#COVID19 Mtazamo, Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Serikali na Wananchi kuhusu Ugonjwa wa Corona - COVID-19
Tangu Corona iingie Tanzania imeau watu watatu tu na wagonjwa wapo 94 kwa Mujibu wa Bi. Ummy.
Juzi ajali imetokea Mkuranga, ajali ya Coaster wamekufa watu 20 na zaidi., sasa ajali moja inaondoa watu wengi kuliko wa Corona.

Daladala za Dar es salaam ambazo nying ni Eicher, Toyota Coaster na Rosa na Nissan Civilian,huwa na beba watu 28-Coaster na 26 -Civilian,lakini kwakuwa watu wa Dar ewapo vululu na viongozi yaani LART hawajali basi huwa wanatoa viti vyote vya katikati na kubaki ukumbi ambao watu husimama wengi kuliko waliokaa.

Baada ya Corona na watu kuambiwa wakae MSAMBWANDA/ LEVEL SEAT basi daladala wamerudisha hizo seat /viti lakini wameweka vigoda vya mbao ambapo mkaaji yaani abiria hana balance, hana pa kuegamia, na gari ikishika breki huwa wanaanguka, hii ni hatari na sheria hairuhusu lakini Makamanda wa polisis wamelala usingizi wa pono, mpaka ajali itokee, watu wafe ndio utaskia tamko linatoka.

IGP una watendaji vilaza na wasio penda kazi zao, wanasubiri watu wafe, narudia wanasubiri vifo maana gari ikipiga breki mtu anatoka na kioo cha mbele
 
Toka huo utaratibu umeanza, ni wangapi wamepata madhara?

Hivi kwa spidi za daladala hapa mjini ambazo sidhani kama hata 60km/hr wanafika, break inaweza kukutisha kweli?
Huo umepewa ni mfano, hivyo ongeza ya kwako. Sio break tu, bali hata kupewa pande na kuishia mtaroni.
 
Mabasi ya mikoani yanayokuja na kutoka,huoni kama ni hatari kusambaza.........??? Kwakifupi bado hatujachukua hatua yoyote zaidi ya maombi
 
Toka huo utaratibu umeanza, ni wangapi wamepata madhara?

Hivi kwa spidi za daladala hapa mjini ambazo sidhani kama hata 60km/hr wanafika, break inaweza kukutisha kweli?
Umewahi kujikwaa ukaanguka na kuvunjika mguu? ulikuwa spidi ngapi?
Nahisi utapia mlo upo sehemu nyingi za Tanzania.
Kwanini dereva akamatwe hajafunga mkanda kwakuwa ajali ikitokea ataumia ila abiria amekaa kwenye kigoda amabacho hakijashikizwa sehemu yeyote asilindwe?
 
Mabasi ya mikoani yanayokuja na kutoka,huoni kama ni hatari kusambaza.........??? Kwakifupi bado hatujachukua hatua yoyote zaidi ya maombi
Maombi bila hatua ni bure, na wanao tangaza maombi watubu otherwise ni kelele mbele za Mungu# Free Tito , bring back Saa nane
 
Umewahi kujikwaa ukaanguka na kuvunjika mguu? ulikuwa spidi ngapi?
Nahisi utapia mlo upo sehemu nyingi za Tanzania.
Kwanini dereva akamatwe hajafunga mkanda kwakuwa ajali ikitokea ataumia ila abiria amekaa kwenye kigoda amabacho hakijashikizwa sehemu yeyote asilindwe?

Mkuu nakubaliana na observations zako kwamba inaweza kutokea.

Swali langu ni, toka huo utaratibu umeanza, imeshatokea?
 
Unapotoa ushauri,, toa na way forward nini kifanyike..
 
Hatima yako haiwezi kuamuliwa na serikali katika kipindi hiki.
Tujifunze kutotoa lawama maana hazitosaidia angali unajua madhaifu ya sereikali yako!
Maisha yako! Familia yako! Uchumi wako! Ww ndo wakuamua au uamuliwe na mwingine abaki kutoa lawama!
Xre! Sijajua ww kama ni mwanasiasa maana ndo zenu kuchafuana!
Mm huko siku mkuu
Mkuu, Serikali lazima ilaumiwe maana inanafasi yake ktk haya mapambano, kwa upande wangu napambana vizuri, Sera, mwongozo na mikakati ya serikali Ni muhimu

House girl(dada wa kazi) Ni binadamu aheshimiwe, apumzike, apewe Uhuru wa kuabudu pia
 
Salamu kwenu wanaJF

Hili janga la corona naona Serikali halichukulii kwa uzito unaostahili kwa sababu zifuatazo

Kushindwa kutoa vifaa muhimu Kama Mask, gloves, vipima joto n.k katika taasisi zake mbalimbali.

Hospitali nyingi na vituo vya afya vingi Sana havina hivi vifaa kwa Wafanyakazi wake achilia

Kushindwa kusimamia swala la mikusanyiko isiyokuwa ya lazima. Ukitembea sehemu nyingi Sana utaona bado vijiwe vingi vya kahawa, mabanda ya video bado watu wanajaa bila tahadhali yoyote na Serikali IPO tu, Serikali ya mtaa/ Kijiji au wilaya!!

Mfano wilaya ya Mkuranga Hali Ni mbaya Sana watu wanajaa kwenye vijiwe vya kahawa huku wakiangalia TV na mabanda ya video bado yanajaza watu tu, hii inaonyesha Serikali haiko makini ktk kukabiliana la corona

Misaada imetolewa na makampuni/ watu binafsi kuhusu kusaidia vifaa mbalimbali vya kujikinga na corona lakini mpaka Leo Hakuna tofauti yoyote mtaani kuonyesha misaada hiyo imesaidia jamii mfano mask bado Bei kubwa 2000/= , sabuni Bei juu, sanitizer bado gharama kubwa hii inatoa picha mbaya kwa Serikali pesa za Rostam Aziz 1bilion, pesa za Mwenge n.k hazijaleta msaada kbs kwa watu,

Ushauri wangu kwa Serikali naomba waonyeshe Nia na juhudi ktk kupambana na corona mfano Jiji la Dsm ndo kitovu Cha maambukizi nchi , hapo ndo itasabsbisha mikoa mingine wapate huu ugonjwa, hivyo Serikali ningethibiti mwingiliano wa watu wa Dar na mikoa mingine, wazuie usafiri wa mikoani walau kwa wiki mbili tu,

Marufuku za mikusanyiko ifanyike kwa nguvu ikibidi patrol za polisi au mgambo ili watu waepukane na maambukizi yasiyo ya lazima!!

Mwisho naomba Watanzania wenzangu tujipende sisi na wenzetu pia tuchukue tahadhari Kabla ya hatari!!


House girl(dada wa kazi) Ni binadamu aheshimiwe, apumzike, apewe Uhuru wa kuabudu pia

Play your part. Sehemu kubwa tushauri Sisi. Serikali imetimiza wajibu Wake kiasi kikubwa. Tujilinde


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Anza kuchukua hatua wewe mwenyewe na wanaokuzunguka..ukisubiri serikali ifanye kitu mwisho wa siku utajikuta karantini na bado utaendelea kuilaumu serikali kwa yaliyokupata.
 
Kwa kweli huku mtaani kwangu mimi ni bora mtu ujiweke lockdown mwenyewe,nikitoka nje naona watu km hawajui lolote kuhusu Corona!

Yaani Inatisha,Sijui km wanajua kinachoendelea kila siku wanachojua wao ni kuweka vile vindoo vya maji na sabuni tuuu yaani wameyaweka mpaka kwenye mabanda umiza halafu wanajazana kuangalia muvi sijui mpira,Hatari sana.
 
Mtaani kwangu mm watu wanajitahidi kuchukua tahadhari kiukweli.. wafanya biashara wana vifaa vya kunawia mikono na wameweka nje watu wanawe kabla ya kuingia.. baadhi yao wanavaa mask pia.. lakini pia mtaani kwangu hakuna kitu kinachosababisha mikusanyiko ya watu


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mtaani kwangu hawana habari, wengi ukiwauliza kwanini hawachukui tahadhari nyingine muhimu mbali na kunawa tu wanajibu huu ugonjwa ni wa watu waliotoka nje ya nchi ama wenye ndugu waliotoka nje ya nchi 😟
 
Mtaa wangu kwa kweli naona watu wameelewa kiasi kikubwa mabanda ya video na vijiwe kwa sasa havina watu , ndoo na sabuni pia wameweka sijajua he wananawa Mara kwa Mara au ni pambo tu
 
Back
Top Bottom