Ndugu katika imaan, inakuwaje nchi ya kiislamu maiti iwekwe wiki nzima bila kuzikwa?

Ndugu katika imaan, inakuwaje nchi ya kiislamu maiti iwekwe wiki nzima bila kuzikwa?

Umeleta ushahidi wa hiki ulichoandika?
Mkuu jibidiishe kusoma.
Katika Uislam kuna vitu vya lazima, hivi huitwa FARADHI, kuacha na kutenda. Vile vya kuacha ukivifanya unapata dhambi na vya kutenda usipotenda unapata dhambi. Mfano sala, usiposali unapata dhambi na usizini, ukizini dhambi. HIYO NDIO MAANA YA LAZIMA katika uislam. Vitu vyote vilivyopigwa marufuku vimeelezwa katika kitabu chao Quran. Hakuna maelezo katika Quran yanayoelekeza mtu azikwe siku gani au azikweje.

Sambamba na hilo, kuna mafundisho na matendo ya Mtume wao (SAW), aliyoyaelekeza kufanya. Haya, sio lazima kwamba yafanyike. Mfano Muhammad ndio kaelekeza wazikane namna gani. Lakini hakuna ulazima mtu azikwe hivyo, lililo muhimu mtu azikwe na uchache wa kumzika mtu ni kumuweka kaburini na kufukia. Hayo mengine ni ziada tu.

Katika maelezo yake Muhammad kapendekeza mambo yafuatayo yafanyike haraka ikiwa yatatokea
1. Mtu akifa azikwe haraka kama hakuna sababu ya kuchelewesha.
2. Mtu akitaka kusilimu asilimishwe fasta.
3. Watu wakitaka kufunga ndoa waozeshwe haraka.

Kwahiyo kwa sababu walizo nazo wenyewe Wairan, wanachelewesha maziko na wala hawapati dhambi.

Kama una hoja lete.
 
Sio ina unafiki,wanafiki ni ngozi nyeusi ambao wanaivamia kuliko kupata elimu yake.Wakiambiwa wasome dini kiundani hawataki,pelekeni vijana wakasome Dini Uarabuni hawataki,kiufupi mtu wa Pwani hapendi elimu
Wewe ndio walewale mtumwa wa fikra 🚮🚮🚮
 
Huu uzi ntajifunza mengi sana, kuna watu hapa jamii forum nawaonaga wana akili ila kupitia Huu uzi ntawajua uwezo wao kiakili, na ntawajua wale ambao wameenda shule na wana hata phd ila bado wametawaliwa kikoloni, yani hawa wazazi wao walipoteza hela bure, waliuza ng'ombe ya maziwa nyumbani wakapeleka ng'ombe nyingine shule isiyo na tija, sasa hawana maziwa tena nyumbani na ile ng'ombe walio ipeleka shule ni tasa. Ukombozi wa fikra ni muhimu sana.
 
Kuna kitu sijakielewa bado, Iran ni Taifa la kiislamu, Rais ameuwawa na chopa jumapili, lakini mazishi yatafanyika Alhamisi, wakati deen inasema muislamu akifa azikwe haraka tena hukohuko alipofia.

Je hamuoni kwamba Iran ni Jamhuri ya kiislamu lakini hawafuati uislamu unasemaje?

IRAN sio taifa la Kiislamu, bali ni taifa linalo ongozwa kwa dini ya KISHIA.
 
Hapo hapo nipewe elimu kidogo, Kuna Ile mwanamke wa kiislam hapaswi kupeana mkono na mtu anayeweza kumuoa.

Lakini Mkuu wetu nimeona Mara nyingi anasalimiana na watu kadhaa Kwa kupeana mikono. Hiyo nayo imekaaje?

Kuna Uislamu na kuna waislamu. Wewe tosheka ya kuwa Uislamu unakataza jambo hilo.
 
Kama wazungu walivyopuuzia ukristo ndio una maana hiyo.?Sasa wanaume kwa wanaume wanaoana na wewe upo kwenye hilo genge?Dini zipo na kuna vitabu na sheria zake.Wewe fuata umagharibi lakini ukitongozwa ukubali usirushe ngumi.Si unapenda umagharibi wewe.

Thibitisha hili.
Endelea kuabudu mizimu ya kiislamu halafu unajiona mjanja
 
Ndivyo kuruani inavyosena? Kuwa Hadhi za mazishi ziko tofauti

Sasa huku mitaani hata ueaambie waislamu subirini ndugu zake wake Wanasema akifa anatakiwa kuzikwa haraka
Kuzikwa haraka imesisitizwa tu. Lakini hapajasemwa kwamba eti mkiacha kuharakisha mnapata dhambi hapana

ndio maan hutamsikia shekh yeyote akisema wanaochelewesha maiti watapata dhambi na wataingia motoni.

Nakupa mfano kwenye swala kuna za lazima na za Sunna (Si lazima), ukiacha kuswali swala ya sunna hupati dhambi lakini ukiacha ya lazima unapata dhambi

Kuzika ni LAZIMA mkiacha kumsitiri mtu mnapata dhambi maana ni lazima, LAKINI kuwahisha kuzika sio lazima hata mkichelewesha hampati dhambi
Kama hakuna nyudhuru zozote ndio pakasemwa wahisheni kuzika ili kutoweka majonzi sana

SASA watu wanashikiliiiiaaaaa suala la kuwahisha kuzika jambo ambalo sio la lazima

Ingekua vizuri kama watu wangeshikilia suala la watu waache Uzinzi maan ilo ni jambo la lazima kuliacha ukifanya unapata Dhambi lakini halisisitizwi maana Kuzini kumekua kama kunywa maji
 
Dini ya kiislamu haisemi ni LAZIMA kuzika siku hiyo hiyo inasema ni vizuri usicheleweshe kuzika maiti kama hamna sababu za maana za kufanya hivyo.
Msiwe mnakurupuka kwenye conclusion huku hamjui chochote kuhusu Uislamu.
Kadhalika ukibanwa sana njaa kula nguruwe
 
Kadhalika ukibanwa sana njaa kula nguruwe
Ndio Ipo hadithi inasema ivo pakitokea unanjaaa na hakuna chakula chochote kile kinachopatikana zaidi ya Ngurue basi kula ili USIFE

Hapa pakawekwa msisitizo KULA KIASI CHA KUKUTOA HIYO NJAA TU.
 
halafu anatokea humu nyumbu mweusi anatetea dini ya mnyaazi mungu kichwani mweupe hajui anachokiamini ni kitu gani kajawa na jazba anatukana watu hovyo akiwaita makafiri
Tunahitaj viongoz wasio wadini ili kukomesha ujinga ka huo.
 
Wale ni Washia wana Uislam wao! Hawa wavaa suruali zilizokatwa na makobazi ndiyo nadhani wanazika siku hiyo hiyo!
Lakini kwa kuwa ni kiongozi wa kitaifa lazima kuwepo taratibu nyingine za kuzika!
Hapa Tanzania alikufa Mzee Ruksa na VP wa Mkapa Dk.Omar Juma walipokufa sikumbuki kama walizikwa siku hiyo hiyo!
 
IRAN sio taifa la Kiislamu, bali ni taifa linalo ongozwa kwa dini ya KISHIA.
Iran ni Jamhuri ya kiislamu tangu mwaka 1979.

Au ulitaka wawe Sunni au Sufi ndio ujuwe ni waislamu?

Kwani hawa Mashia wamewakodea nini? Msifanye siri semeni wazi tulijuwe tatizo.
 
Back
Top Bottom