Naanza kutilia shaka uwezo wa Rais Samia kuongoza Taifa

Naanza kutilia shaka uwezo wa Rais Samia kuongoza Taifa

Kama umeanza kuwa na wasiwasi naye leo basi nakupa pole mkuu, mwenziyo tangu atuambie kuwa tutaomboleza siku 14 badala ya 21 tukajua tayari fwamba.
Kuna uwezekano hajui vyama vya siasa na mikuto yote ya vyama vya siasa ni takwa la Kikatiba na sheria [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Baada ya kusikiliza interview ya Rais Samia Suluhu na Salimu Kikeke, nimegundua mambo matatu kwenye uongozi wa Samia Suluhu, aidha Rais hayuko well informed au anadanganywa/potoshwa au uwezo wake wa kutambua mambo ni mdogo...
Hana uwezo kabisa huyo Rais
 
Mahojiano ya jana yameonesha udhaifu wa huyu mama.

Yote kwa yote nimpongeze kwa kuongea, jambo ambalo limetupa fursa ya kumjua na kumkosoa.
Tofauti kabisa na mkuu Jiwe ambaye alikuwa na 'aleji' na waandishi wa habari.
Ndio maana jiwe alikuwa anaogopa kuhojiwa kwa sababu hizi hizi.
 
RAIS WETU MAMA SAMIA PIGA KAZI HUMU KUNA MAJUNGU TU YASIYO NA MSAADA WOWOTE YASOME YAPUUZE TU PIGA KAZI TURUDISHIE MZUNGUKO WA FEDHA NDANI YA NCHI KHALI NI TETE SANA RAIS WANGU WATU HAWAHEMI WALA HATUPUMUI BIASHARA HAZIZUNGUKI VYEMA PLEASE HELP THIS THINGS GOES PIA HUKU KWENYE MABAA AMBAYO NDIO YANATULIWAZA WANYONGE MSIBANE SANA MAANA ASKARI WETU WANATOLEA MACHO KWELI KWELI UKICHELEWA TU KUFUNGA NI ISSUE MH, WAZIRI SIMBACHAWENE LEGEZA HAPA KIDOGO HATA HUKO TBL KUTUNE KIDOGO NA KODI ZENU ZIONGEZEKE WAACHENI WATANZANIA WAPUMUE KIDOGO YARABI SHAMRA SHAMRA ZIRUDI UPYA.
 
Twende mbele turudi nyuma upinzani lazima ujitafakari why mnakimbilia kumsapoti mtu bila kujiridhisha?? Kuna agenda nyingi za kusimamia ambazo zingewaboost suala la tozo,chanjo then mnakuja kwny katiba sasa nyie mnajua kabisa watanzania wengi Wana mashaka na chanjo nyie kutwa kuwahimiza suala la tozo kimya
Wewe ni kitu gani kinakuambia kwamba kiongozi akiwa madarakani hatakiwi kukosolewa na wanaokosoa ni lazima wawe wapinzani? Inahitaji kupanua wigo wa uwezo wa kuchanganua ili kuwa rational.
 
Kana kwamba sisi wengine hatujaiona ile interview? Kutafuta udhaifu kwenye performance bora kabisa kutoka kwa Rais Samia ni kudhihirisha jinsi miwani yenu ilivyowekwa tinted ili kuona tu yale mnayotaka myaone. Msipoyaona au kusikia Rais kashakuwa mbovu.

Ndio, hata sisi wengine bado tunamchunguza chunguza lakini hatumtafuti kwenye mambo yake ya siasa za CCM na Chadema. Sisi tunataka kila senti ya mvuja jasho itumike kuisogeza nchi mbele basi. Hayo mengine ya siasa zenu za Mbowe mtajifix wenyewe. Nchi ya watu milioni 60 haiwezi kutekwa na kundi maslahi dogo tu la watu waitwao wanasiasa.
Get to know, hapa duniani kila kitu kinaendeshwa na siasa hata hiyo senti unayoitafuta iko controlled na siasa, mfano tozo ya uzalendo imezaliwa na siasa zetu.
 
Watanzaia Nani katuroga,mbona Kila Rais kwetu Ni mbaya na hatufai,Naamini mama yupo vizuri,Ila kwa issue ya mbowe tunasema mama HAPANA.MBOWE hana ugaidi wowote.mama samia ninakukubali Sana ipasavyo Ila busara za kuwatoa kaka zako wa UHAMSHO itumike kumtoa mbowe,mama Leo unavyomuona mbowe kuwa Ni Gaidi Basi unajikosesha imani kwa tuliokuamini.
 
Nilisoma mahali hii kesi mwanzoni ilikuwa na washtakiwa 6, DPP akawaondoa 3 wakabaki 3 ndio akaongezwa Mbowe. Sifahamu Kwa nini hili halisemwi sana, pengine kuna jambo ndani yake. Hawa watatu DPP alioamua hana nia ya kuendelea nao ndio wanaozungumziwa? Waliachiwa na DPP aliyepita au wa sasa? Kwa makubaliano gani?
Lingine nililoliona ni imani inayoendelezwa kwamba kuteua wapinzani kwenye serikali kusaidia kujenga taifa ndio suluhu. Kwamba majibu ya madai ya mabadiliko ya katiba, yatakayoleta chaguzi huru, kurudisha mamlaka kwa wananchi kuteua (na kutengua) wawakilishi wao, uhuru wa mahakama, jeshi la polisi lisiloingiliwa, kurudisha uwajibikaji wa viongozi, na mambo mengine yaendanayo na katiba inayopiganiwa, ni kuteua wapinzani kwenye serikali wasaidie kujenga nchi. Kwamba hata pale Rais atakapokutana nao, akiwaoffer vyeo mambo yatakuwa sawa. Pengine ndio maana Zanzibar wameishia kwenye serikali ya umoja wa kitaifa bila kuonekana Kwa nia ya dhati ya mabadiliko ya kweli, na mapengo yameanza onekana.
 
Thus tunataka katiba mpya.Tumpate mtu tuliyemchagua na mwenye uwezo wa kutuongoza.Na sio mtu kupewa uongozi kama zawadi.
Sijawahi ona Makamu wa raisi akawa Smart kumzidi raisi aliyepo.Kuepuka kuongozwa na wasio na sifa,raisi akifa baada ya siku 90 turudi kwenye uchaguzi Ili tupate chaguo sahihi..
Huyu mama ameshindwa mapema Sana.
 
mama na mimi anaanza kuniudhi, hivi kulikuwa na haja gani ya kuongea na vyombo vya habari kwanza?!! angekausha tu na kuwaachia wenyewe wanayotaka kuyaongea bila kuhusisha sauti yake. ukweli ni kuwa hivi vyombo vya habari lengo kuu haswa ni kutafuta madhaifu ya mtu tu na si kutangaza habari njema zake........ilipaswa alitambue hilo. hapo ameshajikoroga, hayo maneno yake mawili matatu aliyoyaongea yatachambuliwa kwa kila namna kwa muda mrefu hata wa miaka mitatu, na zile point zake muhimu zote hautozisikia zikizungumzwa hata chembe........watakomaaa kwenye tafsiri zao tu na maoni yao. kipindi ambacho hata ndani kuna wasiokutakia mema kama kina pole pole na mwenzake gwajima (sababu ya ukabila, dini na ukanda), ni kipindi cha kuchunga mno ulimi.

by the way, mazungumzo yao sijayasikiliza naishia kuona mashambulizi tu humu mtandaoni (jambo ambalo si jipya kwa wafuasi wa chama fulani hivi kwani wao kuna wanayotaka kuyasikia sasa mtu asipoyaongea tu hayo basi matusi, kejeli, vijembe n.k ndo malipo yake); ninajua athari za vyombo vya habari.hii ni fursa nzuri ya kuanzia mama, afanye mambo ya maendeleo wakati mitandao inapokuwa against nae halafu muda si mrefu utaona watapiga kelele wenyewe za kukupongeza. ilikuwa hivyo kwa magufuli, alikuwa anapondwa mno lakini akaziba masikio na kuendelea na mishe zake, mwisho wa siku leo kila mtu anampongeza. ukiona watu fulani hivi wanakusifia sifia ujue kuna mahali hapapo sawa......wamepata mwanya wa kukuchezea.
 
Get to know, hapa duniani kila kitu kinaendeshwa na siasa hata hiyo senti unayoitafuta iko controlled na siasa, mfano tozo ya uzalendo imezaliwa na siasa zetu.
Nimeisikia sana hiyo kauli "a man is a political animal" kujustify nguvu kubwa ya raslimali watu na raslimali fedha inayotumika kwenye siasa, tena za ushindani.

Nchi hii maskini wanasiasa wanalipwa marupurupu kibao utadhani ni maCEO wa billion dollar companies.

Kuna hadi ruzuku za vyama vya siasa kila mwezi katika chi ambayo kila sehemu unapopita hata mijini ni makorongo, wanafunzi wanasomea chini ya miti.

Unawezaje kuwekeza nguvu kubwa kwenye siasa za tom and jerry wakati real issues zimelala?

Leo hii kijana anamaliza chuo hata hajafanya lolote la maana kwenye jamii yake anataka kazi yake ya kwanza aende bungeni. Kisa? Kwa sababu tumejenga linchi linalothamini wapiga domo wa majukwaani kuliko watu wanaofanya mambo halisi on the ground.

Awkward!
 
Watanzaia Nani katuroga,mbona Kila Rais kwetu Ni mbaya na hatufai,Naamini mama yupo vizuri,Ila kwa issue ya mbowe tunasema mama HAPANA.MBOWE hana ugaidi wowote.mama samia ninakukubali Sana ipasavyo Ila busara za kuwatoa kaka zako wa UHAMSHO itumike kumtoa mbowe,mama Leo unavyomuona mbowe kuwa Ni Gaidi Basi unajikosesha imani kwa tuliokuamini.
Tozo na Mbowe keshameza ndoano kaingia mkenge washammaliza kisiasa.
 
Umempa za uso vizuri sana!

Eti wanataka watukane waangaliwe tu, waandamane waangaliwe tu, wafanye ujinga wote waangaliwe tu!

hawa watu sometimes unaweza sema wana hidden agendas. Nchi gani makini Haina utaratibu mzuri wa kufanya mambo yake?
Uongozi unataka ngozi nene,kama una ngozi nyepesi kakune nazi.
Unasumbukaje na watu wasio na jeshi,wala silaha zaidi ya mdomo.
 
Mama anajina la urais ila ukweli mchungu mama Hana sifa ya kuwa rais hapa ndo watanzania tunakumbushwa kujenga mifumo imara ya kuwapata viongozi wa ngazi za juu nchini.

Mifumo ingekuwa vizuri hasa vetting hakika mama asingekuwa hata mjumbe wa nyumba kumi.
 
Back
Top Bottom