Natabiri jaribio lolote la kubadilisha Katiba na ukomo wa Rais litaibua mazito

Natabiri jaribio lolote la kubadilisha Katiba na ukomo wa Rais litaibua mazito

Uganda haina utamaduni wa marais kuheshimu term limits.

Tanzania tangu aondoke Nyerere marais wote wameheshimu term limits.

Na hata Magufuli amesema hatazidisha muhula wake.

Sasa huu mchecheto wa kusema Magufuli ataongeza muda unatokea wapi?
Naamini hata wewe ukiyapitia haya mawazo yako siamini kama utaamini ni wewe umeandika.

"HISTORIA NI JANA, LEO NA KESHO. HISTORIA SIO KITU STATIC NA SIKU ZOTE NI LAZMA LITOKEE JAMBO AU WATU AU MTU WA KUIBADILISHA NA AKIWA NA NGUVU INAYOTAKIWA, ATAIBADILISHA"..

Alihitajika Mao kuwatoa wachina kwenye Umaskini

Alihitajika Mugabe kuiweka Zimbabwe kwenye endless embargos

Ilihitajika umwagaji wa damu kuhakikisha Moi haendelezi udikteta wake Kenya

Alihitajika Kagame kuendeleza uongozi alionao

Ilihitajika ANC na viongozi wake kukomesha Apartheid

Ilihitajika TANU kuondoa Ukoloni Tanganyika

Monoparty system imekaa na Nyerere akiwa kama Rais kwa Muda gani hadi Leo hii useme itashindikana

Historia Ya namna hiyo haijawahi kuwapo toka enzi za Misri, Rumi, Uingereza na hata sasa Marekani..

Moyo wa Historia ni mabadiliko maana Jana haiwezi kuwa sawa na leo wala Kesho..
 
Ok, mm sipo vizuri kwenye mambo ya fasihi za muziki hivyo sawa.
Mchecheto upo unaweza kuwa na sababu kuu mbili.. Kwanza ni kuweka presha kama kuna kusudio la kuongeza muda, au kupima upepo juu ya kusudio la kuongeza muda.
Hizo ni siasa za kubahatisha.

Kibaya zaidi, hizi kelele zinaweza kumfanya mtu ambaye hana nia ya kuongeza muda aongeze muda.

Kuna mambo muhimu ambayo hayahitaji kubahatisha ambayo yakiwekewa shinikizo yanaweza kuzaa matunda.

1. Mabadiliko ya katiba.
2. Tume huru ya uchaguzi.
3.Upinzani kujipanga kutqfuta haki kimataifa.
4. Upinzani kupinga matokeo ya uchaguzi feki.
4.Kumulika mapungufu ya utawala bora.

Wapinzani wa Magufuli wakianza kuongelea uchaguzi wa 2025 kwa kusema Magufuli atazidisha muda wake, ni kama washakubali wizi uliotokea 2020 na kuupitisha.

Vinginevyo, kwa nini umshitaki Magufuli kwa wizi unaofikiri ataufanya 2025 wakati una ushahidi wa wizi alioufanya 2020?
 
CCM hii haina aibu inaweza kufanya lolote na kama mnavyojua bunge hetu ndilo hilo kama kikao cha Halmashauri ya chama chao yaani ni kuoiga muhuri lolote linalopelekwa humo.
 
Fahamu tu kuhusu haya machache.
1. Hakuna Dikteta aliyebadilisha katiba ili kuongezewa muda akawa analiongea hilo suala kabla. Mara zote hukana au kukaa kimya wakati vuguvugu likishika kasi. Wanaolisema huwa ni wapambe wa watawala.

2. Suala hili limekuwa likipigiwa debe na viongozi waandamizi na wateule wa Magufuli kwa muda mrefu sasa, na hakuna hata mmoja aliyechukuliwa hatua za kinidhamu na Magufuli mwenyewe wala na CCM.

3. Jambo linalosemwa semwa na watu tofauti tofauti kwa nyakati tofauti kuwa linapangwa kutokea, maana huo mpango upo au huenda ukawepo tu nyuma ya pazia. Watu husema kile wanachokiona, kukisikia au kukihisi.
1. Kwamba hakuna dikteta aliyebadilisha katiba ili kuongezewa muda aliyeongelea hilo, hakumfanyi Magufuli aongeze muda.
Sasa, wewe unajuaje kwamba Magufuli ataongeza muda? Una ushahidi gani zaidi ya speculations tu?

2. Wapambe huwa hawakosi. Lakini hao ni wapambe, kitu muhimu ni rais mwenyewe anataka kufanya nini?
Nyerere alihutubia katika hotuba yake moja, akasema, alikuwa anataka kujiuzulu kwa muda mrefu.Lakini kila akitaka kujiuzulu, wapambe wake wakawa wanamuambia "Mwalimu endelea kidogo, taifa linakuhitaji sana".Kila akitaka kujiuzulu akawa anaambiwa hivyo.Mwishowe akasema akaja kugundua kwamba hawa wapambe waliposema "taifa linakuhitaji", maana yao haikuwa taifa linamuhitaji,ila wao wenyewe walikuwa wanahitaji Nyerere aendelee kuwa rais, kwa sababu walihofia akija rais mwingine atakuja na watu wake.

Nyerere alivyowasitukia, akasema aliwapuuza na kujiuzulu.

Kwa hivyo, hawa wapambe wapo tu, hawajaanza leo.Walikuwepo tangu enzi za Nyerere.

Sasa, mnashikia bango suala la wapambe ambalo rais mwenyewe kashasema hataongeza muda?

3.Let's separate facts from speculations.Ukitaka kujadili speculations unaweza kusema lolote. But where are the facts?

The facts are.

1.Mgufuli kakanusha kwamba ataongeza muda.
2.Katiba hairuhusu hilo.
3.Wanalosema hilo ni wapambe tu.

Magufuli ana makosa mengi sana, ambayo kashayafanya.Mengine ya juzi tu kwenye uchaguzi wa 2020.

Kwa nini tunamtungia makosa ambayo hata hajayafanya bado badala ya kuangalia makosa aliyokwishafanya tayari?

Mtu anayemlaumu na kumhukumu Magufuli kwa makosa atakayoyafanya mwaka 2025 ni kama tajiri bilionea mwenye mali nyingi sana, ambaye licha ya utajiri wake na kuwa na hela zote anazohitaji, bado anakwenda benki kuomba mkopo, tena mkopo wa riba ya juu sana.

Mna utajiri wa makosa ya Magufuli, kwa nini mnaenda kukopa benki kwa riba kubwa sana?
 
Mkuu tunapenda iwe hivyo lakini kwa plan za JIWE sidhani ila ikitokea 2025 akastaafu itakuwa ajabu sana.
Ninachoona ni kwamba Jiwe kafanikiwa kuwafanya wapinzani wake wamuogope kuliko njaa.

Yani wanamuhofia kwa mambo yenye mantiki na mambo ya paranoia tu.

Kama nia yake ilikuwa kuogopwa tu, naona amefanikiwa.

Yani wapinzani wamekuwa kama watoto yatima wasiojua kipi cha msingi cha kupinga, na kipi ni uzushi tu.
 
Naamini hata wewe ukiyapitia haya mawazo yako siamini kama utaamini ni wewe umeandika.

"HISTORIA NI JANA, LEO NA KESHO. HISTORIA SIO KITU STATIC NA SIKU ZOTE NI LAZMA LITOKEE JAMBO AU WATU AU MTU WA KUIBADILISHA NA AKIWA NA NGUVU INAYOTAKIWA, ATAIBADILISHA"..

Alihitajika Mao kuwatoa wachina kwenye Umaskini

Alihitajika Mugabe kuiweka Zimbabwe kwenye endless embargos

Ilihitajika umwagaji wa damu kuhakikisha Moi haendelezi udikteta wake Kenya

Alihitajika Kagame kuendeleza uongozi alionao

Ilihitajika ANC na viongozi wake kukomesha Apartheid

Ilihitajika TANU kuondoa Ukoloni Tanganyika

Monoparty system imekaa na Nyerere akiwa kama Rais kwa Muda gani hadi Leo hii useme itashindikana

Historia Ya namna hiyo haijawahi kuwapo toka enzi za Misri, Rumi, Uingereza na hata sasa Marekani..

Moyo wa Historia ni mabadiliko maana Jana haiwezi kuwa sawa na leo wala Kesho..
Sitaki kuamini, nataka kujua.

Just the facts please.

The facts are.

1. Tanzania haina utamaduni wa marais kuongeza muda.
2.Katiba hairuhusu hilo.
3.Magufuli kasema hataongeza muda.
4.Wapambe wa kusema rais aongeze muda walikuwepo tangu enzi za Nyerere.
5.Habari za kwamba Magufuli ataongeza muda ni speculations tu, hazina msingi wa fact.
 
Baada ya watanzania kunyamaza kwenye ujinga uliofanyika, Safari hii wasicheze na katiba nchi italipuka moto, yaani katika jambo ambalo ccm wasicheze nalo ni kubadili ukomo wa Rais.
 
Natabiri yakuwa jaribio lolote la kubadili katiba nakurefusha ukomo wa Rais litazuwa Moto wa kisiasa ambao haukuwahi kutokea tangu kuwepo kwa Taifa hili.

Yani hamtoamini wala kudhania. Itakuwa ni siku mbaya na nzito kwa Taifa ndipo sote tutaamini kweli kuna deep state in side state.

Nasali Jambo hili lisitokee wala kusemwa tu. Madhara yake yatatutesa sana kama Taifa.

Mungu ibariki Tanzania.
Kuna majaribio mengi ya kihuni yamepita na maisha yanaendelea. Kitendo cha kuondoa upinzani bungeni sio cha bahati mbaya, bali ni mkakati maalum kwa ajili ya maamuzi ambayo tutabaki kusikitika na kulaani kwa maneno tu kama ilivyo kawaida yetu. Pamoja na kwamba mzee alisha tamka kwamba hatoongeza hata dakika muda wake ukiisha, lakini tusubiri usemi mwingine kwamba yeye hakuwa na nia hiyo lakini ameombwa kuendelea na ameona akubaliane na maombi hayo kwa sababu anaipenda nchi yake na pia anatupenda wananchi wanyonge wa nchi hii. Na tulivyo wanyonge kweli hilo nalo litafanyika na maisha yataendelea. Tujikumbushe tu kwamba 2015 mzee hakuutaka urais bali alisukumiziwa tu, na muda si mrefu atasukumiziwa na muda wa nyongeza.
 
Kwanza kabisa, niseme mimi si mtetezi wa Magufuli wala CCM. Ni mtetezi wa haki na mchambuzi wa siasa na mantiki.

Magufuli nishamsema sana, hivyo, ninachoandika hapa si kwa sababu ya kumtetea Magufuli.

Twende kwenye hoja baada ya dibaji hiyo.

Magufuli ameshasema mara kadhaa hataki kuongeza muhula wa urais.

Kwa nini mnafanya hili suala kuwa hoja?

Hususan kama kuna makosa mengi sana ambayo Magufuli ameshayafanya ambayo yanaweza kujadiliwa kama hoja halali, factually, na si speculation?

Mimi naona wapinzani wa Magufuli kuongelea hili kunaonesha yafuatayo.

1. Hawana focus. Wanakuwa kama mtu tajiri mwenye hela nyingi sana (wana hoja nyingi sana halali za kumsema Magufuli) lakini ambaye bado anaenda kukopa hela benki kwa riba kubwa sana (licha ya kuwa na hoja nyingi halali za kumsema Magufuli, wanaenda kukopa hoja qmbayo haina uhalali ya kuhusu makisa ambayo hayajafanyika,kiasi cha kufanya watu wahoji umqkini wao).

2. Hawajadili mambo kwa facts. Bali kwa speculations.

3. Wanahukumu kosa ambalo wanafikiri litatetendeka, badalq ya kuhukumu kosa lililotendeka. Hili ni jambo hatari. Kwa msingi huu, Magufuli anaweza kuamka siku moja akasema ameota wapunzabi wanataka kumpindua. Akawafunga wote.

4. Wanapoteza muda na nguvu kujadili speculations wakati kuna mambo muhimu ya kubana sasa hivi kama wizi wa kura katika uchaguzi, tume huru yq uchaguzi, katiba mpya etc.

5. Wanaonesha paranoia. Kitu ambacho hakifai katika uongozi.
Umesahau kama huyu huyu magufuli ndo aliahidi kuwa kutakuwa na uchaguzi huru na wa haki
 
Umesahau kama huyu huyu magufuli ndo aliahidi kuwa kutakuwa na uchaguzi huru na wa haki
Alisema pia kwamba hataki kusikia mtu anayemlipa mshahara kapitisha upinzani. Aliahidi ataumaliza upinzani 2020.

Hakuna kitu factual cha kuonesha Magufuli ataongeza muda.

Kelele zote ni speculations tu.

Ni sawa na kusema Magufuli ni nyonyadamu.

Ni hadithi za kutisha watoto.

Inasikitisha kuona mtu mwenye kesi ya mauaji 2020, ambaye kaua tayari mwaka 2020, na ushahidi upo, kesi yake ya mauaji ya 2020 haitajwi, watu wanalalamika kwamba huyu ataua mwaka 2025, tumhukumu kwa kesi ya kuua mwaka 2025!

Ina maana haya mauaji ya 2020 ndiyo mshayasahau au vipi?
 
Ulais kazi nzito ngumu niombeeni kwa mngu nisijawe kiburi, sitoongeza muda wa kutawara
Fungua uzi wako utakaozungumzia kazi ya ULAIS, kwenye huu uzi sisi wenye ubongo tunamjadili RAIS.
 
Hizo ni siasa za kubahatisha.

Kibaya zaidi, hizi kelele zinaweza kumfanya mtu ambaye hana nia ya kuongeza muda aongeze muda.

Kuna mambo muhimu ambayo hayahitaji kubahatisha ambayo yakiwekewa shinikizo yanaweza kuzaa matunda.

1. Mabadiliko ya katiba.
2. Tume huru ya uchaguzi.
3.Upinzani kujipanga kutqfuta haki kimataifa.
4. Upinzani kupinga matokeo ya uchaguzi feki.
4.Kumulika mapungufu ya utawala bora.

Wapinzani wa Magufuli wakianza kuongelea uchaguzi wa 2025 kwa kusema Magufuli atazidisha muda wake, ni kama washakubali wizi uliotokea 2020 na kuupitisha.

Vinginevyo, kwa nini umshitaki Magufuli kwa wizi unaofikiri ataufanya 2025 wakati una ushahidi wa wizi alioufanya 2020?
Kabla ya 2020 kuna waliobahatisha namna matokeo yatakavyokwenda. Uchaguzi wa 2020 ulishapita.
 
Unakubali mtu kuhukumiwa kwa kosa ambalo hajalifanya?

Yani nikwambie wewe unaonekana utaiba kesho.

Halafu wewe useme sitaiba.

Halafu tukupige mawe kwa madai kwamba utaiba kesho.

Unakubali?

Kwa nini mnamhukumu mtu kwa makosa ambayo mnafikiri atafanya 2025, wakati tayari ana.makosa aliyoyafanya ambayo mnaweza kumhukumu bila kubashiri mambo yatakayotokea mwaka 2025?

Mnafanya ionekane kama vile Magufuli ana uhaba wa makosa aliyoyafanya, na hivyo, mnalazimika kumtungia makosa atakayoyafanya mwaka 2025 na kumhukumu.kwa hayo.

Magufuli ana uhaba wa makosa aliyoyafanya tayari?
Ni kweli hatajiongezea, lakini asipojiongezea nitashangaa sana.
 
Kwa kweli hata mimi nampinga Magufuli kwa mengi sana, lakini katika hii hoja nasema kweli naiona ni hoja dhaifu sana.

Kwa sababu.

1. Magufuli ameshasema haongezi muda.Wapinzani wake wanataka nini zaidi?
2. Kuongeza muda si jambo dogo, ni suala la mabadiliko ya katiba.
3. Kumhukumu mtu leo kwa kosa ambalo unafikiri atalifanya miaka mitano ijayo ni jambo la kijinga kabisa.
4. Hii hoja inaonesha paranoia kwa wanaoipigia mbinja.
5. Hoja hii ina distort message na kuondoq focus kwenye hoja za maana kqma wizi wa kura uliotokea 2020 na hoja nyingine nyingi za maana.

Magufuli alisema uchaguzi huu utakuwa huru na haki, sisi tulisema Magufuli hana tabia ya kuheshimu box la kura. Jitokeze useme waliosema wakati ule walikuwa wanawaza ambayo hajatenda.
 
Back
Top Bottom