Kutokuwa na demokrasia haimaanishi kuwa na udikteta. Tunahitaji mfumo ambao serikali haihitajiki kufanya maamuzi kuwapendeza wananchi bali iweze kufanya maamuzi kwa faida ya wananchi hata kama hayawapendezi.
Wewe unaongea kama peasants wote walivyoongea katika historia. Kwa sababu aliishi wakati wa ujamaa, basi kwake ndiyo mfumo bora kabisa, aliyeishi enzi za utumwa naye aliona hakuna mfumo bora kama huo. Aliyeishi kwenye ukabaila naye anaona huo ndiyo mfumo, aliyeishi kwenye ubepari naye huo ndiyo mfumo bora kabisa, na wewe kwa sababu unaishi zama za demokrasia, na wewe kwako ndiyo mfumo bora kabisa. Usiwe fuata upepo.Kila mfumo una madhaifu yake..democracy included,ni messy na very slow na ugly
Ila hakuna mbadala wake,ndio the best system to human beings ever invented so far
Ku point out mabaya ya demokrasia tulishafanya shule,na swali watoto wakapata 100%
Shida ni kua huwezi leta mbadala maana haupo...kama wewe ni Einstein tuletee mbadala uliovumbua wewe
Yaani wewe leo umetuletea lile lile swali la Civics la Form 4 tulifanya na watoto wakapata A..
Nini udhaifu wa mfumo wa demokrasia?Elezea,na jee una mbadala bora zaidi yake?
HAKUNA!
Shida siyo kukosa demokrasia au udikteta. Shida ni sera mbovu za kiuchumi, na hasa kuingia kwenye soko huria kichwakichwa.Africa ndilo bara lenye madikteta wengi na nchi chache za kidemokrasia ila ndilo bara maskini kupita yote pia.
Wewe umewahi ona nyumba inaendeshwa kidemokrasia?
Na uelewe kuwa kukosa demokrasia haimaanishi kupiga, kuua na mambo mengine uliyotaja hapo juu.
Shida siyo kukosa demokrasia au udikteta. Shida ni sera mbovu za kiuchumi, na hasa kuingia kwenye soko huria kichwakichwa.
Tujibu kwa mifano Pia, je General Park wa Korea? Vipi Kuhusu Lee Kuan Yew na Singapore? Vipi kuhusu CCP na China?Wadada wa kazi mna maneno. Udikteta tangu lini ukawa mzuri? Enzi za nduli Idd ulikuwepo wewe, dikteta Mobutu aliiletea DRC maendeleo gani?
Dikteta wa nchi tajiri sana E. Guinea amefanya Nini E. G zaidi ya kuweka hela zote za nchi kwenye akaunti take huku mwanawe ambaye Ni waziri mkuu akizurula Marekani kwenye makasino.
Yalikuwa ni mambo ya hovyo. Na pengine yaliletwa na demokrasia, ni kawaida kwa viongozi wa kidemokrasia kupeleka maendeleo kwa wale waliowapigia kura kwa wingi japo na madikteta hufanya hivyo.Udikteta ni shida kubwa na ndiyo chanzo cha sera MUFILISI kama kujenga chato Airport, kununua ndege etc. Kama siyo udikteta hayo yote Bungeni yangepigwa chini katika Bunge huru.
Nchi maskini nyingi zina wananchi wajinga wengi kuliko wananchi wenye faida za kujenga taifa.Ili nchi iendelee inahitaji kiongozi mwenye maamuzi magumu na uthubutu. Maamuzi ambayo muda mwingine hayatapendwa na wananchi. Mambo kama haya hayawezekani chini ya demokrasia.
Hata wanaotuhubiria demokrasia kila siku wanajua kuwa haifai pale maamuzi magumu yanapohitajika. Ndiyo maana mataifa yenye nguvu yamejipa kura ya Veto umoja wa mataifa. Na pengine ndiyo maaana wanatuhubiria kila siku tuwe na demokrasia, wakijua kuwa tukiwa na demokrasia tutabaki maskini siku zote.
Demokrasia inabidi kuangaliwa upya
Maana yake itabidi kiongozi atekeleze zaidi sera za kuwapendelea wajinga(serq A kijinga😀)maana kama ni wengi maana yake hata kwenye sanduku la kura ni wengi, usipowatimizia matakwa yao utatoka. Na hakuna anayetaka kutoka.Nchi maskini nyingi zina wananchi wajinga wengi kuliko wananchi wenye faida za kujenga taifa.
Yalikuwa ni mambo ya hovyo. Na pengine yaliletwa na demokrasia, ni kawaida kwa viongozi wa kidemokrasia kupeleka maendeleo kwa wale waliowapigia kura kwa wingi japo na madikteta hufanya hivyo.
Ila nielewe kuwa siungi mkono udikteta, na sijadai kuwa nina alternative ya demokrasia. Nimeweka tu mapungufu yake, na kama mfumo hauwezi kututoa kwenye umaskini, hayo ni mapungufu makubwa sana, ni kama haufai.
Mkuu natumaini kuna watu watakuelewa. Niongezee mfano mmoja wa karibuni. Nchi za Africa mashariki mwaka 2015 zilikubaliana kuwa mwaka 2019 zipige marufuku uagizaji wa nguo na viatu vya mitumba. Lengo ni kukuza uwezo wa ndani wa kuzalisha vitu hivyo. Rais Trump akasema kuwa nchi itakayopiga ban mitumba anaitoa kwenye AGOA. Viongozi wote wakafyata, ni Kagame peke yake(anayesifika kwa kutokuwa mwanademokrasia) ndiyo akabaki na msimamo. Ni wazi kuwa wengine hawa walijua kutolewa AGOA kungeleta makelele mengi kutoka kwa 'wanademokrasia' kwenye nchi zao. Mwisho wa siku mpango mzuri wa maendeleo umekufa kibudu.Makuwadi wa soko huria daima wanahubiri kuwa Demokrasia hii ya Kiliberali ndio msingi wa Maendeleo ya kiuchumi. Lakini historia inaonyesha Demokrasia haileti maendeleo ya kiuchumi bali ni zao la Maendeleo ya kiuchumi na huimarisha zaidi Maendeleo.
Hilo neno Pathetic. Law brain capacity!!Wewe na mleta mada mmechanganya demokrasia na katiba. Kiasi cha demokrasia tunachostahili wote kimeainishwa katika katiba ambayo ndio hao viongozi wameapa kuilinda na kuitenda!!
Ajabu mnaosema kusiwepo na demokrasia hamsemi kuwe na utawala wa namna gani. Wanajeshi wapindue serikali ya kiraia na ku-suspend katiba? Kusiwe na mahakama? Uongozi wa kiraia upatikane vipi??
Mwishoni mnaonekana maamuma msioweza kusema ni mambo gani hamtaki yasiwepo. Kwani kujenga barabara, viwanda ni mambo ambayo hayakubaliani na demokrasia! Hamtaki wabunge, hamtaki wananchi wachague viongozi? Vipi akipatikana asiyependa maendelea wala demokrasia - mtakuwa hivo mpaka afe??
Pathetic. Low brain capacity!!
Taja nchi iliyoendelea huku ikiwa na demokrasia wkt inaendelea.Mkuu samahani nini maana ya demokrasia? Upi msingi wa uwepo wa demokrasia? Na Ni kivipi nchi haiwezi endelea kwa kufuata demokrasia? Na nchi itapata vipi maendeleo isipo kuwa na demokrasia?
Kipindi Cha mfumo wa chama kimoja nchi ilipiga hatua kiasi gani ? Maana kulikuwa hakuna mfumo wa vyama vingi Mpaka 1992.
Taja nchi moja yenye demokrasia duniani.Mkuu utawala Bora, haki na utu ni misingi muhimu katika taifa linalo fuata demokrasia
Dah....wachache sana watakuelewa....hasa wale wasiotumia kilevi Cha magharibi 🤣🤣🤣🤣🤭Ili nchi iendelee inahitaji kiongozi mwenye maamuzi magumu na uthubutu. Maamuzi ambayo muda mwingine hayatapendwa na wananchi. Mambo kama haya hayawezekani chini ya demokrasia.
Hata wanaotuhubiria demokrasia kila siku wanajua kuwa haifai pale maamuzi magumu yanapohitajika. Ndiyo maana mataifa yenye nguvu yamejipa kura ya Veto umoja wa mataifa. Na pengine ndiyo maaana wanatuhubiria kila siku tuwe na demokrasia, wakijua kuwa tukiwa na demokrasia tutabaki maskini siku zote.
Demokrasia inabidi kuangaliwa upya
Uchumi haupo hivyo eti mnafanya harakati za maendeleo alafu pesa zionekane mtaani, watu walitoa machozi jasho na damu kufika walipo, huwezi kujenga nyumba nzuri wakati una kipato cha kawaida zen at the same time ukawa una spend. Uchumi gn mmesoma waafrika?Sasa mbona ktk Afrika, nchi nyingi ambazo kiuchumi ziko juu, ni zile zinazoongoza kwa demokrasia japo kwa kiwango fulani?na zile za makatiri sana hasa za west afrika ndiko umaskini umeshamiri?hii inakiwaje?
mfano mzuri hapa kwetu kwa awamu ya tano, licha ya ukatiri uliokuwepo ni hatua gani kubwa ya kimaendeleo tulifikia?
hali ya kiuchumi kwa wananchi ilikuwa mbaya , lakini waimba mapambio walikuwa wanasifia tu, leo hayupo ndio wanatuambia ukweli kuwa "jamani hali ilikuwa mbaya sana zile zilikuwa propaganda tu" tatizo la dikteta yeye ndiye anajiona kuwa anaakili kuliko wengine!!