Pre GE2025 Nchi imerudi mfumo wa Chama kimoja, Magufuli kaacha utamaduni mbaya kwenye siasa, itachukua miaka 20 kumpata kiongozi kama Kikwete

Pre GE2025 Nchi imerudi mfumo wa Chama kimoja, Magufuli kaacha utamaduni mbaya kwenye siasa, itachukua miaka 20 kumpata kiongozi kama Kikwete

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kwa hiyo unataka ccm ifanye vibaya ili upinzani uboreke maana sijaelewa martini yako. Kaeni mjitathimini, mlisema JPM hana democrasia kaingia mama kawapa demokrasia mmeshindwa kushawishi wananchi. Hivi mnadhani hawa wananchi wa sasa ni wajinga? Kila mkipanda jukwaani badala ya kumwaga sera nyie mnatukana serikali ya awamu ya tano.
 
Another idiot
You're not just an idioot, you are schlemiel infact you are more idiot than that person you tagged as idiot...

Na Mimi nauliza swali lile lile kwani nyie watanzania mliopo Sasa hivi huo mfumo mbovu sijui legacy mbovu iliyoachwa na Magufuli hamuwezi kujiondoa na badala yake mmebaki kulalamika tu?

Kwa hiyo mtaendelea kulalamika hivi hivi kwa miaka 20(ambayo mmejiwekea) pasipo kuchukua hatua yoyote kuurudisha mfumo wa Kikwete mnaoupenda?
 
Magufuli alikuwa shetani. Ameacha laana ambayo itaitafuna Tanzania kwa muda mrefu labda Mungu atuonee tena huruma.
Ona mjinga mwingine huyu aliyejaa lawama tu.

Kwamba hayo mabadiliko hamuwezi kuyaleta nyie wenyewe na badala yake mnasubiri huruma ya Mungu??

Yaani kabisa umekaa hapo unashusha lawama tu kwa mtu ambaye tayari ni Mfu na Wala hajui chochote kinachoendelea huku, wakati huo wewe hapo Bado una uzima wako na hauzuiliwi na mtu yoyote kuleta hayo mabadiliko unayoyaitaji et

No wonder ndio maana Samia anaipeleka hii nchi anavyotaka, sababu anajua watanganyika tayari mna mtu wa kumtupia lawama... Na Mimi napenda aendelee kutuburuza hivi mpaka atakapochoka, maana kuchukua hatua hatuwezi tunajua kutoa lawama tu.
 
me nadhani kwa tanzania tatizo lipo kwa upinzani wenyewe na aina ya upinzani walio nao. Ni vema wafanye mabadiliko ya kwao kwanza ndipo wafanye mabadiliko ya utawala kushikwa na upinzani. Kikwete aliwawekea mazingira ya kushina ila kwa tamaa ya pesa wakauza nafas ya kuongoza nchi.
Magufuli alitawala kwa kutumia sera za upinzan. Wakakosa cha kukosoa wakawa wanapinga miradi yenye tija kwa taifa. Ki ufupi hawaeleweki.

Magufuli alipitia ukosoaji mkubwa ila alijitahid kuchapa kazi na kuifanya nchi ipige hatua. Samia anauza rasilimali zetu na kufukuza wamasai but wanakosoa kwa uoga na wengine ndo wapo kimya kabisa. Naomba uniambie tofauti na chadema na act vyama vingine vya upinzani vinafanya nini..? Kuna faida gani kuwa navyo kama taifa,? Kwa hiyo hao wanaojiita wapinzan hawako sirias na wanachokifanya. Kama kweli malengo ni kulikomboa taifa basi waanze kufanya marekebisho wenyewe, kusiwe na utitiri w vyama dhidi ya chama kimoja na waonyeshe dhamira ya kweli ya mageuzi. Kama ndani ya chama kikuu cha upinzani hakuna demokasia ya kweli itakuwaje wakishika madaraka?
Comment kama hii Hawa wajaa lawama hawawezi kuigusa sababu akili zao nyepesi na hazina uwezo wa kuangalia mambo kwa mapana, Mimi Nina uhakika hata ukiwafuata wanachama waandamizi wa hivi vyama pinzani ukiwauliza haya maswali hawawezi kujibu kw usahihi.
 
Mjinga mimi nampa Magufuli lawama vipi wakati nasema aliyofanya? Onyesha sehemu niliyomsingizia. 1. alikuwa muuaji 2. alivuruga uchaguzi na kuweka vilaza aliotaka yeye ili wamsifie. 3. alipenda sifa na hakutaka kushauriwa hata kwenye mambo ya kisayansi
Kuhusu mabadiliko: mabadiliko hayaji kwa huruma ya Mungu bali ni kwa wananchi wote kuwajibika. Na ili wananchi wawajibike wanahitaji viongozi wazuri wenye maono na miongozo na sheria nzuri za kuongoza nchi.
Kuhusu Samia: wakutupiwa lawama ni wananchi wote kwa kukaa na kimya hata pale anapofanya ufisadi na bila wananchi kuamka basi hakutakuwa na mabadiliko.
Mwisho: mjinga mimi ni mtu mwenye exposure na elimu nzuri tu na sina akili za ki-nyumbu kama wewe. Huwa nasema ukweli tena ukweli mtupu.
Swali: mwerevu wewe, ni nani?
Ona Sasa ulivyozidi kuthibitisha ujinga wako, halafu mbaya zaidu unajinasibu eti umesoma serious huko shuleni bila shaka ulienda kuchukua bachelor of Art in sheer ignorance and incomprehension.

Hakuna sehemu niliyosema umemsingizia Magufuli au nioneshe ni wapi nimekuuliza unitajie hayo uliyoyataja hapo.

Shenzy kabisa, nimekuuliza ukiwa na akili zako timamu umeshindwa nini kubadilisha huu mfumo mbovu ulioachwa na Magufuli na badala yake unasubiri huruma ya Mungu??? Halafu unajinadi msomi, Sasa huo usomi wako una msaada gani kama umeshindwa kuitumia kujinasua kwenye hili Giza mliloachwa na Magufuli???

Eti una exposure si Bora ungebaki unalima viazi tu kwenu huko Uyole kuliko kuzulula kwenye nchi za watu na Bado unaoneka kinabo namna hii..? Haya huko kwa hao wenzetu waliondelea hasa nchi za Asia na wao wangekalia lawama tu serikali zao za nyuma wangefika hapo waliopo leo hii??
 
Mbadala wa CCM ndio kama upinzani tulionao sasa hivi shida inaanzia hapa ndio maana wengine wameamua wasiwe wanapiga kura
Tatizo hawa wajuaji wasichokijua ni kwamba Sasa hivi wanainchi wanachoangalia hasa ni sera na maono ya kiongozi Yana impact gani kwenye maisha yao na Wala sio demokrasia/udikteta

Yaani kupitia sera zako na haiba yako ya uongozi utabadilisha vp maisha yao na vizazi vyao haijalishi ni mfumo upi wa uongozi utaoutumia?

Unaweza ukawa ni mwendekeza demokrasia lakini serikali yako ikaishia kufuga wezi tu na mafisadi na hakuna Cha maana inachofanya na watu wakaichoka haraka sana, Sasa hapo hata hiyo demokrasia yako itakuwa Haina tija yoyote..... Wakati huo vile vile unaweza ukawa ni dikteta na mambo yakaenda kama jinsi inavyotakiwa na watu wakaridhika kabisa na uongozi wako.

Watu siku hizi wanajua nini wanachokitaka hawaendeshwi Tena na propaganda za udikteta na demokrasia uchwara.... Angalia Marekani hao hapo democrats kupitia powerful liberal medias walijitahidi sana kueneza propaganda chafu dhidi ya Trump zikiwemo hizo za udikteta, lakini mwisho wa siku wameamua kwenda na Trump sababu wameona sera za Trump ndio utakuwa muaarobaini wa matatizo waliyonayo kwa Sasa.
 
Tulichokosa sisi ni uongozi bora yaan strong leadership. Pia kama nchi tuna wajinga wengi wasiojitambua na wenye uelewa mdogo wa mambo. Tena hili tatizo liko hasa mijini ambako ndiko tulikotegemea wawepo watu wanaojitambua lakini wapi. Vijana wanawaza kubet na simba na yanga ila maswala yanayohusu taifa hawajali. Vijijini ndo kabisaa sehemu nyingine hawajui hata mambo ya upinzan kuanzia vijana mpaka wazee na ukijitokeza ukaanza kueneza upinzani unapotezwa na kikosi kazi
 
Hivi mnafikir nan anajali kuhusu hali ya kisiasa? Watu tunachotaka ni maendeleo basi. Kama kuna siasa saf na maendeleo hakuna basi hatuitak hata kuisikia hio siasa Safi.
Sahihi kabisa ndio kitu ambacho nimemwambia hata member mmoja kwenye huu Uzi hapa....

Kuwa watu wanachoangalia ni uwezo wa kiongozi kubadilisha maisha yao katika muelekeo chanya ambapo ni kuletewa maendeleo haijalishi kiongozi huyo ni dekteta au mtu wa demokrasia.

Uwe ni mpenda demokrasia umeachia uhuru wa kisiasa kwamba watu wanatukana wanavyotaka, lakini kama hakuna maendeleo au taifa linajikongoja na wizi umetamalaki bila ya watu kuchukuliwa hatua yoyote, basi utaishia kudharaulika na demokrasia yako hiyo.

Pia vile vile unaweza kuwa ni mdikteta ila watu wanaona kazi unayoifanya na taifa linasonga mbele, hakuna atakayekumbuka hata kama Yuko chini ya utawala wa kidikteta.

Asilimia kubwa ya Hawa wajuaji waliopo humu wanaopiga kelele kuhusu demokrasia si kweli kwamba wanahitaji kiongozi mwana demokrasia, Bali wanataka kiongozi dhaifu atakayeruhusu upuuzi mwingi ikiwemo ufisadi kwa mwamvuli wa demokrasia.
 
Sahihi kabisa ndio kitu ambacho nimemwambia hata member mmoja kwenye huu Uzi hapa....

Kuwa watu wanachoangalia ni uwezo wa kiongozi kubadilisha maisha yao katika muelekeo chanya ambapo ni kuletewa maendeleo haijalishi kiongozi huyo ni dekteta au mtu wa demokrasia.

Uwe ni mpenda demokrasia umeachia uhuru wa kisiasa kwamba watu wanatukana wanavyotaka, lakini kama hakuna maendeleo au taifa linajikongoja na wizi umetamalaki bila ya watu kuchukuliwa hatua yoyote, basi utaishia kudharaulika na demokrasia yako hiyo.

Pia vile vile unaweza kuwa ni mdikteta ila watu wanaona kazi unayoifanya na taifa linasonga mbele, hakuna atakayekumbuka hata kama Yuko chini ya utawala wa kidikteta.

Asilimia kubwa ya Hawa wajuaji waliopo humu wanaopiga kelele kuhusu demokrasia si kweli kwamba wanahitaji kiongozi mwana demokrasia, Bali wanataka kiongozi dhaifu atakayeruhusu upuuzi mwingi ikiwemo ufisadi kwa mwamvuli wa demokrasia.
Nakuunga mkono 💯
 
Ishu ni kwamba alileta mwanga kwenye siasa za nchi hii tangu tupate uhuru, ilibidi wanaomfuata waendeleze alipoishia sio kurudi tulipotoka

Kwa mara ya kwanza kabisa wabunge kibao wa upinzani bungeni na ilisaidia sana vitu kama kuibua madudu ya Escrow, Richmond, n.k. Sio bunge linajaa chama kimoja kila kitu Ndioo
Watanzania hawali siasa kenge wewe
 
Kuuawa kwa Mwangosi, kutekwa kwa Ulimboka, watu watatu kuuwawa kwa bomu kwenye mkutano wa CDM kule arusha, bomu kulipuka kanisani Olasiti arusha.. nani alikuwa rais ?
 
me nadhani kwa tanzania tatizo lipo kwa upinzani wenyewe na aina ya upinzani walio nao. Ni vema wafanye mabadiliko ya kwao kwanza ndipo wafanye mabadiliko ya utawala kushikwa na upinzani. Kikwete aliwawekea mazingira ya kushina ila kwa tamaa ya pesa wakauza nafas ya kuongoza nchi.
Magufuli alitawala kwa kutumia sera za upinzan. Wakakosa cha kukosoa wakawa wanapinga miradi yenye tija kwa taifa. Ki ufupi hawaeleweki.

Magufuli alipitia ukosoaji mkubwa ila alijitahid kuchapa kazi na kuifanya nchi ipige hatua. Samia anauza rasilimali zetu na kufukuza wamasai but wanakosoa kwa uoga na wengine ndo wapo kimya kabisa. Naomba uniambie tofauti na chadema na act vyama vingine vya upinzani vinafanya nini..? Kuna faida gani kuwa navyo kama taifa,? Kwa hiyo hao wanaojiita wapinzan hawako sirias na wanachokifanya. Kama kweli malengo ni kulikomboa taifa basi waanze kufanya marekebisho wenyewe, kusiwe na utitiri w vyama dhidi ya chama kimoja na waonyeshe dhamira ya kweli ya mageuzi. Kama ndani ya chama kikuu cha upinzani hakuna demokasia ya kweli itakuwaje wakishika madaraka?
Hakuna mtu aliyeharibu nchi hii kama Jiwe
 
Back
Top Bottom