Pre GE2025 Nchi imerudi mfumo wa Chama kimoja, Magufuli kaacha utamaduni mbaya kwenye siasa, itachukua miaka 20 kumpata kiongozi kama Kikwete

Pre GE2025 Nchi imerudi mfumo wa Chama kimoja, Magufuli kaacha utamaduni mbaya kwenye siasa, itachukua miaka 20 kumpata kiongozi kama Kikwete

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Tatizo lenu kubwa mmeshikwa akili Magufuli alikuwa mbaya. Mnasahau Magufuli alifanya vitu vyote kwa maslahi ya CCM, nyie ndio mlikuwa mnasema mama anaupiga mwingine.
Kama hamtajitazama na kuangalia wapi mnakosea mtaendelea kupambana na marehemu.
CCM gani? Ilikuwa maslahi yake binafsi na kundi lake. CCM inatumika kama tool!
 
Kipindi cha Kikwete alileta mapnduz makubwa mno kwenye siasa za nchi yetu kwenye siasa za upinzani, Uhuru wa kuongea na baada ya kuongea, n.k.

Siwezi kusema kikwete alikuwa mkamilifu kwenye kuleta siasa huru lakini alijitahidi

  • Kwa mara ya kwanza wagombea wapinzani walijaa bungeni
  • matumizi madogo sana ya nguvu ya polisi kuzuia upinzani
  • Aliruhusu yeye na serikali yake kukosolewa
  • Uhuru wa kutoa maoni
  • jitihada ya mchakato wa katiba mpya
  • n.k.

Kwa mara ya kwanza tangu uhuru tulipiga hatua kubwa sana kwenye mazingira ya kisiasa, huwez amini skendo za ufisadi kama escrow na Richmond zilichambuliwa bungeni bila spika kuwazimia mic wapinzani au kukataa hoja izungumziwe, Vyombo vya habari viliweka mambo wazi bila hofu, n.k.

Tulitegemea utamaduni huu utadumishwa but kilichotokea ni opposite

Then came a man known as Magufuli, Siku za mwanzo tu aliwaonya wanaomkosoa "BE CAREFUL" hakuvumilia serikali yake kukosolewa waliodiriki walikiona cha mtemakuni, CAG alitimuliwa kwa kuweka wazi serikali inafuja pesa, Chato alikozalowa ilibustiwa sana, watu wasiojulikana, n.k.

Kinachoendelea ni kile kile part 2, ni utamaduni wa mfumo wa chama kmoja ulodumu miaka mingi na kuongezewa baadhi ya vitu hasa kwenye kuzimisha upinzani.

Itachukua miaka mingi sana kumpata kiongozi kama Kikwete kuleta siasa zenye afya
Kwakuwa watu wa taifa la gizani akili zao zimekuwa giza acha waendelee kuwa gizani kwani ndicho walichochagua.
 
me nadhani kwa tanzania tatizo lipo kwa upinzani wenyewe na aina ya upinzani walio nao. Ni vema wafanye mabadiliko ya kwao kwanza ndipo wafanye mabadiliko ya utawala kushikwa na upinzani. Kikwete aliwawekea mazingira ya kushina ila kwa tamaa ya pesa wakauza nafas ya kuongoza nchi.
Magufuli alitawala kwa kutumia sera za upinzan. Wakakosa cha kukosoa wakawa wanapinga miradi yenye tija kwa taifa. Ki ufupi hawaeleweki.

Magufuli alipitia ukosoaji mkubwa ila alijitahid kuchapa kazi na kuifanya nchi ipige hatua. Samia anauza rasilimali zetu na kufukuza wamasai but wanakosoa kwa uoga na wengine ndo wapo kimya kabisa. Naomba uniambie tofauti na chadema na act vyama vingine vya upinzani vinafanya nini..? Kuna faida gani kuwa navyo kama taifa,? Kwa hiyo hao wanaojiita wapinzan hawako sirias na wanachokifanya. Kama kweli malengo ni kulikomboa taifa basi waanze kufanya marekebisho wenyewe, kusiwe na utitiri w vyama dhidi ya chama kimoja na waonyeshe dhamira ya kweli ya mageuzi. Kama ndani ya chama kikuu cha upinzani hakuna demokasia ya kweli itakuwaje wakishika madaraka?
Hoja yako ni nzito Sana ilipaswa iwe mada kabisa
 
Haya ni mawazo ya watu wachovu na tayari mawazo yao hayo wanaanza kuyafanya sababu ya wao kukwepa uwajibikaji

Tunavyama vya upinzani vichovu na vinaongozwa na watu walafi wa madaraka na hawapo tayari kuwajibika

Ni wakweli katika mwonekano wa nje, ndani ya mioyo yao ni ccm tupu na wagonga glas na kina Mama Abdu huku wakiwang'onga wafuasi wao

Wakati wafuasi wakiamini wana viongozi imara katika kutetea mabadiriko, kumbe viongozi wao wanakula pamoja na viongozi wa chama tawala

Mleta uzi kwani wewe ni nani katika hivi vyma vya upinzani?

Je ni kiongozi? Kama wewe ni kiongozi, tafafhari, acheni kutuona mazuzu sisi kuleeta hoja za kijinga huku ukijua mnakula luzuku za maccm

Kama wewe ni mfuasi, basi elewa wanaokuuzeni ni viongozi wenu, haladu unakuja kumlalamikia marehemu? Jinga kabisa
Hoja yako ni nzito Inafaa kufanyiwa lamination
 
Kipindi cha Kikwete alileta mapnduz makubwa mno kwenye siasa za nchi yetu kwenye siasa za upinzani, Uhuru wa kuongea na baada ya kuongea, n.k.

Siwezi kusema kikwete alikuwa mkamilifu kwenye kuleta siasa huru lakini alijitahidi

  • Kwa mara ya kwanza wagombea wapinzani walijaa bungeni
  • matumizi madogo sana ya nguvu ya polisi kuzuia upinzani
  • Aliruhusu yeye na serikali yake kukosolewa
  • Uhuru wa kutoa maoni
  • jitihada ya mchakato wa katiba mpya
  • n.k.

Kwa mara ya kwanza tangu uhuru tulipiga hatua kubwa sana kwenye mazingira ya kisiasa, huwez amini skendo za ufisadi kama escrow na Richmond zilichambuliwa bungeni bila spika kuwazimia mic wapinzani au kukataa hoja izungumziwe, Vyombo vya habari viliweka mambo wazi bila hofu, n.k.

Tulitegemea utamaduni huu utadumishwa but kilichotokea ni opposite

Then came a man known as Magufuli, Siku za mwanzo tu aliwaonya wanaomkosoa "BE CAREFUL" hakuvumilia serikali yake kukosolewa waliodiriki walikiona cha mtemakuni, CAG alitimuliwa kwa kuweka wazi serikali inafuja pesa, Chato alikozalowa ilibustiwa sana, watu wasiojulikana, n.k.

Kinachoendelea ni kile kile part 2, ni utamaduni wa mfumo wa chama kmoja ulodumu miaka mingi na kuongezewa baadhi ya vitu hasa kwenye kuzimisha upinzani.

Itachukua miaka mingi sana kumpata kiongozi kama Kikwete kuleta siasa zenye afya
Kwahiyo sisi kazi yetu ni kulaumu tu wale waliokwisha kwenda mbele za Haki kwa kile walichokikosea ??!!
😳🙄😀😅😂 !
 
Ni kweli Kikwete aliwapa uhuru vyama vya upinzani.

Ila wapinzani nao waliabuse huo uhuru.

Tatizo la upinzani tulionao ni aina ya siasa wanayofanya.

Imepitwa na wakati. Huwezi kufanya siasa za kiuanaharakati katika karne hii ukaeleweka. Aina ya siasa hiyo imekaa kishari na inaaashiria vurugu. Aina hiyo ya siasa haikubaliki kwa jamii iliyostaarabika. Angalia hata mwitikio wa maandamano kuhusiana na utekaji. Hakuna aliyekwenda.

Vyama vya kisiasa hapa nchini vinapaswa kubadilika na kuwa vyama na sio taasisi za kiuanaharakati.

Lowasa alijaribu sana kuwabadilisha Chadema lakini alishindwa.

Wananchi wanachotaka kusikia ni sera na namna ya kuzitekeleza na sio kuwajengea hofu na kuwapotosha watu.

Wapinzani kamwe hawataishika dola kwa aina hii ya siasa wanayoifanya. Haitatokea.
Shida inaanzia kwa upinzani wenyewe hili wakilijua itawasaidia sana kama wataendelea kukaza fuvu ikulu wataisikia kwenye radio na bahati mbaya sana hawana wafuasi wakuhoji nyendo zao kwa maana yakujenga
 
Viongozi wangu kina nani? Au hujui CCM ndiyo inaongoza nchi? Unaona ulivyo mpumbavu! Kumbe hujui hata nchi inaongozwa nani. Chochote kinachoharibika lawama ni kwa CCM. Bila saka nyie ndiyo wale wajinga wanaoning'iniza magololi kwenye sofa wakisubiri viongozi wa upinzani wawaletee mabadiliko. Wanapoona hakuna mabadiliko wanaanza kutupa lawama kwa wapinzani. Kwa taarifa yako hata huko upinzani kuna matapeli wengi tu. Bila wananchi wajinga kama wewe kujitambua hakuna litakalobadilika.
Wapinzani wenyewe katiba yao hawaifuati sijui tofauti yao na CCM iko wapi
 
Mimi Nakupinga,Magufuli ndo kaja kutuonesha kua sisi hatuna siasa na wanasiasa wa kueleweka…Hakuna tofauti kati ya siasa za chadema na ccm …kwahyo sis kama wananchi tujitahd tuje na solution ili siasa zetu ziwe za manufaa kwetu sisi na nchi yetu….Tofauti na Sasa.
Umeongea hoja kubwa sana shida kubwa wengi wao ni mashabiki wa vyama zaidi ya nchi
 
Shida inaanzia kwa upinzani wenyewe hili wakilijua itawasaidia sana kama wataendelea kukaza fuvu ikulu wataisikia kwenye radio na bahati mbaya sana hawana wafuasi wakuhoji nyendo zao kwa maana yakujenga
Viongozi wa upinzani wengi ni wababaishaji tu. Hamna watu pale.

Hakuna mtu aliyeserious atapoteza muda wake kuandamana na wanaharakati. Hizo nyakati zimeshapita.

Watu wanataka kusikia ubora wa sera na utekelezaji wake.

Hata dola sidhani kama itahangaika na wewe kama upo kwa ajili ya kuuza sera zako na sio kuibua hofu na kusambaza uongo.

Kwa bahati mbaya wapinzani hawana wanasiasa bali wana wajasiriamali tu katika siasa.

Kama wanataka kulisaidia hili Taifa wabadilike.
 
Kipindi cha Kikwete alileta mapnduz makubwa mno kwenye siasa za nchi yetu kwenye siasa za upinzani, Uhuru wa kuongea na baada ya kuongea, n.k.

Siwezi kusema kikwete alikuwa mkamilifu kwenye kuleta siasa huru lakini alijitahidi

  • Kwa mara ya kwanza wagombea wapinzani walijaa bungeni
  • matumizi madogo sana ya nguvu ya polisi kuzuia upinzani
  • Aliruhusu yeye na serikali yake kukosolewa
  • Uhuru wa kutoa maoni
  • jitihada ya mchakato wa katiba mpya
  • n.k.

Kwa mara ya kwanza tangu uhuru tulipiga hatua kubwa sana kwenye mazingira ya kisiasa, huwez amini skendo za ufisadi kama escrow na Richmond zilichambuliwa bungeni bila spika kuwazimia mic wapinzani au kukataa hoja izungumziwe, Vyombo vya habari viliweka mambo wazi bila hofu, n.k.

Tulitegemea utamaduni huu utadumishwa but kilichotokea ni opposite

Then came a man known as Magufuli, Siku za mwanzo tu aliwaonya wanaomkosoa "BE CAREFUL" hakuvumilia serikali yake kukosolewa waliodiriki walikiona cha mtemakuni, CAG alitimuliwa kwa kuweka wazi serikali inafuja pesa, Chato alikozalowa ilibustiwa sana, watu wasiojulikana, n.k.

Kinachoendelea ni kile kile part 2, ni utamaduni wa mfumo wa chama kmoja ulodumu miaka mingi na kuongezewa baadhi ya vitu hasa kwenye kuzimisha upinzani.

Itachukua miaka mingi sana kumpata kiongozi kama
Ni muda mfupi tu mifumo hiyo itasambaratika. Usifikiri itachukuwa miaka yote hiyo. Mungu amesikia kilio cha watu wake na atajibu. Sasa ole wao wote wanaofanya uonevu maana mambo yatawageuka!
 
Viongozi wa upinzani wengi ni wababaishaji tu. Hamna watu pale.

Hakuna mtu aliyeserious atapoteza muda wake kuandamana na wanaharakati. Hizo nyakati zimeshapita.

Watu wanataka kusikia ubora wa sera na utekelezaji wake.

Hata dola sidhani kama itahangaika na wewe kama upo kwa ajili ya kuuza sera zako na sio kuibua hofu na kusambaza uongo.

Kwa bahati mbaya wapinzani hawana wanasiasa bali wana wajasiriamali tu katika siasa.

Kama wanataka kulisaidia hili Taifa wabadilike.
Tatizo ni mfumo. Na sasa mifumo hiyo itasambaratishwa na Mungu. Lakini swali ni hili je mko tayari?
 
Back
Top Bottom