Mtaji wa Milioni 5-10 (TZS): Biashara gani unaweza kufanya?

Mtaji wa Milioni 5-10 (TZS): Biashara gani unaweza kufanya?

Msanii/mbu

Kama mnamaanisha ktk biashara hii ya miti,nipe e mail address zenu halafu tuone tutafanya nini.Sitaki hela ya mtu.Mimi nilishituliwa na mshikaji bure na mimi nitakusaidia bure. Michanganuo yenu mtafanya baadae mkipenda. Mimi sikufanya hiyo michanganuo.

Mkuu Malila kwa nini hilo unalotaka kulieleza usiliweke hapa, lakini kama inahitajika email nami nitakutwangia ya kwangu nifaidike.
 
Mkuu Malila kwa nini hilo unalotaka kulieleza usiliweke hapa, lakini kama inahitajika email nami nitakutwangia ya kwangu nifaidike.

Well said mkuu, Malila weka hiyo mambo hapa bana! if u insist email na mi takumwagia yangu!
 
Kwa ufupi nimekuwa ktk sector hii ya miti kwa muda mrefu sana. Naomba mchague wenyewe eneo mnalotaka nishushe data kati zifuatazo;

1; Ardhi ya bei poa iko wapi? na taabu za huko
2; mbegu zinapatikana wapi? na namna ya kuotesha?
3; Aina ya mti(mbegu,growth rate,soko,na sehemu ya kupanda ktk Tz)
4; Msimu mzuri na maandalizi yake.
5; overhead cost baada ya kupanda.
6; Field management.

Leo niwape item ya tatu tu,mimi nimeajiriwa,najaribu kutumia muda wa mwajiri kwa uangalifu.
Kuna miti mingi ila kwa sisi mizuri ni hii; mitiki(10, nje),milingoti boriti(8),milingoti nguzo (10), milingoti mbao (15),mikrismas(cyprus mbao) (25),
pines (12),ktk mabano ni miaka toka kupanda mpaka kuvuna. Soko la mitiki liko nje ya nchi,locally hakuna commercial market mpaka Kilombero wakijenga kiwanda mwakani. Mbegu zinapatikana kwa wakala wa serikali Morogoro,Iringa,Arusha,Tanga etc. Mbegu za mitiki ni ngarambe kuotesha, kilo moja ni Tsh 6000/ na ukifuata utaalam unapata miche 1000 hivi,lakini wajanja wanafanya kienyeji na wanapata zaidi au wanatumia suckers fulani hivi. Bei ya mche kwa sasa ni Tsh 500/ ya chini na 2000/ ya juu pale dar.

Pine/cyprus kilo moja ni Tsh 18,500/ na unapata miche 30,000 mpaka 35,000 inatosha eka hamsini ya miti ya mbao. Mlingoti kilo moja ni Tsh 22,500/ na unapata miche 120,000. Unapanda boriti eka 100 na unapanda miti ya mbao eka 200.

Utamu uko ktk boriti. Eka moja ni boriti 1200,bei ya boriti moja kwa leo hii ni Tsh 15,000/shambani.kwa hiyo eka moja iliyogharimu Tsh 70,000/ kununua ardhi mpaka kupanda itakupa 1200 x 15,000/=( ) toa gharama za fire break mara moja kwa mwaka. Hakuna kupalilia wala kumwagilia.

Mitiki peke yake inakubali pwani,mingine yote ni ktk nchi za baridi. Nimetoa kwa ufupi sana, ila tutaendelea kuelezana kidogo kidogo, item nyingine kesho.
 
Kwa ufupi nimekuwa ktk sector hii ya miti kwa muda mrefu sana. Naomba mchague wenyewe eneo mnalotaka nishushe data kati zifuatazo;

1; Ardhi ya bei poa iko wapi? na taabu za huko
2; mbegu zinapatikana wapi? na namna ya kuotesha?
3; Aina ya mti(mbegu,growth rate,soko,na sehemu ya kupanda ktk Tz)
4; Msimu mzuri na maandalizi yake.
5; overhead cost baada ya kupanda.
6; Field management.

Tafadhali Mkuu malila usije ingia huko msituni, kabla ya kumaliza lecture hapa! We need this mkuu! Hasa hapo kwenye field management......!

Nilikuwa na kamsitu huko IR ka pines zote ziliungua, so was very discouraged hata sijarudia kupanda tena miti!
 
Mimi ni mfugaji, nitakushauri kufuga ngombe kwa mchakato ufuatao:

Kumbuka ng'ombe huzaa kila mwaka hivyo basi baada ya miaka mitano utakuwa na ng'ombe wasiopungua 25. Kipato chako kwa mwezi unaweza kufikia si pungufu Tsh 18,000,000 endapo utakuwa na ngombe jike 20 kati ya hao 25.

...stanmokiwa, mchakato wako kwa kweli umenivutia. Naomba kuuliza swali la nyongeza. Ni lazima kununua hao ng'ombe walio na miezi sita? Upatikanaje wake ni vipi,..maana kama kila mfugaji atataka ng'ombe aliye na mimba ya miezi sita demand itazidi supply, ama ushauri huo ulilenga kwangu kwakuwa naanza?

Pili, vipi kuhusu aina ya ng'ombe na upatikanaji wake? ni ng'ombe yeyote wa kienyeji naweza kununua, au ndio wale wa 'kidhungu' kina;

View attachment 4493 Ayshire,View attachment 4494 Brown Swiss
View attachment 4495 Guernsey,View attachment 4496 Holstein-Friersien,View attachment 4497 Jersey?

maana nishasikia majina kama 'chotara' nk...

nawakilisha!
 
Tafadhali Mkuu malila usije ingia huko msituni, kabla ya kumaliza lecture hapa! We need this mkuu! Hasa hapo kwenye field management......!

Nilikuwa na kamsitu huko IR ka pines zote ziliungua, so was very discouraged hata sijarudia kupanda tena miti!

Field management,

Zamani tulichukulia shughuli hizi za misitu kiurahisi sana,majanga yanapotokea hasa moto hakuna mwenye uchungu. Unatakiwa kuwa na mtu ambaye anakuwa sehemu ya msitu wako kabisa, hilo limenisaidia mimi mara mbili. Ni lazima kijana/mtu wako ahisi na yeye anafaidika na mradi ule. Badala ya kuwapa fedha cash mimi nawalipa bati za kuezekea,kwa hiyo hata kama ni mzembe akiona bati anakumbuka msitu. Njia hii inafanya familia nzima inawajibika kutunza msitu.Wenyewe wanasema win win situation.

Njia ya pili ni kuanzisha msitu mkiwa wengi kama estate vile,ili firebreak iwe kubwa sana.Hapa mimi nimefanikiwa sana kwa sababu niko na vijana kama 24 hivi na wote tunapanda miti kwa pamoja kwa kugawana eneo moja. Tunaokoa gharama sana kwa kuchangiana,kiasi kwamba kila mmoja anaona raha. Kila mwezi kuna mtu anakwenda kuwatembelea shamba kuwajulia hali zao vijana wetu.
 
tatizo lenu watanzania mnapenda sana kuwabana watu, haya mambo ya uzoefu sijui wa muda gani ndo yanayotunyima kazi vijana wa sasa. Mimi nimepata digrii yangu ya political Science pale Mlimani nimeingia uraini muda si mrefu mnaanza fitna za uzoefu!!! Wewe cha msingi angalia mikakati yangu kama inafanya kazi lete ulaji sio kutoa kauli zakubaniana namna hiyo. Mimi hiyo kazi naiweza na nakuhakikishia ndugu yangu Mbu ukitaka unaingia bungeni bila wasiwasi. Nipe kazi Mkuru


Kumbe kweli wewe ni fiksman, unamdanganya mwenzako atumbukize pesa shimoni !! Kwani hivyo vimilioni 10 havitoshi hata mafuta ya gari ya kuzungukia wapiga kura za maoni!!! Haki ya Mungu Mbu usidanganyike, kuna jamaa yangu alipoteza 30 million kura za maoni na akakosa ubunge na nyumba aliuza hadi sasa amekufa na stroke!!!!!.
 
...stanmokiwa, mchakato wako kwa kweli umenivutia. Naomba kuuliza swali la nyongeza. Ni lazima kununua hao ng'ombe walio na miezi sita? Upatikanaje wake ni vipi,..maana kama kila mfugaji atataka ng'ombe aliye na mimba ya miezi sita demand itazidi supply, ama ushauri huo ulilenga kwangu kwakuwa naanza?

Pili, vipi kuhusu aina ya ng'ombe na upatikanaji wake? ni ng'ombe yeyote wa kienyeji naweza kununua, au ndio wale wa 'kidhungu' kina;

View attachment 4493 Ayshire,View attachment 4494 Brown Swiss
View attachment 4495 Guernsey,View attachment 4496 Holstein-Friersien,View attachment 4497 Jersey?

maana nishasikia majina kama 'chotara' nk...

nawakilisha!

MBU, nimefurahi kuona umekuwa na interest katika ufugaji. Nimeshauri ng'ombe awe na mimba ya miezi sita kwa kuwa ndiyo utakuwa unaanza, hivyo basi itakugharimu miezi 3 kuwalisha kabla ya kuanza production. Ng'omb hawa ni wale "pure" wanaozalishwa hapa nyumbani. Kuna uwezekano wa kutokupata 100% pure, ndiyo maana mchakato wangu nimewekea uzalishaji wa lita 5 asubuhi na 5 jioni, kwa siku lita 10 ambapo hiki ni kiwango cha chini kabisa kwani ng'ombe wengi sasa hivi wakipata matunzo vizuri wanatoa kuanzia lita 8 mpaka lita 15 (asubuhi/jioni) kwa siku lita 16 - 30.

Ngombe hawa wanapatikana katika vituo vya kuzalisha ng'ombe (mitamba) kama pale RUVU, MPWAPWA, IRINGA, MBEYA n.k. kwa bei ya kati 600,00 - 700,000. Lakini katika mchakato wangu nimewekea bei ya wafanyabiashara ambao hukusanya mitamba kutoka kwa wafugaji au vituo vya kuzalisha mitamba huko mikoani na kuwaleta Dar es salaam.

Aina ya ng'ombe ni kati ya hizo ulizoeleza, lakini binafsi nawapenda Holstein - Friersian. Hawa kwa swala la volume ya maziwa sina wasiwasi nao, kadiri utakavyomlisha vizuri atakupa matokea mazuri. Kwangu ng'ombe anayekamuliwa ni "MALKIA".
 
Kama ni ng`ombe, chukua waliozaliwa pwani hii hii, wale wa kutoka mikoani siku za mwanzo wanahitaji uangalifu sana mkuu. Nenda Ruvu mzee.
 
Field management,

Zamani tulichukulia shughuli hizi za misitu kiurahisi sana,majanga yanapotokea hasa moto hakuna mwenye uchungu. Unatakiwa kuwa na mtu ambaye anakuwa sehemu ya msitu wako kabisa, hilo limenisaidia mimi mara mbili. Ni lazima kijana/mtu wako ahisi na yeye anafaidika na mradi ule. Badala ya kuwapa fedha cash mimi nawalipa bati za kuezekea,kwa hiyo hata kama ni mzembe akiona bati anakumbuka msitu. Njia hii inafanya familia nzima inawajibika kutunza msitu.Wenyewe wanasema win win situation.

Njia ya pili ni kuanzisha msitu mkiwa wengi kama estate vile,ili firebreak iwe kubwa sana.Hapa mimi nimefanikiwa sana kwa sababu niko na vijana kama 24 hivi na wote tunapanda miti kwa pamoja kwa kugawana eneo moja. Tunaokoa gharama sana kwa kuchangiana,kiasi kwamba kila mmoja anaona raha. Kila mwezi kuna mtu anakwenda kuwatembelea shamba kuwajulia hali zao vijana wetu.

Mkuu malizia zote basi!
 
wajameni eeh, nimebahatika "kupata" mahala ka-Mtaji. Ni kiasi cha shs. milioni kumi tu, (10,000,000/=) za Kitanzania.

Nipeni mapendekezo nizi invest wapi, kivipi na matarajio ya faida.
(i.e biashara gani inalipa (plus location), kwa muda gani, na SWOT analysis zake)


Nunua kiwanja na ujenge au nyumba mbovu na ikarabati katika miji inayokua na iliyopa maeneo ya ya barabara kuu na wekeza gesti.

Inalipa sana. Assume umejenga gesti moja ya kiwango cha 4m,nauhakika itapata wateja wa uhakika na fedha yako itarudi baada ya muda mfupi.
Kwa miji midogo gesti ya 4m inaonekana ya 5star.
 
Kama ni ng`ombe, chukua waliozaliwa pwani hii hii, wale wa kutoka mikoani siku za mwanzo wanahitaji uangalifu sana mkuu. Nenda Ruvu mzee.

Ni kweli MALILA, inasemekana hivyo. Lakini kwa uzoefu niliopata, ng'ombe nilionao walitoka Arusha na mimi nikawanunua Dar siku ya pili walipofika na kuwasafiri hapa Zanzibar ninapoishi kwa sasa. Kwa kweli niliwaleta wakati wa joto na kiangazi kikali lakini hawakunisumbua kwa kiwango kikubwa, ijapokuwa ndiyo nilikuwa naanza ufugaji hapa Zanzibar.
 
"Tatizo la hili ni kuwa Tshs. 10m sidhani kama inatosha kuanzisha biashara yoyote bongo ambayo revenue yake inaweza kukamatika ( as in you can feel it). "Halafu mabenki ya mikopo yanatoa 50elfu kwa miaka 3. Hao ndipo DECI walipopataia Idea.
Ndugu yangu ni PM, biashara ziko nyingi sana,huo mtaji ni mkubwa sana. Barclays walisaidia watu sana na wana jina kwa sababu ya kutoa hioz million kumi kumi.
Katabazi.
 
changanua mawazo yako uoanishe na juhudi zakooo....
 
Nunua kiwanja na ujenge au nyumba mbovu na ikarabati katika miji inayokua na iliyopa maeneo ya ya barabara kuu na wekeza gesti.

Inalipa sana. Assume umejenga gesti moja ya kiwango cha 4m,nauhakika itapata wateja wa uhakika na fedha yako itarudi baada ya muda mfupi.
Kwa miji midogo gesti ya 4m inaonekana ya 5star.

Ajenge guest house kwa Tsh. 4m? Hapa sijaelewa! Maana 4m ni hela ya kujenga vyumba viwili tu. Au unamaanisha ajenge mbavu za mbwa?
 
Nunua kiwanja na ujenge au nyumba mbovu na ikarabati katika miji inayokua na iliyopa maeneo ya ya barabara kuu na wekeza gesti.

Inalipa sana. Assume umejenga gesti moja ya kiwango cha 4m,nauhakika itapata wateja wa uhakika na fedha yako itarudi baada ya muda mfupi.
Kwa miji midogo gesti ya 4m inaonekana ya 5star.


Wapi huko mzee, na mimi nikajenge guest ya 4Mil ??? Tanzania hii hii??
 
Nunua kiwanja na ujenge au nyumba mbovu na ikarabati katika miji inayokua na iliyopa maeneo ya ya barabara kuu na wekeza gesti.

Inalipa sana. Assume umejenga gesti moja ya kiwango cha 4m,nauhakika itapata wateja wa uhakika na fedha yako itarudi baada ya muda mfupi.
Kwa miji midogo gesti ya 4m inaonekana ya 5star.


Naomba kuliboresha wazo hili kama ifuatavyo, guest house ya gharama hiyo siungi mkono,ila nenda maeneo ya karibu na Mkwawa university Iringa au maeneo karibu na Mzumbe University kajenge vyumba vinne/sita yaani chumba sebule kisha wape madenti kwa mwaka. kwa ulaini unakula kodi bila taabu.

Nawasilisha
 
Ndugu yangu ni PM, biashara ziko nyingi sana,huo mtaji ni mkubwa sana. Barclays walisaidia watu sana na wana jina kwa sababu ya kutoa hioz million kumi kumi.
Katabazi.

Mdugu Katabazi!

Ukiweza kuweka idea mbalimbali za hizo biashara hapa jamvini nitashukuru sana, wengine tunafuatilia pia na tunapenda kujaribu kujiingiza kwenye biashara tuongezee kipato.
Kama hutojali,natangulisha shukrani!!!
 
Wewe ndo ulichagua hii ya mwisho, ya field management,haya chagua tena nyingine nikupe.

Mkuu, 1 & 2.......!

Mzee natengeneza kibooklet for this, so kwenye 2 naomba zungumzia sana mitiki......na acquaire eneo huko Moro for this!

Kifanikiwa tacomeback to you!
 
Back
Top Bottom