My week end is super crazy

My week end is super crazy

Siwezi kuwarudisha hadi wazazi wao warudi,wamesafiri nje ya Tz na mimi mwenyewe ndo nilisema waletwe kwangu coz navipenda ila nimejua hawa inabidi mapenz ya mbalimbal,wakichukuliwa sitarudia tena kuvichukua
.
Poleee dear,
 
My week end is wacko.

Kuna watoto wazuri wa rafiki yangu watakaa na mimi mpaka katikati ya Nov. ila sijui nisemeje nisionekane wicked aunty ila wamekuja J nne na tayari niko super stressed na Nov. naiona mbali sana

Stress zilianzia kwa jinsi mtoto wangu hataki ku share Tv yake na wenzie sbb wenzie ni wadogo na vitu wanavyopenda kuangalia ni tofauti.

Nikatoa amri waangalie kwa kupokezana ila haikusaidia watoto coz bado hao madogo wageni mmoja wa kike wawili wa kiume.Vitu anavyopenda kuangalia wa kike hivi vijamaa viwili havipendi fulu kugombana.

Yaani ni mashitaka kila dakika.Huyu wa kwangu analalamika madogo wanaharibu vitu chumbani kwake na madogo wanalalamika kaka anawapiga na kuwafukuza chumbani kwake wasiangalie Tv.

Nikasema hizi stress zitaisha kila mtoto akiwa na tv chumbani kwake,nikatuma mtu akaninunulie Tv ndogo 4,zikaja zikafungwa kila mtu akafurahi nami nikasema nitapumua sasa ila nimejidanganya😃😃.eti baada ya kila mtu kupata Tv yake na interest ya kuangalia Tv ikaisha.Yaani madogo hawana muda na hizo Tv.Hela zangu zimepotea bure😭😭.

Hao wawili wa kiume ni mapacha wako very smart ila ni WATUNDU sana.Wamekaa siku mbili tu ila wameshaharibu vitu vingi halafu sasa vikiharibu kitu ukifoka unasikia “aunty you don’t look cute when you are angry” au “my daddy will buy you another one”

Leo asubuhi hivi vi twins vimefanya kitu cha hatari sana nikawatisha kuwa leo nawachapeni,nikaagiza niletewe fimbo mbili kubwa.Kumbe watoto wa watu hawajawaji kuchapwa wala kutishiwa fimbo.Kale ka kike kananiambia “aunty ukiwachapa baba yangu atakuchapa na wewe maana baba kasema mama akituchapa atamchapa na yeye” nikamwambia mimi simuogopi baba yako na fimbo zikija nawachapa kaka zako.

Fimbo zimefika ile watoto wanaziona tu waliteteeka hadi kamoja kakajikojolea na kengine kakatapika kwa panic.Nilishangaa sana maana mie wa kwngu keshakula sana mikwqju.Sasa nikajiuliza hata shule havichapwi hadi vitetemeke vile!

Ikabidi niache mkwara nianze kuvibembeleza na kutupa fimbo.Kale kakike kalivyoona nimetupq fimbo kakanimbia “usingenisikiliza baba yangu angekumaliza”

Huwezi kuamini hawa watoto eti kutishiwa fimbo tu wamelia zaidi ya masaa mawili.Na wanalia kwa kupokezana,huyu akinyamaza ukisema sasa wamenyamaza unashangaa mwengine kapokea .

Nimebembeleza nimechoka hadi na mim nikaingia chumbani kwangu kulia.Watoto hawa sijui baba yao uchumi ukiyumba itakuwaje coz wakitaka kitu lazima wapate la sivyo atalia siku nzima.Akitaka pizza kwa aman yako utahakikisha pizza imefika.Naona ajabu sbb mwanangu nikisema leo ni chai na kiporo cha ubwabwa kanakula.Mwanangu nikisema hata chai na ugali atakula with a smile on his face.Asubuhi ya kwanza the way vilitupelekesha ningekua na sukari ingepanda.Bodaboda walikua wanapishana getini kwetu coz kila tunachotumia sisi kwa breakfast walivikataa na kila kinacholetwa anakwambia sio hiyo ana favorite yake na lazima apate hiyo,unamrudisha boda ikija brand tofaut hali na hapo wako watatu na kila mmoja ana favorite yake.Ukisema uvikazie vitoto vya watu vitashinda njaa nafsi inakataa basi ni kuhangaika hadi kila mmoja apate anachotaka.

Hivi wazazi mnaodekeza watoto wenu faida ni ipi?

Mna upendo sana kushinda sisi wengine au?View attachment 3102518
Hongera kwa kuwajali watoto wengine, kuhusu malezi tunatofautiana kuna wengine mtoto hajawahi kuguswa kabisa hata afanye kosa gani anachukuliwa mtoto

Sisi wengine, wazazi wetu walijua kutofautisha kati ya utoto na ujinga

Haiwezekani mtoto unampa chakula anajifanya kwenda kula chumbani afu anakimwaga kisa ugali au mboga ni kitu asichopenda au unaacha hela anapita nayo

Aisee nilichezea sana mikwaju kwa ujinga ila sijawahi kuadhibiwa kisa utoto

Vitu kama umeenda kucheza unarudi mavumbi mwili mzima, hizo nilikuwa natishiwa tu kisha adhabu nayopewa ni kwenda kuoga
 
Ngojea nione nitajaribu polepole.

Hlf vikiongea na mama yao wanasema wanampenda aunty hawataki kurudi nyumbani😁 kirohon nasema mtoto hata akukasirishe vipi ni ngumu kumchukia.Hata havijui kama vinanipa stress masikin na ninataman waondoke nipumur😁
Wanyooshe wakiwa kwako wajue namna ya kuishi bila vurugu.
 
Pole Sana..yani Naelewa unachopitia sasa Mimi nashauli pia kuhusu suala la wazazi humu ndani tuzoeshe watoto wetu kwenda Shule kwa usafiri wa kawaida
Mimi ilishanikututa siku moja sitasahau na Siwezi msimulia mtu Anaenijua ni kwamba toka Mwanangu kazaliwa Alikuwa hajawahi
kupanda Dala dala mpaka Amefika Darasa la Tano
sasa Siku moja nikasema ngoja niende nae tu tupande Dala dala nilikuwa naenda kumnunulia vitu vya Shule Aisee ile tumepanda tukakuta nafasi zimejaa msongamano..jasho..kukanyagwa Aisee Alipiga kelele Dala dala nzima wananishangaa tu Sababu Alikuwa Anadai Ashuke mbona niliona Aibu Mimi toka hapo Asubuhi Alikuwa Anapelekwa na gari Shule Saa ya kuludi ni Dala dala na Nilimwambia kabisa Akae Akijua Labda tu Mvua Inyeshe Nahisi hichi kituko kuna hata wazazi kilishawatokea ila ni Aibu kusimulia kabisa.
🙏🏼🙏🏼 Asante mkuu.

Itakua mlivyoshuka watu waliwafanya mada.
Pole ila sio kosa lake masikini kwake ilikua vitu vigeni ila hongera kumfanya azoee sbb hatujui kesho yetu itakuaje.

Mimi wa kwangu keshazoea kupanda daladala.Hata mimi napandaga hasa nikiwa na mwanangu na nimemfundisha hadi kugombea siti😀Huwa namwambia we wa kiume gangamara tupate siti😀😀 na katapambana tutapata kweli siti na akija mtu mzima bila kumwambia atasimama na kumpisha na ninakua nimemlipia kukaa kama mtu mzima na kuna siku tulipanda nikamwambia sina hela ya kukulipia ukae kwa hiyo utasimama mpaka tufike na huwa hapendi kubebwa.

wa kwangu pia yuko la 5 kama wa kwako ila kwa upande wangu naona bado ni mdogo kutumia daladala akiwa peke yake kwenda shule.Mimi wa kwangu atatumia daladala kwendea shule akifika form one ila kwa sasa naona ni hatari sana
 
Mwisho wa siku ndo wanakuomba kitu unawaambia hauna, Wanajiongeza halafu mnakuja kulalamika watoto wanalawtiwa sana sikuhizi.
Ni kweli ila sio wa kwangu.
Nakubaliana na wewe hayo sio malezi wala upendo ndio maana nimelalamika.

Wa kwangu anajua hapana.
Anajua kuna siku mama hana hela na na kwamba sio kila atakachotaka atapata,anajua kuna watu wanalala
Njaa hivyo chochote kinachopikwa tunapaswa kula kwa furaha
 
KWA HIYO UKAENDA KUMNUNULIA KILA MMOJA TV YAKE 😁😂 MAISHA YA JF NITAAMBIWA SASA HIVI TAFUTA HELA
Why not mkuu?
Iam too old kusikiliza vilio na kesi za kupigana kila saa hadi niwe kama mkimbiz nyumban kwangu wakati laki 6 tu inatosha kutatua hilo tatizo
 
Akina junior hao.
Sawa pesa si zipo acha watumie.
Ila sie wengine hatujalelewa hivyo.
baba kila siku akirudi uwa anarudi na bakora ya dharura.anajua mwamba huko atakuwa kaharibu tu.
Na kweli akifika nyumbani mashitaka kwa mama wa kufikia.
Kabla ya kulala zinatembea kwanza bakora.
Kuna kitabu mpaka leo sikipendi. Kile cha "SOMA KWA HATUA"
KIMENILIZA SANA KILE
 
Honestly,nawaonea huruma sana hawa watoto.

Sijawahi ona watoto wamedekezwa kiasi hiki.
Sijui wazazi wenye haya malezi huwa wanawaza nini?
Ni ujinga kuwaendekeza watoto. Hawataweza ishi na mtu yeyote.
 
Hongera kwa kuwajali watoto wengine, kuhusu malezi tunatofautiana kuna wengine mtoto hajawahi kuguswa kabisa hata afanye kosa gani anachukuliwa mtoto

Sisi wengine, wazazi wetu walijua kutofautisha kati ya utoto na ujinga

Haiwezekani mtoto unampa chakula anajifanya kwenda kula chumbani afu anakimwaga kisa ugali au mboga ni kitu asichopenda au unaacha hela anapita nayo

Aisee nilichezea sana mikwaju kwa ujinga ila sijawahi kuadhibiwa kisa utoto

Vitu kama umeenda kucheza unarudi mavumbi mwili mzima, hizo nilikuwa natishiwa tu kisha adhabu nayopewa ni kwenda kuoga
Umeongea vyema sana mkuu.

Ila pia naamini iko haja wazazi tupate mafunzo ya malezi maana wengine wanachukulia utoto kama ugonjwa.
Wengine wakiwa na vihela kidogo wanaona sifa kulea watoto kwa style ya what the kid wants the kid gets.

Wengi hawajui mtoto ni kama empty card na vile vitu vinavyoingizwa humo mwanzoni iwe vizuri au vibaya vikishaingia humo ni vigumu kuvifuta na wengi hawajui kuwa watoto sio wajinga.Ni binadamu wanaojifunza kwa kujaribu jaribu.Akigusa moto akiungua hatakaa tena maishan mwake aguse moto.

Akikataa kula ugali ataangalia nini kitatokea.Akiambiwa ukila utakua na nguvu kama baba na usipokula nakuchapa atakula na akikataa akichapwa kweli atajua hapa nikikataa ni viboko ila kakataa ugali anataka chips huyoo mbio unaagiza apikiwe chips siku nyingine ukimkatalia atasumbia sana sbb anajua nikikataa uwezekano wa kupata ninachotaka upo.

Na wazazi tunatakiwa wote tuwe na msimamo,baba akisema hapana na mama ni hapana.Sio baba kasema leo hawa wafue nguo zao akitoka mama unawaonea huruma unawasaidia.Au mama kasema hakuna hela wakienda kwa baba wanapewa.
 
Akina junior hao.
Sawa pesa si zipo acha watumie.
Ila sie wengine hatujalelewa hivyo.
baba kila siku akirudi uwa anarudi na bakora ya dharura.anajua mwamba huko atakuwa kaharibu tu.
Na kweli akifika nyumbani mashitaka kwa mama wa kufikia.
Kabla ya kulala zinatembea kwanza bakora.
Kuna kitabu mpaka leo sikipendi. Kile cha "SOMA KWA HATUA"
KIMENILIZA SANA KILE
Kina junia ni hatari.
Wazazi wao ndio wana hizo pesa za kudekezana mimi sina hela za kutumia kuharibu mtoto wangu.

Hapo kwa SOMA KWA HATUA nimekuonea huruma.
Nadhani ulikua mzito kusoma hivyo ikawa kila ukikosea unachapwa na ukweli ni kwamba haukua mzito ila aliyekua akikufundisha alikua hajui kufundisha.Zile fimbo zilifanya ukosee zaidi
 
My week end is wacko.

Kuna watoto wazuri wa rafiki yangu watakaa na mimi mpaka katikati ya Nov. ila sijui nisemeje nisionekane wicked aunty ila wamekuja J nne na tayari niko super stressed na Nov. naiona mbali sana

Stress zilianzia kwa jinsi mtoto wangu hataki ku share Tv yake na wenzie sbb wenzie ni wadogo na vitu wanavyopenda kuangalia ni tofauti.

Nikatoa amri waangalie kwa kupokezana ila haikusaidia watoto coz bado hao madogo wageni mmoja wa kike wawili wa kiume.Vitu anavyopenda kuangalia wa kike hivi vijamaa viwili havipendi fulu kugombana.

Yaani ni mashitaka kila dakika.Huyu wa kwangu analalamika madogo wanaharibu vitu chumbani kwake na madogo wanalalamika kaka anawapiga na kuwafukuza chumbani kwake wasiangalie Tv.

Nikasema hizi stress zitaisha kila mtoto akiwa na tv chumbani kwake,nikatuma mtu akaninunulie Tv ndogo 4,zikaja zikafungwa kila mtu akafurahi nami nikasema nitapumua sasa ila nimejidanganya😃😃.eti baada ya kila mtu kupata Tv yake na interest ya kuangalia Tv ikaisha.Yaani madogo hawana muda na hizo Tv.Hela zangu zimepotea bure😭😭.

Hao wawili wa kiume ni mapacha wako very smart ila ni WATUNDU sana.Wamekaa siku mbili tu ila wameshaharibu vitu vingi halafu sasa vikiharibu kitu ukifoka unasikia “aunty you don’t look cute when you are angry” au “my daddy will buy you another one”

Leo asubuhi hivi vi twins vimefanya kitu cha hatari sana nikawatisha kuwa leo nawachapeni,nikaagiza niletewe fimbo mbili kubwa.Kumbe watoto wa watu hawajawaji kuchapwa wala kutishiwa fimbo.Kale ka kike kananiambia “aunty ukiwachapa baba yangu atakuchapa na wewe maana baba kasema mama akituchapa atamchapa na yeye” nikamwambia mimi simuogopi baba yako na fimbo zikija nawachapa kaka zako.

Fimbo zimefika ile watoto wanaziona tu waliteteeka hadi kamoja kakajikojolea na kengine kakatapika kwa panic.Nilishangaa sana maana mie wa kwngu keshakula sana mikwqju.Sasa nikajiuliza hata shule havichapwi hadi vitetemeke vile!

Ikabidi niache mkwara nianze kuvibembeleza na kutupa fimbo.Kale kakike kalivyoona nimetupq fimbo kakanimbia “usingenisikiliza baba yangu angekumaliza”

Huwezi kuamini hawa watoto eti kutishiwa fimbo tu wamelia zaidi ya masaa mawili.Na wanalia kwa kupokezana,huyu akinyamaza ukisema sasa wamenyamaza unashangaa mwengine kapokea .

Nimebembeleza nimechoka hadi na mim nikaingia chumbani kwangu kulia.Watoto hawa sijui baba yao uchumi ukiyumba itakuwaje coz wakitaka kitu lazima wapate la sivyo atalia siku nzima.Akitaka pizza kwa aman yako utahakikisha pizza imefika.Naona ajabu sbb mwanangu nikisema leo ni chai na kiporo cha ubwabwa kanakula.Mwanangu nikisema hata chai na ugali atakula with a smile on his face.Asubuhi ya kwanza the way vilitupelekesha ningekua na sukari ingepanda.Bodaboda walikua wanapishana getini kwetu coz kila tunachotumia sisi kwa breakfast walivikataa na kila kinacholetwa anakwambia sio hiyo ana favorite yake na lazima apate hiyo,unamrudisha boda ikija brand tofaut hali na hapo wako watatu na kila mmoja ana favorite yake.Ukisema uvikazie vitoto vya watu vitashinda njaa nafsi inakataa basi ni kuhangaika hadi kila mmoja apate anachotaka.

Hivi wazazi mnaodekeza watoto wenu faida ni ipi?

Mna upendo sana kushinda sisi wengine au?View attachment 3102518
Kosa lako la kwanza,hukuuliza hawa watoto wanapendelea nini kwao hizi taarifa unapata Kwa wazazi wake.
Pili ulifanya kosa sana kununua hizo tv kwakua zinawndeleza ubinafsi Kwa mtoto wako na hao wageni,ilitakiwa uwakalishe na kuwaelimisha suala la umoja and team work,wapeleke nje wakakate majani ya bustani mkiwa wote,osha vyombo nao as team.
Tatu,unaingia gharama bila kua mbunifu as long as unawaridhisha wote,all this are wrong and hata mwanao atakua na tabia ya Umimi and mother only.
Change unavyomlea mwanao mtoe nje acheze na wenzie aweze soma mazingira tofauti.
 
Kuna watu wana malezi utadhani wa na guarantee ya kuishi miaka 100 na kuwa na uchumi mkubwa hadi wafe.

Hayo ni malezi mabovu sana, mtu anayejitambua hawezi kuruhusu.
 
Back
Top Bottom