Ndoto tunazoota na tafsiri zake

Amina ndugu yangu. Naendelea kujitahidi kusali sana. Naamini nitashinda.. Nashukuru kunirahisishia kwa kunipa mistari ya kusimamia

 
Wanajamvi Mimi kuna binti nimeachana nae lakini bado naota nataka kukutana nae kimwili au tukianza tu tendo la ndoa nashtuka, maana yake nini wadau, naombeni msaada.
 
Wanajamvi Mimi kuna binti nimeachana nae lakini bado naota nataka kukutana nae kimwili au tukianza tu tendo la ndoa nashtuka, maana yake nini wadau, naombeni msaada.
Pole sio ishara nzuri! Hebu mfukuze maishani mwako kwa damu ya Yesu.
Nilikuwa Nina shida km hiyo ila niling'oa kwa jina La Yesu mapando yote na maneno yote aliyoyapanda kwa kuyanena!
Na sasa Nina nafuu simuoti wala haji akilini mwangu tena.

Pole. Mtumainie Mungu tu.
 

Tumezaa wote mtoto mmoja, ngumu kumsahau kabisa, bado namtegemea anipe taarifa za dogo
 
Tumezaa wote mtoto mmoja, ngumu kumsahau kabisa, bado namtegemea anipe taarifa za dogo
Pole sana, sijui vizuri ila kumuota MTU ktk hali hiyo na km no zaidi ya maramoja sio dalili nzuri..
Jenga utamaduni wa kusali na kujifunika kwa damu ya Yesu.

Pia sali sema.. Nang'oa ushawishi wowote wa nguvu za giza kutoka kwako Fulani.... Ni sala ndogo ila kiukweli nimesaidika sana!
 

Kwann unasema sio dalili nzuri?maana yake mini? Au nilimpenda sana? Nitaongeza maombi usichoke kunielewesha
 
Kwann unasema sio dalili nzuri?maana yake mini? Au nilimpenda sana? Nitaongeza maombi usichoke kunielewesha
Kutokana experience yangu.
Nilikataa kuweka mahusiano na MTU mmoja. Gafla nikaanza hivo nilikuwa nanuota na nakuta nimechafuka KBS, yani hadi sasa kuna pepo mahaba ananisumbua na napambana na maombi. Mwanzoni sikuhisi km inaweza kuwa shida ila sasahivi ndio imekuwa kero kuu. Ila kwanzia nimeanza kufukukuza ushawishi wowote wa nguvu za Giza kutoka kwake Nina nafuu kubwa.

Uchawi upo na unatesa sana.
 
Tumezaa wote mtoto mmoja, ngumu kumsahau kabisa, bado namtegemea anipe taarifa za dogo
Kuzaa naye siyo tiketi ya wewe umuote akujie usiku ndotoni ovyo.
Kwa ufupi elewa kuwa majini yanawajua watu wote ktk ukoo wako hata ambao wewe huwajui na hujawahi kuwaona.
Hukuletea taswira ya watu wako wa karibu ili usishituke kuwakemea ujue ni jamaa zako na kuwakemea uone kama unawasaliti.
Anza kutamka wazi kwa sala maombi ukiwa na akili timamu sema nakataa kuota ndoto za mapenzi kwa kuwa ni za kipepo. Kataa kwa nguvu kuu ya damu ya yesu kristo sema nimechoka kuonewa nahitaji niione njia yako yesu niwe huru. Vunja maagano yaliyopita kwa damu ya yesu sema hapana kwa damu ya yesu. Ujasiri huo utasambaa hata utapata nguvu ya kukemea hata ukutanapo na hali hiyo ndotoni.
Wengi wa watu huendewa kwa waganga kunuiiwa dawa ili warudiane kimapenzi na wapenzi walioachwa hivyo kinachokufuata siyo yule mtu bali majini ya upatanisho ambayo lazima yakulale ama ufanye nayo mapenzi then urudishe roho kwa mhusika.
Usikubali omba na kataa kwa neno utashinda. Acha kunyenyekea ujinga wa mashetani damu ya yesu ina nguvu sana ikiwa utaiamini. Hata ikiwa huna imani nayo bado Mungu wa Ibrahim ukimuomba atafanya miujiza mikuu juu yako. Asante.
 

Bwana Asifiwe, asante sana kwa ushauri wako ndugu
 
Tumezaa wote mtoto mmoja, ngumu kumsahau kabisa, bado namtegemea anipe taarifa za dogo
Mahusiano ya kimwili kwa maana ya kujua taarifa za mtoto siyo issue, hii kitu ipo katika roho, hapa unampeperusha katika ulimwengu wa roho mambo yanakwenda sawa. Kinachofanyika ni kuvunja roho ya mahusiano yasiyo rasmi katika na haya ya sasa yanaendelea pasipo tatizo.
 
Mtumeee!!! Kama umejibiwa PM nifowadie majibu. Nilikuwa nikiota joka lenye rangi nyeusi juu, nyeupe katikati na njano mkiani likinitimua. Na ndoto moja ilifanana kabisa na hii yako. Alipokuwa akinikimbilia kuna watu walikuwa wanampiga mawe halafu yale mawe yananipata mimi ila hayaumi - aliponikaribia aligeuka kuwa kaka ninayemfahamu. Siku zote nilizoota ndoto ya kupambana na hilo joka mazingira ni kijiji nilichokulia, kando ya mtoto penye majani mazuri na miti. Kuna siku bwana nikamkuta katikati ya barabara. Amegawa barabara katikati kama ile mistari ya kutenganisha leni. Alikuwa mrefu sioni kichwa wala mkia. Nikasema huyu kichwa kitakuwa mbali sana acha nimruke nivuke zangu. Lahaula! Ghafla joka liliniinukia na domo kubwa lenye ute ute na meno makali usoni kwangu. Nilishtuka usingizi nikiwa nimetota jasho natetemeka hatari. Nilibaki na hofu mwezi mzima. Nilikuwa shallow sana sijui hata kuomba. Mama yangu ndo akawa ananiombea. Siku moja nikaota nimelikuta mahali limepondwa limekufa. Sijawahi kuota tena. Miaka mingi imepita ila natamani kujua maana ya lile joka, zile rangi na yale mashambulizi.

Hii ya kuota marehemu ndo sisemi. Mtu hata kama sijawahi kumuota akishakufa tu lazima atanihusu kwenye ndoto. Kuna kaka ni ndugu tu wa ukoo alikufa. Sikuwa nimewahi kumuona maisha yangu yote. Baada ya maziko nikamuota. Baadae kwenye ulimwengu halisi nikaja kuona picha yake sura ni ile ile niliyoiona ndotoni. Hii hali ilizidi kunitisha. Majuzi nimeota nauguza watu mahututi ambao tayari walishakufa! Ina maana mimi ni marehemu ila sijijui au ????!
 

Samahani nimecheka. Mwanao wa kipepo ndo nini? Inaelekea maisha yako yako vululuvululu mno. Kiroho sijui ila kisaikolojia unahangaika kutafuta wewe ni nani.
 
Hii inatokana na wivu ulionao kwa mpenzi wako ambae humuamini,huwa unaamini anatoka na mdada mwenye USAFIRI.
Na kwa muda umekuwa ukiamini kuwa USAFIRI ndiyo kivutio kwa mwenza wako.
Nenda kafagilie kaburi la babu yako na bibi,inaonyrsha hujapita siku nyingi,ila usipande gari yoyote yenye rangi NYEKUNDU NA NYEUSI,hata kama ni alama ya nukta tu.
 
Mm huwa naota nakunywa damu ya mbuzi na kisa kichwa chake lakini juu ya paji la uso wa mbuzi na ulimi wake ina alama ya namba 666.

Ni miezi 4 sasa naota hivyo..... Shida ni nini.
 
Samahani nimecheka. Mwanao wa kipepo ndo nini? Inaelekea maisha yako yako vululuvululu mno. Kiroho sijui ila kisaikolojia unahangaika kutafuta wewe ni nani.
No Maisha yangu yako poa sana, pengine yako ndio yako vuluvulu, km sio mtaalamu wa ndoto ukaelewa MTU ameeleza mini, kunyamaza sio ujinga ila ni busara kubwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…