Mungu anawaogopa nini Wanadamu mpaka awatolee Sadaka ya Mwanae?

Mungu anawaogopa nini Wanadamu mpaka awatolee Sadaka ya Mwanae?

Kwa ujumla suala la dini ni sanaa iliyofanywa kwa umahiri mkubwa na wenzetu weupe. Ndo maana kuna mapungufu ya wazi ambayo yanaondoa sifa ya uungu.
 
Kikubwa ni Kwamba Watu wanajua Ukweli ila Wanaupamba Pamba Ili kuficha Aibu. Hapo inamaanisha Hivyo hivyo kwamba Kazaa. Ila wao hawataki kusema Kazaa maana Wanajua Ukweli kwamba Mungu hana Hiyo Sifa ya Kuzaa

Ila Ukienda kwa waumini wengine Maria ni Mama wa Mungu wakimaanisha Mama Wa Yesu ambaye ndie Mungu.

Umeona Vichwa vilivyovurugwa hapa Ndugu yangu
Hawa watu ni mtihani. Kwao inaelekea ukiuliza maswali unafukuzwa. Wanafuata dini kiushabiki badala ya maandiko.
 
Kwa ujumla suala la dini ni sanaa iliyofanywa kwa umahiri mkubwa na wenzetu weupe. Ndo maana kuna mapungufu ya wazi ambayo yanaondoa sifa ya uungu.
Afrika Kulikuwa na Imani Ya Kuleta Watu katika umoja. Ila Zilipoletwa hizi Dini zilizoletwa na Malaika na Majini ndio zinatuharibu ndio maana Hakuna Umoja wamevurugika kila Siku leo Hawa Hawampendi huyu kisa Imani yake tofauti na Yeye. Sasa Huyo ni Mungu kweli
 
Ukitumia akili zako timamu utajua hapa Hakuna Ukweli wowote

Maana hao hao waliotunga hayo maandiko wanakuja Kusema Huyo waliomsulubu alikuwa ni Mungu. Ila Ukiwauliza Kwahiyo Binadamu walimuua Mungu hawana Jibu. Na Ukiwauliza Kwahiyo Dunia ilimuua Mungu na Ikawa haina Mungu kwa Siku 3 mfululizo hawana Jibu
Wanasema et kuna mung roho ,mungu Baba na nin sijui ,ndo utaskia hapo zaman kulikuwa neno Yan ni Sawa na kusema hapo zaman kulikuwa na fundi akageuka kuwa stul ,stul ikageuka kuwa fund
 
Kuna kundi la watu ambao hawajui lakini wanajifanya wanajua. Wewe upo kwenye Hilo kundi. Unaishambulia Biblia na kusema Ni uongo. Jiulize ni kwanini Yesu au Issa anatajwa Sana kwenye Quran?.
Qur'an imekanusha propaganda za biblia na kusema injil ilichakachuliwa ndio maan unaona contradictions nyingi ,Qur'an imekataa yesu hajafa wala hajasulibiwa ,imekataa si mungu na bla bla kibao
 
Wanasema et kuna mung roho ,mungu Baba na nin sijui ,ndo utaskia hapo zaman kulikuwa neno Yan ni Sawa na kusema hapo zaman kulikuwa na fundi akageuka kuwa stul ,stul ikageuka kuwa fund
Tumevurugwa Sana Akili zetu
 
Sawa ndugu. Mie sitaki Uniamini kwa Chochote ninachotaka jaribu kuchunguza Maandiko mnayopewa kama Yana Ukweli ki utu na Kuishi Kibinadamu. Afrika Tumeletewa Mambo mengi sana hatuwezi Walaumu wazee wetu wala mababu zetu kwanini walikubali manaa Hatujui walichopitia kumbuka Walikuwa wanauzwa kama Watumwa na Ukishakuwa Mtumwa Jua Imani yako Inabadilishwa na Kumbuka Mpaka Mnapata Uhuru watu wengi walikuwa washabadilishwa Imani zao na Kupewa Dini hizi walizonazo. Kumbuka Sidhani kama wakoloni wangekupa Kazi Kama Hujafuata Imani zao



Mbegu hiyo Imeshaota na Kuwa Mizizi mikubwa sana ila Ukweli Utawapa Uhuru siku Moja
Ni kweli ndugu.

Tufikiri hivi labda, mimi ni muumini wa katoliki.
Elimu yangu ya kawaida ni ndogo sana naweza kusema ni darasa la saba.

Kiongozi wangu ambaye tunamwita padri ni doctorate.
Kwa maana hiyo yeye anajua mengi sana kwenye maandiko na nje ya maandiko lakini bado ana amini

Mimi ni nani hata niweze kumchallenge haswa tena kwa marejeo ya posti za hapa na.

Kweli kabisa ukisikiliza kwa kina na kutafakari kwa kina kuna walakini mwingi lakini unadhani nitakua mgeni wa nani kwenye jamii ninayo ishi iwapo nitataka kuamini vile unavyo sema ndugu yangu?
 
Mkuu unaonekana unaamini uchawi. kuamni uchawi na unavyoviandiaka kwenye nyuzi zako, inanifanya nikupotezee.
Ndugu yangu Ngoja nikuambie kitu Kimoja. Ambacho najua Kitakufungua Akili kidogo kama Mm unaona Naamini Uchawi.

Yesu alipopatwa na Magumu alikimbilia Kuongea na Musa na Elia ambao walikuwa si malaika wala si Mungu bali Binadamu waliowahi ishi hapa Duniani. Maana Yake ki Utu tu ni kwamba alienda Kuongea na Mizimu ya Musa na Elia

Jiulize kwanza Hilo kabla Hujaanza Kuniuliza naaminj Uchawi(ushirikina) wakati Yesu alishirikiana na Mizimu ya Musa na Elia. Kitu ambacho ww unakiona si Ushirikina. Kwanini Aongee na Musa na Elia wakati Mungu Yupo.

Tafakari hilo kwanza
 
Ni kweli ndugu.

Tufikiri hivi labda, mimi ni muumini wa katoliki.
Elimu yangu ya kawaida ni ndogo sana naweza kusema ni darasa la saba.

Kiongozi wangu ambaye tunamwita padri ni doctorate.
Kwa maana hiyo yeye anajua mengi sana kwenye maandiko na nje ya maandiko lakini bado ana amini

Mimi ni nani hata niweze kumchallenge haswa tena kwa marejeo ya posti za hapa na.

Kweli kabisa ukisikiliza kwa kina na kutafakari kwa kina kuna walakini mwingi lakini unadhani nitakua mgeni wa nani kwenye jamii ninayo ishi iwapo nitataka kuamini vile unavyo sema ndugu yangu?
Ni kweli ni Ngumu Ila Ukweli umuweka Mtu huru na Kumbuka Mwenye maamuzi ni Wewe mwenyewe. Hao Kujiita Doctorate kumbuka Wapo kwenye System walioziunda Wao wenyewe

Maamuzi ni Yako mwenyewe Maana Babu zako nao Walipokuwa wanaenda Kwenye Hizo Dini Wakaacha Asili zao Wazee wao waliwachukia sana maana walijua Hakuna Ukweli huko na Ndio Mabalaa Tunayoyapata Kila Siku kwenye Familia zetu tunakimbilia Makanisani Hatupati msaada. Ukichunguza Kwa Makini Waumini wengi wa Hizo dini Wanaenda Sana kwa Waganga. Sasa Waganga wa Nini wakati wameambiwa Huko Kuna Uponyaji

Wamesahau kuwa Kuna Roho zimewachukia sana Na Zina Visasi vibaya Juu yao na Wakiona Wajukuu mpaka vitukuu vinaingia Bado huko zinazidi kuchukia. Zaidi

Kumbuka Ukiacha Kitu zile Roho za Huko Lazima Zikuchukie. Ukiacha Ukatoliki lazima Roho za Huko zikuchukie.. Ukiacha Uislam lazima Roho za Huko zikuchukuie.. Ukiacha Ulokole lazima Roho za Huko zikuchukie. Angalia Wale wanaohama hama Madhehebu Maisha Yao mengi huishi Kuharibikiwa. Kama Ww Unaamini Kaa Huko Huko Usichanganye Madhehebu utazidi haribikiwa mara 100 km unajua ukweli na ukabaki huko huko jua Roho zinazidi kukukasirikia
 
Hili andiko lako Mungu alishatoa jibu kwamba "msichunguze maandiko maana mnatafuta ubatili"!

Mungu alijua upo na utachunguza lutafuta makosa tuu Wala hutafuti usahihi.

Yesu ni Mungu.
Kwa hiyo Mungu anaogopa kuchunguzwa sio
 
Ni kama ile wewe mwanaume unavmiaka karibia 50 unambaka mtoto wa miaka sita halafu kwa aibu eti unapotezea kwa kumuoa akiwa na miaka 9 na bado unaona sawa tu na mabilion ya waja wanakutuza hadi wanachinjana na kujitoa mhanga. Halafuu unajiona mjanjaaaa eti Mungu kakutuma. Kweli huyo ni Mungu gani wa ajabu anaweza kukutuma.
itakua akili yako ipo upogo na umekalilishwa vitu ambavyo hata waliokukalilisha hawavijuwi unaongea tu .haya kwani Paulo wakwenye biblia alikua mwema hapo awali si mnamuamini ??? Je swali mungu anaweza tuma mtu wa namna hio ???? Swali jingine mbona nyinyi pekee wa enzi hizi ndio mnamuandama kua alioa mara alibaka mtoto mdogo ,ila tukiangalia kwenye jamii yake kipindi hicho mbona tuhuma hizo amna ???? Wewe/ nyinyi mlijuaje labda mtoto anaolewa akiwa naumli gani kwenye jamii yao hebu twambieni ???? Mana Kama mnamtuhumu kua aliowa/ alibaka mtoto mdogo itakua mnajua kabisaa kwenye jamii yake wasichana walipaswa kuolewa wakiwa na umli gani ???? Kama hujuwi basi usiwe unalopoka lopoka na usioyajua ni Bora ukakaa kimya
 
Aliyezaliwa sio Yesu ila ni Kristo
Jina la Yesu lilishushwa toka kwa Mungu na malaika
Mungu anafanya kazi ndani yetu kupitia roho, Mungu alikaa ndani ya Kristo kupitia
Mungu ana nafasi zake katika utendaji wake;
*Mungu ni baba katika nafasi yake ya uumbaji,
*Mungu ni mwana katika nafasi yake ya ukombozi kupitia Kristo,
*Mungu oho mtakatifu katika nafasi yake ya kutenda kazi ndani yetu

Yesu ni Mungu

Duuh[emoji19][emoji23]
 
Unataka kusema Mungu hana uwezo wa kumpa mtu ujauzito bila kufanya matusi, na ndani ya wiki moja akajifungua?
 
Yesu Kristo Ni Mungu. Ndio maana alizaliwa kwa uweza wa Roho Mtakatifu. Na sio kwa njia ya kawaida.

So Mungu aliishi na sisi duniani? Ok..
Na wakati analia asaidiwe na Mungu hapo ilikuaje?! Mara Mungu alimtoa mtoto wake huyo mtoto ni nani kama Yesu tayari ni Mungu?!
 
Yohana 10:17-18
"Ndiposa Baba anipenda, kwa sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena. Hakuna mtu aniondoleaye, bali mimi nautoa mwenyewe. Nami ninao uweza wa kuutoa, ninao na uweza wa kuutwaa tena. Agizo hilo nalilipokea kwa Baba yangu."

Angekufa akazikwa na kuoza ingekua joke. Siku tatu tuu alifufuka na anaishi hadi sasa duniani kote

Agizo anapokea Kwa baba? Baba Mungu? Na Yesu ni mtoto Mungu au?
 
Mungu kamzaa Yesu ? So na Adam nae ni Mungu? Maana yeye hata wazazi hana!
[emoji1787][emoji1787]Hii komenti yako imenichekesha sana.

Ulitegemea Mungu Aseme mwanae wa Pekee ni Adam ila huku wanakuja kukuvuruga kumbe Adam hana Wazazi [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom