Mtu hatoki ndani asubuhi hadi jioni lakini analipa kodi na bills zote kwa wakati

Mpaka leo akili yako inajua kazini ni kwenda kubeba mizigo na (kwa waliopo Dar) ofisini ni lazima uende mjini/Posta!?
Amekariri huyo hajui kuwa kuna mtu yupo Tegeta ila anafanya kazi New York Marekani, mwingine yupo Lushoto ila anafanya kazi Geneva Uswizi ndo working station zao! na watu kama hawa ndo wamejaa serikalini na taasisi za umma ndiyo maana nchi haiendelei hii maana kuna watu akili zao ni za zama za mawe. Na cha kufurahisha ni kwamba hawa ambao wanawork from home aisee wengi wapo very disciplined, very time conscious na wanadeliver kinoumeer
 
Toeni maelekezo hizo kazi zinapatikana wapi vijana wengine nao wafanye
 
Nchi ina vijana waliojizeekea mapema sana
 
Sasa kama hatoki ndani hayo madawa anayauzaje?

Waswahili mnapenda sana mumjue mtu ndani nje ili baadae muweze kumkashifu kwa urahisi.

mtu anaweza kuwa na vitega uchumi kama hisa, majengo kapangisha hela zinatiririka kila baada ya kipindi fulan.i
 
Biashara zinafanyika online, personal nauza VFD, nafanya marketing online, nauza online nalipwa online, nawaunganisha wateja online nalipwa online nalipa mawakala online, inshort silazimiki kutoka nyumbani
Dunia imebadilika na covid ndio kabisa
Kuna watu hawalijui hili kuwa unaweza kuwa Miami beach na laptop yako huku shughuli zikiendelea Bongo
 
Mkuu hata kusoma watu wanasoma online unakuta MTU anasoma hadi anafanakiwa kupata degree , masters kupitia online.


So mambo yanabadilika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…