Mungu wa walokole ana nguvu sana 1997- 2019! Kumbukumbu zangu

Tunazidi kupata elimu
 
NAENDELEA.............!!!
Kuna nyakati baadhi ya walokole wanajihisi kuchoka na kukata tamaa kwa masahibu mbalimbali katika maisha,,na kiroho inakua hv wanapoanza kuomba kwa kulia.....
Wale watu warefu wenye mabawa wanashuka na kukaa karibu yao na kuwatazama kwa upendo huku wakiwazunguka pande zote.Lakini wakiendelea kulia zaidi basi mbingu zinafunguka na Mwana wa mmiliki anashuka mwenyewe mpaka chini kuwatazama na wakizidi kulia na yeye analia na kuwaambia NIPO HAPA USILIE ISHI KWA IMANI NIPO HAPA DAIMA.
Na hata kama wapo sehemu tofauti tofauti duniani yeye anajigawa kwa sekunde hiyo hiyo anafika kote.Hakuna kitu kinachomshusha duniani kwa haraka mwana wa mmiliki kama maombi.
Walokole hawajui ila maombi ni silaha kuu sababu chochote utakachokisema kwenye maombi basi kwenye ulimwengu wa kiroho kinatokea hivyo hivyo.
WAKISEMA WANAFUNGA BASI NJIA ZOTE ZOTE ZA ANGA ZINAFUNGWA NA WAKISEMA MOTO KWELI MOTO HUTOKEA NA WAKIIMBA ILE NYIMBO YA ROHO YA MUNGU WAO ISHUKE BASI INASHUKA KWELI NA WINGU ZIIITO LA MWANGA MKALI KULIKO JUA LINAWAFUNIKA MPAKA WAMALIZE MAOMBI.
Mungu wa walokole huwezi kumtizama kwa macho ya kawaida ila anafanana na binadamu kimuonekano ni kama mzee hivi aliyekula chumvi za miaka usoni ila sio kwa ukubwa wa kimwili,,sababu yeye ni mkubwa mno kuliko dunia LAKINI ANASEMA ALIMUUMBA MTU KWA MFANO WAKE KIMUONEKANO ILA SIO KWA SIZE.Mwana wa mmliki na yeye anafanana na binadamu kimuonekano ila na yeye ni mkubwa mno kimuonekano.Na wale watu warefu wenye mabawa wanafanana na binadamu ila ni wakubwa mno kimuonekano..
Basi walokole wakiendelea kulia na kusali anga lote linafunguka na inakua ni uwanja wa mawasiliano kati yao na mwana wa mmliki,ambae anashuka na kukaa nao huku akiwatizama ila wao hawamuoni.
CHA AJABU WATOTO WOTE WA KIBINADAMU WANAMUONA NA WANAONGEA NAE NA KUCHEKA NA ANAWABEBA KIFUANI WAKATI WAKIWA NA WAZAZI WAO AU WALEZI WAO NA HAIJALISHI NI WATOTO WA WALOKOLE AU LA....YEYE MWANA WA MMLIKI NA WALE WATU WAREFU WENYE KUAKISI MWANGA RAFIKI ZAO WAKUBWA NI WATOTO WA KIBINADAMU KUANZIA UMRI WA SIKU MOJA MPAKA MIAKA KUMI NA NNE MPAKA KUMI NA SITA.
NB: KUNA WATOTO WASIO WA KIBINADAMU PIA IKUMBUKWE
Basi walokole wanapomaliza kuomba wanakua hawaoni wala kujua kua wamezungukwa na viumbe vya kiroho vinavyowatizama ila waga wanajihisi amani sana na utulivu wa moyo.Haijalishi kanisa gani wanatokea ila walokole wote wana alama sawa,,iwe wasabato au wakatoliki au waangilikana au walutheri au wapentekoste,,kwa mwana wa mmliki wote ni kitu kimoja na anawalinda sawa sawa.
Wachawi ni wabishi sana ndio wanaoongoza kwa kuwasumbua walokole wakiamini kua walokole ni wachawi kama wao ila wamewazidi maarifa ya kiuchawi.Na ndio wanaoongoza kwa kuwadhuru walokole kimwili.
KUNA ALAMA SABA ZA WALOKOLE KIROHO ZINAONEKANA WAZIWAZI
1: TUNDA LA UPENDO ( NJIWA WA MOTO)
2: WALINZI WATU WAREFU WENYE MABAWA NA PANGA ZA MOTO
3:NDIMI ZA MOTO JUU YA VICHWA VYAO
4: NGUZO ZA MOTTO ZINAZOZUNGUKA
5: WINGU LA MANUKATO NA MOSHI MWEUPE
6:MAGARI YA DERAYA NA FARASI WA MOTO
7:UTIIFU WA MOYO ULIO WAZI KIMUONEKANO KIROHO KWA MUNGU WA WALOKOLE.
Nitaendelea....................!!!!
 
Kiroho Unajimu ni uchawi uliorembwa rembwa!!!! Walokole wanaishi kwa imani sio unajimu
 
Toka wameanza maigizo ya upako sijui kuuza maji na upuuzi kama huo wamestukiwa kwamba ni matapeli
 
Wateule kiroho wanangaa na wanaongozana na wale watu warefu wenye mabawa na panga za moto.Ambao ni washirika wa Mungu wa walokole.
 
USIHUKUMU HIYO SIO KAZI YAKO KIROHO

Hivi majirani mitaani kugombana kulumbana,
Kunatokana na Nini kirohoni,

Na je , jirani mtaani wa kilokole akichokoswa mtaani kimwili kule rohoni wale malaika wanafanya nini

Na je ugomvi wa kimwili unasababishwa na kirohoni ??

Na je ikoje huko Rohoni mpaka kinatokea mwilini

Je,BARAKA ZA ROHONI ZINAKUJAJE MWILINI KWA NJIA IPI ,

MFANO MLOKOLE KAKUOMBEA UPATE PESA NA KAZI ,KIMWILINI INAKUJAJE ,YAANI ILE BARAKA YA ROHONI INAKUWAJE MPAKA INATOKEA MWILINI.
 
Hivi Kuna malaika ambao wanavaa miili na kuishi nao Katika jamii kama binadam wa kawaida,

Yaani anavaa mwili la umbile na size ya kibinadam na anakuwa yupo na watu mtaani, wako malaika hao,

Au hii ni Agano la kale tu ,agano jipya ,hawaluhuaiwi
 
Hivi hivi vita vinavyopiganwa kimwili,
Kirohoni nchi na nchi zikilushiana kombola kirohoni Hilo kombola la kimwili linaonekanaje,

Na je Israeli kirohoni inonekanaje,

Na kimwili tuna mabara Saba ,kirohoni ardhi Zina mabara mangapi,

Kimwili watu wakiwa Katika ndoa, wanamme na mwanamke kitandani kumtafuta mtoto ,je Roho ya mtoto inaletwa na maraika au vipi na Inaonekana Roho ya mtoto ikipelekwa tumboni,
 
NA MTU AKIOMBA KATIKA ROHO KWA LUGHA ,APATE MKE AU APEWE MKE WA KUMUOWA , KULE ROHONI INAUMBIKAJE YAANI,

MFANO AKAOMBA MPAKA HUYO MWANAMKE AWEJE,
INAUMBIKA, SASA KINAUMBIKA kinakuwa kinaonekanaje Hilo ombi,

Na watu wanaofunga ndoa madhabahuni ,wakiombewa ombi la kufunga ndoa,kinatokea nini
 
Hivi Kuna magari ambayo kimwili ni ya kifahari hasa,
Ila kiroho ni joka linalo jongea,

Zingine zinaonekana kama ndege kumbe popo na mabundi kiroho,

Na wanaviuza bei kubwa mno
Hio imekaaje,
 
Hivi Kuna magari ambayo kimwili ni ya kifahari hasa,
Ila kiroho ni joka linalo jongea,

Zingine zinaonekana kama ndege kumbe popo na mabundi kiroho,

Na wanaviuza bei kubwa mno
Hio imekaaje,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…