Mvua kubwa Dar usiku huu kuamkia 20 Jan 2024. Je maeneo yenu kuna maafa?

Mvua kubwa Dar usiku huu kuamkia 20 Jan 2024. Je maeneo yenu kuna maafa?

Wananzengo,
usiku saa 9 nimejikuta navamiwa na wanangu chumbani, wanaogopa radi kabambe zinazopiga sambaba na mvua hii kubwa yenye upepo wa kuhamisha milima.

Soon kunakucha.

Tujuzane endapo kuna maafa maeneo yenu. Lengo ni kupashana taarifa. Tupia picha .

Nawalinda wanangu hapa wasipigwe na ngurumo ya radi.[emoji3][emoji3][emoji3]..... yaani kha! Wanaogopa sana lile libombastic sound baada ya radi kumulika.

Tanesco aibu sana kwa haya mnayotufanyia.
Yani ndio nimeamka muda huu nikidhani ni alfajiri kumbe ni saa mbili kasoro

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi ni muoga wa radi kuliko kitu chochote ilikua radi zikianza usingizi unakata mazima ntatoa macho mpaka ziishe. Sasa nikanunua ear plugs ambazo kukiwa na radi nazipachika masikioni zinakata sauti sisikii chochote! Balaa lake ni kwamba unalala usingizi kama mfu yaani husikii chochote hata nyumba ikiungua we lazima utafia humo 🙁
Aisee mimi pia ni mhanga wa hili jambo zamani kidogo niliwahi shuhudia rafiki yetu akifariki kwa radi... tangu hapo mimi na radi hatuendani kabisa
 
Mikoani Radi zinapiga za nguvu sana kupita huko mjini.
Naiogopa sana Radi maana kukuondoa ni dk.0 tu
Huko zinawasaidia EarthWire nadhani.
Huku vijijini ni chache sana
Wakati nipo High school Bukoba Kagera kuna mwanafunzi wa shule ya msingi inaitwa Kabugalo alikuwa darasa la nne alikufa kwa kupigwa na radi.

Alitoka darasani na mwamvuli kwenda kumpelekea mwalimu aliyepo kwenye gari ili waje naye darasani asinyeshewe na mvua.

Mvua ilikuwa inapiga vibaya mno na radi za kule Bukoba zinapiga vibaya mno na kumulika mithili ya vimulimuli...

Aiseeeee!! Yule Mwanafunzi anatoka tu nje, iliwaka radi akapigwa na radi akaanguka chini.

Baada ya mvua kuisha kwenda kumcheki amekaushwa na kuwa mweusi tii. Hakuruhusiwa mtu yeyote kumgusa hadi ambulance ilivyokuja kumchukua kumpeleka mochwari.

Niliishi kwa wasiwasi sana hadi nilipomaliza masomo maana mvua za Bukoba ni 24/7 na radi zake zinapiga hadi unaona ule mstari mweupe unatua chini..
 
Sijawahi kuogopa radi za Dar mpaka nilipofika mkoa fedenge ilipiga nikajikuta uvunguni aroo nilijua bati limetoka lote. Ile ilikua sio radi bwana vigagula wanatoa na dedication humohumo wanaongezea mlio
Radi za Rukwa, Tabora, Kigoma, mtwara,Kagera na Ruvuma ni balaa..

Mimi wakati nipo Bukoba nilikuwa naogopa sana, Yani radi ikipiga ule mstari mweupe wa radi unaokuwa zig-zag [emoji298] unauona mbele yako na mwanga ule wa kimulimuli mweupe unaingia hadi ndani utadhani taa imewashwa ...

Baada ya hapo inapiga ngurumo moja unahisi ngoma ya sikio inataka kupasuka..[emoji1]
 
Back
Top Bottom