Nauli hizi za SGR nani atapanda? Kutoka Dar - Moro Tsh 24,000?

Nauli hizi za SGR nani atapanda? Kutoka Dar - Moro Tsh 24,000?

Kutakuwa hakuna maana Kama utachaji nauli ambayo haifikii hata robo ya gharama za uendeshaji na uwekezaji..

Sasa tulijenga Cha Nini Kama tutakuwa tunatumia Kodi ya Nchi kuendeshea sgr? Huu si Ni upumbavu?

Na hapa Sasa ndio huwa inakuja Ile maana ya private sector kujenga na kuendeshwa wenyewe.
Mie nadhani hiyo feasibility study km ilifanyika vizuri lazima ingekuwa imejibu haya maswali.
Study iliyofanywa na world Bank ili recommend against this project.
Tumefika hapa na huu ndio uhalisia.
Tukipunguza hii nauli kwa subsidy kuna wananchi wa Nanjilinji watalipia hizi huduma unnecessarily.
 
Hata kama ni mapendekezo sidhani kama mlifikiria au kuwaza kwa kinagaubaga, huko Anatorglo mnaenda kupaka mafuta ili kung'arisha hiyo nauli na si vinginevyo.

Ukute mmeshaandaa wazungumzaji wenu wa kutetea hiyo nauli na hapo ndiyo watakuwa wengi ukumbini.

--

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imepokea maombi kutoka Shirika la Reli Tanzania (TRC) kuhusu nauli za abiria kwa treni ya njia ya Reli ya Kisasa – ‘Standard Gauge Railway’ (SGR) zitakavyotumika kwa huduma ya usafiri wa treni za abiria.

Kwa mujibu wa Kifungu Na. 21 cha Sheria Na. 3 ya LATRA, 2019 Mamlaka inapaswa kukusanya maoni ya wadau kabla ya kufikia uamuzi wa kuridhia viwango vya nauli kwa huduma zinazodhibitiwa na Mamlaka ikiwemo nauli za treni.

Katika kulitekeleza hilo, Mamlaka imeandaa mkutano wa kupokea maoni ya wadau wa usafirishaji, ikiwa ni pamoja na watoa huduma, watumiaji wa huduma na wananchi kwa ujumla. Mkutano utafanyika tarehe 19 Disemba 2022 jijini Dar es salaam katika Ukumbi wa Anatorglo.

Nauli zinazopendekezwa na TRC ni Kama ifatavyo:

View attachment 2440636

View attachment 2440637

Kutokana na umuhimu wa mkutano huo, LATRA inawaalika wadau wa sekta ya reli na wananchi kwa ujumla kushiriki katika mkutano huo wa kukusanya maoni ya wadau.

Vilevile, wadau wanaweza kuwasilisha maoni yao kwa Mkurugenzi Mkuu kwa maandishi kupitia LATRA Makao Makuu, Mtaa wa Tambuka Reli, Dodoma au ofisi za LATRA zilizopo Makao Makuu ya kila mkoa Tanzania Bara kabla ya tarehe 3 Januari 2023.

Aidha, maoni ya wadau yanaweza kutumwa kwa barua pepe kupitia anuani hizi: info@latra.go.tz na dg@latra.go.tz

Imetolewa na:
Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano – LATRA
06 Disemba, 2022​
Wana CCM TUNAPANDA
 
Uwekezaji ni long term kuna watu wanawekeza ku-break even ni after 200 years au generation...., Uendeshaji ndio ninakuuliza Je watu wakiwa wengi gharama za uendeshaji kati ya train na basi ipi ni nafuu ?

Unajua kwa mizigo kutumia train tunaokoa kiasi gani katika maintanance ya barabara ?, unajua mtu kuja na kapu lake la machungwa Dar kwa bei nafuu au kuleta mchele kwa bei nafuu itapelekea wewe kuweza kupata bei nafuu ?

Hivi ingekuwa pesa tu ndio kila kitu kwanini hata DAWASA au TANESCO wasingechaji maji hata mara nne ya bei ya sasa kama issue ni kupata as much as possible moneywise ? Au ndio ile Unajiibia mwenyewe mfuko wa shati unaweka mfuko wa suruali....

Unadhani private sector ikisema hizo elfu kadhaa hazitoshi sisi na shareholder wetu kugawana faida nani atalipia difference kama sio sisi through kodi zetu ?

Au unadhani kwanini hata nje (UK for example) Privatization ya Rail ime-prove hard to implement na mpaka routes nyingine kuwa re-nationalized ?

Au unadhani Private company ikiona safari ya morogoro jumatatu faida yake ni ndogo kuweza kugawa na shareholders wetu bado watakwenda huko , au watapiga hodi serikalini kwamba gharama ya safari za jtatu nyie ndio mlipie ?
Tanzania hatukujenga reli ije kuwa Huduma bali ilete faida..

Ukisema iwe Huduma huo Ni upumbavu wa kuchagua vipaombele kwa mda ambao sio sahihi..

Ukisema Bei iwe chini au sawa na Basi ndio kusema tuchukue Kodi kuja kuwalipia nyie msafiri bure ,huu utakuwa Ni upuuzi wa Hali ya Juu na matumizi mabaya kabisa ya Kodi yetu..

Barabara zipi zinazoharibika kwa mizigo hapa Tanzania? Kuna uzembe tuu wa kuwa na njia nyingi za Barabara matokeo yake mrundikano njia chache..

Mwisho aliyeamua kujenga sgr kwa Pesa za Umma Ni mpumbavu wa kiwango Cha mwisho,Leo hii hayo Matilioni yengewekezwa kwenye Barabara zingenyenyua Uchumi wa Nchi haraka Sana kuliko huu ujinga wa sgr..

Na wajinga wengi ikiwemo wewe akili yako inawaza prestige kuliko economic significance.
 
Mie nadhani hiyo feasibility study km ilifanyika vizuri lazima ingekuwa imejibu haya maswali.
Study iliyofanywa na world Bank ili recommend against this project.
Tumefika hapa na huu ndio uhalisia.
Tukipunguza hii nauli kwa subsidy kuna wananchi wa Nanjilinji watalipia hizi huduma unnecessarily.
Hakuna Cha feasibility study iliyofanyika zaidi ya prestige ya Jiwe kwa taarifa yako..

Niliwaambia hapa watabadili gia waanze kusema sgr Ni Huduma..

Sasa unajiuliza Kama Ni Huduma he watu walikuwa na hamu Sana ya kufika Dar haraka? Yaani tuanze ku allocate Pesa Tena kuendeshea limradi linaloleta hasara..
 
Yale makopo yana uwezo wa kutumia 60mins?
Hayawezi kabisa mkuu, hata akisema atembee top speed non-stop. Kumbuka kuna vituo lukuki njiani. Labda 2 hrs ukijumlisha na muda wa kusimama vituoni
 
Kwani mjadala ilikuwa ni endapo sekta husika ni huduma ama sio huduma?!

Hoja hapa sio kama sekta husika ni huduma ama sio huduma bali ikiwa sekta husika inaendeshwa kibiashara au "kiujamaa"!!

Hata mtoto wa Darasa la IV anafahamu kwamba maji, usafirishaji, umeme, mawasiliano, and the like... zote hizo ni huduma lakini je, taasisi zake zinaendeshwaje au zinatakiwa kuendeshwaje!

Mifano ipo wazi lakini bado unaganda kwenye hiii huduma... SAWA, HUDUMA lakini wenzako hawaendeshi hizo taasisi kama unavyotarajia wewe!
Okay am glad hilo tumelimaliza haya mambo ni Huduma.., Sasa Je ? Hivi unajua Private Sectors / Business ni answerable kwa shareholders wao wala hawafanyi kazi ya kanisa ? Hawapo pale kutoa huduma bali kutengeneza as much money as possible (kwahio usitegemee msaada kutoka kwao) na sekta ambazo competition ni ngumu kufanyika hata privatization ikifanyika more times than not bei hazishuki na bado mwananchi atatoa kodi / pesa iwapo private sector haitapata faida ili kufidia the difference...

Haya unasema ziendeshwe vipi kibiashara au kijamaa ? Kuendesha kijamaa ni vipi unaweza kunipa mfano ? Kama unamaanisha ni kwa Serikali kutoa ruzuku basi dunia nzima inaendeshwa kijamaa linapokuja suala la hizi sekta za huduma..., Na sio hivyo tu hata Benki ambazo ni Too Big to Fail nazo ni Ujamaa sababu wakipata faida shareholders wanakula chao hasara ikipatikana wananchi ndio wanalipia ili uchumi usishuke (refer Global Financial Crisis huko Marekani)

Nani asiyefahamu umuhimu wa usafiri Dar es salaam! Je, ile Mwendokasi sio huduma ile?! Nauli zake ni ndogo compared to Daladala?!

Hiyo ndo reality ninayokuambia kila wakati!

Hivi unataka kuniambia Nauli ya Daladala Dar es salaam ni kubwa kuliko Mwendo Kasi?

Kama hoja yako ya huduma ingekuwa inatiliwa maanani, what would you expect kati ya nauli za Daladala vs Mwendokasi?
Alafu kabla hatujafika mbali naomba nikwambia am all for competition and free market..., hivi unajua bila Serikali kuwapangia daladala bei kwamba isizidi kiasi fulani ingeshazidi ? Sasa mimi in my way of thinking Serikali haipaswi kuingilia biashara za watu na investment zao, hususan likija suala la bei (sababu they know their investment better) ila katika hio free market sababu na sisi UMMA tuna akili na tunalipia hizi huduma kutoka kwenye kodi zetu kwanini hio mwendokasi isiendeshwe kwa ufanisi na kutoa bei ambazo hao latra ndio wanaona zinaendena na uhalisia na kuwaacha watu na biashara zao wapange bei kulingana na soko wanavyoona ?

Vilevile hata hizo kampuni binafsi za usafiri huko nje unaweza kusema pia zinaendeshwa kwa watu kutumia kodi zao ili mwekezaji alipwe fidia / ruzuku pale ambapo anaona route haina faida - kwahio kuliko kuendesha / kushindana na kupata kinachopatikana na kutumia pesa zetu kulipa watu (private) ili wapate faida hapa equation inabadilika (operations costs + profits for shareholders + Subsidy from Government)=Mtumiaji kugharamikia badala yake ingekuwa (operation costs)=Mtumiaji kugharamikia + government subsidy
Kubadilika kivipi?!

Huduma ni huduma tu at any cost lakini huduma haimaanishi utalipishwa bei ndogo! Na hata kama inatakiwa ulipishwe bei ndogo, uhalisia haupo hivyo na ndo maana nikakupa mifano ya huduma zingine ambazo bado unalipishwa bei zinazolalamikiwa na wananchi!
Ndogo kwako ni ipi mkuu; mimi nimekupa ndogo kwangu lazima iendane na gharama za uzalishaji na uwezo wa mtu wa kawaida kulipia na kipindi ambacho mtu wa kawaida anashindwa kuna ruzuku inatoka (sababu hio ruzuku ni kama kumpa mwanao mtaji ili azalishe zaidi; kwa wafanyakazi kuwahi makazini au kupata umeme wa uhakika au kuoga na kuacha kunuka kikwapa ni faida kwa nchi...)
Hivyo ndo kwako wewe... FINE, sina tatizo na hilo!

The question is: UHALISIA kwa zile huduma zingine upo hivyo unavyojua wewe?

Hata ukiwauliza serikali, watakujibu kama unavyojua wewe, na watakuambia na hiyo ruzuku wanatoa ndo maana pricing ipo kama ilivyo.

How should be?! Sizungumzii "how should be" nazungumzia uhalisia uliopo!

Wewe unataka nifanye janja ya mbuni kana kwamba uhalisia siuoni bali nizungumzie "how should be"!!
Sasa mkuu kama tunazungumzia kinachoendelea na sio jinsi ya kuweza kuboresha hatuna tofauti na wale mababu zetu waliosema wanadiscuss people au events na sio ideas...; Hakuna mtu ambae haoni kinachoendelea kwamba ndivyo sivyo.., ila hio kazi ya ku-report tunawaachia kina Pascal Mayalla wafanye kazi yao wengine sisi hapa tunaongelea mawazo / fikra zetu no matter kama zitafanyika au kutofanyika katika kizazi chetu
Mfano wako wala haufanani...

Nakuambia unaishi kwenye fantansy world kwa sababu uhalisia unauona lakini unajifanya huuoni!!
Kilichopo kama ningeona kipo sawa wala nisingepoteza muda hapa huenda ningekuwa naongelea game la leo usiku au nina-cross check kama ideas za sasa can be made better..., hivyo ndivyo nilivyo na sababu naona ndio maana kila siku natupia comment chache kuhusu walamba asali ndio maana nikaleta uzi wa kufanya Tanesco iwe a better company
(not that it will..., but I think its possible am just putting my views on paper to be criticized and refined) au Jinsi serikali inavyoboronga na kufanya bundles ziwe bei kubwa kutokana na kuingilia kampuni za simu Sakata la Bundles - Suluhisho

Unaona hapo nauli to Morogoro 24K... twice as much-- na huo ndo uhalisia wenyewe na sio "how should be"

Na hata wakisema washushe, maybe to 10K... je, itakuwa imekidhi tafsiri yako ya huduma?!
Tafsiri sio yangu tafsiri itatokana na gharama ya uendeshaji na uwezo wa mlipaji..., vilevile sababu ni hasara kwa hili dude kutokubeba watu wengi na watu wanavyokuwa wengi zaidi ndio huduma gharama ya uendeshaji ina-make sense tofauti na basi (hivyo the only alternative which makes economical sense) ni kuweka bei ambayo itajaza watu kulingana na capacity iliyopo yaani waweke mabehewa mengi as practical possible kulingana na watu waliopo kwa bei wanayoweza without breaking their banks
 
Hiyo ni bei ya nauli walizopendekeza wao trc then latra watakusanya maoni ya wadau ili wacrosscheck pande zote kupata bei sahihi ya mlaji. Kama mlaji napendekeza nauli ya dar moro iwe 6000
Yaleyale ya mwendo kasi serikali hapo inapendekeza viwango vidogo then trc watapokea kishingo upande basi taratibu huduma zitaanza kuzorota mwishowe mambo yanakuwa ovyooo kabisa maana trc watazingizia gharama ni kubwa na nauli ni ndogo mno..
 
Katika sehemu tuliingizwa mkenge na kiongozi wa nchi ni huu mradi. Tutapata maumivu mpk huko kiama kwa huu mradi.
 
Tanzania hatukujenga reli ije kuwa Huduma bali ilete faida..
faida kwa nani na vipi ? na faida ipi ? Monetary yaani Shirika lipate mapato zaidi au faida ya watu kuweza kufika point B kwa gharama nafuu ?
Ukisema iwe Huduma huo Ni upumbavu wa kuchagua vipaombele kwa mda ambao sio sahihi..
Huu ni muda wa kufanya nini na huduma zipi mwananchi anayezipata kwa sasa ? Na hii huduma ya usafiri wakati wake sahihi ni upi ? na kama ni kosa limefanyika / lilifanyika suluhisho ni kuweka bei ambayo sio rafiki kwa mwananchi wa kawaida hence kukosa yote yaani (monetary na socially)?
Ukisema Bei iwe chini au sawa na Basi ndio kusema tuchukue Kodi kuja kuwalipia nyie msafiri bure ,huu utakuwa Ni upuuzi wa Hali ya Juu na matumizi mabaya kabisa ya Kodi yetu..
Wateja wakiwa wengi sana kati ya basi na train ipi ina gharama kubwa ya uendeshaji ?
Barabara zipi zinazoharibika kwa mizigo hapa Tanzania? Kuna uzembe tuu wa kuwa na njia nyingi za Barabara matokeo yake mrundikano njia chache..
unamaanisha ya kuwa na njia nyingi au chache ? Kama nyingi tuongeze njia zaidi ? Hizo njia hazina gharama ya kuzitengeneza na kuzifanyia repair ? Na usafirishaji wa mizigo mizito kipi ni cost effective train au magari / malori ?
Mwisho aliyeamua kujenga sgr kwa Pesa za Umma Ni mpumbavu wa kiwango Cha mwisho,Leo hii hayo Matilioni yengewekezwa kwenye Barabara zingenyenyua Uchumi wa Nchi haraka Sana kuliko huu ujinga wa sgr..

Na wajinga wengi ikiwemo wewe akili yako inawaza prestige kuliko economic significance.
This is another argument ambayo sioni faida ya kuongelea hapa huenda miaka kumi ijayo tukawa tunasema aliyeingia mikataba na hao wachina na sijui kina nani alikuwa mjinga wa kutupwa..., that's a blame game ambayo kwa leo nadhani nina more constructive issues za kufanya..., Na kama tungetaka kama nchi kuondoa uwezo wa mtu mmoja kuamua aliyepo sasa asingekubali kuendelea na Sheria inayomruhusu kufanya anachotaka
 
Kwani bei za United Kingdom za British Rail against mabus Express zikoje? Hizi ndiyo matokeo ya kushabikia vitu bila ku analyse na sasa bado SG Hydro Electric power station
 
Hapa au hii ni kutaka kuwaonyesha wananchi kwamba kuendesha huu mradi ni garama kubwa au wananchi kutumia treni ni anasa.

Yaani kwenda Dodoma -60,000/-!.

Treni kwa waliostaarabika huko ni usafiri wa garama nafuu sana sisi unaenda kuonekana ni anasa.
Siku zote nasemaga fisiemu ni mzigo mzito sana kwa watanzania
 
Back
Top Bottom