Naombeni ushauri wenye busara juu ya hili

Naombeni ushauri wenye busara juu ya hili

Wakuu, Shkaamooni. Mimi ni kijana mdogo ambae niko kwenye ndoa tayari. Ndoa yangu ina miezi kadhaa tu, haijafikisha hata mwaka mmoja...
Pole kijana wa ki sasa. Ndoa ndoano. Vumilia ukiskia ya mwenzako baci ya kwako ni mepeci. Kama unampenda uo mke uliomuoa kwa ridha yako bila kushikiliwa bunduki wala kukalishwa kwa ndoa ya mkeka isipokua ni maamuzi yako. Baci jua kijana Uo mke wako anahaki kwa kila jambo alolitenda.

Kwanza umesha apa mbele ya umati na watumishi wa mungu kua utamlinda na kumpambania kwa kila jambo lake.

Msaidie mwenza wako na acha mfumo dume ulemavu wa homa yake isiwe chambo cha kumvua chupi yake hadharani. Chamgamoto zake ni za kawaida zinatibika hata ma hospitali na kwa wataalamu wa jadi
 
Wakuu, Shkaamooni. Mimi ni kijana mdogo ambae niko kwenye ndoa tayari. Ndoa yangu ina miezi kadhaa tu, haijafikisha hata mwaka mmoja...
Hayo malalamiko ulioamua kufa nayo kiume ndo ambayo baba kaambiwa na anataka kusikia kutoka kwako...

Jingine ulitegemea kitu gani extra special kutoka kwa mkeo kitandani?
 
Wakuu, Shkaamooni. Mimi ni kijana mdogo ambae niko kwenye ndoa tayari. Ndoa yangu ina miezi kadhaa tu, haijafikisha hata mwaka mmoja...
Kwa kuwa uko bussy sana naamini pia uko na kipato cha kutosha,ugonjwa ulioutaja unatibika mtibu mkeo kwa gharama yoyote na mambo yatakuwa murua😁
 
1. Wewe umeyataka mwenyewe. Ulishaambiwa kataa ndoa,ukaona ya nini. Umeshayavulia,yaoge. Kwani,ikitokea ukajikuta we ndilo huna uwezo wa kuzaa? Utupwe? Kama ulijua ana tatizo,ukamkubali hivyo hivyo,umemsaidia nini kulitatua? Wengine wamekaa miaka zaidi ya 10 na wametulia,wewe unalalamika tu.

Pointi namba 2. Eti ulichokitarajia siyo ulichokikuta. Huko kote ulikoonja,kuna mmoja uliona anafaa. Kwa nini usingemchukua huyo kuliko umlinganishe na huyo uliemchagua?

Kwa ushauri,bora uache. Kwa sababu vitu ulivyo navyo akilini hutoweza kuvivumilia,na ufumbuzi hutopatikana. Maana ulichotarajia utakipata kwingine si kwake. Na kwake sasa utakuwa hurudi tena
 
Ulikasirika nn kama sio ukweli?Siungempa ukweli straight akakutaftie ukweli Kwa mke wake?Tatizo Wanaume tunajifanya mambo ya Siri kumbe tunafuga ugonjwa.Kaa na Dingi mwambie ukweli acha Siri za kijinga bro.
 
Upele humuota asiye na kucha. Dogo kupiga mti unashindwa kweli kisa projects? Are u serious?
 
Amaah kweli, Upele humuota asiye na kucha. Dogo kupiga mti unashindwaje kisa projects? Are u serious?
 
Mdogo wangu kila jambo linakuja kwa wakati wake. Hao wenzako ni wakati wao ulifika subiri na wewe wa kwako. Lakini pia wekeza muda wako kiasi na familia yako achana na ubusy usio na maana. Kupitia hilo mnaweza solve matatizo na migogoro midogo midogo kama hii.

Hakuna mwanamke anapenda kuwa ignored hasa katika situation mlonayo sasahivi. Fikiria kwa makini
Aisee ubusy huu jamani yaan kipindi Fulani ukipiga demu dry mwezi unaletewa mimba wakati hata godoro haujanunua...pambana pata pesa Jenga mijengo nunua gari anzisha makampuni then unashangaa changamoto ya kupata watoto & vice versa is true
 
hiyo shida ya mkeo kama ni kuvurugika kwa siku zake au hedhi yake naweza kukusaidia bure atakaa sawa na mbegu zitachipua
 
Nalima, Napanda ila sioni dalili ya mazao. Hili ndio tatizo mpaka nakata tamaa
Nendeni wote hospitalini...

Fanyeni vipimo vya uzazi wote, narudia wote maana naona lawama zipo kwa mkeo wakati wewe hujijui kuwa unatatizo au hauna...

Acha kujipa stress za kufikirika wakati haujaenda hospitalini
 
Mwanamke akiwa na shida kiafya, Me wengi huwa sio wavumilivu.

Wewe ndo una matatizo. Ulimuoa wa nini kama hakuvutii, ana shida kiafya na huwezi kumtimizia takwa la kindoa.

Kama huwezi kumgonga na uko bize sana muache. Alikubali umuoe ili umchape na mkuyenge na sio akupikie tu.

Vijana wa kizazi hiki hamfai kuoana mnalazimisha na kuiga tu. Vijana waliozaliwa 2000 hasa wa kiume bi vizuri wakaoa 2035.
 
nikamtie mtoto wa mtu mimba ndo akili iwakae sawa hawa mana naona kama dharau hivi.
Kumbe unaweza kutia watoto wa watu mimba,why isiwe kwa mkeo ?

Turudi kwenye mawazo.

Mkuu mke wangu ana ile kitu inaitwa "quality time" yaani anapenda utenge muda alafu mzungumzee wawili tu huku mkitazamana.

Wanawake wengi wanapenda hiyo kitu.

Ila jambo lingine kwa ubize wako huyo mke hata hilo tendo la ndoa inaonesha hawezi kuenjoy kwa sababu hamna ile intimacy,hamna ile kuzoeana na kupiga stori za hapa na pale jambo ambaĺo kwa mwanamke linachangia kumfanya afurahi kwenye tendo.

So huyo dada kaleta lalamiko hilo la ubize lakini naamini nyuma ya pazis ana malalamiko mengine ambayo huwenda aliona ni busara asiyaweke wazi.

Chakufanya jitathmini,mchunguxe mwenzio na fikiria ni nini anataka mke wako na jibu utalipata
 
Sasa kijana mdogo kwenye ndoa umefata nini?

Acha uvivu kusingizia kazi! Mpe mtoto wa watu mitiii
Hiyo damu mfululizo inatibika kiroho. Waone watumishi wa Mungu. Wawaombee kwa Jina La YESU litaisha.

Mungu alitupa zawadi kubwa sana, ila sisi hatujitambui tu, kwa Jina la YESU Kila kitu kinakaa sawa.
 
Dah mkuu kwanza umesema we bado yanki, Then still ndo ina muda mfupi sana ila tayari mshaanza migogoro oya weeh mkifika boxing day mmojitahidi sana
 
Wakuu, Shkaamooni. Mimi ni kijana mdogo ambae niko kwenye ndoa tayari. Ndoa yangu ina miezi kadhaa tu, haijafikisha hata mwaka mmoja.

Wiki kadhaa nyuma tulikuwa tukipishana sana na mke wangu sababu ya mimi kuwa busy sana mpaka mida ya usiku mimi nipo busy na kazi.

Hii ikapelekea mimi na mke wangu tugombane mpaka malalamiko kufikia kwa wazazi.

Malalamiko ya mke wangu kwa wazazi wangu ni juu ya ubusy wangu na kupelekea kukosa muda na mke wangu, na mimi nikajitetea kwamba nina project zinazonibana sana nikashindwa hata kuwaza mambo mengine tofauti na project inayonikabili.

Nilitoa sababu hio japokuwa ndani ya nafsi yangu kuna malalamiko mengine ambayo nimeamua kufa nayo kiume siku hiyo.

Jambo la kwanza ni kuhusu hali ya mwenza wangu kuwa na matatizo ya hedhi, hili tatizo alikuwa nalo muda mrefu sana na mpaka wazazi wake waliwahi mwambia kuwa anaweza pata shida kwenye kutafuta mtoto. (hili aliniweka wazi baada ya kubleed kwa miezi miwili mfululizo).

Jambo la pili ni ubora wa shughuli. Yaani sipati kile nilichokitarajia.. ila hii sio tatizo kubwa kwangu as long as tabia zake zinaniridhisha.

Sasa mpaka naandika uzi huu.. Mzee(Baba yangu) aliniuliza swali ambalo limenipa hasira na kuniweka na mawazo sana. Ameniuliza kama nina tatizo la mwili nimwambie nisimfiche ( yaani kama sina nguvu za kiume nisifiche ).

Hili swali limenikwaza sana na limenipa hasira mpaka napatwa na mawazo ya kishetani. Najisemea au nikamtie mtoto wa mtu mimba ndo akili iwakae sawa hawa mana naona kama dharau hivi.

Naombeni ushauri nifanyeje kwenye hii situation?
Je ingekuwa wewe ungefanyaje au kama uliwahi pitia je ulikabiliana nalo vipi?
Umeoa kwa kumuonea huruma, kijana wangu Mimi sina cha kukushauri we pambana tu na huo mzigo wako umeuchagua mwenyewe hakuna aliekuchagulia, ulipofika hapo kwenye hedhi bleeding mwezi mzima miezi miwili mfululizo mtu anavuja damu tu, ningekua Mimi ningejitoa mapema sana Ila wewe ulimuonea huruma mgonjwa wako endelea nae mpaka apone, olevwa!
 
Back
Top Bottom