NECTA yathibitisha tuhuma alizotoa mwanafunzi wa Chalinze Modern Islamic ni za kweli, Yaifungia shule

NECTA yathibitisha tuhuma alizotoa mwanafunzi wa Chalinze Modern Islamic ni za kweli, Yaifungia shule

Kawaida wazazi wana shirikiana na walimu ktk hizi tuhuma

Pia walimu utumia kusaidia vijana wao wasio jiweza waweze kutusua ili waweze kupata marks za kwenda shule nzuri private au government
.... mbaya sana! Ni zaidi ya ushetani kumnyima mwenye haki haki yake!
 
Halafu kwa uandishi huo unakuta kijana amesoma mpaka form 4 pengine mpaka chuo ila anaandika hivyo[emoji1787]
Mie nawaona wengi tu siku hizi sijui tatizo nini?.
Enzi tunasoma sisi miaka ya 90 ilikuwa mwanafunzi wa darasa la tatu anajua kuandika vizuri, kupangilia sentensi na herufi lakini hawa wa siku hizi sielewi!
Kwaiyo hichi ulichokiandika ndio kimepangilia vizuri?
 
Huyo binti Serikali impeleke shule za vipaji maalumu anaonyesha ana akili nyingi mno kuanzia darasani hadi uelewa mkubwa wa kisheria wa kudai haki zake

Mbeleni aweza ifaa nchi huyo Nadhani naeleweka kwa wenye uelewa
... yuko vizuri sana upstairs! Kitendo cha kuwa bold kudai haki yake tena kwa level yake ya STD7 yuko vizuri sana. Wengine hata F4, F6, hata vyuo huko wangeogopa kudai haki zao kama kawaida ya watanzania walio wengi.

Mfano, mtu mzima anaenda kununua bidhaa iwe dukani, sokoni, buchani, n.k anaona kabisa mizani "imechezewa" lakini kumwambia live muuzaji anaogopa! Huyo binti achongewe sanamu kama mdai haki mdogo zaidi kuwahi kutokea nchini.
 
Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA), limethibitisha kuwa mwanafunzi wa darasa la 7 Iptisum Suleman Slim, alibadilishiwa namba ya mtihani na uchunguzi umepelekea kugundulika kwa wanafunzi wengine 7 kubadilishiwa namba zao za mitihani, na kuchukua hatua ya kuifungia shule ya Chalize Modern kuwa kituo cha mitihani ya baraza hilo.

Waziri wa Elimu na Sayansi na Teknolojia, Mhe.Prof.Adolf Mkenda, amesema uchunguzi umebaini taarifa zilizotolewa na mwanafunzi huyo ni kweli.

ITV

=========

Uchunguzi uliofanywa na Baraza la Taifa la Mitihani, umebaini kuwa mwanafunzi Iptisum Suleman Slim, wa Shule ya Chalinze Modern Islamic Pre and Primar alibadilishiwa namba yake akiwa chumba cha Mtihani.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda amesema uchunguzi pia umebaini wanafunzi wengine sita walibadilishiwa namba ya mtihani katika mtihani wa taifa wa darasa la saba.

Kutokana na kosa hilo, Profesa Mkenda pia amesema Serikali imeifungia shule hiyo kuwa kituo cha mtihani kwa muda usiojulikana pamoja kuagiza watumishi waliohusika na udanganyifu kuchukuliwa hatua.

Pia soma:
Hao walimu waliohusika kwenye ujinga huo wamelaaniwa na watapata laana kubwa hapa duniani na akhera. Hawawezi kucheza na maisha ya watoto kwa sababu za kipuuzi wanazozijua wao wenyewe.
 
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda amesema uchunguzi pia umebaini wanafunzi wengine sita walibadilishiwa namba ya mtihani katika mtihani wa taifa wa darasa la saba.

Kutokana na kosa hilo, Profesa Mkenda pia amesema Serikali imeifungia shule hiyo kuwa kituo cha mtihani kwa muda usiojulikana pamoja kuagiza watumishi waliohusika na udanganyifu kuchukuliwa hatua.
ccm mna vituko 😄
Tuhuma si za kweli. Shule imefungiwa.Hau?
🤣
 
Hii ni habari kubwa sana kwa watu wanaotaka mfumo wa kuendesha elimu yetu ubadilishwe. Hiyo ilikuwa ni English Medium.

Jinsi vyombo vyetu vya habari vilivyo dhaifu unakuta kumuita huyo mtoto kufanya naye stori, inakuwa ngumu.
... ha ha ha! Inaonekana unachukia sana mfumo wa elimu kwa Kiingereza Mkuu. Kwenye hii issue English inaingiaje?
 
Halafu kwa uandishi huo unakuta kijana amesoma mpaka form 4 pengine mpaka chuo ila anaandika hivyo[emoji1787]
Mie nawaona wengi tu siku hizi sijui tatizo nini?.
Enzi tunasoma sisi miaka ya 90 ilikuwa mwanafunzi wa darasa la tatu anajua kuandika vizuri, kupangilia sentensi na herufi lakini hawa wa siku hizi sielewi!
Yaani ni shida qumeermake,sijui wanafundisha nini huko shuleni siku hizi!!
 
... yuko vizuri sana upstairs! Kitendo cha kuwa bold kudai haki yake tena kwa level yake ya STD7 yuko vizuri sana. Wengine hata F4, F6, hata vyuo huko wangeogopa kudai haki zao kama kawaida ya watanzania walio wengi.

Mfano, mtu mzima anaenda kununua bidhaa iwe dukani, sokoni, buchani, n.k anaona kabisa mizani "imechezewa" lakini kumwambia live muuzaji anaogopa! Huyo binti achongewe sanamu kama mdai haki mdogo zaidi kuwahi kutokea nchini.
Huwa kuna tuzo ya Mwanamke jasiri nimesahau watoaji huyu msichana watetezi wa haki za binadamu ,vyama vya wanasheria nk wampe tuzo ya jasiri

Msichana kusimama single handedly kutafuta haki yake

Hakuna mijitu mibwege nchi hii kama hao wanaojitia watetezi wa haki za binadamu Tanzania. njaa tu unawasumbua.Mtoto kwa kuwa hakuwa na hela hakuna hata taasisi moja ya kutetea haki za jamii iliyojitokeza kumsaidia.Waliufyata sababu wanaona hamna maslahi ya hela.

Hata Chadema wanaojifanya watetezi wa wananchi hawakujitokeza walijifungia kwenye vyoo vya ofisi ya makao makuu ya Chadema Ufipa.Utafikiri hata hawakusikia malalamiko ya huyo mtoto

Huyo msichana apewe nisha ya ujasiri ita motivate wasichana wengine kuwa bold kwenye kudai haki zao ns kuwa na misimamo wanapoonewa au kutaka kuonewa

Niwapongeze waandishi wa habari wamefanya kazi kubwa sana
 
Huwa kuna tuzo ya Mwanamke jasiri nimesahau watoaji huyu msichana watetezi wa haki za binadamu ,vyama vya wanasheria nk wampe tuzo ya jasiri

Msichana kusimama single handedly kutafuta haki yake

Hakuna mijitu mibwege nchi hii kama hao wanaojitia watetezi wa haki za binadamu Tanzania. njaa tu unawasumbua.Mtoto kwa kuwa hakuwa na hela hakuna hata taasisi moja ya kutetea haki za jamii iliyojitokeza kumsaidia.Waliufyata sababu wanaona hamna maslahi ya hela.

Hata Chadema wanaojifanya watetezi wa wananchi hawakujitokeza walijifungia kwenye vyoo vya ofisi ya makao makuu ya Chadema Ufipa.Utafikiri hata hawakusikia malalamiko ya huyo mtoto

Huyo msichana apewe nisha ya ujasiri ita motivate wasichana wengine kuwa bold kwenye kudai haki zao ns kuwa na misimamo wanapoonewa au kutaka kuonewa

Niwapongeze waandishi wa habari wamefanya kazi kubwa sana
... hapo Chadema inaingiaje? Sio lazima kila kitu uingize siasa.
 
... ha ha ha! Inaonekana unachukia sana mfumo wa elimu kwa Kiingereza Mkuu. Kwenye hii issue English inaingiaje?
Kwanza sichukii mfumo wa kutoa elimu kwa Kiingereza. Lakini kama Kiingereza ni kuelewa mbona kuna watoto ilibidi wafanyiwe mitihani yao na wengine??

Kufundisha kwa Kiingereza kuanzia darasa la Kwanza mpaka chuo Kikuu siyo suluhisho kwa matatizo ya mfumo wetu wa elimu uliojaa mataka taka ya kutosha.

.. yuko vizuri sana upstairs! Kitendo cha kuwa bold kudai haki yake tena kwa level yake ya STD7 yuko vizuri sana. Wengine hata F4, F6, hata vyuo huko wangeogopa kudai haki zao kama kawaida ya watanzania walio wengi.
Umeona ulichokuwa umeandika hapa. Kumbe watu wapo F4,F6 au chuo kikuu hawajafikia daraja ya Iptsum.

Elimu na Lugha ni kama Kapu na kinachobebwa. Kama kinachobebwa ni kinyesi hata kapu liwe zuri kiasi gani bado harufu itatoka na karaha itapatikana. Lakini kama kinachobebwa ni dhahabu, basi hata kama kapu ni bovu kiasi gani, haliwezi kupunguza thamani ya dhahabu.
 
Kwanza sichukii mfumo wa kutoa elimu kwa Kiingereza. Lakini kama Kiingereza ni kuelewa mbona kuna watoto ilibidi wafanyiwe mitihani yao na wengine??

Kufundisha kwa Kiingereza kuanzia darasa la Kwanza siyo suluhisho kwa matatizo ya mfumo wetu wa elimu uliojaa mataka taka ya kutosha.


Umeona ulichokuwa umeandika hapa. Kumbe watu wapo F4,F6 au chuo kikuu hawajafikia daraja ya Iptsum.

Elimu na Lugha ni kama Kapu na kinachobebwa. Kama kinachobebwa ni kinyesi hata kapu liwe zuri kiasi gani bado harufu itatoka na karaha itapatikana. Lakini kama kinachobebwa ni dhahabu, basi hata kama kapu ni bovu kiasi gani, haliwezi kupunguza thamani ya dhahabu.
... kwenye ule uzi mwingine nili-comment "... English inajenga confidence sana ..."; na ndicho kinachoshuhudiwa kwa huyo binti kwa sababu msingi wake wa Kiingereza ni mzuri hali iliyompa confidence of course along with her other personal traits. Angekuwa shule za Kiswahili, I believe, haki yake ingekuwa imepotea.
 
Wazazi tuwe makini sana.
francis.png
 
Ndio maana inafanya tuwe na baadhi ya Viongozi mbumbumbu.
 
Back
Top Bottom