Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu wa shule kaigeuza shule ya kiislamu(Islamic School) kuwa ya kutengeneza mapoyoyo.Kaabishaje uislam
Breaking news:
Profesa Mkenda asema wanafunzi saba walibadilishiwa namba za mtihani
Profesa Mkenda asema wanafunzi saba walibadilishiwa namba za mtihani
Jumanne, Oktoba 25, 2022
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknlojia, Profesa Adolf Mkenda akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaamu jana,akitolea ufafanuzi tukio la mwanafunzi aliyemaliza darasa la saba katika shule ya awali na msingi ya Chalinze Modern Islamic, Iptisum Slim (wa kwanza kulia) ambaye alilalamika kufanya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi kwa namba isiyo yake. Picha na
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda amesema kuwa ni kweli mwanafunzi wa Shule ya Chalinze Modern Islamic Pre and Primary, Iptisum Slim pamoja na wanafunzi wengine sita walibadilishiwa namba ya mtihani katika mtihani wa taifa wa darasala saba.
Profesa Mkenda amebainisha hayo leo Jumanne Oktoba 25, 2022 akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
“Uchunguzi uliofanywa na Kamati ya Uendeshaji Mitihani ya Mkoa wa Pwani kwa kushirikiana na wataalamu wa maandishi kutoka Jeshi la Polisi (Forensic Bureau) umebainika jumla ya watahiniwa saba walibadilishiwa namba za mtihani katika kituo cha mtihani namba PS1408009 shule ya Awali na Msingi Chalinze Modern Islamic” amesema Profesa Mkenda
Uchunguzi huo ulifanywa baada kusambaa kwa video katika mitandao ya kijamii ikimuonesha mtahiniwa Iptisam Suleiman Slim wa kituo cha mtihani cha shule ya Awali na Msingi Chalinze Modern Islamic akieleza kwamba, alibadilishiwa namba yake ya mtihani wakati akifanya Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi (PSLE) uliofanyika Oktoba 05 na 06/10/2022.
Profesa Mkenda amesema kuwa baada ya kupata taarifa hiyo Serikali kupitia Baraza la Mitihani ilielekeza Kamati ya Uendeshaji Mitihani ya Mkoa wa Pwani kufanya uchunguzi kuhusu malalamiko ya mtahiniwa na kuwasilisha taarifa Baraza la Mitihani.
Amesema kuwa uchunguzi uliofanyika pia umebaini kuwa mwanafunzi huyo pamoja na wanafunzi wengine sita walibadilishiwa namba ya mtihani katika mtihani wa taifa wa darasala saba.
“Mtahiniwa Iptisam Suleiman Slim alifanya masomo matano kwa kutumia namba PS1408009/0040 na somo la sita (mwisho) kwa kutumia namba PS1408009/0039 na Watahiniwa wengine wanne pia walibadilishiwa namba katika somo la sita katika kituo hicho,” amesema.
Profesa Mkenda pia amesema Shule ya Chalinze Modern Islamic Pre and Primary iliyoko mkoani Pwani imefungiwa kuwa kituo cha mtihani kwa muda usiojulikana.
Vilevile, Profesa Mkenda ameagiza watumishi waliohusika na udanganyifu katika mtihani wa darasa la saba Shule ya Chalinze Modern Islamic Pre and Primary kuchukuliwa hatua.
Pia, Profesa Mkenda ameiagiza Necta kumefanya marekebisho ya namba za mitihani za watahiniwa husika ili kila mtahiniwa aweze kutunukiwa matokeo yake halali.
“Nisisitize kuwa shule yoyote itakayobainika kufanya vitendo vya udanganyifu wa mitihani, itafungiwa na hata kufutwa kabisa kuendesha shughuli za elimu nchini,” anasema.
Source: Mwananchi
Naunga mkono hoja.Afande mmoja,afisa usalama mmoja, wa walimu kadhaa walikuwepo hapo wanarinda hawa nao Kwa taarifa za chini chini nao walikula mgao je tunawaachaje?
Mh Waziri futa kazi hao waliokuwepo siku hiyo Ili liwe funzo Kwa wote
Nakazia hapaMaswala ya namba za wanafunzi afande anahusika vipi,yeye kazi yake ni kulinda mitihani tu
Ha ha ha! Afande kashikilia bunduki yake sawasawa ana-monitor pande zote nne za dira hata kinachoendelea huko ndani hana habari wala hayamhusu.Maswala ya namba za wanafunzi afande anahusika vipi,yeye kazi yake ni kulinda mitihani tu
Mi naona wahusika wote wapewe kesi ya Jinai, shule isifungiwe, maana bado ina Wanafunzi wengi tu wasiokua na hatia, na Wana haki ya kupata elimu!Afande mmoja,afisa usalama mmoja, wa walimu kadhaa walikuwepo hapo wanarinda hawa nao Kwa taarifa za chini chini nao walikula mgao je tunawaachaje?
Mh Waziri futa kazi hao waliokuwepo siku hiyo Ili liwe funzo Kwa wote
Kuna watu huwa mnakurupuka kama Mkojo wa janaba. Afisa Usalama anaingia chumba cha mtihani? Anahusikaje na mpangilio wa Namba za Watahiniwa?Afande mmoja, afisa usalama mmoja, wa walimu kadhaa walikuwepo hapo wanalinda hawa nao Kwa taarifa za chini chini nao walikula mgao je tunawaachaje?
Mhe. Waziri futa kazi hao waliokuwepo siku hiyo Ili liwe funzo Kwa wote.
Wapi monde arabeNoma sana
Hapa imetumika methali ya samaki mmoja akioza wote wanaoza wakati siku hizi tunamwondoa aliyeoza wengine tunaanika juani mambo yanaendelea.Mi naona wahusika wote wapewe kesi ya Jinai, shule isifungiwe, maana bado ina Wanafunzi wengi tu wasiokua na hatia, na Wana haki ya kupata elimu!!
Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Kuna mtu alikuletea hilo swali nyumbani kwenu?Au umelikuta tu nimeandika?Kwa nini limekusumbua?Sasa unamuuliza nani tena wakati wewe umesema tuhuma si za kweli?
Huwa kuna tuzo ya Mwanamke jasiri nimesahau watoaji huyu msichana watetezi wa haki za binadamu ,vyama vya wanasheria nk wampe tuzo ya jasiri
Msichana kusimama single handedly kutafuta haki yake
Hakuna mijitu mibwege nchi hii kama hao wanaojitia watetezi wa haki za binadamu Tanzania. njaa tu unawasumbua.Mtoto kwa kuwa hakuwa na hela hakuna hata taasisi moja ya kutetea haki za jamii iliyojitokeza kumsaidia.Waliufyata sababu wanaona hamna maslahi ya hela.
Hata Chadema wanaojifanya watetezi wa wananchi hawakujitokeza walijifungia kwenye vyoo vya ofisi ya makao makuu ya Chadema Ufipa.Utafikiri hata hawakusikia malalamiko ya huyo mtoto
Huyo msichana apewe nisha ya ujasiri ita motivate wasichana wengine kuwa bold kwenye kudai haki zao ns kuwa na misimamo wanapoonewa au kutaka kuonewa
Niwapongeze waandishi wa habari wamefanya kazi kubwa sana
SasA hapo kajiaibisha yeye au kauabisha uislam?Mkuu wa shule kaigeuza shule ya kiislamu(Islamic School) kuwa ya kutengeneza mapoyoyo.
Bahsti nxuri huyo mtoto mdigo kawaumbua vibaya.
Rubbish fool mother***"erRubbish.
Akili kichwani kwako.SasA hapo kajiaibisha yeye au kauabisha uislam?