Mwalimu amchapa mwanafunzi na kumuumiza shule ya Msingi Kinondoni, Walimu mmelogwa?

Waalimu hawajielewi,mimi binafsi nimewaambia walimu wengi tu,waache kuadhibu wanafunzi kwa adhabu zisizo na manufaa.Hawajielewi.
 
Halafu mtoto anachapwa hadi kufikia hatua hiyo walimu wengine wanakuwa wako wapi? Na kama mhusika ni mwalimu mkuu anajifanya ana mammlaka, kwa nini wasimchape makofi na kumripoti kwenye mamlaka za juu ili na huo ukuu wake unyofolewe kabisa?
Possibly inabidi tuweke kanuni kwamba inapotokea mtoto amechapwa shukeni kwa mtindo huu, WALIMU WOTE WALIOKUWEPO SHULENI SIKU HIYO, WAWAJIBIKE KATIKA KIWANGO SAWA NA CHA MCHAPAJI
 
Basii aqwaahi ona matako ya babazaooo .dah Pugu sec alikuwwepo.mwamba anajiita mabagala sura nyeusi yaan bila kupiga ovyo aridhiliki baba yule ila ndie liechangia tukaiona udsm wallahi na kujua jinsi y kuishi na watu
Mabagala alikuwa hachapi, ulikuwa ni mkwara tu wa mdomoni na kutembea huku akiwa ameshika fimbo mkononi.
Namkumbuka sana niliwahi kumuuzia sponge yangu ya kulalia nilipomaliza F6, ilikuwa na viwango aliipenda!
 
Huyo haujui ualimu ,mimi natamani kumpiga mpaka Mkuu wa shule,

My life is not your life, mind your own business
Kwenye shule kama hizi, mimi naweza kujeruhi walimu wapumbavu halafu nikapata matatizo. Hasa hao miamba wanaojiita wakuu wa shule.

Huu upumbavu mimi ulishanikifu milele tangu nasoma O-level, na mtu wa kwanza kabisa mimi kuwahi kumchukia katika maisha yangu, nilimchukia kwa sababu ya upumbavu huu
 
Sio wiki sku tatu tuu zinamtosha kujua jinsi ilivyo kazi kufundisha watoto wa mlo mmoja Kwa sku
Si siku tatu , akikaa masaa matatu tu atakuwa amenyoosha mikono juu na kuacha kabisa kuwalaumu walimu milele.
 
Dawa ni kususa tu , walimu waitishe miikutano waulize akina nani wanaruhusu watoto wao wachapwe wale ambao hawataki waache kuwachapa mwisho yapimwe matokeo nina uhakika wale wanaochapwa watakuwa na alama bora kuliko hawa wasiochapwa.

Tusilete uzungu Africa katika hili la fimbo lazima tujadili upya kabisa ,wachapwe kwa standard zinazotakiwa , afu wazazi mbona wanawachapa watoto hadi na mafyekeo kabisa ila wanaona sawa tu?

Walimu Mungu atawalipa mwenyewe
 
Wewe ni mwalimu?
 
Mkuu wa shule ameambiwa ufaulu usipovuka 90% anapigwa chini unategemea awe mlendamlenda? Atakushughulikia ipasavyo tu kama unahisi mwanao anaonewa kaa naye nyumbani mfundishe mwenyewe , usiingie mashuleni atapigwa tu bara bara.

Unamwita mwl mpumbavu afu unatamani umpige , hiyo kanuni ya kumpiga mpumbavu umeitoa wapi?

Kama unavyotamani umpige mwl unayedai ni mpumbavu ndivyo anavyoshindwa kuvumilia kutokumpiga mwanao mpumbavu+
 
Kwa uandishi huu waanza kwanza na wewe kukupima UTI
 
Wewe ni mwalimu acha uongo na ualimu ni wito sio vita kwa watoto,
Unataka upewe ahsante kwani hulipwi mshahara? Kila kada ikitaka ahsante tutafika kweli?
 
Waalim wana stress, hawako sawa, pesa haitoshi
Waache kazi wakatafute kwenye pesa nyingi, yanini kuishi kwa majuto ya kazi yako mwenyewe.
Na haya mambo ni kwa shule za serikali tu, sijawahi sikia shule za privates huo ujinga
 
Tatizo tunaloongelea hapa siyo kuchapa watoto bali NI AINA YA UCHAPAJI. Watoto si wanachapwa tu kila mahali, hata nyumbani kwako wewe huwa unawachapa watoto wako? Hapa tunachoongelra ni AINA YA UCHAPAJI na si uchapaji. Kweli ni lazima watoto wachapwe viboko, hata mimi mwenyewe huwa siwacheleweshi ISIPOKUWA KANUNI YA UCHAPAJI LAZIMA IFUATWE. Kanuni za uchapaji zinapokiukwa, wanaokiuka wanakuwa ni wapumbavu
 
Yeah, Selemani alikua ana bakora zake hivi [emoji1787], alafu kama anasinzia , masalu namkumbuka yule. Walikuepo wengine pia Mwl Rose, Katakula (Mkuu) Mwl Mpapi, Nyanusi etc
Emu ngoja kwanza huyu Katakula ndio yule aliyekua anaishi Ipuli? Mshua mmoja wa kujipenda.
 
Sio hivi hivi wana shida ya utimamu wa akili jamani. Yaani mwenzio kachafua hali ya hewa hana wiki na wewe unaenda kurudia yale yale
This is unusual, usikute kuna ujumbe ambao walimu wanataka kuufikisha lkn bado wang'amuzi wa mambo bado kung'amua....na huenda wanaendelea hadi waeleweke!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…