Mzee Makamba: Watu wazuri huwa hawafi ndio sababu Kinana yupo na Jakaya yupo!

Mzee Makamba: Watu wazuri huwa hawafi ndio sababu Kinana yupo na Jakaya yupo!

Mzee Makamba amesema Wanaccm Wana Iman kubwa sana na Rais Samia na 2025 atashinda kwa kishindo

Mzee Makamba ametaka CCM kupitisha Azimio la kumpitisha Rais Samia kuwa mgombea Urais pekee kea ticket ya CCM 2025

Makamba amesema hakuna haja ya kuogopa kwani Watu wazuri na wanaopendwa hawafi ndio sababu mzee Kinana yupo na mzee Jakaya yupo

Makamba amesema Wapinzani akina Chadema ajenda zao ni 2 tu Katiba mpya na Tume Huru ya Uchaguzi lakini Wananchi hawali Katiba. Kule kwetu kwa mfano Wananchi wanataka Maji, Umeme, Huduma Bora za Afya na Elimu ambazo zimo kwenye ilani ya CCM hivyo Wapinzani wasahau kabisa habari ya Ushindi 2025

Hata hivyo Rais Samia amesema Mzee Makamba ameteleza tu ulimi kwa Kauli hiyo ya kwamba Watu wazuri hawafi kutokana na kuwa emotional

Source TBC
Hivyo ule msemo wetu wa WATU WAZURI HAWADUMU ulikuwa umekosewa?
 
Magufuli wenu sikumpenda hata kidogo baada ya kuanza kuua watu hovyo na kuona upinzani ni uadui, lakini lazima nikiri kuwa watu wanafiki kama huyu ndiyo alitakiwa awafanye kitu kibaya kabisa ikibidi awapoteze. Angekuwa amewashughulikia na kuona upinzani ni washirika wake Tanzania ingekuwa mahali pazuri sana leo. Maskini hakujua kuwa maadui wake halisi ni wana CCM wenzake. Huyu mzee anawakilisha mawazo ya akina Kinana, Kikwete na wengine wengi.
Angeweza vipi kushirikiana na upunzani wakati walikua bize na mashirika ya habari yabkimataifa kumchafua?

Sera zote za upinzani bwana magufuli amezitekeleza kwa kishindo ndiyo maana walamba asali hawakumpenda..

Upunzani ulishindwa kumuelewa magufuli.. ila magufuli aliwachukua wapinzani wenye uwezo akawapa nafasi kubwa kwenye chama na hata uwaziri.. ndiyo maana hakupendwa na ccm wenzake..
 
Kwa kauli yake Mzee Makamba anamaanisha wazi kuwa mtume Mohamed kiongozi wa dini yake alikufa sababu alikuwa mbaya

Wao akiwemo yeye, Mzee Makamba, Mzee Kinana na Mzee Kikwete wako hai saba6ni wazuri kuliko marehemu mtume Mohamed
Umeenda mbali mno.....acha uchokozi
 
Mkuu kama Magufuli angekuwa kweli kama hivyo mnavyomuelezea kwamba alikuwa anauwa watu hovyo basi angekuwa keshawamaliza hawa watu maana aliwajua toka yupo hai asingewaacha walikuwa wabaya wake, labda tuseme aliona noma au kuna namna iliyomfanya ashindwe kuwauwa kama alivyokuwa anauwa hovyo hao wengine.
Taizo itikadi za upinzani zinawapoteza.. kabisa mtu unamjua adui yako ni huyu na hakutakii mema unaacha kumuua unaenda kuua mwenyekiti wa chadema wa mtaa? Hawa upinzani hawajielewi..wangejielewa na kuelewa wananchi wana akili gani muda huu, wangekua na nguvu sana
 
Angeweza vipi kushirikiana na upunzani wakati walikua bize na mashirika ya habari yabkimataifa kumchafua?

Sera zote za upinzani bwana magufuli amezitekeleza kwa kishindo ndiyo maana walamba asali hawakumpenda..

Upunzani ulishindwa kumuelewa magufuli.. ila magufuli aliwachukua wapinzani wenye uwezo akawapa nafasi kubwa kwenye chama na hata uwaziri.. ndiyo maana hakupendwa na ccm wenzake..

Magufuli ndio alianza uchokozi kwa wapinzani. Kwanza kuwapiga marufuku kufanya mikutano ya hadhara, kumbuka UKAWA walikuwa wanaandaa mikutano ya shukrani jamaa akapiga marufuku.

Pili, Magufuli akadai wapinzani ndio wamechelewesha nchi isipate maendeleo. Mbona wamekataza mikutani miaka Saba Sasa lakini mgao wa maji na umeme bado upo?.

Tatu, ni huyu Magufuli alimwambia Spika ndugai awashughlikie upinzani ndani ya bunge yeye atawashughulikia nje ya bunge.

Magufuli alitakiwa atengeneze mazingir ya yeye kufanya mambo yake na kuwaacha wapinzani wafanye yao.
 
Magufuli wenu sikumpenda hata kidogo baada ya kuanza kuua watu hovyo na kuona upinzani ni uadui, lakini lazima nikiri kuwa watu wanafiki kama huyu ndiyo alitakiwa awafanye kitu kibaya kabisa ikibidi awapoteze. Angekuwa amewashughulikia na kuona upinzani ni washirika wake Tanzania ingekuwa mahali pazuri sana leo. Maskini hakujua kuwa maadui wake halisi ni wana CCM wenzake. Huyu mzee anawakilisha mawazo ya akina Kinana, Kikwete na wengine wengi.
Magufuli huwezi mpenda ukiwa na akili ya kuvukia barabara tu.
 
Uimla ulikuwa ni tatizo, sijui tungeishia wapi yarabi, hata hujuma zake zilikuwa ni za ma trillion, hakuchukuwa kitoto!, alibeba furushi kabisa.
 
Ukisikiliza kwa makini yule mzee anamhakikishia mtukufu kuwa hatakufa
ataishi miaka mingi kama wale wazee wengine..
Nauliza kwani nani amesema atakufa!?
Yule mwingine anasema mambo labda yakiharibika sana ndio tutarajie
mabadiliko 2025, je ni ccm(cham cha mambuzi) wote wanaweza kuvumilia mpaka yaharibike sana
ili kubadilisha mtukufu au ni yeye ndiye huwa anawabadilisha watukufu
kwa hiyo anauhakika bila yeye kusema mambo yameharibika sana hakuna kitakacho badilika.
Mwisho, mambo ili yaharibike sana yanatakiwa yawaje!?
Hizi kauli za wazuri hawafi, mungu(sio Mungu) kaamua ugomvi, na wazee tulisema hapana
zina maana gani!?
Je ccm huwa kuna mungu(sio Mungu) amabaye huwa anaamua ugomvi anaamua
nani afe na nani aishi milele!?
Wazee wapi waliosema hapana enzi zile!?
Naomba majibu wakuu
Enewei wazuri wataishi milele....
 
Magufuli ndio alianza uchokozi kwa wapinzani. Kwanza kuwapiga marufuku kufanya mikutano ya hadhara, kumbuka UKAWA walikuwa wanaandaa mikutano ya shukrani jamaa akapiga marufuku.

Pili, Magufuli akadai wapinzani ndio wamechelewesha nchi isipate maendeleo. Mbona wamekataza mikutani miaka Saba Sasa lakini mgao wa maji na umeme bado upo?.

Tatu, ni huyu Magufuli alimwambia Spika ndugai awashughlikie upinzani ndani ya bunge yeye atawashughulikia nje ya bunge.

Magufuli alitakiwa atengeneze mazingir ya yeye kufanya mambo yake na kuwaacha wapinzani wafanye yao.
Wapinzani walikuwa na tabia ya kisenge ya kumchafua raisi na lengo hasa kum frastruate ili akiwajibua waseme wameonewa
 
Back
Top Bottom