Naomba kuuliza kwa wote wanaomuamini Yesu

Unaweza nipa andiko lolote kweny Bible yenu yesu yy mwenyewe akijiita mim ndie mungu ,nipe Hilo andiko yey akijiita sio paulo
Nitakupa maandiko mengi tu maana nina hakika husomi Biblia bali huwa wanakuhadithia wanachotaka ukisikie. Kila mstari nitakaoweka nitakuuliza swali la ufahamu. Usiandike majibu yake hapa, ni maswali ya kujiuliza na kujijibu mwenyewe

Yohana 5:15 - 18 (Ukiweza soma sura nzima upate utamu wa hii habari)
"Yule mtu akaenda zake, akawapasha habari Wayahudi ya kwamba ni Yesu aliyemfanya kuwa mzima. Kwa sababu hiyo Wayahudi wakamwudhi Yesu, kwa kuwa alitenda hayo siku ya sabato. Akawajibu, Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi. Basi kwa sababu hiyo Wayahudi walizidi kutaka kumwua, kwa kuwa hakuivunja sabato tu, bali pamoja na hayo alimwita Mungu Baba yake, akijifanya sawa na Mungu."

Swali la kujiuliza: Kwa nini Wayahudi walizidi kutaka kumwua Yesu?

Luke 5:18-23
"Na tazama, wakaja watu wanamchukua kitandani mtu mwenye kupooza; wakataka kumpeleka ndani na kumweka mbele yake. 1Hata walipokosa nafasi ya kumpeleka ndani kwa ajili ya lile kundi la watu, walipanda juu ya dari wakampisha katika matofali ya juu, wakamshusha yeye na kitanda chake katikati mbele ya Yesu.

Naye alipoiona imani yao, alimwambia, Ee rafiki, umesamehewa dhambi zako. Basi, wale waandishi na Mafarisayo wakaanza kuhojiana wakisema, Ni nani huyu asemaye maneno ya kukufuru? N’nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake? Na Yesu alijua hoja zao, akajibu akawaambia, Mnahojiana nini mioyoni mwenu? Lililo jepesi ni lipi? Kusema, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Ondoka, uende? Lakini, mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi

Swali la kujiuliza: Kama ni Mungu pekee ana amri ya kusamehe dhambi, na Yesu anasema alifanya maksudi ili wajue ana amri ya kusamehe dhambi, Yesu anasema yeye ni nani?

Yohana 8:48-59
"Wayahudi wakajibu, wakamwambia, Je! Sisi hatusemi vema ya kwamba wewe u Msamaria, nawe una pepo? Yesu akajibu, Mimi sina pepo; lakini mimi namheshimu Baba yangu, na ninyi mwanivunjia heshima yangu. Wala mimi siutafuti utukufu wangu; yuko mwenye kutafuta na kuhukumu. Amin, amin, nawaambia, Mtu akilishika neno langu, hataona mauti milele. Basi Wayahudi wakamwambia, Sasa tumeng’amua ya kuwa una pepo. Ibrahimu amekufa, na manabii wamekufa; nawe wasema, Mtu akilishika neno langu, hataonja mauti milele. Wewe u mkuu kuliko baba yetu Ibrahimu, ambaye amekufa? Nao manabii wamekufa. Wajifanya u nani? Yesu akajibu, Nikijitukuza mwenyewe, utukufu wangu si kitu; anitukuzaye ni Baba yangu, ambaye ninyi mwanena kuwa ni Mungu wenu. Wala ninyi hamkumjua; lakini mimi namjua. Nikisema ya kwamba simjui, nitakuwa mwongo kama ninyi; lakini namjua, na neno lake nalishika. Ibrahimu, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi. Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu? Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko. Basi wakaokota mawe ili wamtupie; lakini Yesu akajificha, akatoka hekaluni.

Maswali ya kujiuliza:
1. Ibrahimu aliionaje siku ya Yesu wakati aliishi miaka mingi kabla ya kuzaliwa Yesu kama Yesu hakuwepo kabla ya kuzaliwa?
2. Kama Yesu alikuwako kabla ya Ibrahimu kama mwenyewe anavyosema, ni mwanadamu wa aina gani huyu?
3. Unajua jina la Mungu wa Wayahudi ni NIKO? Kwa nini Yesu hakusema kabala ya Ibrahimu nilikuwako ambayo ni gramatically correct akasems kabla ya Ibrahimu NIKO?
3. Kwa nini waliokota mawe ili wamwue? Ni kosa gani alifanya kwenye mazungumzo kustahili kupigwa mawe mpaka kufa?


Luka 22:66 - 71
"Hata kulipokucha, walikutanika jamii ya wazee, na wakuu wa makuhani, na waandishi, wakamleta katika baraza yao, wakisema, Kama wewe ndiwe Kristo, tuambie. Akawaambia, Nijapowaambia, hamtasadiki kabisa. Tena, nikiwauliza, hamtajibu. Lakini tangu sasa Mwana wa Adamu atakuwa ameketi upande wa kuume wa Mungu Mwenyezi. Wakasema wote, Basi, wewe ndiwe Mwana wa Mungu? Akawaambia, Ninyi mwasema kwamba mimi ndiye. Wakasema, Basi, tuna haja gani tena ya ushuhuda? Maana, sisi wenyewe tumesikia maneno ya kinywa chake"

Swali la kujiuliza: Kwa nini Yesu alikubaliana na walichosema Wayahudi kuwa Yeye ni Mwana wa Mungu? Na Kwa nini Wayahudi walichukulia huu ni ushahidi wa Yeye kukufuru na kustahili kifo?

Bonus:
Yohana 19:6 - 7
"Basi wale wakuu wa makuhani na watumishi wao walipomwona, walipiga kelele wakisema, Msulibishe! Msulibishe! Pilato akawaambia, Mtwaeni ninyi basi, mkamsulibishe; kwa maana mimi sioni hatia kwake. Wayahudi wakamjibu, Sisi tunayo sheria, na kwa sheria hiyo amestahili kufa, kwa sababu alijifanya kuwa Mwana wa Mungu"

Swali la kujiuliza: Je kwa nini Wayahudi waliona ni kosa linalostahili kifo kwa Yesu kujiita Mwana wa Mungu?

Hayo yakutoshe kwa sasa. Sihitaji ujibu chochote, kwa sababu sitahangaika kukujibu. Umeomba mstari, nimekupa mistari.
Sasa hangaika nayo mwenyewe!
 
Ameandikwa wapi? Nimeshasema hili na ushahidi nimeweka. Kama una mpango wa kusoma na kuelewa pitia comments zangu kuhusu hilo.
Kama umeweka pamba masikioni na umeziba macho basi endelea na unachotaka kuamini. Una uhuru wa kuamini unachotaka. Utumie!
 
Ameandikwa wapi? Nimeshasema hili na ushahidi nimeweka. Kama una mpango wa kusoma na kuelewa pitia comments zangu kuhusu hilo.
Kama umeweka pamba masikioni na umeziba macho basi endelea na unachotaka kuamini. Una uhuru wa kuamini unachotaka. Utumie!
Umeisoma Qur'an yte na kama umeisoma io verse nloiquote iko sura gan
 
Hakuna Surah wala hadith inayomtaja Yesu. Haipo!
Sasa unataka ninukuu sura ambayo haipo naitoa wapi?
Kwel wakristo Weng ni kondoo ndo mana hata mambo ya kutumia akili ya kawaida hawawez kuona ,Qur'an huijui popote ila ngoja nisibishane mn tushaambiwa ht tuliongea nany vipi hamtaelewa
 
Kwel wakristo Weng ni kondoo ndo mana hata mambo ya kutumia akili ya kawaida hawawez kuona ,Qur'an huijui popote ila ngoja nisibishane mn tushaambiwa ht tuliongea nany vipi hamtaelewa
Sasa kejeli za nini? Wewe mwenyewe unayedai kuijua Quran hujaleta verse zaidi ya hizi taarabu.
Leta ayat inayomtaja Yesu, au hata hadith, ndio ulete hizi taarab!
 

Ok tusema mtu wa kwanza kufa alikuwa Yuda msaliti wakati Yesu mzima,baadaye akafuata Yesu akapalizwa mbinguni,swali langu walibaki mitume wake peke yao"je wao walikuwa wanafanya ishara ya msalaba?
 
Quruani imeteremshwa na Mwenyezi Mungu kupitia Jibril mmoja wapo wa Malaika wakubwa wenye heshima kubwa huko mbinguni.Quruani iliteremka kwa njia ya Wahyi au ufunuo katika muda wa miaka 23 wakati wa utume wa mtume Muhamad (S.A.W)
 
Wewe ndiye hujakomaa,hujui vyombo vya mziki na hizo anasa zipo toka enzi za kina Daudi,nikupe pole Yesu amekuja juzi ameikuta dunia inahayo yote unayoyasema, lakini sababu yeye ni Mtume wa mwenyezi Mungu hakujishughulisha nayo
 
Mwisho wa siku utakuja na hoja ya alitumia lugha gani na chakula gani? Hahahaha! Kwa Bwana Yesu Kristo aliyesulubishwa, akafa, akazikwa, siku ya tatu akafufuka , akapaa mbinguni kila goti litapigwa na kila ulimi utakiri hata kwa kuchelewa.
 
Nitajibu mambo machache;

1. Yesu alivaa kanzu, hii ilitokana na utamaduni wa mahali alipozaliwa mashariki ya kati huvaa kanzu.

2. Mariamu alifunika kichwa kwa desturi za wakazi wa mashariki ya kati mwanamke apaswa kufunika kichwa hasa akiwa ibadani.

3. Si Yesu wala Maria aliyepiga ishara ya msalaba nitaeleza kama ifuatavyo;

MSALABA
Kabla ya Yesu kuzaliwa na kufa, msalaba ilikuwa ni ishara ya kulaaniwa.

Watu wasifaa katika jamii waliangikwa/kutundikwa msalabani hadi wafe ikiwa ni ishara ya kuondoa mtu mchafu mwenye laana na kila uovu katika jamii.

Msalaba uliwekwe nje ya mji kabisa sawa na tunavyotenga dampo nje ya mji.

Mtu kuuawa msalabani ilikuwa kama kusafisha jamii kuondoa kilicholaaniwa kwa isemavyo biblia " Amelaaniwa aangikwaye msalabani.

HESHIMA YA MSALABA
Baada ya Yesu kuteswa na kuangikwa msalabani ndipo historia ya msalaba ilibadilika badala kuwa alama/ ishara ya LAANA ikiwa ni Alama ya USHINDI

1. ushindi wa kifo na mauti
2. Ishindi wa dhambi
3. Ushindi dhidi ya magonjwa nk.

Hivyo si Yesu wala Maria aliyepiga ishara ya msalaba.
 
Kweli mwamba mi nipo unguja huku mara kadhaa naona vijana wanabadili dini kwa hoja za kijinga sana, uislam ni dini ya mazumbukuku kibao....mazinge anawasilimisha kijinga sana watu wengi
 
Kwani kanzu si ni vazi tu la majira,nenda oman kwanza ni nguo tu kama ilivyo pens
 
Mbona mnakwepa swali,labda uulizwe Yesu alishawahi kupiga ishara ya msalaba
 
Mbona mnakwepa swali,labda uulizwe Yesu alishawahi kupiga ishara ya msalaba
Utakua na kichwa panzi labda.
Jibu ni hapana kwasababu enzi za Yesu msalaba ulikuwa najisi.
Msalaba umeheshimishwa kwa kufa na kufufuka Yesu.
Ikawa alama ya Ushindi.
Ndipo watu walipoanza kupiga ishira ya msalaba kama ishara ya ushindi.

Ishara ya msalaba haipo kibiblia ni mapokeo ya baadhi ya imani za kikristo tu


SOMA NO 3. KATIKA POINTS ZANGU
 
Ata kuandika huku jamiiforums hakuwahi. Hakuwahi mambo kibao tu mbona? Kutumia simu je? Au we ndio umeona hayo tu? Pumzika usijichoshe na vitu vidogo.
 
Mim Sina jibu na sielewi kama ww....Swali lako limekaa kichokozi, kiukakasi....me naona tuachane na hayo tu

Sent from my Infinix PR652B using JamiiForums mobile app
 
Endelea kuwapa vitasa mkuu atae jaliwa ataifuata haki
Hawa ni wabishi mno
wana masikio lakini hawasikii
wana macho lakini hawaoni
hlf hao ni sawa ukiwaonya au.usiwaonye hawaamini mna mioyo yao wameielekeza huko kwa shetani

tupo pamoja mkuu hmna swali nitakaloshindwa kulijibu ila wananikimbia mna hawawezi kujibu
 
Kweli mwamba mi nipo unguja huku mara kadhaa naona vijana wanabadili dini kwa hoja za kijinga sana, uislam ni dini ya mazumbukuku kibao....mazinge anawasilimisha kijinga sana watu wengi
Na mimi pia nipo unguja huenda nikakusilimisha na ww mbona kma hawaingii kwenye ukristo kma ni dini ya kweli? dini ya mazumbukuku ni yenu mnomuabudu mtu tena kama wewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…