Tetesi: Muda wowote kuanzia sasa Samia ataachana na DP World!

Kwa akili zako za kiccm unafikiri wewe upo sahihi zaidi?
Huo ndio ukweli, hakuna mwenye madaraka ya kuuza bandari ni maneno ya upotoshaji yenye lengo la kucheza na hisia za watu ili wauchukie uwekezaji.

Lakini uwekezaji unalenga kuipaisha nchi hii kuipeleka kwenye uchumi wa kati ngazi ya juu.
 
Makubwa
 
Sawa ila gharama za kuvunja mkataba ni zipi? Acheni propaganda za chekechea,,, mkataba hauvunjwi kiwepesi hivo hiyo ni kama ndoa ya kikristo kuivunja ni hekaheka na hata ikivunjwa ndio itakuwa maamuzi ya busara lakini Mama samia haitomsaidia kitu ndo atazidi kuamsha watu ,,, 2025 labda nguvu ya dolla imuweke pale kama wanavofanya siku zote ila tofauti na hivo ndo atakuwa raisi wa kwanza tanzania kutoka madarakani kwa kula chache kuwahi kutokea,,, OVER OVER
 
Abinafsishe TANESCO kwa muwekezaji mzuri aone kama tutapanua domo letu
 
Haya

Wenzenu Akina Salah na Neymar wanakimbilia Arabuni Kule Ulaya na Marekani wazungu wamefirisika Lakini Nyie mnapishana na Gari la hela [emoji1][emoji1][emoji23][emoji91]
Nadhani vifungu vya mikataba ya hao unaowasema si sawa na vya DP
 
IPTL 1994 Rais alikua Mwinyi
Hela zimechukuliwa wakati wa Kikwete muulize yule mama aliesema 10 million ni shillings ya mboga hizo hela walizogawana ndio sasa inabidi ziwayokee puani na sio kodi za Watanzania maskini
 
Haya

Wenzenu Akina Salah na Neymar wanakimbilia Arabuni Kule Ulaya na Marekani wazungu wamefirisika Lakini Nyie mnapishana na Gari la hela 😄😄😂🔥
Pesa si msingi wa maendeleo, uhuru, haki, heshima na utu bwashee.
 
Kama ni kweli nampongeza na kumshukuru sana Mama.
Lakini jambo hilo limetujeruhi sana CCM kiasi ambacho imani ya wananchi imepungua sana.Nashauri CCM tujihadhali siku za mbeleni katika kufanya maamuzi.
 
Dp world wapo bandarini milele.Nyie jitekenyeni tu ila hambadili chochote.
 
Huko kunaitwa kubwabwaja na kuhororoja bila mpango.
 
Hii ndo hoja. Maana nilikuwa nafuatilia huu mjadala na mmojawapo wa watetezi wa huu mkataba ni wewe.

Kinachobishaniwa ni vifungu tatanishi...kurekebisha vifungu hivyo vikaendana na matakwa ya wananchi ndo suala la msingi lakini kukataa kuvirekebisha basi kutakuwa na hidden agenda.

Lakini pia,kushindwa kuendesha bandari isiwe hoja ya kubinafsisha maana kila tunaposhindwa kusimamia mashirika basi yabinafsishwe je,itakuwaje kama tunashindwa kusimamia taasisi za serikali na ofisi mbalimbali za serikali kama taasisi ya Urais,huko kwenye halmashauri za wilaya,miji,manispaa na jiji...napo zibinafsishwe kwa nani?

Tuboreshe usimamiaji wa taasisi zetu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…