Mufti Zubeir: Serikali inunue chombo cha kutazamia mwezi
Swali, Je ni jukumu la Serikali kufanya masuala ya dini?

Pili,Kuomba Serikali ifanye sio vibaya maana ni ombi.

===
Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir amekemea ufisadi, akihimiza jamii kulinda maadili, umoja na mshikamano, huku akiwaomba viongozi wa Serikali na wadau kusaidia upatikanaji wa darubini ya kukusanya taarifa za mwandamo wa mwezi ili kumarisha uhakika wa taarifa.

View attachment 2596212

Mwezi mtukufu wa Ramadhani ni kipindi ambacho waumini wa Kislamu duniani hufunga kwa siku 30 kabla ya kusherehekea siku hiyo kupitia taarifa rasmi va mwandamo wa mwezi huo.

Hata hivyo, kabla ya kusherehekea, kifaa hicho (moon sighting machine) ndio hutumika kupata uhakika wa mwandamo wa mwezi huo kimani ili kuondoa utata au mabishano miongoni mwa waumini hao.

Sheikh Zubeir amesema hayo leo Jumanne Aprili 22, 2023 katika swala ya Eid EI- Fitr iliyofanyika kitaifa katika msikiti wa Mfalme Mohamed VI uliopo Wilaya ya Kinondoni, jijini hapa, ikihudhuriwa na Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, mabalozi, mawaziri na watu mashuhuri.

Chanzo: Mwananchi
Ila ameiomba serikali, sio kitu kibaya, serikal inaweza kukubali ombi lake au kukataaa...

Sion sabbu ya kukemea, au kumkosoa mufti... Kwa sabbu sio kila unachoomba lazima upate

Sent from my M2010J19SI using JamiiForums mobile app
 
Siku zote Tanzania hutegemea Mitambo ya nchi zingine au yetu tu Wenyewe kujua Kama Mwezi umeshaonekana ili tukagombee Pilau na Ndizi zetu Mifukoni na kulikuwa hakuna tatizo lolote lile.

Yaani Mama apoteze Pesa za Walipa Kodi Kununua Kifaa cha kujua kama muache Kufunga au muendelee wakati Mitambo ya Kisasa ya TMA inaweza kufanya hivyo?

Tulitarajia Ufafanuzi wa kwanini nchi za Jirani nasi Wao Eid wamesheherekea Jana wakati Sote tuko EAC na kwa miaka mingi tumekuwa tukitegemeana Kitaarifa ( hasa linapokuja Suala la Mwezi Kuonekana ) cha Kushangaza na Kusikitisha mnakimbilia kuomba Kifaa cha Kisasa cha Kuuona Mwezi.

Acheni kutulazimisha tuwadharau.
 
.
20230324_092143.jpg
 
Hii dini huwa inashangaza sana kuomba vitu visivyo na maana. Kuandama kwa mwezi hata kwa ufahamu wa kawaida tu unaweza kujua kuwa mwezi tayari umeandama kwa kuangalia anga kwa macho ya kawaida, au mabadiliko ya hali ya hewa kwa siku, au hatua kwa hatua za mwenendo wa mwezi kuzunguka dunia unajua mwezi upo wapi. Kingine walichoomba cha ajabu ni somo la dini yao kuwa rasmi. Hii nchi kwa mujibu wa katiba yake si ya kiislam na haiongozwi kwa misingi ya dini hiyo. Unaombaje somo la dini ya kiislam lirasmishwe katika nchi ambayo ina mchanganyiko wa dini nyingi, je na dini zingine wakiomba nao masomo ya dini zao nayo yarasmishwe itakuaje? Bora wangeomba wasaidiwe kujenga hospitali za kutatua changamoto za kiafya wangeeleweka vizuri. Kama vile ni wabinafsi hupenda kuombaomba au kuombewa vitu vyao binafsi kwa ajili ya dini yao tu. Wawe wanaomba vitu kwa ajili ya watanzania wote
 
Walutheri huwa wana kitabu kidogo cha kalenda ya mwaka mzima kinachoonesha mwenendo wa mwezi mchanga mpaka mwezi mpevu (full moon). Kinaonesha mpaka tarehe ya kuandama, waislam wanashindwa nini kuwa na kalenda ya kuonesha mwenendo wa mwezi kama kwa mtazamo wa macho ya kawaida wanashindwa kuangalia anga na kujua mwezi umefika wapi? Kama tu manual wanashindwa kubainisha muandamo wa mwezi, je hicho chombo kitabaini vipi wakati hata kwa hesabu za kawaida tu zinaweza kujua kuwa mwezi umeandama?
 
Sioni ubaya kwenye ombi la mufti. Chombo hicho kinaweza kununuliwa na Serikali. Na kikawa chini ya mamlaka ya hali ya hewa. Na waislam wakakitumia kwa mahitaji yao ya kiimani.
acheni kuingiza serikali kwenye mambo ya dini, BAKWATA si taasisi ndogo kiasi cha kuombaomba na kuombewa misaada kila uchao. Mara ujenzi wa msikiti mkubwa, mara chombo cha kuangalia mwezi. Kuna taasisi nyingi za kidini nazo zinahitaji kusaidiwa mambo yao ya imani zao.
 
Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir amewaomba Viongozi wa Serikali na Wadau kusaidia upatikanaji wa darubini ya kukusanya taarifa za mwandamo wa mwezi ili kumarisha uhakika wa taarifa.

Sheikh Zubeir amesema hayo leo Aprili 22, 2023 katika swala ya Eid El- Fit iliyofanyika kitaifa katika msikiti wa Mfalme Mohamed VI uliopo Wilaya ya Kinondoni ambapo miongoni mwa waliohudhuria swala hiyo ni Rais Samia pamoja na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

"Tuna Mabalozi hapa tuna Mawaziri mbalimbali na Wadau wengine, kuna chombo tunakihitaji cha kutazamia mwezi, wenzetu Zanzibar wanacho, wenzetu Kenya wanavyo vingi tunaomba na sisi wale wanaoweza kutushika mkono watusaidie na sisi” ——— Mufti

Source: MillardAyoUPDATES
 
Kauli sahihi ingelikuwa serikali iwatafutie wafadhili wa kuwapatia hicho kifaa kama walivyowapatia wafadhili wa kujenga huo msikiti. Wapo tele... wasiombe tende na nyama tuu
 
Swali, Je ni jukumu la Serikali kufanya masuala ya dini?

Pili,Kuomba Serikali ifanye sio vibaya maana ni ombi.

===
Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir amekemea ufisadi, akihimiza jamii kulinda maadili, umoja na mshikamano, huku akiwaomba viongozi wa Serikali na wadau kusaidia upatikanaji wa darubini ya kukusanya taarifa za mwandamo wa mwezi ili kumarisha uhakika wa taarifa.

View attachment 2596212

Mwezi mtukufu wa Ramadhani ni kipindi ambacho waumini wa Kislamu duniani hufunga kwa siku 30 kabla ya kusherehekea siku hiyo kupitia taarifa rasmi va mwandamo wa mwezi huo.

Hata hivyo, kabla ya kusherehekea, kifaa hicho (moon sighting machine) ndio hutumika kupata uhakika wa mwandamo wa mwezi huo kimani ili kuondoa utata au mabishano miongoni mwa waumini hao.

Sheikh Zubeir amesema hayo leo Jumanne Aprili 22, 2023 katika swala ya Eid EI- Fitr iliyofanyika kitaifa katika msikiti wa Mfalme Mohamed VI uliopo Wilaya ya Kinondoni, jijini hapa, ikihudhuriwa na Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, mabalozi, mawaziri na watu mashuhuri.

Chanzo: Mwananchi
BAWATA, BAKWATA, JUWATA, na mengine kama hayo, wala haihitaji shahada ya chuo kikuu kutambua asili na madhumuni ya uwepo wake.
 
Back
Top Bottom