Naibu Waziri mteule wa Madini, Francis Kumba Ndulane ashindwa kusoma kiapo kwa ufasaha, uteuzi wake watenguliwa

Naibu Waziri mteule wa Madini, Francis Kumba Ndulane ashindwa kusoma kiapo kwa ufasaha, uteuzi wake watenguliwa

Habari wakuu

Leo nimeona kituko ambacho sio cha nchi hii ,hadi mimi niliekuwa naangalia nimeona aibu


How comes,mtu unashindwa kuaapa tena kwa kiswahili ,mbaya zaidi mtu kasoma ana master's ya science

Hadi mheshimiwa raisi kasema hio degree yake ichunguzwe, huenda hata hivyo vyeti ni fake


TAMISEMI angalien mfano wa mh raisi, mnamwaibisha sana, yale majina hewa ya walimu mliyoyatoa nasema hivi ipo siku tu mtakula matapishi yenu.

Ninaiman kabisa tamisemi mkiambiwa mkalete Wale watu mlioajiri na vyeti vyao orginal kuanzia secondary mpaka chuo kikuu, hawana Wale watu


Mh raisi pita tamisemi, narudia tena pita tamisemi kuna wahuni ambao hawajitambui wanaendesha hio taasisi, mpaka watanzania wanaichukia nchi yao.


Uzi tayar
Wewe kama mie, niliangalia nikaona aibu nikabadili chaneli kidogo. Ukweli kabisa!
 
Siamini kuwa hajui kusoma,kikubwa ni kupanic au kuna michezo ya ushirikina kachezewa na maadui zake,ni matumaini yangu Mh.raisi ataweza kubatilisha maamuzi yake kama itagundulika kuwa si tatizo la elimu yake...
 
Naibu waziri aliyeshindwa kuapa ameambiwa nafasi yake atachaguliwa mtu mwingine na yy atabaki kuwa mbunge tu.
Kwa maoni yangu si SAHIHI kumpiga mtu chini.Tuliofanya mitihani ya oral hilo ni jambo la kawaida kabisa.Na kwa kuwa huu haukuwa mtihani nilitegemea apewe muda awe composed.Kuapa mbele ya Magufuli kunahitaji makamanda kama sie.
 
Back
Top Bottom