tatizo lenu watanzania mnapenda sana kuwabana watu, haya mambo ya uzoefu sijui wa muda gani ndo yanayotunyima kazi vijana wa sasa. Mimi nimepata digrii yangu ya political Science pale Mlimani nimeingia uraini muda si mrefu mnaanza fitna za uzoefu!!! Wewe cha msingi angalia mikakati yangu kama inafanya kazi lete ulaji sio kutoa kauli zakubaniana namna hiyo. Mimi hiyo kazi naiweza na nakuhakikishia ndugu yangu Mbu ukitaka unaingia bungeni bila wasiwasi. Nipe kazi Mkuru
........in a nutshell, nili/nimewekeza sehemu tatu.
1. Long term; kilimo (mashamba)
-changamoto hapa ni hali ya hewa vs aina ya mazao.
- Faida niwezayo kukwambia ili niwape changamoto wengine ni; ardhi nilipo invest ishapanda thamani kwa 75%
2 . Midterm; Ufugaji kuku wa nyama.
-Faida, mzunguko wa pesa hapa ni monthly.
3. Short term; Usafiri Bajaj mbili tatu,
- Faida, mzunguko wa pesa hapa ni weekly.
BTW, hii thread ni ya muda mrefu kiasi, kiasi kwamba hata graph ya mafanikio imekuwa inapanda mwaka hadi mwaka.
Biashara ni discipline tu, kama muuza njugu anaiweza, why wewe na mimi tusiwe na ustahmilivu wa kutotumia mpaka ule na mtaji?
Hii thread ukiisoma tangu mwanzo, utafaidika sana na ma nguli wa biashara mbali mbali kuliko hata hizi nilizojiamulia mie Mbu
kwani akijenga nyumba akapangisha hiyo sio biashara??????????/
Mkuu una mawazo mazuri sana kwa kutafuta uushauri wa kibiashara ila Mimi nakushauri yafuatayo chagua moja.
1.Tafuta washauri wa biashara ambao siku hizi wako wengi.
2.Jichunguze we we una kipaji au uwezo gani halafu anzia hapo.Fundi,Mkulima,Mwandishi n.k
3.Jaribu biashara yenye mtaji mdogo halafu uone matokeo take ndio utapata picha ya biashara kubwa itakuwaje.Usione aibu hata nyanya toka kariakoo kauze mtaani kwenu uone,au SAMAKI toka ferry uza uone.Usisahau anza na mtaji mdogo mfano 120,000
Hawa vijana ni pasua kichwa. Hawatakaaa kamwe wakuletee pesa yote. Wana a lot of excuses. Nakumbuka kwenye boda boda tano nililetewa siku mbili tu jumla ya 250,000 kwa week baada ya hapo zote zilikua majanga. Baada ya mwezi moja ikaibwa, insurance wakagoma kunilipa. Miezi mitatu baadae boda moja tena ikapata ajali Tabata- Matumbi. Dogo akakimbia boda ikakaa polisi miezi sita. Wakati huo huo hawa wengine wanazingua balaaa mara alete pesa mara asilete mara hivi mara vile iliishia kuniletea stress tupu. Kwa ufupi hivyo ndivyo nilivyopoteza 8.5 investment. Nakushauri usifanye maana hata huo uzima wa pikipiki ni mdogo sana na mizigo na suluba wanazozifanyia hizo pikipiki hao vijana waweza kuua mtu. Usifike huko
utajenga kwa muilioni kumi?
Wadau mimi ni Mwajiriwa,
Katika mambo ya urithi leo hii nimepewa mgao wangu wa 10mil cash. Nimeweka kwenye Account yangu nafikiria kitu cha kuifanyia.
Kwa nyie wazoefu, nipeni ushauri kibiashara ila mkizingatia mie ni mwajiriwa.
Nitashukuru kwa kila wazo chanya
Mkuu pesa ya urith haifanyiwi biashara....ujui mzee kapataje..nenda tafuta kiwanja jenga then pangisha itakusaidia maisha yako yoote
simshauri hapo kwenye bold atapoteza pesa yake.
hapa atahitajika kununua eneo pia?akinunua hela hiy haitatosha nazan
Mkuu pesa ya urith haifanyiwi biashara....ujui mzee kapataje..nenda tafuta kiwanja jenga then pangisha itakusaidia maisha yako yoote
vipi umepata kitu hapa e?
mimi nimeboleshwa kwa wazo nililo kua nalo kwa kuwa nitaanza mwezi wa tisa mwanzoni walio nishauri kukopesha sitafanya hivyo, bari hela nitaitunza tu hadi shamba liwe wazi nianze uwekezaji, pia nafikiria kufuata viazi mviringo tarime na kuleta hapa na mwanza angalau kwa kujaribu nianze na gunia tano ili nione soko likoje nipelekako