Ndoa ina mwezi mmoja, nishaanza kukosa amani

Ndoa ina mwezi mmoja, nishaanza kukosa amani

Dini inaruhusu kuoa wapili?
Mathayo 19:4-6,10
[4]Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,

[5]akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?

[6]Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.

[7]Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha?

[8]Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi.


[10]Wanafunzi wake wakamwambia, Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa.

Ukimuacha ama ukaoa mwingine huyu uliemuoa unazini nae
Haya kama kanisa likikufungisha ndoa nyingine na suti nzur ukavaa
maandiko yanasema ww unazini nae maisha yako yote mbele za Mungu
Ndio maana maandiko yanasema hakikisha unaemuoa ni mungu amekupatia.
Sio tamaa zako.

Ww hutaweza kumuacha isipokuwa wakati unamuoa hukumkuta na bikira na yeye hakukuambia tangu mwanzo kuwa alishafanya uasherati kabla ya kuwa na ww na akakuomba msamaha kwa hilo

Mwanamke ndie anaevunja ndoa
Maandiko yanasema sio mwanaume ni mwanamke anaeivunja kwa ujinga wake.
 
Uchumba ni muhimu ukae na mtu ndani atleast hata miezi mitatu tu ....ya kuona je tabia vipi au miezi sita mkae ndani nyumba moja ndo uoe mambo ya mtu anatoka kwao straight kwako ndo anakuyaaona mambo

Mimi sasa hivi kama hatak kukaa na mimihuwa nampangia nyumba mimi naendelea kukaaa kwangu kuna siku naenda huko kwake nakaa hata week ...siku ingine mwezi nasoma tu mchezo nikiona hali sio nachimba so sasa hivi kuna mtu nimepangia naangalia ili nimuoe ...akizengua natimba tena kutafuta mwingine naamini hadi nikafike miaka 35 nitakuwa nimempata wa uhakika...
Hiki kitu niliwahi kuwashauri wadau humu ndani ila wakaniona mi muhuni, mara ooh binti atakujaje kukaa kwako ikiwa ana wazazi wake 😅 ila kwa wenye jicho la tatu walielewa vyema ile concept. Inasaidia sana hasa zama hizi ambazo watoto wakike hawana malezi.
 
Mathayo 19:4-6,10
[4]Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,

[5]akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?

[6]Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.

[7]Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha?

[8]Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi.


[10]Wanafunzi wake wakamwambia, Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa.

Ukimuacha ama ukaoa mwingine huyu uliemuoa unazini nae
Haya kama kanisa likikufungisha ndoa nyingine na suti nzur ukavaa
maandiko yanasema ww unazini nae maisha yako yote mbele za Mungu
Ndio maana maandiko yanasema hakikisha unaemuoa ni mungu amekupatia.
Sio tamaa zako.

Ww hutaweza kumuacha isipokuwa wakati unamuoa hukumkuta na bikira na yeye hakukuambia tangu mwanzo kuwa alishafanya uasherati kabla ya kuwa na ww na akakuomba msamaha kwa hilo

Mwanamke ndie anaevunja ndoa
Maandiko yanasema sio mwanaume ni mwanamke anaeivunja kwa ujinga wake.
Utajuaje kama Mungu ndie amekupatia maana wote uomba Mungu awape wenza lakini shetani huwahi kujibu maombi
Wengi ni malaika uchumbani wakiingia kwenye ndoa ugeuka chui.
 
Kama anakupoteza, kwanini umeleta hii mada humu? Au haujaelewa anamaanisha mrudishe kwao.

Mimi nashauri ufanye maamuzi ili ashike adabu na ujue kama aliingia kwenye ndoa kuonekana kaolewa Tu au laaaah!! Na kama ana bwana mwingine tangu unafahamu tu.

N.b.Mwanamke anayekupenda hasingekuwa hivyo kama wewe hauna makosa kwake.. fikra zako ziende nje ya boksi. Pole
Shida iliyopo sasa wanawake wanatafsiri kupendwa na mwanaume ni kama ataonyesha kuvumilia tabia za kipuuzi na hapo hapo ulizivumilia anakutoa thamani tena kuwa umeshindwa kuwa mwanaume imara na kumsimamia.

Mimi ndio maana siruhusu mizaha na mwanamke hata siku moja. Utani tunataniana sana na huwa nafanya nae comedy zile za couple hadi anajua hapa yupo na best friend wake ila anajua the moment akianza leta mizaha na makusudi mimi namchenjia na sina haya nae usoni.
 
yaelekea umeoa mwanamke ambaye hukumfahamu hapo awali. Hilo ni kosa ulilofanya. Sasa pima, kama mema ya msingi yake ni mengi basi vumilia, yakubali hayo mapungufu & ishi nae.
Hawa ndio wale siku ya ndoa unashangaa mwanaume anafuraha kuliko mwanamke mara akate viuno mbele ya hadhira bila hata soni, mara atoe risala ndefu akimsifia mwanamke wake utadhani alimpata kwa jackpot, mara apige goti kumvisha pete, mara alie tena. Yaani upuuzi mtupu.
 
Mbona hayo yote ni kawaida subiri phase two ndo utajue wanawake ni nini, rafiki yangu hu ni mwezi wa pili analala kwenye gari lake ila ndoa yake in miaka 4, hapo kwako hiyo inaitwa cooling break mechi bado kabisa.......
Sasa kuna faida gani ya kuoa au kuolewa. Mtakufa kabla ya siku zenu. Ndoa sio kuvumiliana ujinga.
 
kitu kimoja nakushauri, ndoa yangu inakaribia miaka 20 huko. kwenye ndoa, mkaribishe Yesu atawale maisha yenu, utaenjoy sana. Mimi ndoa yangu sikuanza na Mungu, ndani ya mwaka mmoja tulikuwa tunavurugana hadi najuta kuoa, nilikuwa hadi nampiga mke wangu ngumi na mateke kama mbwa, nakumbuka kuna mwaka niliwahi kumpiga mke wangu tukiwa na first born wetu akiwa na miaka kama mmoja. katoto kalivyo kadogo vilevile kalilia sana kakawa kanamsaidia mamake. ilinipa uchungu mno. zamani niliamini labda ni ile story kwamba mkiwa wote mmekutana ukubwani, kila mtu amelelewa na tabia zake, mkizichanganya lazima miaka miwili mitatu ya mwanzo mvurugane na mtakuja kuwa compatible baadaye. THIS IS VERY WRONG.

NIlikuja kuthibitisha hili ni la uongo baada ya kumpa Yesu maisha, ghafla kila kitu kilibadilika, upendo kwa mke wangu ulijaa, naye kwangu ulijaa, hadi tendo la ndoa hamu iliongezeka na utamu hata wa tendo la ndoa ukawa wa ajabu na yeye upande wake nikaona amebadilika nikimfanya anaonekana anaenjoy zaidi na anaonyesha kuridhika, tukawa kama mapacha hadi leo. sikatai, kumekuwa na ups and down kwenye hilo kwamba hatujakaa kama malaika, ila hata tukigombana kidogo tu kwa kauli, haipiti siku, tumeshapatana na tumekumbatiana. sisi huwa tunalala kwa kukumbatiana hadi leo, nilichojifunza ni hiki;

1. shetani ni roho, huwa anaweza kuingia kwa mmoja na kumtumia mgombane, hadi huwezi jua why mnagombana ila mnagombana tu, yeye shetani anawagongesha vichwa, anakaa pembeni anafurahia mnavyoumizana mioyo tena bila sababu za msingi, na kwa njia hiyo, anawarudisha sana nyuma kimaendeleo na kifamilia, anasababisha hadi magonjwa, hadi kuchepuka kwa silaha yake hii.

2. ukimpa Yesu Maisha yako (ukiokoka) akaondoka, kuna kuwa hakuna kugombana na ndoa inabadilika, manake kila mtu anamhofu Mungu, na kuchepuka kunapotea. ELEWA HILI, sisemi wote waliookoka hawagombani, no, hata ukiokoka unaweza kugombana na kuwa na ndoa mbaya, KAMA UMEOKOKA KWA JINA TU SIO KWA ROHO, wokovu wa Mungu ni wa uhakika, kama kweli umempa Yesu maisha na HUNA MICHANGANYO, Mungu akiwa maishani mwako shetani anafanya nini hapo? ataondoka tu, na kama ukienenda kiroho, shetani anaondoka. hao walokole unaona wanahangaika na ndoa, wamefanya michanganyo na wanafungua milango wao wenyewe shetani anaingia na kuwasumbua.

3. hata unyumba, unakuwa mzuri sana kama nyote mmeokoka kwa kweli. why? shetani huwa anaweza kuharibu chochote kama umemruhusu akaingia maishani mwako, kuna pepo mahaba, huwa yanawaingia wanaume kwa wanawake, hao ni maajenti wa shetani, ukiwa nalo utakuta mkeo wa kawaida tu, unaweza hata kulala naye kitanda kimoja ukaenda mzunguko mmoja tu, ila ukitoka unaenda mizunguko mingi na unaenjoy sana, ndio lengo la shetani, anaweza kukukosesha hamu ya tendo kwa mwenza wako ila nje upo fresh tu.

4. kuna watu wanakosa watoto, kumbe shetani amekaa kwenye vizazi vyao, mapepo ambayo ndio maajenti wa shetani, wanakaa kwako, wanakuoa, wanakuotesha mandoto unazini nao, na kiroho unayazalia hadi watoto. hayo ndiyo yanazuia mimba usipate, au mbegu zako zisizalishe. jaribu kwa Mungu, okoka kwa kweli, sio kwa dini, uone. Mungu atakushangaza.

5. kuna mengi naweza kuongea, mwenye shida ajaribu kumtafuta Mungu. Mungu anasema onjeni muone kuwa Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemtumaini Bwana, jaribu tu wala usisimuliwe.

Mwenye kunielewa amenielewa.
Ukiwa ndani ya Yesu utajawa Raha Sana in every aspect UTA experience rahaa
 
Tukisema msioe mnatuita mashoga, sasa pambana na hali yako.
Dunia ya sasa kwenye wanawake 20 unaweza kupata wawili au mmoja tu mwenye sifa ya kuwa mke.
Kwa sasa hata mmoja hakuna , amini usiamini huu ndiyo ukweli.
 
Jaman ndoa ndo zilivo.
Yaan tangu nimuoe nimuweke ndani naanza kuona tabia zinazoanza kuninyima aman.Had natamani nimwambie bana tumeshindwana

Tabia anazoonesha
1. Kisiran
2. Kununa
3. Kuzalisha migogoro

Haya yote alivyokuwa kwao sikua nayaona aisee nishachoka.Nimeukumbuka uhuru wangu
Hypergamy.
Hilo ni jaribio, women will always try to test men to see if they are strong enough.
Suluhisho sio kuoa mwingine, weka boundaries, zikivunjwa, you know what to do.
Ila usitafute mke wa pili, jua jinsi ya kudeal naye.
 
Utajuaje kama Mungu ndie amekupatia maana wote uomba Mungu awape wenza lakini shetani huwahi kujibu maombi
Wengi ni malaika uchumbani
Umewah kuwa kwenye shida ukamuomba Mungu ikapoteapotea.
Ama ukaomba kisha watu ata watatu wakaota ndoto moja inayofanana kila kitu kuhusu ww na hata hukuwaambia kitu kuhusu.
Ama umewahi kuomba kuwa na uhitaj na ukapata

Mungu hujihusisha sana na mamb matatu kwa mwanadamu
Kuhakikisha anapata wokovu.
Anapata mweza sahihi katika safari ya duniani.
Na kumpatia uzima wa milele.
Ayo mengine ni nyongeza.
Kuzaliwa kuoa/kuolewa na kufa.

Mungu hakupi usipomuomba.
Alimpa adam mke pasipo kuombwa akaishia kulalamikiwa kuwa ni huyu mwanamke ulienipa

Tangu siku hio Mungu hampi mtu mwenza isipokuwa uyo mtu amemhitaji na aakamuomba.

Kuhusu njia anazozijibu kasome visa mbali mbali vya watu waliotaka mke wakamshirikisha Mungu
Wakwanza akiwa ni isaka.

Ila kwakuwa umekishwa kosea.
Ww chakufanya ni kimoja

KUDUMU MWAMINIFU.
ENDELEA KUMPENDA TUU.
MUOMBEE SANA.
MUONYESHE UPENDO ZAIDI YA WA MWANZO BILA KUJALI,

Maana ibilisi alishakupata kupitia mke.
Kumbuka adam hakudanganywa na nyoka miaka yote mpaka pale mwanamke alipotumiwa na shetani.
Na ni hvyo kila wakati.

Huyo ni ibilisi kabisa amemvagaa mkeo.
Wala mkeo yeye hana shida.
 
Jaman ndoa ndo zilivo.
Yaan tangu nimuoe nimuweke ndani naanza kuona tabia zinazoanza kuninyima aman.Had natamani nimwambie bana tumeshindwana

Tabia anazoonesha
1. Kisiran
2. Kununa
3. Kuzalisha migogoro

Haya yote alivyokuwa kwao sikua nayaona aisee nishachoka.Nimeukumbuka uhuru wangu
KATAA NDOA
 
Back
Top Bottom