Naibu Waziri mteule wa Madini, Francis Kumba Ndulane ashindwa kusoma kiapo kwa ufasaha, uteuzi wake watenguliwa

Naibu Waziri mteule wa Madini, Francis Kumba Ndulane ashindwa kusoma kiapo kwa ufasaha, uteuzi wake watenguliwa

Ni hali ya kawaida kitalaamu huitwa Emotional Shock n yaweza kumtokea Mtu yeyote, pole sana Francis K. Ndulane
 
Mada tumeshajadili na tumeshamshauri mhe.Rais mambo yetu na tuna imani atatusikiliza ushauri...kumbuka thawabu huwa zinakuja kupitia njia mbalimbali...Ni Mambo mengi huyu Mungu ametutendea katika Taifa letu na Mhe.Rais ametamka kwenye hotuba yake...watu huko duniani wanatushangaa....Sasa suala la waziri mteule Hilo ni dogo Sana..hakuna lisilowezekana kwa Mungu.
Lingekuwa dogo Mh rais angesema atamuapisha kesho. Lakini amechukia na ametengua uteuzi.
 
Amshukuru Mungu kwa kila jambo,alipangalo Mungu lina Makusudi.Huenda angekula "mzinga" kwenye v8 wakati wa kutimiza majukumu ya wizara.

Amshukuru Mungu sana tu.kama ni ulaji hata ubunge hufi njaa.aseme Asante Mungu[emoji120][emoji120].
 
Kwani kampeni alifanyia porini?
Alikuwa haongei na wapiga Kura wa jimboni kwake?
Ndio ujiulize,Ni dhahiri huyu alifungwa speed governor!Wanasiasa wanazijua sana hz habari,MTU anashindwa kabisaaaaa kujieleza na kuomba kuomba kura
 
Nasikia wateule wa rais huwa wanafanyiwa vetting ya hali ha juu.

Nani huwa anamfanyia rais vetting? Mpaka anampa majina ya watu ambayo hawawezi hata kusoma kiapo na kutamka!

Hawa watu mbona kama wamemtia doa mkuu wa nchi, maana sinawahi kushuhudia mtu akitumbuliwa kwa kushindwa kusoma kiapo na kutamka!

Hii inaleta picha gani? Kuwa kama ni kweli kwamba watu wanaomfanyia vetting mkuu wa nchi hawako makini mpaka wanampa majina ya watu ambao wanashindwa kuapa!

Au ni mambo ya kijamii yameitawala Tanzania,ndio maana watu wengi wenye IQ kubwa huwezi kuwakuta kuwa ni viongozi?

Inasikitisha sana kwa Taifa ambalo linajinasibu kuwa ni moja ya taifa kubwa hapa Afrika mashariki, waziri mdogo anashindwa hata kusoma na kula kiapo. Nafikiri maneno aliyosema Askofu Rashid kuwa wengi wa wabunge wa CCM walipita kwa mgongo wa kiongozi wao wa chama,sababu 70% walikuwa hawana uwezo na hata kukubalika ilikuwa ni kwa mashaka

Kwa ujumla aliyeshindwa kuapa na aliyemtumbua wote wameaibika.

Kwahiyo mtu akifanyiwa vetting is not bound to make any mistake or fail?

Unajua kwamba watu huwa overwhelmed?

Unajua kwamba people react differently under pressure?

Unaposema "watu wengi wenye IQ kubwa huwezi kuwakuta kuwa ni viongozi?" inakuaje mtu mwenye IQ kubwa akubali kuongozwa na mwenye IQ ndogo? Huoni sentensi yako inakinzana? Hiyo IQ kubwa imemsaidia nini? Sawa na kusema mwenye nguvu kapigwa na mnyonge ni jambo ambalo haliwezekani.
 
Niliona clip ya Tale yule ndo hafai kabisa ila sikumshangaa. Huyu na Masters yake nae hajui kusoma duh!
Kabisa siasa ni Kipaji ,TALE/FA wangeendelea na Muziki tu,Siasa hawawezi!! Siasa uwezo wa kujenga hoja na ushawishi ,hao watu ni ZERO FLAT.
 
kampeni alipigaje mbele ya umati mkubwa si Bora hata angepiga Faru John 1 kuondoa aibu
Wazee wa suti wakikunusanusa wakijua umejifarujohn wanakuchomea utambi Bora upinge ujani then unajibigjii au kuber.
 
Kabisa siasa ni Kipaji ,TALE/FA wangeendelea na Muziki tu,Siasa hawawezi!! Siasa uwezo wa kujenga hoja na ushawishi ,hao watu ni ZERO FLAT.

Well, FA yupo vizuri na ana matumizi mazuri sana ya lugha labda ashindwe kwenye utendaji.

Huyo Tale kusoma shida, kujenga hoja ndo kabisa.
 
Labda amekataa ubunge na unaibu waziri kwa ujanja!!!! Lazima itafutwa namna ya kumuokoa 'mpiganaji mwenzetu' kadhia hii! Hatuna namna. LAKINI DUH! Naona maluweruwe!!! Yaani kama siamini vile.
 
Kwahiyo mtu akifanyiwa vetting is not bound to make any mistake or fail?

Unajua kwamba watu huwa overwhelmed?

Unajua kwamba people react differently under pressure?

Unaposema "watu wengi wenye IQ kubwa huwezi kuwakuta kuwa ni viongozi?" inakuaje mtu mwenye IQ kubwa akubali kuongozwa na mwenye IQ ndogo? Huoni sentensi yako inakinzana? Hiyo IQ kubwa imemsaidia nini? Sawa na kusema mwenye nguvu kapigwa na mnyonge ni jambo ambalo haliwezekani.
Huwezi kuelewa nilichoandika sababu Iq yako ni ndogo. Kwa hiyo watu wenye Iq kubwa kukaa mitaani na kuacha wenye Iq ndogo kuingia kwenye siasa, unadhani ndio kuwa hawana Iq kubwa?
 
Habari wakuu,

Leo nimeona kituko ambacho sio cha nchi hii, hadi mimi niliyekuwa naangalia nimeona aibu....
Huenda ana shida ya "VISION". Hilo hutokea hata wasoma masomo kanisani. Huyo alitakuwa awe na miwani
 
N uchawi kwa kwendaa mbele ...sio rahs kuwaa mbunge wa ccm usiende kwa sangatiti never
 
Huwezi kuelewa nilichoandika sababu Iq yako ni ndogo. Kwa hiyo watu wenye Iq kubwa kukaa mitaani na kuacha wenye Iq ndogo kuingia kwenye siasa, unadhani ndio kuwa hawana Iq kubwa?

Nakwambia hivi, kama mwenye IQ kubwa bado yupo mtaani na mwenye IQ ndogo katoka, nani mwenye IQ kubwa hapo?

Kwanini ukubali kuongozwa na uliyemzidi uishie kulalamika tu badala ya kuchukua hatua na kubadilisha mustakabli wako?
 
Back
Top Bottom