NINAENDELEA.......!!!!
WANAJIMU NA WAGANGA :Wanajimu na waganga hawana usharika na walokole katika lolote lile.Wao ni washirika wa wale watu warefu wa baharini.Unajimu haufundishwi kwenye mikusanyiko ya kilokole sababu una makufuru na hatua zake nyingi zina ushirikiano na uganga.Wanajimu wanachukua nyota za wangu na kuzitumia kwa manufaa yao.Wanajimu wanafanya tafukuri ambayo ni laana kiroho.Wanajimu hawana utii kwa mkuu wa mamlaka aliye mkuu wa wote,bali wao wanatii uganga wako na miungu ya kwenye sayari za ndani ya mfumo ww jua wa ulimwengu.Wanajimu wanashirikiana na wale viumbe wa baharini kumuhujumu mwanadamu aliepo duniani.Wanajimu wanatafuta elimu ya anga kwa njia za uchawi wa kale wa kiarabu na kiajemi.Wanajimu hawana maombi ya kubariki bali wana maombi ya kulaani,kwani kwao laana ni sehemu ya matambiko yao.Hivyo wanajimu ndani ya ulimwengu wa kiroho sio watu wema.
WALE VIUMBE WAREFU :Kama nilivyosema pale mwanzo kua,kuna aina mbili za wale viumbe warefu
MOJA :Watu warefu wa angani wanaoakisi mwanga
MBILI :Watu warefu wa baharini wasioakisi mwanga.
WATU WAREFU WA ANGANI WANAOAKISI MWANGA :Wale watu warefu wazuri kwa muonekano,wanaoshika panga na kulinda walokole ni watu wa ajabu sababu ya tabasamu zao na upendo wao.Akikusogelea kwa karibu utatamani ulie kwa furaha maana unapata amani ya moyo iliyopitiliza.Wana upendo mkuu sababu ukiona jinsi wanavyowahudumia walokole lazima upendezwe nao.Walokole ni kama vitoto vidogo mbele ya hawa walinzi wao ""Watu warefu""..Upenda na ulinzi ndio sifa yao kuu.Wao ni moto ndani ya moto wa shaba,wana nguvu kama umeme wa radi.Kimuonekano wengine wana mabawa na wengine hawana mabawa ila wote warefu kwa vimo.
WATU WAREFU WA BAHARINI WASIOAKISI MWANGA :Hawa ni washirika wa waganga na wanajimu na wachawi.Kimuonekano ni watu wa kubadilika badilika.Hawana muonekano mzuri wa kudumu bali wanachukua sura halisi za binadamu,hasa binadamu wa bara hindi na uajemi.Hawana usharika na walokole sababu walokole wanaharibu kazi zao wanazofanya na wanajimu na wachawi.Hawana upendo wala amani ya moyo wakikusogelea,zaidi zaidi utasisimka na kuogopa.Ni washirika wa mkuu wa ulimwengu mwenye vita vya kudumu na walokole.Tusiwazungumzie sana hapa maana lengo sio kuwazungumzia wao bali Mungu wa walokole.
Kwa binadamu wa kawaida unakua na amani ukikutana na hawa watu warefu wa angani ambao ni walinzi wa walokole,maana wanalinda watoto,wanalinda wagonjwa,wanalinda walokole na wasiokua walokole na wanazuia majanga ya kutengenezwa na wale watu warefu wa baharini na washirika wao ambao ni wachawi na wanajimu na waganga na washirikina wa kibinadamu.Popote pale duniani kwenye ulimwengu wa kiroho utawaona wanaruka huko na huko.
Afu mungu wa walokole ambae ni mkuu wa mfumo wa anga kuu nje ya mfumo wa sayari za ulimwengu kaficha siri ya mfumo wa ulimwengu nje ya mfumo wa anga na sayari zote,,maana angani ni kama mfumo wa anga na sayari unaelea ila huwezi jua umejishikiza wapi.
Hesabu za kinajimu zina kikomo ila hesabu za unajimu wa nje ya mfumo wa ulimwengu hazina kikomo na zinaongozwa na mwana wa mmliki.Na ndio maaana huyo mwana wa mmliki na wale watu warefu weupe wanaishi milele toka dahari ya kwanza mpaka dahari isiyo na ukomo kwa kingereza wanaita""Eternity's""".
Walokole wanaposali ndio mda mzuri wa kua nao sababu mungu wao anashuka kwa njia kuu tatu(3)
MOJA :Kama njiwa mweupe wa dhahabu
MBILI :Kama moto wa mataji ya viduara na kukaa vichwani mwa walokole
TATU :Kama wingu za moto unafunika eneo zima.
Sasa kama walokole wakiwa wanasali na wewe upo karibu basi baraka zao kiroho zinakufikia mpaka wewe.Mungu wa walokole hana ubaguzi katika kutoa baraka kwa bunadamu,ni kama anatusubiri tumjue atubariki.Lakini pamoja na upole wake,huyu mungu wa walokole ana mzaha pale unapotaka kudhuru walokole wake na haoni hasara kukuua kwa pumzi yake ya moto.Anawapenda walokole wake kuliko kitu kingine chochote.
NITAENDELEA..... ....!!!!