Naombeni ushauri kuhusu kubadili dhehebu ili kufunga ndoa

Naombeni ushauri kuhusu kubadili dhehebu ili kufunga ndoa

Sijui, ndo naomba unijuze
Kwa ufupi kabisa na kwa msisitizo.
Ni wanaume wachache sana wanakubaliana na takwa lako. Yaani wewe uanze kum-control mumeo mapema tu hivyo? Yeye kapanga kufunga ndoa ya kanisani, wewe unataka umbadilishie utaratibu wake mfunge ndoa ya serikali. Sasa nani kichwa cha familia yenu? Ni wewe au mumeo? Unaelewa maana ya kichwa cha familia? Wewe unatafuta kuanza kumtawala mumeo mapema kabisa.


Nakushauri, kama huwezi kuwa msabato, vunja huo uchumba. Tafuta mkatoloki mwenzio mfunge ndoa. Afu katoliki nfo dhehebu la wakristo wengi huwezi kukosa mchumba in huko.

Hivi unajua changamoto wanazopata wale ambao wanapeana uhuru wa mke kwenda kanisa analotaka?
 
Mchumba wako; unampenda sana; mwanaume wako.
Kwanza hapa ni kwamba nyie ni mke na mme,issue tu ni kwamba bado hamjahalalisha. Na ndo mnachokitaka.

Ushauri tu mdogo. Siku zote nafsi yako ikisitasita,ikasita zaidi ya mara moja,jihadhali.
Kama anaoa dini,sawa,muache atafute wengine,usilazimishe. Kila mtu ana uhuru wa kuamini kile anachokiamini. Maana hata ukibadili,ili tu uolewe,si kwamba utakuwa umependa,bali ni shinikizo. Sasa basi, we uidhalau nafsi yako utakuja kujuta
 
Mm Sina shida na watt wake kunifu

Ata mm, m nachotaka tu niwe na Ile freedom of worship bhc...na stk nifanye kwa kujificha
Tafuta mkatoliki mwenzio binti. Unataka kwenda kwenye ndoa ambayo hata hutaki kujua watoto wako wanaendaje kanisani? Yaani ukazae watoto halafu huna time nao kuhusu issue za kanisa!

Halafu huna freedom ya masuala ya mapishi? Wewe utanunua chakula flani, mumeo atasema hicho chakula usipikie hapa. Utafanyaje?

Kifupi, kwenye ndoa inataka watu mna mtazamo unaofanana kiimani na kijamii.
 
Mimi sioni tatizo kwa vile kwa Tz hasusani mila zetu mke anamfuata mume ...Mnaweza kufunga kwa upande wa mume ila bado wote ni wakristo na kila mtu atafuate dhehebu lake baada ya hapo..

Ila tambua watoto watafuate kwa baba.
Huo mstari wa mwisho,Sasa mama atawafundisha watoto Nini wakati Dini ya baba haijui? Kumbuka mlezi mkuu wa watoto ni mama.Mfano huyo dada ni mkatoliki ,katika ukatiloki kuna stages mfano,kubatiza watoto wakiwa bado wachanga,komunio,na kipaimara lkn kwa wasabato hiyo hamna.

Sasa nani atawasimamia Hawa watoto katika misingi ya Dini?
Ndio maana ni vizuri sana kuoana watu wa dhehebu Moja,na ikiwa mmependana madhehebu tofauti ni lazima mmoja afate Dini ya mwenzake(,Hasa mwanamke).

Ndio maana siku huzi unakuta familia Moja lakn watoto wana Dini tofauti.
 
Mchumba wako; unampenda sana; mwanaume wako.
Kwanza hapa ni kwamba nyie ni mke na mme,issue tu ni kwamba bado hamjahalalisha. Na ndo mnachokitaka.

Ushauri tu mdogo. Siku zote nafsi yako ikisitasita,ikasita zaidi ya mara moja,jihadhali.
Kama anaoa dini,sawa,muache atafute wengine,usilazimishe. Kila mtu ana uhuru wa kuamini kile anachokiamini. Maana hata ukibadili,ili tu uolewe,si kwamba utakuwa umependa,bali ni shinikizo. Sasa basi, we uidhalau nafsi yako utakuja kujuta
Asante 🥺🥺🥺
 
Nakuambia.
Ukisikia Watu wengi wakisema ndoa ndoano hicho ndicho nilichoeleza.
Mtu hamfanani alafu unalazimisha kuanzishwa familia.

Unajua maana ya familià?
Familia ni kuwa kitu kimoja.
Sasa huyu anaimani hii, yule anaile, huyu anaelewa hivi yule anaelewa vile.
Huyu ndiyo yake ni hii, mwingine ndoto yake ni ile. Hapo ni machafuko hakuna familia.

Usabato au Ukatoliki haufanyi ndoa iwe na furaha. Ila mkiwa na imani sawa kumhusu Mungu hapo ndoa lazima iwe na furaha.

Wasabato wanaamini, siku ya ibada ni Sabato, jumamosi. Wakatoliki hamuamini. Wasabato hawaamini katika Kuombea marehemu, wakatoliki mnaamini. Wasabato hawaamini katika sala ya Mama Maria, wakatoliki wanaamini.
Wasabato hawali nguruwe, Wakatoliki mnakula.
Hivi hapo kuna familia kweli?

Mtakuwa pamoja kweli? Mtaweza kulea watoto au ndio mtawachanganya au kuwaacha walelewe na ulimwengu?

Kama ni mimi nashauri achaneni ikiwa kila mmoja amebaki kwenye ubinafsi wake.
Na isitokee yeyote akahamia kwa mwenzake kinafiki. Huko ndio kubaya zaidi.
 
Tafuta mkatoliki mwenzio binti. Unataka kwenda kwenye ndoa ambayo hata hutaki kujua watoto wako wanaendaje kanisani? Yaani ukazae watoto halafu huna time nao kuhusu issue za kanisa!

Halafu huna freedom ya masuala ya mapishi? Wewe utanunua chakula flani, mumeo atasema hicho chakula usipikie hapa. Utafanyaje?

Kifupi, kwenye ndoa inataka watu mna mtazamo unaofanana kiimani na kijamii.
🥺🥺🥺🥺🥺
 
Nimeshaongea nae kila kitu na kwa namna niwezavyo lkn hataki..afu kinachonishàgaza sio ata mtu wa kanisani enda yake ya Mara moja au mbili kwa mwaka..Ila tu nyumban kwao baba yake ni mchungaji wa kanisa nahisi ndo Mana inakuwa hivi
Kuwa makini sana na huyu mtu.

Utakuja kunishukuru badae
 
Nakuambia.
Ukisikia Watu wengi wakisema ndoa ndoano hicho ndicho nilichoeleza.
Mtu hamfanani alafu unalazimisha kuanzishwa familia.

Unajua maana ya familià?
Familia ni kuwa kitu kimoja.
Sasa huyu anaimani hii, yule anaile, huyu anaelewa hivi yule anaelewa vile.
Huyu ndiyo yake ni hii, mwingine ndoto yake ni ile. Hapo ni machafuko hakuna familia.

Usabato au Ukatoliki haufanyi ndoa iwe na furaha. Ila mkiwa na imani sawa kumhusu Mungu hapo ndoa lazima iwe na furaha.

Wasabato wanaamini, siku ya ibada ni Sabato, jumamosi. Wakatoliki hamuamini. Wasabato hawaamini katika Kuombea marehemu, wakatoliki mnaamini. Wasabato hawaamini katika sala ya Mama Maria, wakatoliki wanaamini.
Wasabato hawali nguruwe, Wakatoliki mnakula.
Hivi hapo kuna familia kweli?

Mtakuwa pamoja kweli? Mtaweza kulea watoto au ndio mtawachanganya au kuwaacha walelewe na ulimwengu?

Kama ni mimi nashauri achaneni ikiwa kila mmoja amebaki kwenye ubinafsi wake.
Na isitokee yeyote akahamia kwa mwenzake kinafiki. Huko ndio kubaya zaidi.
🙌 Hatari...ni kweli usemacho🙏
 
Back
Top Bottom