#COVID19 Mtazamo, Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Serikali na Wananchi kuhusu Ugonjwa wa Corona - COVID-19
balimar, Italy hakuna Yesu? Au hawajui kukemea? Walitembeza hadi sanam la bikira Maria liweke baraka na bado halikufua dafu, hapa kwetu wakemeaji maarufu wote kimya, wametuaminisha wanafufua wafu na kuombea wagonjwa hilo la Corona simsikii hata mmoja akisema atakwenda mloganzila akawaombee wagonjwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Italy hakuna Yesu? Au hawajui kukemea? Walitembeza hadi sanam la bikira Maria liweke baraka na bado halikufua dafu, hapa kwetu wakemeaji maarufu wote kimya, wametuaminisha wanafufua wafu na kuombea wagonjwa hilo la Corona simsikii hata mmoja akisema atakwenda mloganzila akawaombee wagonjwa

Sent using Jamii Forums mobile app
Gwajima aliulizwa juzi na baby kabaya clouds pale
Alimwambia umeshawahi mleta mgonjwa wa Corona kuombewa ikashindikana kupona?
Mbebe mmoja mpeleke pale akaombewe uone
 
Wakuu tunatishana sana
Kaugonjwa haka ni kadogo sana tunakakemea kwa Jina la Yesu Kristo kanapotelea huko
Tena haka ni kakukakemea kwa Jila la Yesu
Yaani hapa ndio ulimwengu unahitaji Yesu Kristo alie hai
Karibuni kwa Yesu nafasi bado zipo huku bhana kuishi ni faida kufa ni Kristo
Aisee umenena. Yaani huku raha tupu. kuishi kufa kwetu ni Kristo tu. Msiogope wala msifadhaike Bwana Yesu ataponya nchi yetu. Amina
 
Mungu ametupa akili tuzitumie na akili zenyewe ndio hizi; vaa mask, safisha mikono kutumia sanitizers kwa maji yanayotiririka n.k.

Kusema tumuombe Mungu tena wakati ameshatupa maarifa ya kujikinga na ugonjwa tunamchosha kwa uzito wa akili zetu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aisee umenena. Yaani huku raha tupu. kuishi kufa kwetu ni Kristo tu. Msiogope wala msifadhaike Bwana Yesu ataponya nchi yetu. Amina
Haya ni mambo ya Imani sio inshu za Dini
Kiukweli mtu ukiwa na Imani huwezi kuogopa haka kaupepo Corona
Hatusemi hatuchukui tahadhari 'but it is not a big deal'
Sasa ugonjwa wenyewe kumbe ni airborne unategemea nini?
Bwana Yesu yupo upande wetu twendeni mbele na Rais wetu
 
Why mnaogopa kufa? usipokufa kwa korona utakufa kwa ajali. Tuendelee kupiga kazi ili tupate cha kuwalisha watoto wetu. Haka ni kaugonjwa ka shetani tu.
 
Kwani ukiamua kujifungia ndani na familia yako, serikali unahisi itakukataza?
Wanakera sana wapuuzi hawa, serikali ishakuambia chukua tahadhari sasa ukisubiri Rais aje akulinde wewe na familia yako utasubiri sana.
IMG_20200411_163847.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Why mnaogopa kufa? usipokufa kwa korona utakufa kwa ajali. Tuendelee kupiga kazi ili tupate cha kuwalisha watoto wetu. Haka ni kaugonjwa ka shetani tu.
Hii lugha yenu ya "kuchapa kazi" kama siipendi. Nani anamkumbusha mtu juu ya kulisha watu wake ?!. Kazi tunazifanya hata bila kauli hizi za viongozi .

Corona ni hatari ni bora serikali na watu wakajiandaa na dhoruba hii bila kuleta siasa

Odhis *
 
Odhiambo cairo,
Brother, kuna viongozi hawajielewi kabisa. Hawapo kwa ajili ya watu bali kwa matumbo yao na familia zao tu.

Tunaohangaika ni sisi wenye kipato cha chini. sambamba na hayo huu ugonjwa wa COVID19 umeumbua baadhi ya nchi za Afrika kwa sababu ya kutokuzingatia vitu vya muhimu na vya msingi mfano afya za watu.
 
Wakuu tunatishana sana
Kaugonjwa haka ni kadogo sana tunakakemea kwa Jina la Yesu Kristo kanapotelea huko
Tena haka ni kakukakemea kwa Jila la Yesu
Yaani hapa ndio ulimwengu unahitaji Yesu Kristo alie hai
Karibuni kwa Yesu nafasi bado zipo huku bhana kuishi ni faida kufa ni Kristo
Naona mmeanza
 
Mbona hotuba za tahadhari zinatolewa kila kukicha. Unataka uchapwe viboko na Rais ndio uende kama punda?
 
Back
Top Bottom