Nafikiria kufungua kesi ya Madai dhidi ya Lissu na Wenzie

ili ionekane kaleta taharuki waseme yupo wapi na ana hali gani atakuwa hatiani ikiwa alivyoonena ni tofauti na uhalisia
Waziri mkuu ametutangazia majuzi kuwa Rais yupo na anaendelea na majukumu. Si lazima azurure kariakoo ndo tujue yupo. Hivyo hadi sasa kwa kauli hiyo tunaamini yupo. Ikingundulika vinginevyo nayo tutashitaki bado. Ndo maana kwa madai yangu serikali nayo nimeihusisha katika mashitaka.
 
Pole kwa kumwabudu Lissu. Sijaja hapa kushindana na Lissu namuheshimu na ninampenda kama Mtanzania mwenzangu. Lakini kama kuna sehemu ambayo kasababisha athari kwangu nitamshitaki yeye si Mungu wa kuogopwa. Mahakama itatoa haki hayo mengine hayanihusu.
 
Lakini kama Lisu anawajua kwanini asifungue kesi? Mpaka leo hakuna ajuae alie fanya hicho kitendo.
Hii kauli tukisikia ndiyo hasira na chuki zinatuzidia. Kweli serikali isijue watu walioingia kwenye makaazi ya Mawaziri? Na unamlaumu Lissu hajafungua kesi? Kwenye mahakama zipi? Acheni unafiki

Kama hamna cha kuongea ni heri mnyamaze.
Hamuwezi kufanya watu ni wajinga kiasi hiki. Hata wao wana mioyo ya nyama kama nyie.

Kuhusu kusamehe. Hata ningekuwa mimi ni Lissu singewasamehe mpaka kiama. Lazima waliompiga walipe na ana haki ya kuwachukia milele. Na siyo dhambi kuwachukia waliotaka kukua mchana kweupe. Awapende au kuwasamehe kwa lipi jema?
 
Afungue kesi kwa nani ?!. Hawa waliomjibu kule Dodoma kuwa hamna uchunguzi wowote !!. Kwamba kuna waliotendewa zaidi yake . Nani Alphonse Mawazo aliyecharangwa mashoka ?!.
 
Sipendi kubadili mada siongelei hilo. Kama unajua taratibu za makosa ya jinai usingesema haya. Ushahidi namba moja uwa ni maelezo ya mhusika au yoyote alokuwepo wakati wa tukio. Hivyo Dreva maelezo yake ni muhimu, na Lissu mwenyewe. Tuyaache haya hayanihusu.
 
Afungue kesi kwa nani ?!. Hawa waliomjibu kule Dodoma kuwa hamna uchunguzi wowote !!. Kwamba kuna waliotendewa zaidi yake . Nani Alphonse Mawazo aliyecharangwa mashoka ?!.
Naomba nisikujibu mie naongelea madai yangu hayo niwaachie wahusika kwani sijui lolote. Wakati yanatokea hata Tanzania sikuwepo nilikuja sikia tu nisiwe muongo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…