Basi Nenda
JF-Expert Member
- Jul 29, 2017
- 20,774
- 47,866
Ndio nakumbuka Dear, ile ajari ndio ilisababisha serikali itowe Amri gari ziende garage Kila mwezi na zilipelekwa kweri, naona yule Waziri alipoondoka na utaratibu ukafaHizi taaratibu zikianza katikati huko zinapotea.
Unakumbuka ya Lucky Vicent?
Ndiyo kama hivyo...Ndio nakumbuka Dear, ile ajari ndio ilisababisha serikali itowe Amri gari ziende garage Kila mwezi na zilipelekwa kweri, naona yule Waziri alipoondoka na utaratibu ukafa
Mtoto amekuaga kuwa anaenda shule na muda sio mrefu unaletewa taarifa kuwa mtoto wako amefariki,kwa mzazi inauma sana tena sana japo ukweli ndio huoNjia inaelekea ni ya maporomoko kuinama,
Poleni
Ova
Gari nyingi sana za shule ni mbovu. Na mamlaka zimekaa kimya. Naona maafa yanaweza kuongezeka. Tujiulize gari y shule inayozunguka hpo mjini inapata ajari kirahis namna hiyo.Kuna taarifa kuwa basi la Shule ya King David iliyoko Manispaa ya Mtwara Mikindani limepata ajali mbaya iliyopelekea vifo vya wanafunzi na dereva wa basi hilo aliyetambulika kwa jina moja Hassan anayekadiriwa kuwa na umri wa mika (54-60)
Miili imehifadhiwa katika hospitali ya rufaa ya Ligula na majeruhi wanaendelea na matibabu hospitalini hapo.
Kama Kuna mzazi au mlezi mwenye mtoto huko afuatilie kinachoendelea. Pole kwa wafiwa na majeruhi, Mungu mwenye Enzi awaponye.
======
TAARIFA YA AWALI YA JESHI LA POLISI
Gari namba T207 CTS la Shule ya Msingi na Sekondari ya King David iliyopo Mtwara limepata ajali maeneo ya Mji Mwema, leo Julai 26, 2022 na kusababisha vifo vya Wanafunzi, dereva na Msaidizi.
Msaidizi wa Kamanda wa Polisi wa Mtwara, ACP Nicodemus Katembo amesema kuwa taarifa za awali waliofariki ni Wanafunzi Nane, Dereva mmoja na Mwangalizi wa Wanafunzi.
Naye RPC mwenyewe ACP Nicodemus Katembo alipopatikana alisema majeruhi wamepelekwa Hospitali ya Ligula lakini watatoa taarifa zaidi baadaye.
UPDATES: 1130HRS
Watu kumi wamefariki dunia wakiwemo wanafunzi nane wa shule ya King David, huku wengine 19 wakijeruhiwa baada ya gari walilokuwa wamepanda kufeli break na kutumbukia kwenye korongo, Mji Mwema mkoani mtwara. Kamanda wa polisi mkoani humo, Nicodemus Katembo amethibitisha
RAIS SAMIA ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI
Kupitia akaunti yake rasmi Twitter, Rais Samia ameandika hivi
''Nimesikitishwa na vifo vya wanafunzi 8 wa shule ya msingi ya King David na watu wazima 2 vilivyotokea leo asubuhi huko Mtwara Mikindani baada ya gari la shule kutumbulikia shimoni. Nawapa pole wafiwa, Mkuu wa Mkoa na jamaa. Mwenyezi Mungu awarehemu Marehemu na kuwaponya majeruhi.''
View attachment 2304245View attachment 2304246
View attachment 2304248
View attachment 2304261
Seat belt itoke wapi magari haya asilimia kubwa ni mabovu. Mamlaka zimafanya kaz kwa matukio.Seat belt kwa dereva au abiria wa nyuma,
Maana kwa kawaida nchi yetu seat belt ni kwa dereva na mtu mbele
#Pole kwa wafiwa
"Mipango ya mungu"Pole kwao wahanga. Chanzo cha ajali ni nini?
Inaonekana kule upande ilipoangukia imejibamiza kwa nguvu na body likarudi huku upande wa dereva na kuwabana ukiangalia kwa makini.Duh! taarifa mbaya sana hii...
Lakini hadi sasa najiuliza hiyo ajali imekuaje imeua watu wengi hivyo, ukitazama picha ni kama impact sio kubwa na gari imeingia kidogo tu katika korongo...
Kinda ndio nini tena dadaa?Ajali haina kinda wakati mwingine. Wapumzishwe kwa amani
Seatbelts zinaweza kusaidia sana. Lakini ukiangalia school buses za wenzetu huwa hazina seatbelts. Watoto wengine wadogo sana. Lakini barabarani wana sheria ambazo zinayapa magari ya wanafunzi. Mfano gari ya wanafunzi ikisimama kupakia wanafunzi, gari zingine zote zinasimama.Kiwepo kitabu maalum katika Kila gari ambacho Trafic watakagua seat belts za school Bus na kusign, pia ule utaratibu kwa lazima school bus zote zipelekwe garage Kila mwezi uzingatiwe, kwa kupeleka Traffic mmoja Kila garage ili ahakikishe gari zinatengenezwa