Mungu ni mwema kaniokoa na Kifo japo nipo kitandani hospitalini muda huu

Saa tisa kasoro naingia humu nakuta hii habari. Nimesikitika kweli, get well soon. .

Utamuwa sawa usiwaze
Powa best angu gily Asante ndio ivyo naianza safari yangu ya kuponyesha miguu yangu..

Hapa siwez kugeuka Wala kujimudu Kwa chochote

Sikuwai kujua kama siku Moja namini ntakua victim wa kuvunjika miguu....

Ni safar ndefuu naelezwa hapa mpaka naogopa
 
Lengo lake ni kuanzisha ligi hakuna kingine, Hawa watu wanaojiita atheist ni kama watu fulani waliorukwa na akili kwa namna navyowaona sasa hivi.


Hata kama mnatofautiana mitazamo kwa mtu ambae ni mwenye busara na akili zake timamu atakaa kimya kutokana na mazingira ya muda huo, ila wao wanataka ligi muda wote
 
Shukuru Mungu Kwa Kila Jambo.

Yote Hutokea Kwa Sababu.

Ukiwa Hai Tu Shukuru Mungu.
Sasa unachomshukuru mungu ni kipi?
Kukufanya upande hiyo bodaboda, au kukufanya uvunjike huo mguu? Ama kukufanya uheme na mguu huna?
 
Pole sana, chief. Speedy recovery
 
Diclofenac injection imedunda na maumivu balaa

Hapa ndio nimechoma TRAMADOL INJECTION

At least maumivu yameanza kupungua maana nilianza kuugulia Kwa saut

Asante woteeeee kwa upendo mwing na neno la matumaini ambayo mme show kwangu...
Uombe pethedine Pole sana kaka.
 
So kesho utaenda kwa ajili ya ORIF jitahidi kutafuta mtu atakayekuwa anakusaidia siku ukitoka hospital Maana hospital nyingine manurse hawawezi kukusaidia kwa kila kitu
 
Pole sana, usukumani huku Wana dawa za kienyeji za kuunga mfupa, Nzuri sana. Mwezi mmoja tu unatembea kama hakuna kitu ulipata. unaenda na picha Yako ya x ray tu. Jamaa angu alipata ajali ya pikipiki mwaka Jana akavunjika mguu, tukampeleka Kwa mtaalamu wilayani Magu akamuunga. Kimsingi hii dawa ipo Kanda ya ziwa Karibu Kila mahali maana wanasema ni aina flani ya miti , mtu yeyote akielekezwa anaweza kufanya.
 
Pole
 
Pole sana mkuu.
Utakuwa sawa..nakuombea upone haraka.
 
Duuuh! Pole sana ndugu. Mwenyezi Mungu akufanyie wepesi upone kwa haraka uendelee na majukumu yako
 
Ndugu wana jamii mnaoleta maneno ya kejeli na dharau kwa mwana jamii mwenzetu.....hebu jaribuni kuuvaa ubinadamu hata chembe katika hali kama ya mtoa mada.........

Kama huna la kuchangia la kutia moyo na kushauri kwanini usikae kimya tu........

Ninacho waasa ni kuwa maisha ni safari na safari bado ni ndefu angali tupo hai...... unaweza kufikwa na jambo lolote kwa wakati wowote........

Pole sana ndugu.....
 
Pole sana jiandae tufanye ORIF
MAINTAIN NPO
 
Naikumbuka hiyo, pole sana brother
 
Pole sana mkuu..Mungu akuponye ili uendelee kupambania maisha ya kila siku
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…