Naomba ushauri kuhusu biashara yangu inakoelekea inaenda kukata roho sio muda

Naomba ushauri kuhusu biashara yangu inakoelekea inaenda kukata roho sio muda

ww ndio mwenye matatizo na hao waliokushauri huko juu eti sijui kuna uchawi au ubadili biashara wengi wanakupotosha siku zote biashara ni uvumilivu.. ww ni mgeni na mpya kwenye biashara ya mchele eneo hilo ndio kwanza una miezi sita alafu eti unaumia roho kwa uliowakuta wanauza hadi tani 30 kwa siku lakini hutaki kujiuliza hao wenzio wana mda gani eneo hilo usikute wana miaka kuanzia 3 hadi 5 wanafanya biashara hapo washatengeneza connection za wateja wao wa kudumu na pia washaweka jina si unajua biashara za uswahilini nyingi zinaenda kwa kujuana na kiaminiana..sasa ww mgeni wa miezi sita tu apo unataka uuze na kupata faida sawa na hao waliokaa miaka hata 5 washatengeneza wateja wao wa kudumu.! tatizo wabongo wengi tunataka faida ya haraka kwenye biashara bila kutengeneza msingi kwanza mfano mleta mada anaona wivu na hasira kali jirani yake kuuza tani 30 kwa siku wengine mtaji hadi million 100 wakati hao wenzie wametumia miaka kibao kufika hapo walipo alafu yeye na miezi yake sita anataka awe level hizo wakati nao walianza chini miaka imepita kama anavyoanza yeye leo.. pambana na ww kutengeneza connection zako na wateja wako wa kudumu miaka miwili mbele utaanza kula matunda
Dah hii kweli
 
Biashara ya hasara sana hiyo....uchawi mwingi mno.Unaweza dhani wauza mchele kumbe wateja waona chumvi ya mawe.

Kuna mtu jirani hapa yalimkuta,yeye anauza kuni Kila siku wateja wanalalamika kuwa Kuni mbichi haziwaki.

kimuonekano Kuni ni kaukau balaa...kumbe.

walishambadilishia walimwekea miwa yeye hajui
Nkamu umenikumbusha mbali sana, huo mchezo niliwahi kuchezewa dukani waliniwekea soda… 😂😂😂
Mteja wangu alikuja akaniambia naona umebadilisha biashara, namuuliza biashara gani ananiambia anaona vinywaji 😹😹

Kuna watu mafala sana
 
Mbagala kawaida me mwenyewe nipo mbagala nauza viatu vya kike nilikuwa nauzia ndani kule stendi ndogo nimepata hasara siuzi nyingi nikahamia puma kule hasara siuzi kabisa nataka kupakimbia kodi nimelipa miezi 4 nina wiki moja
Miezi minne ushakata tamaa?? 😹😹
Mwanzo ulikuwa unafanya biashara gani?
 
Anza kutafuta mama lishe na wale wapishi wanaopika kwenye masherehe, halafu mchele wa 1400 au ulitaka kuandika 2400?
 
Watu hawanunui wanapita tu tena wengi hela ya kula nakosa me nauza viatu vya kike ila eneo nilipo wote vya kiume
Hapo ndipo ulipokosea, ilitakiwa na wewe ungeweka biashara ile ile km ya wenzio, huo mtaa wateja washazoea wakija wakute viatu vya kiume, wewe umeweka vya kike ni ngumu..!

Km ulitaka kuuza vya kike basi ungeenda mtaa ambao wanauza vya kike na wewe ungeuza..!
 
Hapo ndipo ulipokosea, ilitakiwa na wewe ungeweka biashara ile ile km ya wenzio, huo mtaa wateja washazoea wakija wakute viatu vya kiume, wewe umeweka vya kike ni ngumu..!

Km ulitaka kuuza vya kike basi ungeenda mtaa ambao wanauza vya kike na wewe ungeuza..!
Sawa kwa hiyo kuhama sahihi niache kodi
 
Anza kutafuta mama lishe na wale wapishi wanaopika kwenye masherehe, halafu mchele wa 1400 au ulitaka kuandika 2400?
unashangaa mchele kilo 1400 huamini au.. mbona ndio bei ya kuanzia sehemu nyingi tu dar huku gongo la mboto bei inaanzia 1500 kilo mchele umeshuka bei sana mkuu
 
Napambana ila napoteza tu kila siku mzee mpka kwenda kufungua ofis mtu unaona kaziii kwasabab unajua kabisa naenda kuuza mzgo ambao haunipii faida yani kama nacheza tu na mwisho wa mwezi watu wanalamba kodii zao daah
Bora wewe kinaeleweka,Faida utapata tuu mkuu tunakoelekea ni pazuri miezi ya sikuku na wakulima wanajiandaa na mashamba, mchele utapanda nawe utapata Faida kubwa,Mungu Mwema
 
ww ndio mwenye matatizo na hao waliokushauri huko juu eti sijui kuna uchawi au ubadili biashara wengi wanakupotosha siku zote biashara ni uvumilivu.. ww ni mgeni na mpya kwenye biashara ya mchele eneo hilo ndio kwanza una miezi sita alafu eti unaumia roho kwa uliowakuta wanauza hadi tani 30 kwa siku lakini hutaki kujiuliza hao wenzio wana mda gani eneo hilo usikute wana miaka kuanzia 3 hadi 5 wanafanya biashara hapo washatengeneza connection za wateja wao wa kudumu na pia washaweka jina si unajua biashara za uswahilini nyingi zinaenda kwa kujuana na kiaminiana..sasa ww mgeni wa miezi sita tu apo unataka uuze na kupata faida sawa na hao waliokaa miaka hata 5 washatengeneza wateja wao wa kudumu.! tatizo wabongo wengi tunataka faida ya haraka kwenye biashara bila kutengeneza msingi kwanza mfano mleta mada anaona wivu na hasira kali jirani yake kuuza tani 30 kwa siku wengine mtaji hadi million 100 wakati hao wenzie wametumia miaka kibao kufika hapo walipo alafu yeye na miezi yake sita anataka awe level hizo wakati nao walianza chini miaka imepita kama anavyoanza yeye leo.. pambana na ww kutengeneza connection zako na wateja wako wa kudumu miaka miwili mbele utaanza kula matunda
Huyu anahangaika pale kuna ulozi mkubwa tu. Mbagala ile ina mambo mengi sana
 
Back
Top Bottom