Nani aliwachagua kuwa viongozi wa dunia? G7 ni viongozi wa nchi 7 tu si zaidi ya hapo

Hao ndio wanaoishape Dunia iwe namna ilivyo. Ndio wamiliki wa karibu tekinolojia tekinolojia zote za Dunia.
 
Kuna wanaoitwa "maskini jeuri". Wanajali heshima yao na hawako tayari kuiuza kwa gharama yoyote!! Watakuambia "potelea mbali na pesa yako". Watu kama mwalimu Nyerere, Robert Mugabe, Fideral Castro nk.
Asikudanganye mtu. Hayo mataifa hakuna cha maskini jeuri. Unaweza kupigapiga tu kelele halafu wakakudharau.

Nyerere alikuwa anabishana nao lakini hakuwahi kuwagomea. Alihudhuria UN ambayo hakuwahi kuianzisha. Aliheshimu nguvu ya mataifa yenye veto. Aliendelea kutumia magari yao, ndege zao, na tekinolojia zao mbalimbali.

Mwenye jeuri ni yule atakayesema sitaki kutumia chochote chao, nitajitegemea, sitawapigia magoti kwa chochote. Mwalimu aligomea masharti ya IMF, mpaka wananchi walikosa hata sabuni za kufulia, sukari, chumvi, n.k. Mwishowe alusalimu amri, akashusha thamani ya shilingi.

Hao G7, mmoja tu ana uwezo wa kuwaimbia nchi yote ya Tanzania laleni na kucheza bao, tutawahudumieni, na mkaishi vizuri kuliko mnavyoishi sasa, na wao wasihisi kuna kitu kimepungua.

Utalii wa mji wa Paris pekee yake kwa mwaka unaingiza mapato kati ya dola bilioni 85 mpaka bilioni 90. Serikali ya Tanzania ikiambiwa ikusanye mapato tu ya utalii ya jiji la Paris pekee, ni zaidi ya mara 4 ya bajeti yote ya Tanzania.

Hapo ndiyo utaelewa kwa nini ukipewa hata msaada wa dola milioni 300 na hayo mataifa, kwao ni vijihela tu. Wakikupa wanachohitaji zaidi uwaheshimu na kuwasikiliza, siyo eti wanategemea kuwa wewe utawatajirisha kwa kupitia huo msaada kama wengi wanavyodhania.
 
Kelele za Mchina zina nguvu ndogo sana. US ilipeleka pendekezo UN la kutaka China itambulike kama Taifa tajiru ili mchango wake UN uongezwe, China ilikataa katakata na kudai kuwa ukubwa wa pato la China unasababishwa na uwingi wa watu, na siyo kipato kikubwa cha wananchi wake, na kwamba wachina wengi wanaishi kwenye umaskini mkubwa.

Sasa kama hutaki kugharamia hizo taasisi za kimataifa, huwezi kuwa na nguvu sawa na hao wanaozutegemeza.
 
Hata utaratibu wa kuvaa chupi hao ndio waliouleta. Kila tunachojivunia kuwa ni maendeleo ni chao, halafu eti ghafla uwazidi, haiwezi kuwa karne hii.
 
Hauna hoja mkuu, Sema basi Japan wanainyonya Tanzania kwenye sekta ipi...siyo kuleta nadharia yasiyokuwa na uhalisia.
Sema Japan wanainyonya vp Tanzania au Kenya.
 
Sasa ukikataaa unasidia nini?
Nyie wenyewe kila mkipata shida mnakimbilia huko kifedha kisiasa na kila kitu sasa mkishaenda wote si lazima ataona yeye ni baba lao
 
Watu kama nyie magufuli alikuwa anawachapa viboko tu maana hamna akili.
 
Kabla ya Wazungu kuja Africa walikuwa na Empire kubwa tu zenye Nguvu,

Na umekua brainwashed kuamini Akili ni kitu Fulani, hizo Nchi za Asia zinazoendelea kila siku zingekua na Mentality kama yako Leo zingekua Mazombie tu ya west.

Huwezi kuendelea kamwe kwa kufuata ama kuiga wenzako, mfumo wa west ni Pyramid jinsi mnavyokuwa wafuasi wengi ndio jinsi mnavyowanufaisha wao na ndio jinsi Nyie chance yenu ya kuendelea inavyokua Ndogo.

Kila Nchi ilioendelea ilijitathmini strength zake na kufuata ilichoamini hadi kutoboa na sio kutegemea misaada ya west.

Indonesia, China, Singapore, Korea, Malyasia, Brunei, Japan, Taiwan etc unafikiria wameendelea kwa Kumfuata West?

Hata Nchi za Middle East Leo zimeendelea kwa kutokufuata west, Leo Hii King Faisal asinge Nationalize Mafuta yao Pengine Saudia ingekua kama Venezuela ama Angola tu.
 

Na ushoga pia wanatuletea ili watu wapungue duniani
Na hakuna ruhuhusa ya nchi kama Tanzania [emoji1241] na wenzake ambao maleria ni number one killer nchini, haturuhusiwi dawa ya kupuliza juu kwa ndege ili kumaliza na kutokomeza kabisa ugonjwa huo!
Bali tuna ambiwa tununue dawa ambazo zina tengenezwa na makampuni yao!
Ni vitu vingi vya kusikitisha!
Ndio maana nchi nyingi za kiafrika zinazo jielewa ziko na simba Vladimir Putin, na tunasema nchi yeyote itakayo weza kubadilisha huu mfumo wa sasa hivi tuko nao walahi kuliko mashoga na ukoloni mambo leo wao![emoji2959][emoji3062]
 
Hao ndio wanaoishape Dunia iwe namna ilivyo. Ndio wamiliki wa karibu tekinolojia tekinolojia zote za Dunia.
Wanaishape Dunia kwa manufaa yao sio Manufaa yako.

Chukulia Mfano China vs India wote hawa ni MA Giant wenye watu sawa na Mabara.

China Akienda against nao akafungia YouTube, Google, Fb, na Tech Nyingi za Nje, Akacopy na kutengeneza vyengine vya kwake, akatumia hela alizokua anafanya manufacturing kuboresha sector nyengine kama Kilimo Leo hii ni Uchumi Mkubwa mno na wamefanikiwa kiasi kikubwa kutoa umasikini. Leo hii Social Network za China sio inferior kwa US, kampuni kama Tencent ipo valued around 400B usd na FB around 600B.

Muangalie India Sasa kubwa jinga ambaye kama Africa yupo proud kuwa kibaraka wa west na kumsifia kila Akipata muda, wapo level Moja na sisi bado wanajenga vyoo na kuvizindua
 
Baada ya kuwabwatukia ikawaje sasa? Imeondoa uhalisia wa kuwa wao ni World Leaders?
 
Sikia huyu nae, yaani uibe pesa ya mradi wa kuangamiza vizalia vya malaria then lawama ziende kwa West...Simba Putin kama unavyomwita, Russia ilikwepo tokea Enzi na Enzi lakini hakuna ata teknolojia ya kutengeneza sabuni iliwapatia.
Kubali tu kuwa hatuchangii chochote kwa west bali tunawanyonya sisi...yaani bure kabisa.
 
Kumbe wewe hujui ata maendeleo ya Indonesia, Taiwan, Japan, China, Brunei, Singapore zimechangizwa na kuwa pamoja na West? Bure kabisa...nenda China uone wanavyopigania kwenda kusoma Ulaya na USA ili kupata elimu iliyo bora...wewe unapigania kwenda kusoma China, huko Korea Kaskazini kwenyewe kwa Jeuri Mapanki amepata elimu yake West.

Ukitaka kula na wewe kubali kuliwa wakati huo unapangilia mambo yako vyema ili unachokula kidogo kije baadae kikupe jeuri ya kupunguza kuliwa.
 
Itikadi za kijamaa ndizo zinakufanya na wewe uwasifie China. Mbona Mzee wa Vikwazo Joe Biden kamchimba Mkwara Xi asithubutu kuthubutu kuwapa Siraha Warusi, bila ubishi wowote Xi ametii?
 
Nadhani hata hayo maangamizi ya Nuclear hujui kuwa kwa sasa hayawatishi hao jamaa wa G7. Kwamba USilisha unda mitambo Patriots ambayo kazi yake ni kudungua makombora yenye vichwa vya siraha za Nuclear kama yatarushwa na Kichaa Putin au Dishi Kuyumba Kiduku, makombora hayo yataduguriwa yakiwa kwenye anga za nchi zao? Hivyo makombora hayo yakirushwa watakao athirika zaidi ni Warusi, Wakorea na nchi za jirani? Lakini pia US ilisema ikiiona Urusi iko kwenye maandalizi ya kutaka kuyarusha makombora yenye kubemba vichwa vya siraha za Nuclear tu. US itavurumisha makombora yake kuyabonda makombora yenye vichwa vya siraha za Nuclear kabla ya kurushwa? Kwa Sasa endelea kuelewa kuwa US bado ni Police wa Dunia, ikifuatiwa kwa mbali na Uchina.
 

Acha na hiyo G7. Ukienda kwenye baraza kuu la usalama la UN utakutana na kundi linaitwa P5, URusi, Marekani, China, UK na Ufaranza. Sasa hao ndio wenye usemi wa mwisho kwenye UN. Mwaka 1996 walipiga kura ya Veto kukataa mmisri boutrous ghali kuendelea kuwa Katibu mkuu wa UN.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…