Mwenge wa Uhuru upo kwa faida ya nani?
Itafutwe Tu Namna Ya Kuuenzi Huu Mwenge Na Si Hii Tulonayo.

Mwenge Ufungue Miradi Hata Ukiwa Dar Then Mwaka Unaofuata Arusha, Kigoma Na Kwingineko.

Lengo Ufungue Miradi Sio Lazma Ukimbizwe Nchi Nzima, Unaweza Tu Kuazimishwa Hapa Kisha Kule Wakafungua Miradi.
 

kama umezaliwa Kinondoni, ukakulia kinondoni umesomea Bunge, sekondari mzizima chuo IFM kazi umepata crdb tawi la millenium tower

wikiend bata mlimani city sijui bahari beach kamwe huwezi jua thamani ya Mwenge

mwenge tuulize sie tunaokaa wilayani Namtumbo

Kwa miaka kumi ya utawala wa JK kitu ambacho kimem boost sana JK angalau kuna sehemu ambazo ameonekana kafanya kazi ni MWENGE

kwa sababu mwenge unaharakisha sana miradi VIJIJINI ... mkisikia mradi fulani MWENGE unakuja kufungua utawaona ma dc, ded, na viongozi wa halmashauri na wilaya wanavyokimbizana kufanikisha mradi ule ili mwenge unavyokuja kufungua uwe tayari umekamilika

atlest viongozi walikuwa wanazionea haya pesa za miradi ambayo mwenge ulikuwa unakuja kuzindua


SOMWENGE UWEPO MIAKA 1000 na rais Magufuli aupe sana nguvu huu mwenge
Lakin kiujumla kwa sasa mwenge hauna faida mwana namtumbo mwenzangu, iz9 ulizomention hapo ni faida za zaman
 
Mwenge uhifadhiwe makumbusho ya taifa.Haina umuhimu wowote,tusidanganyane.
 
kwani mkuu hiyo miradi lazima izunduliwe na mwenge?! hatuwezi kufanya na kuzindua miradi mpaka mwenge ufike?
Ulishawahi kufikiria kwani nini mkuu wa Wilaya, Mkoa, Waziri ama Rais anazindua mradi?
 
Nikuulize wewe unayesema umeishi Namtumbo, Ruvuma.....hivi hapo Namtumbo ukiwa na milioni 2, wewe binafsi hakuna mradi unaweza ukafanya?! Milioni 2 mkoani, tena Namtumbo ambaye nimepata kukaa, ni pesa ndefu mno, mno😱
Unaongelea mradi wa kuuza vitumbua au mradi gani?
 
Walikuja has shule niliyopo etc kuzindua mizinga ya nyuki kumi tu hahahahaaaaa
 
Itafutwe Tu Namna Ya Kuuenzi Huu Mwenge Na Si Hii Tulonayo.

Mwenge Ufungue Miradi Hata Ukiwa Dar Then Mwaka Unaofuata Arusha, Kigoma Na Kwingineko.

Lengo Ufungue Miradi Sio Lazma Ukimbizwe Nchi Nzima, Unaweza Tu Kuazimishwa Hapa Kisha Kule Wakafungua Miradi.
Sasa huo Mwenge utafunguaje miradi bila kuzunguka/ kukimbizwa?
 
Sasa huo Mwenge utafunguaje miradi bila kuzunguka/ kukimbizwa?
Kuwe Na Mwenge Wa Mkoa Mkuu Au Hata Huu Mmoja Uazimishwe May Be Arusha Kisha Miradi Yote Tz Hufunguliwa Na Wakuu Wa Mikoa Au Wengineo.
 
Mwenge ukimbizwe dadoma tu inatosha mikoa mingine wakitaka kuuona waangalie taarifa za habar.
 
Ifutwe tu!mwenge inatiaa hasara tu,inaongeza magonjwa tu ikiwemo ukimwi,wakati wa mbio za mwenge watu wanachapana hadi kupeana mimba na kufanya watoto wanaozaliwa kutowafahamu baba zaoo
Tupaaa kule mwenge
 
Mwenge ukimbizwe dadoma tu inatosha mikoa mingine wakitaka kuuona waangalie taarifa za habar.

Uwashwe na kuzimwa kulekule kileleni kwani kuna Shida yoyote si unamulika mipaka kisha unapumzika me naona mwenge usisumbuliwe tens uwake tuu kule kule kileleni tu
 
Uwashwe na kuzimwa kulekule kileleni kwani kuna Shida yoyote si unamulika mipaka kisha unapumzika me naona mwenge usisumbuliwe tens uwake tuu kule kule kileleni tu
Hapana mkuu, barafu itaisha...dom ndio pazuri, mji mkuu wa nchi yetu[emoji2]
 
Hapana mkuu, barafu itaisha...dom ndio pazuri, mji mkuu wa nchi yetu[emoji2]


Ukiwaruhusu waushushe tu basi tayari Ni jipu njia Ni makomandoo wawili wapande na kiberiti wauwashe Kwa dk mbili ili Barafu isiyeyuke kisha wauzime tu ahahahahahahhaha no more mbwembwe
 
Kuwe Na Mwenge Wa Mkoa Mkuu Au Hata Huu Mmoja Uazimishwe May Be Arusha Kisha Miradi Yote Tz Hufunguliwa Na Wakuu Wa Mikoa Au Wengineo.
Kwanza unafahamu dhana ya Mwenge? Ukifahamu dhana ya Mwenge basi haiwezekani kabisa kufanyika hivyo unavyodhani.

Pili, huu ni Mwenge wa Uhuru hivyo haiwezekani kuwa na Mwenge wa mkoa.

Tatu, Kwa taarifa yako Mwenge ni zaidi ya huyo mkuu wa mkoa, hivyo Mwenge hauwezi kuzindua mradi halafu mkuu wa mkoa atie kidole chake pale,
Mwisho, hauzimishwi ila unakimbizwa. Asante.
 
sio mwaka huu tu, bali kusiwe na mbio za mwenge kabisaaa, mbio za mwenge ni katika matumizi makubwa yasiyo na maana kabisa, nini maana halisi ya kukimbiza mwenge baada 45 ya uhuru na hali duni ya maisha. Hivyo vijisenti ya kugharamia mbio za mwenge si zingetumika kujenga maabara na kuziequip fully katika mshule ya msingi na sekondari. Kukimbiza mwenge 1962 na sana sana 1963 kulimake sense, baada ya hapo ni ufujaji tu.

hili nalo jipu linahitaji kutumbuliwa...hakika mzee magu angeanza na hilo kwanza maana mm binfsi sijaona faida za huo mwenge zaidi ya ufujaji tu wa pesa za wananchi walipa kodi..
 
hili nalo jipu linahitaji kutumbuliwa...hakika mzee magu angeanza na hilo kwanza maana mm binfsi sijaona faida za huo mwenge zaidi ya ufujaji tu wa pesa za wananchi walipa kodi..
Ni kiasi gani cha fedha kinafujwa?
 
Back
Top Bottom