Nape Nnauye: Mwenyezi Mungu ameamua ugomvi

Nape Nnauye: Mwenyezi Mungu ameamua ugomvi

Ilikuwaje akakuacha mkuu??maama kama ufala ni mwingi uko nao
Maiti kwenye sandarusi kwenye fukwe za bahari, zika fastaaa hakuna cha uchunguzi.

Any way, hivi yule zakaria tajiri wa mabasi walimkosakosaje
 
Maiti kwenye sandarusi kwenye fukwe za bahari, zika fastaaa hakuna cha uchunguzi.

Any way, hivi yule zakaria tajiri wa mabasi walimkosakosaje
hawakumtaka serious labda walifika wakaanza tamaa za kutaka kumpiga hela.

hao wa kwenye viroba viranga vyao viliwaponza,mtu unafanya ugaidi unategemea nini??
 
Habarini JF GT!

Jana wakati Membe akirudishiwa kadi ya CCM, Mbunge wa Mtama na Wazari wa Habari nchini aliongea kauli mbaya Sana Na Yenye kufedhehesha kwa Marehemu.

Kwa tamaduni za kitanzia Sio sawa kumsema Marehemu, na hata Ukitaka kumsema Marehemu utamsema kwa Mazuri. Lakini hii imekuwa Tofauti kabisa kwa baadhi ya Wanachama wa CCM na Viongozi wa CCM, wamekuwa Wakimsema Hayati Magufuli Hadharani mbele ya wananchi waliomchagua kwa kura nyingi. Hakika CCM inajiua Yenyewe

Jana Ndugu Nape (Namuita Ndugu kwasababu kwangu mimi sioni kama Anafaa kupewa heshima ya Jina Mheshimiwa) wakati wa Sherehe zile alisimlia mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na Yeye alivyo nusurika kufukuzwa CCM na Membe kumsadia, kipindi hicho naamini Magufuli hakuwa Kiongozi mkubwa wa CCM, Nape aliongea kumaanisha kuwa Magufuli alikuwa chanzo kikubwa cha Membe kuondoka CCM na Kutengeneza ugomvi mkubwa na Wana CCM wengine.

Nape akaenda mbali zaidi na Kusema Kuwa Ugomvi huo Mungu ndio ameamua na sasa bahari imetulia iko shwari, akimaanisha Kifo cha Magufuli ni Maamuzi ya Mungu katika Kutatua ugomvi wa Wana CCM na Membe… Akaendelea mbele na Kusema nani Kama Rais Samia Suluhu.

Ikumbukwe kuwa Huu utamaduni uliopo sasa kwa kumsifia rais hata pale anapo fanya Baya ulianza kipindi Cha Magufuli na Umeendelea hadi awamu hii kwa kusema Mama anaupiga mwingi. Nyakati za Kikwete, Mkapa hakukuwa na huu ujinga.

Turudi kwenye mada, Nape Nauye ni lini Ataacha kuwa na Kinyongo na Marehemu? Nilini ataacha Kumsema Marehemu? Huu umekuwa muendelezo wake toka Awe Waziri tena Wa Habari, Je aliteuliwa kuja Kumsema Marehemu?

Ni wakati sasa Wa Nape kumuacha Marehemu Apumzike Mahali pema na kwa amani. Asitafute chuki na watu zisizo za msingi
Naunga mkono hoja
 
Ahaaaaaaaaaaa!!!,
ALIKUWA JEMBE HUYU JAMAA, yaani mpakasasa hawaamini kama amekufa!! Duh!!ahaaaaaaaa!
Kumbe waliumizwa sana!
KITENDO CHA KUMSEMEA MWENYEZI MUNGU ETI AMEAMUA NI KUMKEBEI MWENYEZI MUNGU!,

Mwenye akili asingefurahi kifo cha Magu!,
Angepata funzo kwamba magereza ni ya watu wote!
 
Nape kinachomuuma zaidi ni kitendo cha yeye kwa kujipendekeza kutembea kwa,magoti Ikulu huku akirekodiwa alipokwenda kumuomba,msamaha Magufuli. Hiyo rekodi haifutiki milele. Magufuli hakumwambia Nape atembee kwa magoti bali kiherehere chake cha kinafiki. Nafikiri hilo jambo linamtesa sana. Laiti angejua .Magufuli angekufa punde baadae asingefanya lakini too late.

Nape aliwahi kufukuzwa CCM na mzee Makamba huku akitamba kuwa amemfuta duniani na mbinguni, isingekuwa Jk kumuokoa angekuwa historia mbona hamuwekei kinyongo Makamba;

Kuendekeza nja kubaya sana.
Dawa ya hila ni hila!
 
Haya ukitoa Nape na hasira zake kwa Mwendazake lakini chama pia kinayabariki. Amezungumza hadharani na viongozi wakiwepo. Hizi mbegu wanazipanda wenyewe tena kwa msisitizo! Hicho chama visasi havitakoma, bahati mbaya vitagharimu Taifa.
MTAZAMO, ndugu yangu, wacha watu wateme nyongo zao!
NAKUKUBALI SANA LAKINI KWA HILI NAOMBA TUGAWANE MISIMAMO! ... JAMAA ALIKUWA SIO, NAWEWE UNAJUA!
 
Angalieni sana haya mazumbukuku yanayomtetea Magu ndiyo yaliyomuharibia utawala wake! Ikumbukwe kuwa Magu hakuwahi kuteka/kuua binafsi. Ni hii mijambazi iliyomzunguka ndiyo iliyojipendekeza kwa kuua ili yaibe kwa amani. Kwa vile jamaa alikuwa hana uzoefu wa uongozi wa juu yaani urais aliyaamini haya majitu yakamuharibia. Narudia tena bila hizi mbwa/ aina ya sabaya na makonda Magufuli angeng'aa duniani!
 
Ila kina Nape haya maneno ya shombo yatawacost ikitokea Rais Ajaye akawa na akili atawapiga chini wote

Ningekuwa Rais uchaguzi ujao Kuna majimbo Bora niwape wapinzani tu, Nape ni mropokaji

Unaamini raisi ndiye anagawa majimbo?
Kweli tunahitaji Katiba Bora itakayowaamsha waliolala kama wewe?
 
Angalieni sana haya mazumbukuku yanayomtetea Magu ndiyo yaliyomuharibia utawala wake! Ikumbukwe kuwa Magu hakuwahi kuteka/kuua binafsi. Ni hii mijambazi iliyomzunguka ndiyo iliyojipendekeza kwa kuua ili yaibe kwa amani. Kwa vile jamaa alikuwa hana uzoefu wa uongozi wa juu yaani urais aliyaamini haya majitu yakamuharibia. Narudia tena bila hizi mbwa/ aina ya sabaya na makonda Magufuli angeng'aa duniani!

Hatumtetei Magu, tunazungumzia kauli ya nape
 
Fikiria sasa hivi Ole Sabaya angekuwa RC wa Kilimanjaro na Muro wa Dar, Makonda waziri wa mambo ya ndani, Bashiru Katibu mkuu kiongozi, Polepole waziri wa Habari, Mnyeti waziri wa katiba na sheria, Mambosasa IGP, Musiba bado mwanaharakiti huru, Ndugai Spika.
 
Fikiria sasa hivi Ole Sabaya angekuwa RC wa Kilimanjaro na Muro wa Dar, Makonda waziri wa mambo ya ndani, Bashiru Katibu mkuu kiongozi, Polepole waziri wa Habari, Mnyeti waziri wa katiba na sheria, Mambosasa IGP, Musiba bado mwanaharakiti huru, Ndugai Spika.
Umewaza mbali sana, ila Mungu ni mwema kwa Watanzania
 
Habarini JF GT!

Jana wakati Membe akirudishiwa kadi ya CCM, Mbunge wa Mtama na Wazari wa Habari nchini aliongea kauli mbaya Sana Na Yenye kufedhehesha kwa Marehemu.

Kwa tamaduni za kitanzia Sio sawa kumsema Marehemu, na hata Ukitaka kumsema Marehemu utamsema kwa Mazuri. Lakini hii imekuwa Tofauti kabisa kwa baadhi ya Wanachama wa CCM na Viongozi wa CCM, wamekuwa Wakimsema Hayati Magufuli Hadharani mbele ya wananchi waliomchagua kwa kura nyingi. Hakika CCM inajiua Yenyewe

Jana Ndugu Nape (Namuita Ndugu kwasababu kwangu mimi sioni kama Anafaa kupewa heshima ya Jina Mheshimiwa) wakati wa Sherehe zile alisimlia mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na Yeye alivyo nusurika kufukuzwa CCM na Membe kumsadia, kipindi hicho naamini Magufuli hakuwa Kiongozi mkubwa wa CCM, Nape aliongea kumaanisha kuwa Magufuli alikuwa chanzo kikubwa cha Membe kuondoka CCM na Kutengeneza ugomvi mkubwa na Wana CCM wengine.

Nape akaenda mbali zaidi na Kusema Kuwa Ugomvi huo Mungu ndio ameamua na sasa bahari imetulia iko shwari, akimaanisha Kifo cha Magufuli ni Maamuzi ya Mungu katika Kutatua ugomvi wa Wana CCM na Membe… Akaendelea mbele na Kusema nani Kama Rais Samia Suluhu.

Ikumbukwe kuwa Huu utamaduni uliopo sasa kwa kumsifia rais hata pale anapo fanya Baya ulianza kipindi Cha Magufuli na Umeendelea hadi awamu hii kwa kusema Mama anaupiga mwingi. Nyakati za Kikwete, Mkapa hakukuwa na huu ujinga.

Turudi kwenye mada, Nape Nauye ni lini Ataacha kuwa na Kinyongo na Marehemu? Nilini ataacha Kumsema Marehemu? Huu umekuwa muendelezo wake toka Awe Waziri tena Wa Habari, Je aliteuliwa kuja Kumsema Marehemu?

Ni wakati sasa Wa Nape kumuacha Marehemu Apumzike Mahali pema na kwa amani. Asitafute chuki na watu zisizo za msingi
Angesema mpinzani tusingelala
 
Acha hiyo ya eti marehemu hasemwi. ukifa kwa kutenda mabaya utasemwa mpaka basi. Magufuli was a dictator, amepoteza, ameua, amedhulumu etc etc wengi. Akifa acha watu wasee mabaya yake.
Umesahau kuwanyima wanafunzi mikopo,..mxiuuu zake jiwe.
 
Back
Top Bottom