga siyo issu?? Kisa ya kupigwa imo kwenye bajeti?
Nchi hii tunashida pesa ya kupiga ipi? kupanda ndege? Hivi ukimpa mkeo alfu 20 ya chakula ukarudi ukakuta chakula mezani hapo katumia 15 tu 5 kafanya matumizi mingine utasema kapiga? pesa ya budget kama mfano ofisi ya Raisi wanapeleka bungeni kuomba kiasi fulani na kuna kuwa na details ya gharama zote ikipita ni juu ya ofisi ya Rais kutumia kwa mujibu wa maombi yao kama iliombwa 100 kwa ajili ya usafiri basi watumie 0-100 kwa usafiri tu wala hawezi kwenda kuchukuwa ya chakula kutumia kwa usafiri. Ndio maana auditor kazi yake kupitia mahesabu je ulitumia 100 kuna invoice zililipwa kwa ajili ya usafiri au invoice hakuna na pesa hakuna hapo ndio wanauliza hii pesa imeenda wapi sasa hicho cha juu ni kipi. labda Mama kapanda Emirates na kuomba cha juu Emirates. acheni siasa katika professional job.
 
Peleka ujinga wako
 
Umenena vyema mkuu, maraisi wote husafiri na ndege zao binafsi, zile zipo special kwa shughuli hizo,ni za masafa marefu,na hutumia muda mfupi angani,kwa mfano kutoka belgium au ufaransa c zaidi ya saa 6-7 ila ukipanda commercial inabidi utumie muda mrefu mpaka Dubai ubadilishe ndege uanze kuja, naona gharama ndio zinazidi, kuliko ndege binafsi ambayo inafly destination to destination. na ni special jet kwake,na usalama ni mkubwa zaidi, kwani hata calibrated altitute ni kubwa kuliko commercial
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…