Naibu Waziri Mkuu majukumu yake Kikatiba ni yapi? Wafahamu waliowahi kuwa Manaibu Waziri Wakuu nchini

Naibu Waziri Mkuu majukumu yake Kikatiba ni yapi? Wafahamu waliowahi kuwa Manaibu Waziri Wakuu nchini

Hata Sasa hiki cheo kimetolewa kwasababu maalumu Ili kudhoofisha utendaji wa Majaliwa, maana alikuwa haungi mkono uwekezaji wa bandari
Pongezi sana kwa Majaliwa.
Kimya yake ni jibu kwa utawala huu wa hovyoo
 
Ndo nimeskia leo kuna nafasi ya naibu waziri mkuu
 
Hapa staki kuongea sana kwa sabu sielewi mambo ya Kisheria

Naongelea hii nafasi aliyopewa na kuteuliwa mh Dotto Biteko kuwa Naibu waziri mkuu, sjawahi kuisikia na wala kuona tangu nchi yangu ipate uhuru

Hii inamaana gani? Ni mh Rais kuogopa kulivunja bunge kwa kutokumtengua waziri mkuu?

Au lipo kikatiba?

Tafadharini Waheshimiwa sana viongozi wetu meza kuu Maadimin wetu Jf

Msiunganishe huu uzi
Walowahi kupewa.

1. Salm A Salim
2. Lyatonga Mrema
3. Ernest Nyanda. Huyu alikuwa mbunge wa Magu/ Busega

4. Doto Biteko

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hicho cheo hakipo kisheria! Kwenye katiba yetu pendwa hicho cheo hakipo!
Cheo hakipo ila katiba inamruhusu prizidenti kuanzisha cheo chochote nakufuta cheo chochote,, tukililia katiba mpya tuwe tunaeleweka
 
Kipara ngwidu Kila sehemu anayo wekwa hatoshi, hii ni hasara nyingine kwa jamuhuri ya uswahilini
 
Aha
Mpaka leo hii, hiki cheo kiliwahi kushikiliwa na watu 2 tuu tena kwa sababu maalumu sana na nyeti, na zenye maslahi mapana kwa taifa.

1. Dr. Salim Ahmed Salim.

Salim alipewa cheo hiki 1986 mpaka 1990, kwasababu aliwahi kuwa Waziri Mkuu kwa mwaka mmoja enzi za Mwalimu Nyerere (Baada ya Kifo cha Sokoine), hivyo baada ya Rais Mwinyi kuingia akaona ni Busara Waziri Mkuu wake aliyemteua Joseph Sinde Warioba awe na Naibu ambaye ni Salim.

2. Augustino Lyatonga Mrema

Akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Augustino Mrema alitumia ujuzi wake kama KACHERO WA USALAMA WA TAIFA, kudadisi na kukamata wezi na wala rushwa katika kila wizara ya Serikali aliyogundua mambo si shwari.

Hali hiyo ikawaudhi baadhi ya mawaziri wenzake serikalini. Wakamwambia "MREMA USIVUKE MIPAKA YAKO, Wewe ni waziri kama sisi na huwezi kuingilia mambo ya ndani kwenye wizara zetu bila kujadiliana nasi kwanza." Mrema anasema alikomaa nao, na ndipo Rais Mwinyi akagundua dhamira yake njema.

Rais Mwinyi mnamo mwaka 1992 akamuongezea cheo kipya Mrema. Akamteua kuwa NAIBU WAZIRI MKUU.

1993, Mrema alipopewa Unaibu Waziri Mkuu anasema "wenzangu walianza kuniogopa na kuniheshimu. Hata kama wanaenda sehemu walikuwa wanalazimika kusimama kwanza ili kupisha msafara wenye ving'ora wa Naibu Waziri Mkuu."

Akiwa Waziri wa Mambo ya ndani na Naibu Waziri Mkuu alishughulika na kila aina ya ubadhirifu, wizi na magendo kwa kadri alivyopata taarifa. Akawa waziri maarufu sana kwa wananchi mijini na Vijijini.

"Rais Mwinyi kila akirudi kutoka mikoani alikua akiniita na kuniambia Mrema nimetoka kwenye ziara, wananchi wanakusalimia sana. Unafanya kazi nzuri," alinisimulia Mzee Mrema katika mahojiano hayo ya MSUMARI WA MOTO.

Miongoni mwa mambo yaliyompa umaarufu Mrema zama hizo za uwaziri wake wa mambo ya ndani na Naibu Waziri mkuu ilikua ni kuhamasisha ujenzi wa vituo vya polisi kwa nguvu za wananchi ili kuimarisha ulinzi lakini pia "Tajirika na Mrema" - UTOAJI WA ZAWADI KWA WATU WANAOFICHUA WAHALIFU.

Nani angekubali kukaa na taarifa za mwizi au muhalifu wakati ana uhakika akimfichua atapewa zawadi?
★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★

Swali ni je, Biteko kateuliwa kuwa Naibu Waziri Mkuu kwa merits alizonazo, ama ameteuliwa kwa sababu Majaliwa ameonekana anapwaya kwenye u Waziri Mkuu?
Like fadher like a daughter
 
1693463341578.png

Agosti 30, 2023, Rais Samia alimteua aliyekuwa Waziri wa Madini, Dkt. Doto Mashaka Biteko kuwa Naibu Waziri Mkuu, nafasi ya Uongozi ambayo mara ya mwisho ilitumikiwa mwaka 1994 na Hayati Augustino Mrema.
1693463764644.png

1693463696853.png

Pia, Balozi Dkt. Salim Ahmed Salim ambaye amewahi kuwa Rais wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, alihudumu katika nafasi hiyo mwaka 1986 hadi 1989 chini ya Serikali ya Rais Ali Hassan Mwinyi.

Ikumbukwe, Katiba ya Tanzania Ibara ya 36(1) imempa Rais Mamlaka ya kuanzisha na kufuta nafasi za madaraka ya aina mbalimbali katika Utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
 
Cheo cha Waziri mkuu hakina tija kama makamu wa Rais yupo.

Kuwa na VP pamoja na PM kwa nchi masikini kama Tanzania ni mzigo mkubwa kwa walipa kodi walalahoi.
 
Nilikuwa sioni upungufu wowote kwenye UTATU wa Rais, Makamu wa Rais na Waziri mkuu

Na hata sasa sioni upungufu wowote kwenye UTATU ni kwamba Kazi zote zinakwenda sawia

Anyway Siasa ni Sayansi 😂
 
Back
Top Bottom