Hii imekuingia!
Dogo Jifunze kutumia lugha nzuri unapowasiliana na wengine uwe unawafahamu au huwafahamu!
 
Covid19 ni janga mkuu,nakumbka italy ilianza na visa vi2 tu vya corona lakini kwa sasa ni shida,tuna watu Tz wanakinga dhaifu wakiupata ni shida.
 
Awamu ya kikwete alianza kuwekeza kwenye TEHAMA hasa kwa walimu kwenda kujifunza kwa njia ya semina na kwa shule kuletewa Kompyuta nyingi zaidi,,lengo lilikuwa kila shule lifundishe SOMO la kompyuta kwa kila mwanafunzi lakini baada ya awamu hii ya kizalendo kuingia program zote za mafunzo kwa walimu zikafyekwa hakuna tena,ndoto za kuanzisha somo la kompyuta kwa wanafunzi ili wasome halisikiki tena ni kama limekufa kabisa.
Watanzania tujiulize kwa umakini zaidi maana dunia ya sasa ni ya kiteknolojia kwa kila kitu sasa kama bado tunaishi katika kipindi cha giza wakati wenzetu wanaishi kipindi cha mwanga tusitegemee mabadiliko ya haraka hata siku moja.
 
kandamatope, Mimi nakuunga mkono kwa 100%
Na anayebisha hatakuwa na akili sawasawa. Kwajinsi Watanzania tulivyo careless sisi tungekuwa nchi ya kwanza kwa Maambukizi na vifo.

Hakuna hatua zile kali ambazo serikali zimechukua ni hatua za kawaida tu. Hii nchi kuna watu wanaomba sana. Na hilo kwanzia Mw.

JPM anafahamu na katu hawezi pinga watu wasiende misikitini na Makanisani kutokana akifanya hivyo kwa siku tunaweza anguka 1000.
Mimi naweza sema ni Mungu anatulinda na kama huamini nahisi hata kama ni profesa jua ww ni Mbumbumbu wa mwisho.

Unaishi kutokana na mgongo wa wanaomuomba Mungu
 
Naomba huu uzi usiufute, baada ya mwezi kuanzia leo turejee hizi PUMBA zako.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna na haitotokea na kama ikitokea itakuwa kwako.
Nyie msioamini ndo mnaturetea uchuro. Hivi unataka kuniambia Tz ni smart kuliko Marekani, Italy , S.A basi tusiende mbali hapo kenya wametuzidi Mbali mno unajua kwanini wanakufa , wamehisi Corona ni Mkubwa kuliko Mungu wakafunga Makanisa na Misikiti watu wakashindwa kumuomba Mung hapo tu
 
Watanzania tusilizike na matamko ya wanasiasa kwamba serikali inatoa elimu bure,,tujiulize je!elimu bure hii inayohubiliwa na hawa viongozi inamuandaa mtoto kuwa nani?kwa maarifa yepi? Inamfanya awe mshindani duniani au Watchers ya kile kinachoendelea duniani? Watanzania wanasiasa sio rafiki zetu huuata kidogo hawapo kwa ajili ya shida zetu hebu angalia yanayoendelea toka awamu hii ilipoingia madarakani muda wote wanahangaikia uchaguzi ujao,akina polepole wanabema maburungutu ya fedha kwenda kulipa faini ya watuhumiwa wa mauaji yakubumba wakati wanafunzi hawana vitabu,hawana madawati,shule hazina maabara za kutosha,walimu wanadai madeni lukuki na wanajibiwa serikali haina fedha jifikirie mtoto wako masikini atafundishwa ipasavyo na mwalimu mwenye kinyongo? Rudi kwenye miundombinu ya shule kuna baadhi ya shule ni magofu hayatamaniki hata kidogo,madarasa yamechakaa haswa lakini watu wanabeba pesa kwenda kulipia faini za kijinga kabisa huku wakiacha mambo ya msingi yakijiendesha bila kusimamiwa ipasavyo. Tanzania nchi yangu
 
sidhani kuna mzazi atafurahia kurudisha shule wanae sasa, it is too soon!! at least tuone kwanza data zetu for a month more, na hasa hawa wagonjwa wanaotibiwa sasa wakipona itakuwa safi sana. turudi zero with extremely tight entry to Tanzania, mimi bado siamini sana kama tumedhibiti ipasavyo uingiaji wa waleta Coronavirus mipakani na Airport hadi nisikie JWTZ wamechukua kazi hiyo, but wenyewe wakiamua shule zifunguliwe tutawapeleka shingo upande!
 
Black kule wanatelekezwa hawapatiwi tiba sahihi ndiyo maana wanakufa wengi kuliko weupe!
Yaani hata manyeusi wenzao hawawatibu? Kuwa serious mkuu.Nina jamaa yangu pale Minneapolis Minnesota ni daktari na juzi juzi alikuwa ananiambia anataka aende The Empire state kuchukua zile dollsr 10,000 kwa wiki zilizotangazwa na meya wa Empire state
 
Bado mfumo wa elimu THEORY ORIENTED hausaidii sana
 
Watoe taarifa mapema ili wazazi waanze kuandaa na wengine kukopa nauli
 
Taifa kutofundisha wanafunzi, walimu, manesi, madaktari, maengineer, madereva, walinzi kwa Mwaka mzima Ni janga.nashauri shule Na vyuo vifunguliwe Mara moja.maeneo ya shule Na taasisi za elimu huduma za Afya ziboreshwe.nje ya hapo tunaenda kuangamiza taifa.
 
Jamaa umeandika mada bilayakufikiria kabsa
Kwanza swala la smartphone/computer si kila mwanafunzi wa chuo anayo na hivi vitu vinaenda sambamba unaweza kutumia smartphn peke yake ila kwa computer lazma uwe na router au simu kwaajili ya tathering hotspot so iko hivo
Pili hata hao wenye smartphone hali ni ngumu sasa kwa wanafunzi wengi unakuta hata mb ni shida mtu kuwa online kwa week ni mara moja pesa ya bando hamna sasa kwa hali hiyo mtu atasomaje online
Tatu mitandao yetu haiko reliable hasa vijijini huko hii ni changamoto
Mm ni mwanafunzi pia so nazungumzia nayoyaona

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Wewe inaonekana unekulia mjini na kila kitu unakichukulia poa sana,kuna maeneo simu kushika hadi upande juu ya mti,harafu wewe unarahisisha tu,ajira yangu ya kwanza ilikuwa ni Lindi liwale ,amini kunasehemu ili uwasiliane na ndugu zako hadi mtu asubiri mwisho wa mwezi anapokuja kuchukua mshara,baada ya hapo hadi next month,na hadi naandika hivi bado maeneo hayo hayana network,sasa wewe unapojenerolaizi sijui unamaanisha nini

Pili kuna maeneo yana mtandao rakini hauruhusu INTERNET na wala hata kusoma E nu shida sasa hawa unawasaidiaje?

Tatu simu ,unapokuwa na simu wewe usidhani kila mwanachuo ana smartphone,kuna wafanya kazi wako ajirani for 20+ years hawazijui smartphone ,sasa hao unawasidiaje?

Sidhani kama kuna sehemu hakuna network, HALOTEL ndo mpango mzima hadi huko nanjilinji. Kuhusu simu, wananzo kama hana smart, sidhani kama kuna kijiji hakina mtu mwenye smart, watz ni wazalendo tunaazimana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hivi hata mitandao ya kufundishia tunayo?

hizo mb za kuunga unga za makampuni ya simu utaweza kuona lecture ya saa nzima?

Hatuna miundombinu ya kufanya hayo. Sisi mitandao yetu ni ya kutongozana na kuandika siasa na Clips ndogo ndogo za dakika tano.

kufundisha online kunahitaji internet ya nguvu. TTCL wameshindwa kazi ya kujenga mtandao wenye tija kwa wananchi wote.

 
Sisi tunaweza siasa za kukomoana tu basi mengine sio kipaumbele chetu kabisa,,kuendesha nchi unahitaji mikakati thabiti sio longolongo za akina Polepole and the like
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…