Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Hakuna kipengele kinachozungumzia uuzwaji wa Bandari, na hakuna mkataba wowote ulioingiwa

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Hakuna kipengele kinachozungumzia uuzwaji wa Bandari, na hakuna mkataba wowote ulioingiwa

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Eliezer Feleshi atoa maneno mazito mjadala wa DP World

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Dkt. Eliezer Feleshi, amejitosa kwenye mjadala wa uwekezaji wa kampuni ya Dubai ya DP World unaotarajiwa kufanywa kwenye bandari ya Dar es Salaam kwa kusema kuwa kuna upotoshaji mkubwa usio na tija katika mjadala huo.

Akizungumza kwa mara ya kwanza katika mahojiano maalumu ofisini kwake Dodoma, Jaji Feleshi amesema kuwa upotoshaji huo unaweza kuifanya Tanzania ionekane kama inabagua wawekezaji kutoka nchi fulani.

"Mtu anasema mkataba ni wa miaka 100 na hiyo ilikuja hata kabla Bunge halijaazimia. Wengine wanasema ni mkataba wa maisha. Unatafuta hicho kipengele cha maisha unapekua kifungu kimoja mpaka mwisho, hakuna," alisema Feleshi.

Ameonya pia kuwa lugha za kibaguzi zinazotolewa na baadhi ya watu dhidi ya wawekezaji kutoka nchi fulani zinaweza kuharibu sifa ya Tanzania kama taifa linaloongoza kuvutia watalii kwenye ukanda huu wa Afrika.

"Je sasa tunataka tujenge mazingira ya kuwatia hofu wawekezaji kwamba nchi yetu haitaki wawekezaji?" Alihoji Jaji Feleshi.

Aliongeza kuwa Tanzania imekuwa inajulikana kama nchi ambayo haifungamani na upande wowote miaka mingi na inayokaribisha wawekezaji kutoka sehemu zote duniani.

"Leo unapoanza kuona Waarabu ni kama shida, unachagua (wawekezaji watoke) wapi?" Aliongeza.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali pia amepangua upotoshaji kuwa bandari ya Dar es Salaam inauzwa kwa kusema kuwa hakuna kipengele chochote kwenye mkataba kati ya Tanzania na Dubai (intergovernmental agreement au IGA) kinachozungumzia uuzwaji wa Bandari.

"Tunaposema bandari imeuzwa, je ni kweli imeuzwa? Kile kiambatisho kimeeleza maeneo ya mahusiano kwa mujibu wa ile ibara ya 4 ni kwenye gati ngapi kati ya ngapi na hizo zinazobaki ni ngapi," alisisitiza.

Alifafanua kuwa Bunge limepitisha azimio la Ushirikiano kati ya Serikali ya Dubai na Tanzania kwenye eneo la bandari, lakini hakuna mkataba wowote ambao umesainiwa kati ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) na Kampuni ya DP World.

"Mpaka sasa TPA haijaingia makubaliano au mkataba wowote na DP World kwani muda wake haujafika," alisema.

Alikanusa upotoshaji unaonezwa na baadhi ya watu kuwa Tanzania au TPA haitaweza kujitoa katika makubaliano itakayoingia na DP World.

"Kama kuna kushindwana framework (msingi) umeshawekwa. Tangu mwanzo kwenye preamble (utangulizi wa makubaliano) imetajwa mikataba itakayokuja kuingiwa kama HGA (host government agreement) na project agreement (mtakaba wa uendeshaji wa magati ya bandari)," alisema.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali ameongeza kuwa katika mkataba ambao TPA itasaini na DP World, mwekezaji huyo atapewa masharti mahsusi na malengo ya utendaji na endapo mwekezaji ataonesha ufanisi, ataweza kuongezewa maeneo mengine kwa mujibu wa matakwa ya serikali.

Feleshi, ambaye amewahi kuwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DDP) na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

Credit: Jambo TV
Hajajibu hata moja. Angesema ardhi gani inaongelewa? Bandari ipi? Vipi kuhusu air space? Angefafanua je ni miaka mingapi iliyotajwa?
 
An intergovernmental agreement (IGA) is any agreement that involves or is made between two or more governments in cooperation to solve problems of mutual concern. Intergovernmental agreements can be made between or among a broad range of governmental or quasi-governmental entities. Governments use IGAs for cooperative planning, development review, resource sharing, joint planning commissions, building inspection services, and more.
Mkuu barua ya uchumba ikikubaliwa inakupeleka kwenye posa, hadi katika hatua hiyo hakuna mme wala mke halali hapo. Bunge lilipewa nafasi ya kusoma na kupitia barua ya uchumba- azimio lao linaruhusu sasa majadiliano kuanza na kuzaa mikataba mahususi kwa jambo mahususi. Rudisha akili zako kutoka kwa wapotoshaji
Mbona huku binafsi nilishapita siku nyingi sana; kuna lipi jipya tena la kuelezwa amablo silijui.

Unachoniambia hapa ni kwamba hiyo "barua ya uchumba" hata ikiwa na matakataka mengi siyo neno?

Unakwenda kuchumbia, hapo hapo unaonyesha dalili zote za kuwa mme katili kwa huyo mchumba wako, utafanikiwa kweli?

Hao wazazi wenyewe watakuwa na upungufu mkubwa, kwa kudhani tu kwamba kwa kuwa "posa" inaletwa na mtu mwenye ukwasi mkubwa, hayo mapungufu yanayojionyesha kwenye barua ya "uchumba" siyo neno. Yapuuze tu?

Hao wazazi zitakuwa haziwatoshi kichwani, na huyo binti yao hawamthamini kabisa.
 
ACHANA NA NDOTO ZA NATIONALISM EAT YOUR PRIDE
hakuna kitu kama hicho.
Watu kama nyinyi kwenye jamii tunajua hamkosekani. Hii ni kawaida ya nyakati zote tokea enzi za utumwa hadi leo hii.

Watu mnaodhani utu wenu ni chini ya thamani ya hayo makombo mnayotupiwa chini.

Baadhi yetu hatuyakubali hayo; na tutaendelea kupoambana.

Na kama bado huelewi, hakuna mahali popote duniani, mapambano ya wenye kulinda hadhi ya utu wao iliposhindwa kufanikiwa.
 
Alitakiwa atoe ufafanuzi mwanzoni kabisa sasa kasubiri bajeti ipite ndiyo anaelezea. Nimemuona hapa kwenye newz domo zito km uji mmbichi.
 
Hiyo hatua haijafikiwa ikifikiwa tahadhari zipo kwa mjibu wa sheria za Tanzania
Nenda kawadanganye wapumbavu.
Watu kama wewe hapa uwepo huko TPA utakuwa na akili tena za kusaini chochote chenye maslahi ya Tanzania, tena makubaliano mtakayofanyia gizani?
 
Mambo yakijadiliwa kisheria watu wanasema hawaelewi
Watu wanataka mambo mazito kwa hoja nyepesi nyepesi maana ndio zinavutia
 
Anafanya watu wajinga! Hakuna mtu anapinga uhalali watu wanahoji na kushauri marekebisho wa vipengele vya MOU ili isije kutuletea matatizo kwenye mkataba huko baadae.
Huyu mwanasheria ni mkuu ndumilakuwili!..

Hivi anafanya watanzania ni mbumbumbu na mataahira kiasi hatuelewi nini Maana ya MoU!?

Hivi vipengele hakuna nchi inawezakubali kusaini huu ujinga zaidi ya Tanganyika tu!!!👇👇👇👇

So sad!!!👇👇👇
 

Attachments

  • Screenshot_20230621-201611.png
    Screenshot_20230621-201611.png
    37.2 KB · Views: 3
  • Screenshot_20230621-201742.png
    Screenshot_20230621-201742.png
    37.1 KB · Views: 3
  • Screenshot_20230621-201509.png
    Screenshot_20230621-201509.png
    39.5 KB · Views: 3
Hiv mwanasheria wetu mbna unatuchnganya, kwanza unagombeza ama unatueleimisha maana naona kama vile mm sikuelew kabisa Kwa sababu insu nzima ulitakiwa kuongelea mafanikio ya bandari ama hasala ya bandali kutokana na Sheria yako ama uwanasheria wako lakin hapa unategemea upande mmoja ambao ni upande WA mkataba WA maisha na lakin hujazungumzia upande WA mkataba WA miaka 100 WHY???
 
Mahakama ndiyo sehemu sahihi; wameshaenda tayari wataeewana huko
Mahakama za bongo hazitoshi kwani zinapokea maelekezo kutoka serikalini. Mashauri mengine hayana budi kufunguliwa mahakama za kikanda ambazo ziko huru zaidi.
 
Na usomi wake amekosa hata namna ya kujibu hoja tata, akaishia kunanga kama mswahili.
Dah! Labda ndio namna alivyoona ya kumridhisha 'mwajiri' wake.
 
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Eliezer Feleshi atoa maneno mazito mjadala wa DP World

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Dkt. Eliezer Feleshi, amejitosa kwenye mjadala wa uwekezaji wa kampuni ya Dubai ya DP World unaotarajiwa kufanywa kwenye bandari ya Dar es Salaam kwa kusema kuwa kuna upotoshaji mkubwa usio na tija katika mjadala huo.

Akizungumza kwa mara ya kwanza katika mahojiano maalumu ofisini kwake Dodoma, Jaji Feleshi amesema kuwa upotoshaji huo unaweza kuifanya Tanzania ionekane kama inabagua wawekezaji kutoka nchi fulani.

"Mtu anasema mkataba ni wa miaka 100 na hiyo ilikuja hata kabla Bunge halijaazimia. Wengine wanasema ni mkataba wa maisha. Unatafuta hicho kipengele cha maisha unapekua kifungu kimoja mpaka mwisho, hakuna," alisema Feleshi.

Ameonya pia kuwa lugha za kibaguzi zinazotolewa na baadhi ya watu dhidi ya wawekezaji kutoka nchi fulani zinaweza kuharibu sifa ya Tanzania kama taifa linaloongoza kuvutia watalii kwenye ukanda huu wa Afrika.

"Je sasa tunataka tujenge mazingira ya kuwatia hofu wawekezaji kwamba nchi yetu haitaki wawekezaji?" Alihoji Jaji Feleshi.

Aliongeza kuwa Tanzania imekuwa inajulikana kama nchi ambayo haifungamani na upande wowote miaka mingi na inayokaribisha wawekezaji kutoka sehemu zote duniani.

"Leo unapoanza kuona Waarabu ni kama shida, unachagua (wawekezaji watoke) wapi?" Aliongeza.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali pia amepangua upotoshaji kuwa bandari ya Dar es Salaam inauzwa kwa kusema kuwa hakuna kipengele chochote kwenye mkataba kati ya Tanzania na Dubai (intergovernmental agreement au IGA) kinachozungumzia uuzwaji wa Bandari.

"Tunaposema bandari imeuzwa, je ni kweli imeuzwa? Kile kiambatisho kimeeleza maeneo ya mahusiano kwa mujibu wa ile ibara ya 4 ni kwenye gati ngapi kati ya ngapi na hizo zinazobaki ni ngapi," alisisitiza.

Alifafanua kuwa Bunge limepitisha azimio la Ushirikiano kati ya Serikali ya Dubai na Tanzania kwenye eneo la bandari, lakini hakuna mkataba wowote ambao umesainiwa kati ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) na Kampuni ya DP World.

"Mpaka sasa TPA haijaingia makubaliano au mkataba wowote na DP World kwani muda wake haujafika," alisema.

Alikanusa upotoshaji unaonezwa na baadhi ya watu kuwa Tanzania au TPA haitaweza kujitoa katika makubaliano itakayoingia na DP World.

"Kama kuna kushindwana framework (msingi) umeshawekwa. Tangu mwanzo kwenye preamble (utangulizi wa makubaliano) imetajwa mikataba itakayokuja kuingiwa kama HGA (host government agreement) na project agreement (mtakaba wa uendeshaji wa magati ya bandari)," alisema.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali ameongeza kuwa katika mkataba ambao TPA itasaini na DP World, mwekezaji huyo atapewa masharti mahsusi na malengo ya utendaji na endapo mwekezaji ataonesha ufanisi, ataweza kuongezewa maeneo mengine kwa mujibu wa matakwa ya serikali.

Feleshi, ambaye amewahi kuwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DDP) na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

Credit: Jambo TV
Hapa kajibu kitu gani?

Kama AG alipaswa kujibu Kwa kutoa ufafanuzi wa ibara kwa ibara kwa kila hoja inayolalamikiwa kwa kuuchambua mkataba wenyewe..

Cha ajabu na yeye kajibu ki - Tulia Ackson na wabunge wenzake huko bungeni..

Kwa kifupi, he's too shallow. Likely kapigwa mkwara na kuambiwa huko kimeumana, toka na toa neno na neno lake ndo hili..!!

Kama ni alama, huyu angepaswa ku - supp hii paper..
 
Walioelewa mtuambie mm sijaelewa lolote..Nilitegemea kama AG ungetambaa na ulalo wa Sheria ukichambua issues ambazo wananchi wana mashaka nazo mfano..Useme hii miaka sio milele wala sio mia ila iko hivi na vile..useme pia nchi itafaidika hivi na vile kuanzia mwaka huu mpaka huu...sasa ukianza kusema miradi inakwama kweli bandari ikiendeshwa na DP world ndio miradi haikwami??? Nchi hii dah ni ya kuhurumia sana
Hawa jamaa ni blablaa tuu.
Alikuwa wapi wakati wa mjadala bungeni?
Leo kajitokeza kisa Mbowe kaongea jana?

Halafu nani kaongea kwamba ana pinga uwekezaji??? Wasi tuchanganye.
 
Kama amelazimishwa kujitokeza hadharani kutokea ufafanuzi.Mwanasheria Mkuu hajasema Kama ofisi yake ilishiriki kwenye timu ya majadiliano ,kwa nini Mwenasheria Mkuu wa Serikali hakuhudhuria/Kuwakilishwa kwenye tukio la kusaini MOU, Bandari/ Bahati masuala ya Muungano kwa nini tunaingia mikataba bila kushirikishs Tanzania Zanzibar, halafu tunajinasibu kuwa tutadumisha Muungano. Hamza Johari hayupo kwenye daftari la Mawakili wa Serikali, kanuni zinaruhusu kutoa legal opine,etc.Watanzania hawana Shida na ubinafusishaji au ukodishaji wa bandari zetu.Lakini Serikali ichukue tahadhari kuepusha migogoro siku za usoni,tumepigwa sana na Ticts Rights wa India (TRC),SAA(ATCL) nk
 
Mbowe ana nguvu sana kuongea kidogo , mwanasheria katoka mafichoni ...hata ivyo aje afafanue kwa nini mkataba una sahihi ya wapemba watatu
Hili nalo neno, maana hakuna sahihi hata moja ya mtanganyika........tukisema wamefanya conspiracy kujitajirisha kwa hila kwenye rasilimali za watanganyika tutakuwa tumekosea!!?
 
Ubaya hamko makini na madai yenu, watu wanasema wanapinga Makubaliano na wakatangaza kuandamana ila hakuna aliyejitokeza kuandamana.
Ukiwambia wanakasirika na kutoa matusi.


Binafsi naunga mkono uwekezaji wa Mwarabu
 
Back
Top Bottom