Nani anapaswa kulipa hela ya udalali kati ya mwenye nyumba na mpangaji?

Nani anapaswa kulipa hela ya udalali kati ya mwenye nyumba na mpangaji?

Inaonekana ni lile group la bibie mnaniandama sikia njoo na ID yako unayotambulika ila ujue hili ukooo wenu ndio unatabia yakuzalia nyumbani na kuoa au kuolewa ni ngumu hata maaza ako alikuzaa nyumbani nyie kila mtu ana baba ake
🤣🤣🤣🤣 uko wapi nije kuona kama kweli una mtu ?
 
1. Makubaliano yenu yakoje?
2. Kwa nini utafute Dalali Wakati nyumba zipo nyingi? Hiyo sababu inayokufanya umtafute Dalali ndio hiyo itakayokufanya umlipe.
3. Kama ni mwenye nyumba, Kwa nini usitafute mwenyewe wateja, hiyo si ni biashara yako? Sababu uliyoona ya kutafuta Dalali wa kukukodishia nyumba yako ndio hiyo itakayokufanya umlipe.

Maswali ya namna hiyo huulizwa na watu wa Aina ifuatavyo;
1. Washamba, ambao hawajakulia mijini.
Kijijini huwezi kuta mambo ya hivyo.
Ila Miji mikubwa hayo ni mambo ya kawaida.

2. Wanaroho ya korosho.
Roho Mbaya ndio inaweza kukufanya uulize maswali ya kijinga kama hayo.
Mkataba WA Dalali na mwenye nyumba unakuhusu nini wewe mpangaji?
Wewe umekutana na Dalali mkaingia makubaliano yenu, kwamba labda utamlipa kiwango Fulani Kwa kazi ya kukutafutia Apartment. Bali kwenye makubaliano yenu. Masuala ya kuuliza mwenye nyumba mbona anamlipa Dalali au hamlipi hiyo haikuhusu.
Labda kama na wewe unataka kuwa Dalali.

Ni Sawa na udalali wa kuuza magari, umemuambia mtu akuuzie Gari yako au umepeleka kwenye Kampuni la kuuza magari ya mtumba. Mmepatana Bei kuwa aliuze Kwa milioni 10, alafu umekabidhi Kadi na kila kitu. Alafu Dalali akapatana na mteja aliyemtafuta kwamba Gari milioni 20 alafu wewe Kwa Roho Mbaya unaona mbona amechukua nyingi. Come on!
Hizo ni Akili za Roho Mbaya, husda na Wivu wa kijinga.
 
Hakuna tatizo mwenye nyumba na mpangaji wote kumlipa dalali kwa vile nyote mlimtumia yeye katika kufanikisha malengo yenu, Tatizo linakuja ni charge ya Udalali ni kubwa sana, yani hela ya mwezi mzima umlipe na yeye dah, mda mwengine chumba kikiwa cha bei ya juu kidogo tu ndipo inapokuwa shida.
 
🤔🤔 nani anamuweka dalali? Tuanzie hapo... nyumba nyingine ukienda wenye nyumba anakabidhi kia kitu kwa dalali yaani hataki kudeal na wapangaji, hili unalizungumziaje?
Tafuta nyumba isiyo na Dalali.
Au tafuta website za Rent and real estate Agency. Hayo mambo yote yatajumuishwa kwenye Kodi yako.

Utalipia Kodi,
Umeme
Mlinzi
Na vitu vya ndani utavikuta humohumo.

Ukiona unajiuliza maswali hayo ujue Urbanisation inakutoa kwenye mfumo.
 
Hakuna tatizo mwenye nyumba na mpangaji wote kumlipa dalali kwa vile nyote mlimtumia yeye katika kufanikisha malengo yenu, Tatizo linakuja ni charge ya Udalali ni kubwa sana, yani hela ya mwezi mzima umlipe na yeye dah, mda mwengine chumba kikiwa cha bei ya juu kidogo tu ndipo inapokuwa shida.

Inategemea na maelewano.
Kwengine kwenye nyumba vya gharama, unalipia nusunusu, mfano kama nyumba Kodi yake ni Tsh 500k basi utalipia 250k kisha mwezi unaofuata 250k.

Biashara ni maelewano
 
Hata TRA nao wanafanya hivyo hivyo, kuna pesa ya pango badala ya kumkata mwenye fremu wanamkata mpangaji
 
Hivi njia rahisi ya kujua sehemu fulani wanapangisha bila kutumia dalali ni ipi?🤔🤔

Njia rahisi ni wewe kuingia kwenye kazi ya udalali. Yaani kuwa Dalali.

Ukiwa Dalali hizo Pesa huwezi kuzitoa, gharama pekee ni kukusanya taarifa za nyumba zote za Kupanga Kwa Kata nzima unayoishi na kuwa na mawasiliano na wenye nyumba hizo. Pia kujuana na madalali wa Kata za mbali(maeneo mengine).
Ndio utajua kuwa hiyo nayo ni kazi
 
Back
Top Bottom