Natafuta Audio Clip ya zaidi ya Dk 5 ambayo Rais Samia anazungumza Kiingereza

Natafuta Audio Clip ya zaidi ya Dk 5 ambayo Rais Samia anazungumza Kiingereza

Nitafurahi sana nikipata audio Clip ambayo itazidi dk 5 Rais wetu Mpendwa akichana mistari kwa kiingereza katika mahojiano au maelezo flani sehemu yoyote. Iwe imenyooka haijaungwa ungwa.

Nitafurahi sana. Tuachane na haya madai ya watu kuwa yeye huwa mara nyingi anasoma tu... Tunataka kuwaonesha watu kuwa hata amewahi hojiwa kwa English au akahutubia watu wa English.

Mpaka sasa ni Maraisi wawili tu wamewahi kuongea na Wasomi vyuoni. Mwalimu Julius K. Nyerere na Benjamini Mkapa. Hawa nimewahi wasikiliza. Kwa kweli tunahitaji miaka mingi kupata Marais Smart kama hawa wanaojiamini.

Mkapa hadi Midahalo alikuwa anakubali. Baada ya yeye hakuna ambaye amewahi kukubali midaharo.
Mtu keshakuwa rais, ni ishara kuwa tumechelewa. Haya masuala ya lugha kama ni muhimu sana tuyaainishe kwenye katiba. Na kuweka vigezo vya lugha kwenye fomu ya wagombea ikiwa ni sambamba na ulazima wa kushiriki midahalo kwa lugha husika!
Mpaka tufike huko, kwa sasa twende hivyo hivyo make hata lugha ya taifa haijulikani ni ipi.
 
Kwanza si kweli ,Putin anajua English,pili Russia hujifunza darasani jwa lugha yao sasa hawa wetu wamejifunza English tangu darasa la tatu hadi Phd ila hata kutamka neno enterpreneur hawezi

na sio enterpreneur ni entrepreneur[emoji3061]
 
Alifeli huyo ,Kasoma kwa kuunga unga.


Sasa ukweli nikwamba, hiyo nidalili tosha kua KICHWAN HAMNA KITU.
Wengi tu wamesoma kwa kuunga unga lakini kichwani wako vizuri sana. Watu wanakatisha masomo kwa sababu nyingi tuu. Hata stress nyingine zinachangia mtu kufeli ingawa uwezo anao. Tusimdhihaki mtu kwa kusoma kwa kuungaunga. Mtu huyo anastahili sifa ya kutokukubali kushindwa mpaka akatimiza malengo yake. Hivi karibuni tumeona wasomi wetu wenye Ph.D na uprofesa walivyo watupu. Makaratasi hayana maana tena.

Amandla...
 
Nitafurahi sana nikipata audio Clip ambayo itazidi dk 5 Rais wetu Mpendwa akichana mistari kwa kiingereza katika mahojiano au maelezo flani sehemu yoyote. Iwe imenyooka haijaungwa ungwa.

Nitafurahi sana. Tuachane na haya madai ya watu kuwa yeye huwa mara nyingi anasoma tu... Tunataka kuwaonesha watu kuwa hata amewahi hojiwa kwa English au akahutubia watu wa English.

Mpaka sasa ni Maraisi wawili tu wamewahi kuongea na Wasomi vyuoni. Mwalimu Julius K. Nyerere na Benjamini Mkapa. Hawa nimewahi wasikiliza. Kwa kweli tunahitaji miaka mingi kupata Marais Smart kama hawa wanaojiamini.

Mkapa hadi Midahalo alikuwa anakubali. Baada ya yeye hakuna ambaye amewahi kukubali midaharo.
Msikilize Nyerere kwenye mdahalo wa ana kwa ana. Interviews zake nyingi haziptikani sasa kwa sababu ya technoloy ya wakati huo.





Msikilize Mkapa ana kwa ana; huyu zipo nyingi sana kwa vile technology iliianza kukomaa wakati wa utawala wake



Msikilize Kikwete ana kwa ana hapa. Pamoja na technology wakati wa utawala wake. Siyo interviews nyingi zinazopatikana za papo kwa papo.



Msikilize Magufuli ana kwa ana. Huyu hakufanya interview kabisa wakati wa utawala wake.

 
Mpaka sasa ni Maraisi wawili tu wamewahi kuongea na Wasomi vyuoni. Mwalimu Julius K. Nyerere na Benjamini Mkapa. Hawa nimewahi wasikiliza. Kwa kweli tunahitaji miaka mingi kupata Marais Smart kama hawa wanaojiamini.

Mkapa hadi Midahalo alikuwa anakubali. Baada ya yeye hakuna ambaye amewahi kukubali midaharo.
Tufanye nini ili kusahihisha makosa yaliyofanyika kuwakosa watu wa aina ya Nyerere na Mkapa
 
Msikilize Nyerere kwenye mdahalo wa ana kwa ana. Interviews zake nyingi haziptikani sasa kwa sababu ya technoloy ya wakati huo.





Msikilize Mkapa ana kwa ana; huyu zipo nyingi sana kwa vile technology iliianza kukomaa wakati wa utawala wake



Msikilize Kikwete ana kwa ana hapa. Pamoja na technology wakati wa utawala wake. Siyo interviews nyingi zinazopatikana za papo kwa papo.



Msikilize Magufuli ana kwa ana. Huyu hakufanya interview kabisa wakati wa utawala wake.


Mbona hujamtaja Alhaji Mwinyi
 
Kweli hi Ni africa , mpaka mwaka 2022 na Karne hii bado tuna mawazo ya Nani muongeaji mzuri wa kiingereza.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
I’m always game. Nipigie tu simu tulonge hata masaa mawili au hata ukipenda siku nzima…
Nisingependa kuzungumza kwani sikijui lkn nataka kusikia cha kwako. Nadhani nitasikia Kiingereza cha Kisukuma, Kinyamwezi au Kikurya. Samia yeye anapiga RP hata kama ni cha kuandikiwa.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Mada iliyojaa fikra kale za kitumwa na isiyo na adabu!🙏🙏
 
We mjinga, tega sikiontukuelimoshe. Huwezi kutenganisha uelewa wa mtu na kujua kiingereza kwa hapa Tanzania. Asiyejua kiingereza maana yake hajaelimika. Kwasabb elimu yetu inatolewa kwa lugha ya kiingereza. Sasa mtu ataipataje elimu kama lugha inayotumika kuipata hiyo huijui??

Nchi unazoona zomeendelea lkn watu wake hawajui kiingereza ni kwamba wanatumia lugha zao kufundishia. Hawatumii Kiingereza.

Umenielewa we mfuasi wa jiwe?? Halafu hata wewe hujui kiingereza ndiyo maana inakuuma sana tukiwakosoa wasiojuq kiingereza. Pole sana
Hizo nchi ambazo wanatumia lugha zao kufundishia huwa kuna somo la english na lengo ni kuwafundisha kujua english, sasa iweje mtu asijue english wakati ni katika vitu alivyofundishwa shuleni?
 
Nitafurahi sana nikipata audio Clip ambayo itazidi dk 5 Rais wetu Mpendwa akichana mistari kwa kiingereza katika mahojiano au maelezo flani sehemu yoyote. Iwe imenyooka haijaungwa ungwa.

Nitafurahi sana. Tuachane na haya madai ya watu kuwa yeye huwa mara nyingi anasoma tu... Tunataka kuwaonesha watu kuwa hata amewahi hojiwa kwa English au akahutubia watu wa English.

Mpaka sasa ni Maraisi wawili tu wamewahi kuongea na Wasomi vyuoni. Mwalimu Julius K. Nyerere na Benjamini Mkapa. Hawa nimewahi wasikiliza. Kwa kweli tunahitaji miaka mingi kupata Marais Smart kama hawa wanaojiamini.

Mkapa hadi Midahalo alikuwa anakubali. Baada ya yeye hakuna ambaye amewahi kukubali midaharo.
Acha kuwa na fikra za kitumwa we mtu,sijui nani ameturoga sisi watu weusi
 
Tufanye nini ili kusahihisha makosa yaliyofanyika kuwakosa watu wa aina ya Nyerere na Mkapa
Ni hao tu wachache ndio wanaosifiwa sana humu hali ya kuwa tuna wazee kibao tu waliyosoma zamani na akina Nyerere na Mkapa, inafikirisha.
 
Kweli hi Ni africa , mpaka mwaka 2022 na Karne hii bado tuna mawazo ya Nani muongeaji mzuri wa kiingereza.
Ni kwamba elimu yetu tunafundishiwa kwa kutumia english na hivyo english imekuwa ni kipimo cha moja kwa moja cha kiwango cha elimu ya mtu kwa maana kama kawa huwezi kuzungumza vizuri kiingereza tafsiri yake hukuwa unaelewa masomo darasani.
 
Kwahiyo, unamanisha. Hawezi kuongea au unqaona kingereza Ni kigumu Sana?mbona Idd Amini alikuwa anaongea hivyo hivyo1?
 
Benjamin mkapa apewe heshima yake kwenye upande wa kuongea kiingereza kilichonyooka.
 
Back
Top Bottom