#COVID19 Mtazamo, Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Serikali na Wananchi kuhusu Ugonjwa wa Corona - COVID-19
Nakumbuka msanii MwanaFA ni miongoni mwa watanzania wa mwanzo kabisa kujitangaza kuwa na maambukizi ya ugonjwa wa Covid 19. Na baadaye RC Makonda alithibitisha hilo pale stendi kuu ya mabasi ya mikoani Ubungo alipozungumza na wananchi kuhusu athari za Corona.

Kwa kuwa mwanaFA amepona kabisa ni vema wizara ya afya ikamtumia kama balozi wa kuelimisha jamii na kuitoa hofu kwa kuiaminisha kwamba Covid 19 inapona.

Aunganishwe na Mrisho Mpoto kwenye zoezi la kuelimisha Umma linaloendelea.

Ni hayo machache,

Maendeleo hayana vyama!
Mabalozi wote wameshaenda kwenye nchi zao atumike ili iweje

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nani mkweli sasa, wanaotuambia tuchape kazi tusiogope, au wanaotuambia tusiende kwenye mikusanyiko?! Wanaotuambia tushone Barakoa za khanga au wanaotuambia hazitusaidii chochote kutukinga kwa virus vya Corona? Nimeona Tweet ya Dr.Ndugulile akisema Mapua hayastahimili joto lakini Rais kasema tujifukizie dawa za asili?
Nimeona Dr.Mabula kateuliwa kuwa katibu mkuu, nilidhani Dr.Ndugulile kastaafu au kastaafishwa kumbe bado.
Kwa hiyo mapafu hayastahimili temperature flactuations, vipi mtu anaweza kuishi nchi yenye baridi kali kama urusi na mwengine kwenye joto kali kama arabuni, anaongelea mapafu kuungua au mapafu kushindwa kuhimili joto linaloingia kupitia upumuaji? hii korona imeibua wataalamu haswaa.....
 
Tunapambana na Corona, kalipoanza ndio kalikuwa ka Corona sasa ni Corona, tuwasikilize viongozi wetu kwa kutekeleza kila maelekezo tunayopewa.
Tufuate maelekezo ya kitaalamu ya jinsi ya kujikinga lakini pia tuongezee na tiba asili na tiba mbadala.
P
Kumbe hiki ka corona kalianza kwetu?

Wataalamu nchi hii ni Mamagufuli pekee.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa Taarifa yako hata huko Ulaya

Serikali inawatibu wagonjwa walio serious kweli kweli Wanaotakiwa kupelekwa ICU
Lakini kwa wale wenye nafuu wanajitibu wenyewe,,

Kuna ndugu yangu kapelekwa hapo kutokea Temeke wailes anaitwa Hamisi
Dereva wa dala dala temeke kwenda Mbagala

Kutokea juzi alikuwa temeke hospital amewekwa pale anatumia dozi yake mwenyewe aliyonunua mtaani amoxilin na panadol

Baada ya kuchukuliwa sampuli na kupelekwa maabara jana Yamekuja majibu anamaambukizi ya virus wa corona
Akapelekwa Amana

Mbaka jana jioni tunawasiliana nae hakuna huduma yeyote amana aliyopewa zaid ya yeye mwenyewe kuendelea na dozi yake ile ile aliyotoka nayo Uswazi

Amoxilin na panadol

Mbaka saa 4 usiku jana Alikuwa anaendelea vizuri
Lakini bado ajapewa huduma yeyote ile pale amana..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hao waliokufundisha Natural Selection ya Charles Darwin ndio haohao wanakuambia uchukue tahadhari. Wewe na wao nani anajua zaidi?
Kwako, mzungu hata akizaliwa leo anakuzidi akili? Maana natural selection inafundishwa kwa wazungu na kwa waAfrika vilevile. Kwa kiwango hichohicho cha elimu.
 
Wewe ni mtu wa ajabu sana, you're more than an embicile, muwe mnasikiliza hotuba nzima na si kuchukua point moja na kuja na final say; sikiliza pia wasomi ambao naamii hata wewe huwafikii mbuzi wewe
prof Tibaijuka ulimsikiliza???

Jana umesikia bungeni Dokta mwanamama mbunge wa Viti maalumu alichokiongea kuhusu tiba mbadala? Your level of appreciation of things is diminished , your coconut is also full of fuddy duddy ideas!

get time to understand things,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Moja kwa moja kwenye mada.

Kufuatia mwendelezo wa hatua za serikali kuhusiana na ugonjwa wa Corona nchini ikiwamo hotuba ya jana ya mheshimiwa rais, ni wazi sasa mheshimiwa anahitaji mawazo mbadala.

Mawazo mbadala hatayapata tokea kwa hao waliomzunguka wala hao wakuu wanaomzunguka ambao kwa sababu zilizo wazi wana matumbo yao yanayohofia tumbuzi.

Ilikuwa muhimu sana, kwa maslahi ya taifa hili mheshimiwa rais akakutana sasa na watu wengine wanaowasilisha mawazo tofauti, angalau kwa mazungumzo tu:

1. Baba Askofu Niwemugizi
2. Askofu Dr. Bagonza
3. Mheshimiwa Zitto Kabwe

Na wengine wa namna hiyo waliojipambanua kuwa hawana maslahi binafsi.

Mkuu watu hawa watakusaidia kuliokoa taifa hili. Kumbuka umoja ni nguvu.

Kwa nini Uganda waweze?


Kwa hiyo hao uliowataja ndiyo pekee wenye mawazo mbadala? Acha dharau kijana. Anza wewe kutoa mawazo mbadala, au ndio haya?
 
Nani mkweli sasa, wanaotuambia tuchape kazi tusiogope, au wanaotuambia tusiende kwenye mikusanyiko?! Wanaotuambia tushone Barakoa za khanga au wanaotuambia hazitusaidii chochote kutukinga kwa virus vya Corona? Nimeona Tweet ya Dr.Ndugulile akisema Mapua hayastahimili joto lakini Rais kasema tujifukizie dawa za asili?
Nimeona Dr.Mabula kateuliwa kuwa katibu mkuu, nilidhani Dr.Ndugulile kastaafu au kastaafishwa kumbe bado.
Sikiliza na ufuate maagizo ya viongozi wako.
 
Raisi yuko sawa sana, hizo barakoa wengi tu tulitilia mashaka toka mwanzo, na huo mvuke hajasema ukiwa wa moto hivo watanzania tuache mambo ya kujua sana, maji yanapata moto na kuua vidudu yakifikia nyuzi joto Mia moja, Sasa hapo yapo tayar kutumika, tumuamini raisi wetu hizo taarifa wa chini yake ndio wanamfikishia wako na ujuzi mwingi kuliko wengi wetu humu ndani ambao tunaendeshwa na mihemko

Sent using Jamii Forums mobile app
Asante kwa ushauri kuwa tumwamini Ndugu John Magufuli. Alisema corona isitutishe tuchape kazi na tumefuata. Sasa barakoa haziaminiki na tutumie njia asili na tiba asili tumesikia na tutafuata.
Ila mtangulizi wake mzee JK alituasa kuhusu neno "changanya na za kwako" sasa sijui kama mkuu nawe umeshachanganya na za kwako?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hotuba ilikuwa nzuri ila ukiwa na chuki huwezi kumuelewa raisi kwa sababu ya chuki tulizonazo,kuhusu barakoa zinazotoka nje kuwa na virus,si Tanzania tu..hilo hata mataifa ya nje yamewahi kulalamika hadi kufikia hatua ya kuamua kujitengenezea vifaa vyao binafsi...sisi tutakufa kutokana na chuki yetu kwa raisi na serikali kwa ujumla...binafsi siwezi napinga ufanyanyi wa test na kutumia barakoa kutoka nje,yaani ni mara kumi niende kwa fundi juma anishonee ya kitenge
 
Raisi yuko sawa sana, hizo barakoa wengi tu tulitilia mashaka toka mwanzo, na huo mvuke hajasema ukiwa wa moto hivo watanzania tuache mambo ya kujua sana, maji yanapata moto na kuua vidudu yakifikia nyuzi joto Mia moja, Sasa hapo yapo tayar kutumika, tumuamini raisi wetu hizo taarifa wa chini yake ndio wanamfikishia wako na ujuzi mwingi kuliko wengi wetu humu ndani ambao tunaendeshwa na mihemko

Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo wabongo tuko na chuki na mheshimiwa,hilo ndo litakalotu-cost
 
Hiyo ya mashine ya kupulizia ni ujinga, sababu ukipata corona inakaa ndani ya mwili wako yaani kwenye mapafu ukipumua ndio mwingine ana pata, sasa unapulizia ili iwe nini?. ni ujinga mkubwa sana.
Kwenye nguo,viatu,,,ukirudi nyumbani ukimkumbatia mtoto unahamisha hizo virus ama ukijishika ,hizo Ni tahadhari tu,just in case virus wako kwenye nguo ulizovaa
 
Back
Top Bottom