Nchi masikini haiwezi kuendelea ikiongozwa kidemokrasia

Nchi masikini haiwezi kuendelea ikiongozwa kidemokrasia

Kila mfumo una madhaifu yake..democracy included,ni messy na very slow na ugly

Ila hakuna mbadala wake,ndio the best system to human beings ever invented so far

Ku point out mabaya ya demokrasia tulishafanya shule,na swali watoto wakapata 100%

Shida ni kua huwezi leta mbadala maana haupo...kama wewe ni Einstein tuletee mbadala uliovumbua wewe

Yaani wewe leo umetuletea lile lile swali la Civics la Form 4 tulifanya na watoto wakapata A..

Nini udhaifu wa mfumo wa demokrasia?Elezea,na jee una mbadala bora zaidi yake?

HAKUNA!
Wewe unaongea kama peasants wote walivyoongea katika historia. Kwa sababu aliishi wakati wa ujamaa, basi kwake ndiyo mfumo bora kabisa, aliyeishi enzi za utumwa naye aliona hakuna mfumo bora kama huo. Aliyeishi kwenye ukabaila naye anaona huo ndiyo mfumo, aliyeishi kwenye ubepari naye huo ndiyo mfumo bora kabisa, na wewe kwa sababu unaishi zama za demokrasia, na wewe kwako ndiyo mfumo bora kabisa. Usiwe fuata upepo.

Mfumo usioweza kuzitoa nchi kwenye umaskini unasemaje ni best? Ni mfumo wa hovyo, ni kitu cha anasa kwa nchi tajiri kisichokuwa na manufaa yoyote, hata kwao.Kitawafelisha maana demokrasia inaenda sambamba na welfare ya kiwango cha juu. Na welfare inaenda sambamba na kodi kubwa na mikopo.

Demokrasia haina tofauti na ujamaa, ni mzuri kwenye makaratasi, lakini kiuhalisia una matatizo makubwa.
 
Africa ndilo bara lenye madikteta wengi na nchi chache za kidemokrasia ila ndilo bara maskini kupita yote pia.
Shida siyo kukosa demokrasia au udikteta. Shida ni sera mbovu za kiuchumi, na hasa kuingia kwenye soko huria kichwakichwa.
 
Nyumba nayo inafanya uchaguzi? Tangu lini? 😜
Nyumba ina taasisi mbali mbali zinazotumika katika kuminya uhuru na haki ya wanaoishi katika nyumba hiyo? Acha kuleta mifano buti isiyohusu kitu.

Wewe umewahi ona nyumba inaendeshwa kidemokrasia?

Na uelewe kuwa kukosa demokrasia haimaanishi kupiga, kuua na mambo mengine uliyotaja hapo juu.
 
Udikteta ni shida kubwa na ndiyo chanzo cha sera MUFILISI kama kujenga chato Airport, kununua ndege etc. Kama siyo udikteta hayo yote Bungeni yangepigwa chini katika Bunge huru.

Shida siyo kukosa demokrasia au udikteta. Shida ni sera mbovu za kiuchumi, na hasa kuingia kwenye soko huria kichwakichwa.
 
Wadada wa kazi mna maneno. Udikteta tangu lini ukawa mzuri? Enzi za nduli Idd ulikuwepo wewe, dikteta Mobutu aliiletea DRC maendeleo gani?

Dikteta wa nchi tajiri sana E. Guinea amefanya Nini E. G zaidi ya kuweka hela zote za nchi kwenye akaunti take huku mwanawe ambaye Ni waziri mkuu akizurula Marekani kwenye makasino.
Tujibu kwa mifano Pia, je General Park wa Korea? Vipi Kuhusu Lee Kuan Yew na Singapore? Vipi kuhusu CCP na China?

Ingekuwa Demokrasia ndio msingi wa Maendeleo duniani, basi Marekani wasingemuweka madarakani dikteta Pinochet na kumtoa mwanademokrasia Allende.
 
Udikteta ni shida kubwa na ndiyo chanzo cha sera MUFILISI kama kujenga chato Airport, kununua ndege etc. Kama siyo udikteta hayo yote Bungeni yangepigwa chini katika Bunge huru.
Yalikuwa ni mambo ya hovyo. Na pengine yaliletwa na demokrasia, ni kawaida kwa viongozi wa kidemokrasia kupeleka maendeleo kwa wale waliowapigia kura kwa wingi japo na madikteta hufanya hivyo.

Ila nielewe kuwa siungi mkono udikteta, na sijadai kuwa nina alternative ya demokrasia. Nimeweka tu mapungufu yake, na kama mfumo hauwezi kututoa kwenye umaskini, hayo ni mapungufu makubwa sana, ni kama haufai.
 
Makuwadi wa soko huria daima wanahubiri kuwa Demokrasia hii ya Kiliberali ndio msingi wa Maendeleo ya kiuchumi. Lakini historia inaonyesha Demokrasia haileti maendeleo ya kiuchumi bali ni zao la Maendeleo ya kiuchumi na huimarisha zaidi Maendeleo.

Na logic yake ni nyepesi tu, ili taifa lolote liendelee kiuchumi, ni lazima lilinde uzalishaji wa ndani, ni lazima liweke kodi kali kwa washindani, ni lazima lidhibiti mipaka yake na uingizwaji wa bidhaa shindani na lazima lihimize ufanya kazi kwa kujitoa. Sasa haya yote huchukua miaka takribani 30 kuyatenda na kufikia Maendeleo hayo. Katika mchakato huo kuna maadui wa nje na ndani, ambao hutumia watu na mbinu mbalimbali kuvuruga, pia yanasababisha uhaba wa bidhaa fulani fulani ambazo kwa mwanzo kuyumbisha ustawi wa jamii. So, haya huweza kutumiwa kuleta chokochoko na kuvuruga michakato hiyo. Ndio hufanya watawala wa wakati husika kuwa wakali na wababe (madikteta). Na hawa huwa ni madikteta wanaojenga jamii (Benevolent dictators). Ndio njia walizopitia Singapore, Korea kusini, China, Vietnam n.k. Baada ya kuendelea kiuchumi, jamii yenyewe automatically inakuwa na mapambano na uhitaji wa Demokrasia hii ya Kiliberali.

Kichotokea Afrika huku, Hii Demokrasia tunayolazimishwa kuitumia, haina lengo la kuleta Maendeleo, bali ni nyenzo ya wezi wa dunia kuiba huku.
 
Ili nchi iendelee inahitaji kiongozi mwenye maamuzi magumu na uthubutu. Maamuzi ambayo muda mwingine hayatapendwa na wananchi. Mambo kama haya hayawezekani chini ya demokrasia.

Hata wanaotuhubiria demokrasia kila siku wanajua kuwa haifai pale maamuzi magumu yanapohitajika. Ndiyo maana mataifa yenye nguvu yamejipa kura ya Veto umoja wa mataifa. Na pengine ndiyo maaana wanatuhubiria kila siku tuwe na demokrasia, wakijua kuwa tukiwa na demokrasia tutabaki maskini siku zote.

Demokrasia inabidi kuangaliwa upya
Nchi maskini nyingi zina wananchi wajinga wengi kuliko wananchi wenye faida za kujenga taifa.
 
Nchi maskini nyingi zina wananchi wajinga wengi kuliko wananchi wenye faida za kujenga taifa.
Maana yake itabidi kiongozi atekeleze zaidi sera za kuwapendelea wajinga(serq A kijinga😀)maana kama ni wengi maana yake hata kwenye sanduku la kura ni wengi, usipowatimizia matakwa yao utatoka. Na hakuna anayetaka kutoka.
 
Mambo ya hovyo yaliyoletwa na demokrasia lakini huna mifano ya hayo mambo ya hovyo yaliyosababishwa na demokrasia!? 😳😳

Yalikuwa ni mambo ya hovyo. Na pengine yaliletwa na demokrasia, ni kawaida kwa viongozi wa kidemokrasia kupeleka maendeleo kwa wale waliowapigia kura kwa wingi japo na madikteta hufanya hivyo.

Ila nielewe kuwa siungi mkono udikteta, na sijadai kuwa nina alternative ya demokrasia. Nimeweka tu mapungufu yake, na kama mfumo hauwezi kututoa kwenye umaskini, hayo ni mapungufu makubwa sana, ni kama haufai.
 
Makuwadi wa soko huria daima wanahubiri kuwa Demokrasia hii ya Kiliberali ndio msingi wa Maendeleo ya kiuchumi. Lakini historia inaonyesha Demokrasia haileti maendeleo ya kiuchumi bali ni zao la Maendeleo ya kiuchumi na huimarisha zaidi Maendeleo.
Mkuu natumaini kuna watu watakuelewa. Niongezee mfano mmoja wa karibuni. Nchi za Africa mashariki mwaka 2015 zilikubaliana kuwa mwaka 2019 zipige marufuku uagizaji wa nguo na viatu vya mitumba. Lengo ni kukuza uwezo wa ndani wa kuzalisha vitu hivyo. Rais Trump akasema kuwa nchi itakayopiga ban mitumba anaitoa kwenye AGOA. Viongozi wote wakafyata, ni Kagame peke yake(anayesifika kwa kutokuwa mwanademokrasia) ndiyo akabaki na msimamo. Ni wazi kuwa wengine hawa walijua kutolewa AGOA kungeleta makelele mengi kutoka kwa 'wanademokrasia' kwenye nchi zao. Mwisho wa siku mpango mzuri wa maendeleo umekufa kibudu.

Demokrasia na soko huria ni nyenzo za ukoloni mamboleo.
 
Wewe na mleta mada mmechanganya demokrasia na katiba. Kiasi cha demokrasia tunachostahili wote kimeainishwa katika katiba ambayo ndio hao viongozi wameapa kuilinda na kuitenda!!

Ajabu mnaosema kusiwepo na demokrasia hamsemi kuwe na utawala wa namna gani. Wanajeshi wapindue serikali ya kiraia na ku-suspend katiba? Kusiwe na mahakama? Uongozi wa kiraia upatikane vipi??

Mwishoni mnaonekana maamuma msioweza kusema ni mambo gani hamtaki yasiwepo. Kwani kujenga barabara, viwanda ni mambo ambayo hayakubaliani na demokrasia! Hamtaki wabunge, hamtaki wananchi wachague viongozi? Vipi akipatikana asiyependa maendelea wala demokrasia - mtakuwa hivo mpaka afe??

Pathetic. Low brain capacity!!
Hilo neno Pathetic. Law brain capacity!!
umenitukana mimi ama ni signature yako!!
 
Mkuu samahani nini maana ya demokrasia? Upi msingi wa uwepo wa demokrasia? Na Ni kivipi nchi haiwezi endelea kwa kufuata demokrasia? Na nchi itapata vipi maendeleo isipo kuwa na demokrasia?

Kipindi Cha mfumo wa chama kimoja nchi ilipiga hatua kiasi gani ? Maana kulikuwa hakuna mfumo wa vyama vingi Mpaka 1992.
Taja nchi iliyoendelea huku ikiwa na demokrasia wkt inaendelea.
 
Ili nchi iendelee inahitaji kiongozi mwenye maamuzi magumu na uthubutu. Maamuzi ambayo muda mwingine hayatapendwa na wananchi. Mambo kama haya hayawezekani chini ya demokrasia.

Hata wanaotuhubiria demokrasia kila siku wanajua kuwa haifai pale maamuzi magumu yanapohitajika. Ndiyo maana mataifa yenye nguvu yamejipa kura ya Veto umoja wa mataifa. Na pengine ndiyo maaana wanatuhubiria kila siku tuwe na demokrasia, wakijua kuwa tukiwa na demokrasia tutabaki maskini siku zote.

Demokrasia inabidi kuangaliwa upya
Dah....wachache sana watakuelewa....hasa wale wasiotumia kilevi Cha magharibi 🤣🤣🤣🤣🤭
 
Sasa mbona ktk Afrika, nchi nyingi ambazo kiuchumi ziko juu, ni zile zinazoongoza kwa demokrasia japo kwa kiwango fulani?na zile za makatiri sana hasa za west afrika ndiko umaskini umeshamiri?hii inakiwaje?

mfano mzuri hapa kwetu kwa awamu ya tano, licha ya ukatiri uliokuwepo ni hatua gani kubwa ya kimaendeleo tulifikia?

hali ya kiuchumi kwa wananchi ilikuwa mbaya , lakini waimba mapambio walikuwa wanasifia tu, leo hayupo ndio wanatuambia ukweli kuwa "jamani hali ilikuwa mbaya sana zile zilikuwa propaganda tu" tatizo la dikteta yeye ndiye anajiona kuwa anaakili kuliko wengine!!
Uchumi haupo hivyo eti mnafanya harakati za maendeleo alafu pesa zionekane mtaani, watu walitoa machozi jasho na damu kufika walipo, huwezi kujenga nyumba nzuri wakati una kipato cha kawaida zen at the same time ukawa una spend. Uchumi gn mmesoma waafrika?
 
Back
Top Bottom