Mfikirishi
JF-Expert Member
- Jan 16, 2012
- 8,939
- 10,403
Mtu keshakuwa rais, ni ishara kuwa tumechelewa. Haya masuala ya lugha kama ni muhimu sana tuyaainishe kwenye katiba. Na kuweka vigezo vya lugha kwenye fomu ya wagombea ikiwa ni sambamba na ulazima wa kushiriki midahalo kwa lugha husika!Nitafurahi sana nikipata audio Clip ambayo itazidi dk 5 Rais wetu Mpendwa akichana mistari kwa kiingereza katika mahojiano au maelezo flani sehemu yoyote. Iwe imenyooka haijaungwa ungwa.
Nitafurahi sana. Tuachane na haya madai ya watu kuwa yeye huwa mara nyingi anasoma tu... Tunataka kuwaonesha watu kuwa hata amewahi hojiwa kwa English au akahutubia watu wa English.
Mpaka sasa ni Maraisi wawili tu wamewahi kuongea na Wasomi vyuoni. Mwalimu Julius K. Nyerere na Benjamini Mkapa. Hawa nimewahi wasikiliza. Kwa kweli tunahitaji miaka mingi kupata Marais Smart kama hawa wanaojiamini.
Mkapa hadi Midahalo alikuwa anakubali. Baada ya yeye hakuna ambaye amewahi kukubali midaharo.
Mpaka tufike huko, kwa sasa twende hivyo hivyo make hata lugha ya taifa haijulikani ni ipi.